Wednesday, December 29, 2010

Taarifa ya Hoja Binafsi Juu ya Mchakato wa Katiba Mpya


Nikikabidhi taarifa ya hoja binafsi ya kudai Katiba Mpya kwa Kaimu Katibu wa Bunge, Bw. Eliakim Mrema.

Hoja ya katiba mpya kuwasilishwa bungeni

Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika, leo anatarajia kuwasilisha rasmi kwa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano taarifa ya Hoja Binafsi kuhusu mchakato wa Katiba Mpya.

" Nachukua fursa hii kutoa taarifa kwamba Jumatatu (leo) nitakwenda kuwasilisha kwa Katibu wa Bunge taarifa ya Hoja Binafsi kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya," alisema katika taarifa yake.

Desemba 19, mwaka huu, Mnyika alikutana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kudokeza kusudio lake la kuwasilisha hoja hiyo katika mkutano wa pili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakaoanza Februari mwakani. Vilevile aliahidi kwamba atawasilisha taarifa ya hoja hiyo wiki moja baada ya kukutana na waandishi wa habari.

" Taarifa hiyo nitaiwasilisha kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge kifungu cha 55 (1) kwa ajili ya Bunge kupitisha maazimio ya kuweka utaratibu wa kiusimamizi na wa kisheria wa kuratibu mchakato mzima wa kuandikwa kwa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," alisema Mnyika katika taarifa yake hiyo jana.

Hata hivyo, alisema tangu aeleze kusudio lake, baadhi ya watu wamekuwa wakiipotosha hoja yake kupitia vyombo vya habari.

Alisema ieleweke kwamba yeye kama Mbunge, anapokwenda kuwasilisha hoja hiyo kuhusu katiba mpya anafanya hivyo kama sehemu ya kutimiza wajibu wa kuwawakilisha wananchi na kulinda ukuu wa katiba katika taifa.

" Izingatiwe kwamba ibara ya 8 (1) imeeleza bayana kwamba mamlaka na madaraka ni ya wananchi na kwamba ibara ya 63 (2) (3) imeeleza kwamba Bunge ndicho chombo kikuu chenye madaraka kwa niaba ya wananchi kuisimamia na kuishauri serikali kupitia kupitisha mipango, kutunga sheria nk. Ibara ya 98 (1) imekwenda mbali zaidi kwa kutoa mamlaka kwa bunge kutunga sheria kwa ajili ya kufanya mabadiliko ya kikatiba," alisema na kuongeza kuwa:

" Hivyo, hoja binafsi ninayokwenda kuiwasilisha ni kwa ajili ya Bunge kwenda kutimiza wajibu huu wa kikatiba ambao wabunge wote tumeapa kuulinda na kuutetea, kufanya hivyo hakuwezi kuwa tendo la ’unafiki’," alisisitiza.

Mnyika ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, alisema pamekuwepo pia na upotoshoji unaoeleza kuwa anakusudia kwenda kuwasilisha rasimu ya katiba mpya bungeni kupitia hoja binafsi.

" Izingatiwe kwamba siendi kuwasilisha rasimu ya katiba mpya, kwa kuwa sio jukumu la mtu mmoja, au chama kimoja, au taasisi moja, au dini moja kuandaa katiba; ni jukumu la Watanzania,” alisema.

Mnyika alifafanua kuwa anachokwenda kuwasilisha bungeni ni hoja binafsi kwa ajili ya Bunge kuazimia kuweka utaratibu utakaoanzisha, kusimamia na kuwezesha Serikali kuratibu mchakato wa katiba mpya utaohakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu kuandika katiba kupitia tume inayohusisha wadau, elimu kwa umma, mkutano mkuu wa taifa wa katiba, kura ya maoni (referundum) na kadhalika.

Alisema mtu binafsi, taasisi, chama au dini kinaweza kuwa na maoni yake kuhusu katiba ambayo kinaweza kuyatoa kwa njia ya taarifa au hata kuandaa rasimu sifuri, lakini hatimaye lazima kuwe na mfumo wa pamoja ili kuwe na makubaliano ya kitaifa kwa kuwa katiba sio mali ya chama chochote, dini yoyote au mtu yeyote, bali ni sheria mama na mkataba kati ya wananchi na Serikali.

Alisema suala la Bunge kuweka maazimio na utaratibu ikiwemo kutunga sheria ya kuratibu mchakato wa mabadiliko ya katiba ni la muhimu na la haraka wakati huu ambao tmakundi mbalimbali ya kijamii yamejitokeza na kuweka misimamo yao wazi ya kutaka katiba mpya na mengine kutangaza kuanza kuandika miswada ama rasimu ya katiba husika.

