Wednesday, August 28, 2013

Uzinduzi wa Kampeni ya Kuchangia Maabara na Madawati chini ya Shirika la UDI



Mhe. John Mnyika akishirikiana na Mratibu John Mallya kuonyesha bango lenye ujumbe wa harambee ya kuchangia maabara na maktaba iliyozinduliwa Agosti 21, 2013

Thursday, August 15, 2013

Leo Agosti 15, 2013: Sengerema na Mwanza Mabaraza ya wazi ya Katiba Mpya

Sengerema: Endeleeni kutoa maoni kwa maneno na maandishi kwenye baraza letu la katiba linaloendelea uwanja wa Wenje kata ya Nyamburukano

Mwanza: Baraza la wazi la Jiji likijumuisha pamoja Wilaya za Ilemela na Nyamagana litaanza saa 9 alasiri Uwanja wa Magomeni kata ya Kirumba.

Mwenyekiti Mbowe na mimi tutashiriki katika michakato hiyo.

Maslahi ya Umma Kwanza!!

Monday, August 12, 2013

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; tukutane tushiriki mabaraza ya wazi ya katiba.

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; ni kushiriki kikamilifu baraza la wazi la katiba. Mwenyekiti Mbowe na mimi tutajumuika nanyi kupitia rasimu ya katiba mpya.

Busega: Baraza la wazi la katiba leo litaanza saa 3 asubuhi.

Maswa: Wanachana na wapenzi hudhurieni baraza la wazi la katiba kuanzia saa 5 kamili

Meatu: mtaanza baraza la wazi la katiba saa 7 mchana. Wanachama na waalikwa mkifika anzeni kutoa maoni yenu juu ya rasimu; tuko pamoja!

Bariadi: ni haki na wajibu kushiriki baraza la wazi la katiba leo tarehe 13 Agosti kuanzia saa 9 alasiri.

Shime tushiriki kikamilifu na kuitumia fursa hii kwa maslahi ya taifa letu.

Thursday, August 8, 2013

Salamu za Eid-Al-Fitr na kutembelea kata ya Malamba Mawili!

Saa 5 mpaka 8 mchana nitakuwa pamoja na viongozi wenzangu Malamba Mawili (Eneo la Stendi Mwisho). Tutagawa zawadi kwa watoto pamoja na kutoa salamu za Eid-Al-Fitr. Tutasambaza nakala za rasimu ya katiba mpya vijiweni na kwa wawakilishi wa makundi ya kijamii yenye malengo yanayofanana.

Tunaanza muda huo ili kuheshimu wajib wa salaat ya Eid na sunnah ya khutbah asubuhi. Imekuwa ni kawaida kwa siku ya Eid kuwa pia ni wasaa kwa kusikiliza hotuba juu ya wajibu kwa Allah lakini pia kwa binadamu wengine. Ni wakati wa ummah kukumbushwa masuala muhimu katika jamii. Tunamaliza mapema kutoa fursa ya mikusanyiko mingine.

Nitazungumza na umma kuhusu mchakato wa katiba na kutoa pia mrejesho juu ya masuala ya maendeleo ikiwemo juu ya ujenzi/matengenezo ya Barabara ya Kinyerezi-Malamba Mawili Mbezi, kuhusu maji na juu ya masuala mengine muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Kwa wakazi wa maeneo jirani yanayozunguka Malamba Mawili ya Kifuru, King’azi, Msingwa, Msigani na mengineyo mnaweza kuja kujumuika nasi. 

Kwa maelezo zaidi na maelekezo naomba muwasiliane na Ali Makwilo 0715/0784691449.

Eid Mubarak!

Kwa mkazi wa Kisopwa, Sinza, Manzese, Mbezi Makabe, Malambamawili, Mshikamano au Msigani; naomba usome hapa na kunipa mrejesho juu ya ardhi na mipango miji

Tarehe 12 Julai 2012 katika mchango wangu bungeni ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kuwawakilisha wananchi na kuisimamia Serikali niliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na mambo mengine:

Itatue mgogoro kati ya Manispaa ya Kinondoni na Halmashauri ya Kisarawe kuhusu wananchi wa Kisopwa na Mloganzila kuitwa kwamba wako Kisarawe badala ya Kinondoni.

Ichukue hatua juu ya maeneo ya wazi/umma yaliyovamiwa katika kata ya Sinza ambapo mabango yamewekwa, muda wa notisi umeisha lakini majengo bado yapo.

Imtaje wazi mwendelezaji mwenza wa Mji wa kiungani (satellite town) wa Luguruni, masharti ya mkataba na lini uendelezaji unaanza.

Itoe nakala ya mipango ya uendelezaji upya kata ya Manzese.

Iharakishe mipango ya uhakiki na urasimamishaji katika maeneo ya Mbezi Makabe, Malamba Mawili, Mshikamano na Msigani.

Mwaka mmoja umepita, kuna mambo nimepewa na majibu na kazi imefanyika na kuna masuala bado.

Mkazi wa Mabibo na maeneo jirani nakutaarifu kuwa nitahutubia mkutano wa hadhara kwenye eneo la Sahara leo siku ya 8/8 kuanzia saa 9 alasiri mpaka 11 jioni ulioandaliwa na chama. Njoo na waalike na wengine.

Mkutano huo una malengo matatu: Mosi; kuwasilisha mrejesho wa kazi jimboni za utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyogharamiwa na Mfuko wa Jimbo katika maeneo yenu.

Pili; nitafanya kazi ya kuuchambua mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea ikiwemo kuhusu rasimu ya katiba mpya.

Tatu; kupokea maoni/mapendekezo ya masuala muhimu ya kuyazingatia katika kazi ya kuwawakilisha wananchi kwenye vikao vya kamati za Bunge vinavyoanza wiki ijayo na Mkutano wa Bunge unaoanza mwishoni mwa mwezi huu.

Itakumbukwa kwamba tarehe 21 Julai 2013 nilitaka kutimiza azma hiyo kwenye eneo tajwa lakini Jeshi la Polisi lilizuia mkutano kwa maelezo yasiyokuwa ya kweli kwamba kulikuwa na ziara ya Makamu wa Rais katika Jimbo la Ubungo.

(Msaidizi katika Ofisi yangu ameeleza hapa kwa kirefu: http://www.youtube.com/watch?v=VyHF5O-P-Vk&feature=c4-overview&list=UUs0TcFkgqs2OYd6x5E68nhg ).

Nitashiriki kwenye Iftar nyumbani kwa Marehemu Mbwana Masoud Makurumla leo 8/8 jioni; wasiliana na Aziz (OMU) 0784/0715-379542 kutuunga mkono kwa hali na mali. Ramadan Kareem.

Kwa ndugu zangu na wenzetu waislamu, ni siku ya 30 ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan. Siku ya 30 ni kati ya siku kumi za mwisho za mfungo ambazo wapo wanaomini kwamba usiku ni siku ya “usiku wa nguvu”. Siku na usiku ambao Mtume Muhammad (SAS) alipokea ufunuo wa kwanza wa Q’uran yaani Laylat al-Qadr.

Katika siku hii ya 30 nitaungana pamoja na familia ya Marehemu Mbwana Masoud, majirani zake wakazi wa Kata ya Makurumla na wengine mtakaojumuika nami katika Iftar nyumbani kwa familia ya marehemu . Jioni tutaanza na tende na futari itafuata baada ya swala ya maghrib.

Marehemu Mbwana Masoud alikuwa ni mmoja wa wanachama wa CHADEMA walijitolea kusafiri kwenda Igunga kwa ajili ya kuwa wakala kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 2 Oktoba 2011.