Wednesday, March 26, 2014

Mnyika: Dawasco toeni taarifa mtambo wa Ruvu

26/03/2014 | Posted by Shehe Semtawa

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, ameitaka Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco), kutoa taarifa kwa umma kuhusu kuchelewa kukamilika matengenezo ya mtambo wa Ruvu Juu, kunakosababisha upungufu wa maji katika maeneo ya jiji hilo.

Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima Jumatano jana, Mnyika alisema baada ya kutokea tatizo hilo aliwasiliana na Dawasco ili kujua hatua walizochukua.

Alisema maelezo waliyompatia ni kuanza kwa matengenezo, hivyo hatua ya kuchelewa kukamilika kwa matengenezo hayo ilipaswa Dawasco kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari, matangazo ikiwemo tovuti yake.

Monday, March 24, 2014

Kuhusu Kituo Kipya cha Daladala Ubungo, Uendelezaji wa Kiwanja na. 2005/2/2 Sinza (Former Simu 2000) na fursa kwa Wafanyabiashara Ndogo Ndogo

Leo 25 Machi 2014 Ofisi ya Mbunge wa Jimbo Ubungo itafanya kazi ya kufuatilia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Kinondoni na Kamati ya Wafanyabiashara ndogo ndogo kuhusu utekelezaji wa mapendekezo niliyotoa tulipofanya ziara ya kikazi katika Stendi mpya ya Daladala ya Ubungo tarehe 6 Januari 2014.

Aidha, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo itatumia nafasi hiyo kufuatilia kwa mamlaka mbalimbali juu ya masuala ambayo mbunge aliyahoji jimboni na bungeni kuhusu wafanyabiashara ndogo ndogo na wazalishaji wadogo ambayo yako katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Ikumbukwe kwamba tarehe 6 Januari 2014 nilipofanya ziara ya kikazi ya kufuatilia ujenzi wa Kituo kipya cha daladala katika Kiwanja na. 2005/2/2 Kitalu C Sinza eneo ambalo zamani lilikuwa chini ya “Simu 2000” uendelezaji ulikuwa umefanyika katika ekari nne.

Saturday, March 8, 2014

Ujumbe wangu kwenu siku ya Wanawake: Dhima ni mabadiliko kutimiza dira ya usawa kwa maendeleo ya wote

Tarehe 8 Machi ni Siku ya Wanawake Duniani (IWD). Ujumbe wa siku hii kwa mwaka huu wa 2014 kwa mujibu wa internationalwomenday.com ni “inspiring change” (kuhamasisha mabadaliko). Wakati kwa mujibu wa unwomen.org ni “equality for women is progress for all” (usawa kwa wanawake ni maendeleo kwa wote”.

Mchango wa wanawake katika taifa letu unapaswa kuheshimiwa na kila mtu; wanawake ni wazazi, walezi na ni wengi katika jamii yetu. Hata hivyo, ni kundi linalokabiliwa na changamoto nyingi ambazo ni muhimu kuunganisha nguvu za pamoja katika kuzikabili.

Katika kuadhimisha siku hii ofisi ya mbunge jimbo la Ubungo inafanya kazi nne mahususi zenye kuhamasisha mabadiliko na maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla.

Mosi; kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano Ofisi ya Mbunge inapokea mapendekezo toka kwa wanawake na wadau wa masuala ya jinsia ya kuboresha rasimu ya katiba kwenye ibara zenye kasoro. Mkazo haupaswi kuwa kwenye uwiano wa kijinsia na haki za wanawake za ushiriki kwenye chaguzi na uongozi wa kisiasa pekee au kupata ujira sawa kama ilivyo sasa katika rasimu ibara ya 47, bali kuwezesha ushiriki wa wanawake katika uchumi, kumiliki mali na maendeleo kwa upana wake.

Thursday, March 6, 2014

Taarifa kwa Umma: “Kuendelea kwa ‘Kashfa ya IPTL’ mpaka hivi sasa ni matokeo ya udhaifu wa Rais Kikwete, uzembe wa uongozi wa Bunge, ufisadi wa baadhi ya viongozi wa CCM na uongo wa Waziri Muhongo”.

Kwa nyakati mbalimbali kati ya tarehe 27 Februari 2014 na tarehe 5 Machi 2014 vyombo mbalimbali vya habari vimeandika habari na kuchapisha matangazo juu ya TANESCO na IPTL.

Umma uzingatie kwamba ‘kashfa ya IPTL’ ni ya miaka mingi katika taifa letu na inaendelea mpaka hivi sasa kutokana na udhaifu, uzembe, ufisadi na uongo unaotawala. 

Kumbukumbu zangu zinanionyesha kwamba wakati wa kuanzishwa kwake IPTL ilikuwa ni ubia wa kampuni mbili; Mechmar Corporation ya Malysia Bhd na VIPEM ya Tanzania. 

Udhaifu wa Rais unaendeleza ‘kashfa ya IPTL’:

Mwaka 1994 IPTL ilikutana na aliyekuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini wakati huo Jakaya Kikwete na aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO wakati huo Simon Mhaville.