Alisema kusipokuwa na utaratibu wa haraka wa pamoja, kila mdau atakwenda kwa mfumo wake hali ambayo inaweza kuzalisha mpasuko katika jamii kutokana na suala la katiba mpya.

" Sio jambo baya makundi ya kijamii kuandaa rasimu sifuri za katiba, lakini kama kila kundi likaandaa rasimu yake halafu utaratibu wa kuunganisha maoni ya makundi mbalimbali kupitia chombo kinachokubalika na kinachohusisha wadau wote kuchelewa taifa linaweza kuingia kwenye malumbano, ndio maana ni muhimu kwa utaratibu huo kuwekwa kupitia mkutano wa bunge wa Februari," alisema. Alisema hoja binafsi anayokwenda kuiwasilisha bungeni haihusu maadhui ya katiba bali inahusu mchakato, ingawaje katika kuiwasilisha kuna masuala ya kimaudhui yatajitokeza kama sehemu ya kujenga hoja.

Alisema kama mwakilishi wa Chadema kwenye Kongamano la Madai ya Katiba Mpya, anatumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi na wadau kuendelea kutoa maoni kuhusu rasimu sifuri ya katiba iliyopitishwa na Kongamano la Wadau tarehe 17 Februari mwaka 2007 baada ya kuwasilishwa na Kamati ya Wataalamu iliyoongozwa na Dk. Sengondo Mvungi. Alisema katika kongamano hilo pamoja na kueleza ubora wa rasimu hiyo sifuri ikilinganishwa na katiba inayotumika kwa sasa wajumbe walieleza kasoro zilizopo kwenye rasimu sifuri ambazo zinahitaji kufanyiwa marekebisho kabla ya rasimu husika kukabidhiwa katika vyombo vya maamuzi hivyo kongamano likaazimia kwamba rasimu husika isambazwe na kila mshiriki kwa wadau kwa ajili ya kupata maoni.

Katika muktadha huo kongamano liliazimia kuipokea na kujadili rasimu ya sifuri kama mkusanyiko wa mawazo ya awali yaliyotoka kwa wadau kwa ajili ya kuchochea mjadala na fikra za umma kuhusu mchakato wa Katiba mpya.

"Maoni yaliyopokewa na Chadema kama mdau katika kipindi cha 2007 mpaka 2010 kwa ujumla yanaeleza kwamba rasimu sifuri iliyotolewa ina ubora zaidi ya katiba inayotumiwa sasa na Tanzania hasa katika maeneo ya: Muundo wa shirikisho; kuwatambua Watanzania; kutambua mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu, kuwepo kwa maadili/tunu na misingi mikuu ya taifa, haki za binadamu nyingine zimeongezwa na zile zilizokuwemo awali zimepewa tafsiri pana, kupewa uzito wa ulindwaji, madaraka ya rais yamepunguzwa, mawaziri wanateuliwa nje ya wabunge, wabunge kuwepo wa majimbo, wa uwiano na wabunge wa taifa kutoka katika wagombea urais waliofanya vizuri; tume ya uchaguzi imeundwa na watu huru na kuwekewa uwakilishi mpana zaidi; uwakilishi katika kutunga katiba umepanuliwa kujumuisha wadau wa kisekta. Suala ni namna na hatua za kufanya ili serikali ikubaliane na matakwa ya umma kuhusu katiba mpya," ileleza taarifa hiyo.

Chanzo: Nipashe 27/12/2010

Mnyika awasilisha taarifa ya hoja binafsi kuhusu katiba mpya

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, leo anawasilisha taarifa ya hoja binafsi kuhusu mchakato wa Katiba Mpya kwa Katibu wa Bunge.

Mnyika alisema jana kuwa atawasilisha hoja hiyo kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge kifungu cha 55 (1) kwa ajili ya Bunge kupitisha maazimio ya kuweka utaratibu wa kiusimamizi na wa kisheria wa kuratibu mchakato mzima wa kuandikwa kwa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Nichukue fursa hii kufafanua kuhusu upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya watu kupitia baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya kueleza kusudio langu la kuwasilisha hoja binafsi kuhusu Katiba mpya. Mimi kama mbunge ninapokwenda kuwasilisha hoja binafsi kuhusu Katiba mpya nafanya hivyo kama sehemu ya kutimiza wajibu wa kuwawakilisha wananchi na kulinda ukuu wa Katiba katika taifa letu.

“Hoja binafsi ninayokwenda kuiwasilisha ni kwa ajili ya Bunge kwenda kutimiza wajibu huu wa Kikatiba ambao wabunge wote tumeapa kuulinda na kuutetea; kufanya hivyo hakuwezi kuwa tendo la ’unafiki’ moja ya gazeti lilivyoeleza (sio Tanzania Daima),” alisema.

Alieleza kuwa kumewakuwapo na upotoshoji unaoeleza kuwa anakusudia kwenda kuwasilisha rasimu ya Katiba mpya bungeni kupitia hoja binafsi na kueleza kuwa hilo si jukumu la mtu mmoja, chama, taasisi au dini bali ni jukumu la Watanzania wote.

Mnyika alieleza kuwa anachowasilisha ni hoja binafsi kwa ajili ya Bunge kuazimia kuweka utaratibu utakaoanzisha, kusimamia na kuwezesha serikali kuratibu mchakato wa Katiba mpya utakaohakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu kuandika Katiba kupitia tume inayohusisha wadau, elimu kwa umma, mkutano mkuu wa taifa wa Katiba na kura ya maoni.

“Mtu binafsi, taasisi, chama au dini kila kimoja kinaweza kuwa na maoni yake kuhusu Katiba ambayo kinaweza kuyatoa kwa njia ya taarifa au hata kuandaa rasimu sifuri, lakini hatimaye lazima tuwe na mfumo wa pamoja ili kuweza kuwa na makubaliano ya kitaifa kwa kuwa Katiba sio mali ya chama chochote, dini yoyote au mtu yeyote bali ni sheria mama na mkataba kati ya wananchi na serikali,” alisema.

Alieleza kuwa suala la Bunge kuweka maazimio na utaratibu ikiwemo kutunga sheria ya kuratibu mchakato wa mabadiliko ya Katiba ni la muhimu na la haraka wakati huu ambapo tayari makundi mbalimbali ya kijamii yamejitokeza na kuweka misimamo yao wazi ya kutaka Katiba mpya na mengine kutangaza kuanza kuandika miswada ama rasimu ya Katiba husika.

Aidha, mbunge huyo alionya kutokuwapo na utaratibu wa haraka na wa pamoja kila mdau atakwenda kwa mfumo wake, kunaweza kuzalisha mpasuko katika jamii kutokana na suala la Katiba mpya.

“Sio jambo baya makundi ya kijamii kuandaa rasimu sifuri za Katiba, lakini kama kila kundi likaandaa rasimu yake halafu utaratibu wa kuunganisha maoni ya makundi mbalimbali kupitia chombo kinachokubalika na kinachohusisha wadau wote kuchelewa, taifa linaweza kuingia kwenye malumbano; ndio maana ni muhimu kwa utaratibu huo kuwekwa kupitia mkutano wa Bunge wa Februari,” alisema.

Wakati huohuo, mbunge huyo aliwataka wananchi na wadau mbalimbali kuendelea kutoa maoni kuhusu rasimu sifuri ya katiba iliyopitishwa na Kongamano la wadau Februari 17 mwaka 2007, baada ya kuwasilishwa na Kamati ya Wataalamu iliyoongozwa na Dk. Sengondo Mvungi.

Katika kongamano hilo pamoja na kueleza ubora wa rasimu hiyo sifuri ukilinganisha na Katiba inayotumika hivi sasa wajumbe walieleza kasoro zilizopo kwenye rasimu sifuri ambazo zinahitaji kufanyiwa marekebisho kabla ya rasimu husika kukabidhiwa katika vyombo vya maamuzi.

“Hivyo, tunakaribisha maoni ya umma kuhusu rasimu husika inayopatikana kwenye tovuti www.chadema.or.tz, maoni yatumwe kupitia info@chadema.or.tz au yatumwe moja kwa moja kwa kamati ya madai ya Katiba mpya,” alieleza mbunge huyo.

Muda mrefu sasa, kumekuwa na vuguvugu la madai ya kuwepo kwa Katiba mpya kutoka kwa taasisi mbalimbali, viongozi wa dini na wanasiasa. Joto hilo liliongezeka baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilipoamua kuvalia njuga madai ya Katiba mpya.

Kilio hicho cha CHADEMA kimekuwa kikipata watu wanaoikiunga mkono wakiwamo wanasiasa mashuhuri nchini, viongozi wa dini, asasi zisizo za kiserikali na wananchi wa kawaida.


Chanzo: Tanzania Daima 27/12/2010

Mnyika awaanzia yatima mfuko wa elimu

Mbunge wa Jimbo la Ubungo,(Chadema), John Mnyika ameanzisha mfuko wa elimu utakao wasaidia watoto yatima katika jimbo la Ubungo na ameahidi kuweka asilimia 20 ya mshahara wake kwenye mfuko huo.

Alisema hayo jana jijini Dar es salaam alipo kuwa anatoa msaada wa shilingi 100,000 akishirikiana na Ubungo Development Initiative (UDI) waliotoa vifaa vya shule na chakula katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Boona-Baana Center for children kilichopo Sinza Mori jijini.

"Watu wengi wanafikiri kuwa mahitaji makubwa ya watoto yatima kuwa ni mavazi,chakula,makazi na kuwatembelea wakati wa sikukuu ila mimi naona sisahihi kabisa, elimu ni kitu cha muhimu sana kwani itawasaidia baadae,"alisema Mnyika.

Mnyika alimpongeza mratibu wa kituo hicho, Marco Barra kwa kuweza kuwasomesha watoto hao ili waweze kujikomboa kimaisha.

Alitoa wito kwa Watanzania kuwasaidia watoto yatima ili waweze kupata elimu itakayo wasaidia kujikomboa kimaisha.

Chanzo: Nipashe 27/12/2010

Mnyika awaasa maafisa ustawi wa jamii

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika, amewataka maofisa ustawi wa jamii nchini kuepuka tabia ya kukaa ofisini huku wakiwaacha watoto wa mitaani wakihangaika bila ya kuwa na msaada wowote.

Amewataka maofisa hao kuvitembelea vituo vya watoto yatima ili kubaini maendeleo na mwenendo wa wake baada ya malalamiko mengi kutolewa juu ya vituo hivyo, kuwa vingi vinaendeshwa kwa ajili ya maslahi ya wanaosimamia au kumiliki vituo hivyo.

Mnyika alitoa kauli hiyo jana wakati wa chakula cha mchana alichokiandaa na watoto wa Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha ‘Boona Baana’ kilichopo Sinza Mori, Dar es Salaam.

Alisema hivi karibuni, Taifa limekuwa na idadi kubwa ya watoto yatima na wale wa mitaani, jambo linalohitaji ustawi mkubwa wa kuhakikisha wanapata elimu, malazi na huduma zingine, na kusisitiza kwamba hilo halitaweza kufanikiwa endapo maofisa hao wataendelea kujifungia ofisini.

“Idara ya Ustawi wa Jamii ndiyo yenye jukumu kubwa la kuwashughulikia watoto hawa wanaoishi katika mazingira magumu, kamwe tatizo hilo halitaweza kuisha endapo maafisa hawa wataendelea kulifumbia macho hilo kwa kukaa maofisini,” alisisitiza Mnyika.

Aidha, alisema hivi sasa kuna idadi kubwa ya vituo vya kulelea watoto yatima katika maeneo mbalimbali, hivyo maofisa hao wa ustawi wa jamii wanatakiwa wavichunguze vituo hivyo ili kubaini namna vinavyoendeshwa kwani yapo madai kuwa baadhi yao vinaendeshwa kwa maslahi ya waliovianzisha.

Katika chakula hicho, Mnyika alitoa msaada wa vifaa vya shule pamoja na vyakula vyote vikiwa na thamani ya Sh 500,000 kwa ajili ya watoto hao wanaoishi katika kituo hicho wapatao 10.

Mratibu wa kituo hicho, Marco Bara, aliwaomba wananchi kuacha tabia ya kuwachukulia watoto wa mitaani kama wakaidi na badala yake wasaidiane kuwaondoa katika maisha magumu yanayowakabili.

Chanzo: Habari Leo 27/12/2010

Mnyika: Katiba ina mapungufu 90

HATIMAYE Mbunge wa jimbo la Ubungo jijini Dar e Salaam, John Mnyika (CHADEMA), amewasilisha taarifa ya hoja binafsi ya Katiba kwa Katibu wa Bunge na kueleza mapungufu 90 yaliyo katika Katiba ya sasa. Akiwasilisha hoja hiyo jana na kupokewa na Kaimu Katibu na Mkurugenzi wa Idara ya Taarifa za Bunge, Eliakim Mrema, kwa barua yenye kumbukumbu namba BJMT/01/2010 ambapo Mrema aliahidi kuifanyia kazi barua hiyo kwa mujibu wa kanuni za Bunge ya Mwaka 2007.

Akizungumza mara baada ya kuwasilisha taarifa hiyo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisi ya kambi ya upinzani, Mnyika alisema Katiba ya sasa haikidhi mahitaji ya Watanzania kwa kuwa ilitungwa katika mfumo wa chama kimoja.
“Nichukue fursa hii kueleza kwamba Katiba ya sasa inampa mamlaka makubwa mno Rais, pamoja na vyombo vya kiutendaji; hakuna Mtanzania mwenye uwezo wa kuhoji hasa katika mfuno huu wa vyama vingi na Katiba hii imekuwa na matundu mengi ambayo yanakibeba chama kimoja waziwazi. Hakika mchakato huu ni wa Watanzania wote!” alisema Mnyika.

Alisema taarifa ya hoja binafsi aliyoiwasilisha ni kwa ya ajili ya Bunge kwenda kutimiza wajibu wa Kikatiba ambapo wabunge wana wajibu wa kuilinda kwa kutambua uwakilishi wao kwa wananchi waliowapa dhamana ya uwakilishi katika chombo hicho cha maamuzi.

Alisema hivi sasa taasisi za utendaji kama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na Tume ya Maadili ya viongozi wa umma uteuzi wa watendaji wake uko chini ya Rais hivyo kushindwa kutoa mwanya wa kuhoji.

Alisema Katiba ni muhimu na ya haraka wakati huu ambapo tayari makundi mbalimbali ya kijamii yamejitokeza na kuweka misimamo yao wazi ya kutaka Katiba mpya na mengine kutangaza kuanza kuandika miswada ama rasimu ya Katiba husika


Chanzo: Tanzania Daima-28/12/2010

MP to seek people’s views on law review

Dar es Salaam. Ubungo MP John Mnyika (Chadema) intends to make public his draft of a private motion on the country’s Constitution for people to provide views on its improvement.
He expressed his intention yesterday when he submitted a letter of information to the office of the Clerk of the National Assembly on his plan to table a private motion in the next Parliamentary session to be held in February.
The letter with reference number OMU/BJMT/01/2010 was received by the acting Clerk of the Assembly, Mr Eliakim Mrema. “As an institution we have received the letter and normal procedures will be followed,” said Mr Mrema.

Regulation number 55 (1) of parliament requires an MP to inform the Clerk on plans to table a private motion at least a day before the start of the meeting.
But, Mr Mnyika said he decided to forward the letter one month before the parliamentary session to give room for public debate on the motion to be tabled.

After formally informing the Clerk as required by Parliamentary regulations, Mr Mnyika said during the first week of January the draft would be published in the media and its hard copy made available in his office.
“I need people to contribute their views on how they would want the motion to be because this is a public matter through a private motion,” he said.
He explained that the forum would give the public an opportunity to point out shortcomings in the current Constitution and why they think there is a need for a new Constitution.
He said the public could send their opinions physically to his office or forward them to his email address: mbungeubungo@gmail.com or through phone number 0783552010. In addition, in the second week of January Mr Mnyika intends to hold an open forum for stakeholders to brainstorm on the draft of the motion.

So far, Mr Mnyika said, he had identified about 90 shortcomings in the current constitution.
“Imagine, out of 152 Sections of the current Constitution, I have discovered 90 shortcomings, but I need people also to express their concerns,” he pointed out.
Following the existence of numerous weaknesses in the current constitution, Mr Mnyika said, the country would not want the amendment but a new document altogether.
Explaining some of the deficiencies, he said the current constitution gives the President excessive power of appointment without authorization.

“For a democratic nation like ours, the president should not perform such powers,” he argued.
He also said the current constitution denies independence to government institutions as their top officials are appointed by the President. Among them are members of the Judiciary, National Electoral Commission as well as the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB).
On the other hand, he continued, the change in the Zanzibar Constitution forces a review and rewriting of the Union Constitution.

His move of forwarding the private motion follows several concerns from his constituents who asked him to push for the matter.
It was also triggered by the recent pronouncement by Prime Minister Mizengo Pinda that he would advise President Jakaya Kikwete to form a team to consider demands for the new constitution

Source: The Citizen-27/12/2010

Thursday, December 23, 2010

Mnyika kusaidia shule Goba kupata umeme

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) ameahidi kuisadia shule ya mchepuo wa Kingereza ya Kings iliyoko Kata ya Goba wilayani Kinondoni, Dar es Salaam kutatua kero ya umeme inayoikabili.Mnyika alitoa ahadi hiyo mwishoni mwa wiki kwenye mahafali shuleni hapo na kuongeza kuwa pamoja na shule hiyo kujiwekea nishati ya umeme inayotumia nguvu za jua kama msingi wa maendeleo bado nishati hiyo haitoshi kutokana na ukweli kwamba nguvu yake ni ndogo katika matumizi.

“Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia tunatakiwa kutumia mitandao mbalimbali ikiwamo kompyuta, intaneti na printa sasa umeme huu wa jua hauwezi kufanya yote hayo; kikubwa katika umeme huu ni kuwasha taa tu,” alisema Mnyika.

Aidha, aliwataka wakazi wa eneo hilo wajiorodheshe kwa lengo la kujua idadi yao kisha atalifuatilia kwa kukutana uongozi wa Shirika la umeme nchini (TANESCO), kuwafahamisha kuwa kuna jamii kubwa inahitaji huduma hiyo.

Katika hatua nyingine Mnyika alishiriki katika kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike na wa kiume wa shule hiyo.

“Kwa hili la ujenzi wa bweni nawapongeza sana, kwani litakapokamilika litasaidia kupunguza uchelewaji wa wanafunzi kufika shuleni pia litawafanya wanafunzi kuwa karibu na mazingira ya shule,” alisema Mnyika.

Chanzo: Mwananchi

Mnyika vows to end Ubungo water woes

Ubungo constituency Member of Parliament John Mnyika announced yesterday he plans to form a special committee which will formulate and oversee implementation of appropriate strategies for ending chronic problems of water in the area.

Addressing his first public rally after being elected as the constituency MP in the 2010 general elections, Mnyika said yesterday that water was one of his top agendas in his “long-journey” to solve people’s problems.

He said that the committee would comprise people from Dar es Salaam Water and Sewerage Corporation (Dawasco), ministry of water and irrigation, and academicians.

“I know there are many problems facing this area, but water is a critical problem. That is why I have decided to form a special committee which will come with suggestions on how to solve this problem,” said Mnyika.

He said his office was currently collecting views of people on problems facing Ubungo constituency, and would later on present them to the government through parliamentary sessions.

According to the Ubungo MP, about 5m/- has been allocated by Kinondoni Municipal authority for construction of a police post at Kimara Msewe in a bid to control the rising wave of crimes in the area.

Mnyika mentioned other problems facing residents of Ubungo constituency as lack of a market, poor road infrastructures, increasing crime and environmental pollution.

Source: Guardian (13 December 2010)

Serikali itoe tamko vurugu Arusha

KATIBU wa Kambi ya Upinzani Bungeni,John Mnyika amelitaka Jeshi la Polisi, Waziri Mkuu, Ofisi ya Bunge na chama tawala cha CCM kutoa tamko kuhusu kitendo cha kupigwa kwa mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.
Lema alipigwa vibaya na askari wa Jeshi la Polisi wakati alipokwenda kwenye mkutano wa madiwani kupinga uchaguzi wa meya wa Jiji la Arusha, akidai kuwa mkutano huo wa uchaguzi uliitishwa kinyemela kwa kushirikisha madiwani wa CCM na TLP tu.

Katika mkutano huo wa uchaguzi, diwani wa CCM wa Kata ya Olorien, Gaudence Lyimo alichaguliwa kuwa meya na nafasi ya naibu meya kwenda kwa diwani wa Kata ya Sokoni (TLP), Michael Kivuyo.
Mnyika, ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, alisema ameshangazwa na tukio hilo kwa kuwa polisi wameamua kuwapiga wananchi ambao hawakufanya fujo wala kuwa na silaha ya aina yoyote.

“Tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema kutoa tamko kali dhidi ya askari polisi waliohusika kupiga wananchi, akiwemo mbunge wa Chadema,” alisema Mnyika.

“Picha zipo wazi na askari waliohusika katika tukio hili na wanaonekana wazi, kwa hiyo IGP pia achukue hatua kali kwa askari waliohusika. Hakuna sheria inayomtaka polisi kupiga raia ambao hawakufanya fujo wala kuwa na silaha za aina yoyote.”
Alisema pia anamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutoa tamko la kulaani kitendo hicho kwa kuwa limetokea katika uchaguzi wa Umeya ambao kimsingi upo chini ya Wizara ya Tamisemi.

“Ili uingie bungeni kama si mbunge kuna kanuni na taratibu zake, sasa iweje leo polisi waingie katika mkutano wa baraza la madiwani tena wakiwa na silaha,” alihoji Mnyika.

Mnyika alifika mbali na kusema kuwa pia Ofisi za Bunge zinatakiwa kulitolea tamko tukio hilo kwa kuwa linamhusu mbunge ambaye alikuwa akitekeleza majukumu yake na kwamba kitendo cha kupigwa ni sawa na kuingilia maslahi ya mbunge.
“Chadema nao wanatakiwa kulitolea tamko tukio hili, nasema hivi kwa kuwa Chadema iliwahi kusema kuwa vyombo vya dola ndio vitakavyosababisha umwagaji damu na jambo hilo limedhihirika wazi,” alisema Mnyika.
“Hata CCM nao wanatakiwa kusema kitu kuhusiana na suala hili kwa kuwa ulikuwa uchaguzi unaokihusisha chama hicho.”
Lakini imesema itakuwa vigumu kutoa tamko au kulizungumzia suala hilo kwa kuwa lina mwelekeo wa kisheria.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili na kueleza kuwa hata hivyo serikali haina taarifa ya kupigwa kwa mbunge huyo.

“Siwezi kuzungumza lolote kuhusu tukio la kupigwa kwa Mbunge Lema, kwa kuwa bado sijapata taarifa rasmi ya tukio hilo. Nimelisikia kupitia vyombo vya habari,’’ alisema Lukuvi.
Wakati huohuo, hali ya mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema inaendelea vizuri na sasa ameruhusiwa kutoka hospitalini.

Mbunge huyo aliliambia gazeti hili jana kuwa aliruhusiwa kutoka hospitalini juzi saa 1:30 usiku baada ya kuona hali yake inaendelea vizuri.

Lema alisema baada ya kufanyiwa vipimo mbalimbali madaktari hao walibaini kuwa alipatwa mshituko wa shinikizo la damu kutokana na kipigo hicho cha polisi.
“Ni ajabu sana polisi kupiga raia kama mimi hovyo; nimeumia sana na nimedhalilishwa lakini ninajiandaa kuwachukulia hatua kwa kuwa nawajua kwa sura na nitaendelea kupambana kudai haki yangu hadi kieleweke,” alisema mbunge huyo
Diwani wa Kata ya Elerai (Chadema), John Bayo alisema leo wanatarajia kwenda mahakamani kufungua kesi kupinga uchaguzi huo kutokana na baadhi ya kanuni kutofuatwa.

Chanzo: Mwananchi (20 Disemba 2010)

Mnyika awataka polisi kufichua majambazi

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), John Mnyika, amelitaka Jeshi la Polisi kushirikiana na wananchi katika kuwafichua majambazi ambao wamekithiri katika maeneo mengi jiji la Dar es Salaam.
Mnyika alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya vyombo vya habari kuripoti matukio ya ujambazi yaliyokuwa yakifanywa katika eneo la Kimara hivi karibuni ambayo yamezidi kushamiri bila mafanikio; mbunge huyo amelitaka jeshi hilo kuweka nguvu kazi katika maeneo hayo ili kunusuru mali za wananchi pamoja na maisha yao.

Mnyika aliyekuwa katika kikao na wananchi wa kata ya Saranga jana alipokea malalamiko na kero hiyo ambayo imeshindwa kutatuliwa jambo linalohatarisha maisha kutokana na eneo hilo kukumbwa na matukio ya ujambazi kila mara kwa kutokuwa na ulinzi.

Mnyika alimtaka kamanda wa mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, kuchunguza kwa kina sababu za kuwepo kwa ujambazi wa mara kwa mara katika maeneo hayo unaohusisha matumizi ya silaha za moto kwani kumekuwepo na tuhuma za polisi kupokea rushwa kutoka kwa majambazi hao jambo linalosababisha hali hiyo izidi kuendelea.

Mnyika alitumia fursa hiyo kuwapongeza wananchi wa kata ya Kimara kwa kuunga mkono jitihada za kuboresha kituo cha polisi cha Temboni na kujitolea pikipiki mbili, ‘radio call’ na upanuzi wa kituo pamoja na kuendesha harambee kwa ajili ya ujenzi wa choo katika kituo cha polisi ambapo sh 800,000 zilipatikana na ahadi ya mifuko 12 ya saruji ilitolewa.

Wakati huo kamanda polisi wa mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela alitoa wito kwa wananchi kuweka mazingira bora ya ulinzi na usalama kwenye makazi yao ikiwemo kujiandaa na majanga huku polisi wakijitahidi kuweka mikakati ya kuongeza nguvu katika eneo hilo.


Chanzo: Tanzania Daima (Disemba 2010)

Serikali ilaani vurugu Ivory Coast

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka serikali kulaani hadharani matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya demokrasia ya kimataifa unaofanywa na Rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo na wafuasi wake nchini humo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya chama hicho iliyotolewa na Mkurugenzi John Mnyika (Mb) ilisema, Rais Jakaya Kikwete anatakiwa kutamka hadharani kumtambua Alassane Ouattara kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo na kulaani vitendo vinavyofanywa na Gbagbo na wafuasi wake.

“Inashangaza kwamba wakati Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Afrika (AU) na serikali za nchi mbalimbali ndani na nje ya Afrika zimetoa matamko ya wazi serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya diplomasia ya kimya.

“Hii ni tofauti kabisa na wakati Mwalimu Nyerere ambapo Tanzania ilikuwa mstari wa mbele na kutoa misimamo ya wazi ya kukemea vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo ilieleza CHADEMA inatambua kwamba Rais Kikwete alizungumzia kidogo matatizo ya Ivory Coast wakati akihutubia Mkutano wa Kimataifa wa Amani katika eneo la Maziwa Makuu (ICGLR) uliofanyika hivi karibuni nchini Zambia.

Katika mkutano huo Rais Kikwete alieleza kwamba suala la Ivory Coast linashughulikiwa na mikono salama na akaonyesha matumaini yake kwamba pande mbili zenye mgogoro zitafikia makubaliano.

“Kauli hii ya Rais Kikwete inalea vitendo vya ukiukwaji wa misingi ya demokrasia vinavyofanywa na Laurent Gbagbo na wafuasi wake kwa kuwa inatoa fursa kwa mgombea ambaye taasisi zote huru zimetamka kuwa ameshindwa katika uchaguzi kuanza majadiliano na aliyeshinda badala ya kumpisha katika uongozi wa nchi,” ilieleza taarifa hiyo.

Aidha, taarifa hiyo ilisema serikali ya Tanzania inatakiwa kueleza msimamo wake kwa uwazi, ili kuondoa mashaka kwamba ukimya wake unatokana na Rais Kikwete kukosa uhalali wa kimaadili wa kukemea vitendo vya ukiukwaji wa demokrasia na mchakato wa uchaguzi uliomuingiza madarakani kuhojiwa kutokana na tuhuma za matokeo ‘kuchakachuliwa’ katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.


Chanzo: Tanzania Daima (Disemba 2010)

Mnyika acharuka kupigwa Mbunge Lema

KATIBU wa kambi ya upinzani bungeni na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amelaani kitendo kilichofanywa na Jeshi la Polisi mkoani Arusha mjini cha kumpiga Mbunge Godbless Lema na kumtaka Mkuu Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, kuchukua hatua dhidi ya askari hao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mnyika alisema kitendo kilichofanywa na polisi hao hakipaswi kunyamaziwa na inaonyesha wamefanya kazi hiyo kwa maelekezo, hivyo IGP Mwema anapaswa kuchukua hatua za kinidhamu na za kisheria kwa polisi hao.

Alisema taratibu za kiuchaguzi haziruhusu polisi kuingia katika ukumbi wa uchaguzi na bunduki au silaha hivyo ni hatua ya kujiuliza polisi hao walipata baraka za nani za kuingia ndani ya Baraza la Madiwani wakati uchaguzi ukiendelea?

Aidha, Mnyika alisema ni vema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akatoa kauli juu ya suala hilo kutokana na kitendo hicho kutokea kikiwa chini ya ofisi yake ambayo ndiyo wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa (Tamisemi).

“Ni vema Pinda akaliangalia suala hili kwa kwenda mbali zaidi tangu ndani ya ukumbi wa uchaguzi; ni kinyume na taratibu za uchaguzi, ilikuwaje polisi wakaingia na bunduki? Walipata baraka kutoka kwa nani?” alihoji Mnyika.

Alisema pamoja na hilo bado ofisi ya Bunge inawajibika kutoa tamko haraka kwa kitendo kilichofanyika kutokana na kuingilia maslahi ya Bunge na ni kinyume na Katiba.

“Ofisi ya Bunge inapaswa kuchukua hatua zinazostahili; ni taasisi inayostahili kulinda wabunge wake,” alieleza.

Hata hivyo, Mnyika alisema CHADEMA inahitajika kutafakari na kuchukua hatua za kisheria, ili kukomesha vitendo hivyo vinavyoashiria vyombo vya dola kutaka kusababisha umwagaji damu.

“Vyombo vya dola havifanyi kazi bila maelekezo hali inayoonyesha kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinahusika na hivyo inatakiwa itoe kauli ya kulaani na kulichunguza jambo hilo,” alisema.

Akizungumza na Kituo cha Televisheni cha TBC1, Kamanda wa Polisi wa Arusha, Thobias Andengenye, alikanusha polisi kuhusika kumpiga mbunge huyo na kudai kuwa baada ya kuachiwa kwa dhamana Lema alipita maeneo waliyokuwepo wapenzi wa chama chake ndipo alipoanguka.


Chanzo- Tanzania Daima (Disemba 2010)

Monday, December 20, 2010

Mnyika kuwasilisha hoja ya katiba mpya

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika amesema kuwa atawasilisha bungeni hoja binafsi ya kutaka mabadiliko ya katiba na kupinga moja ya mapendekezo ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda la kuunda tume ya kuangalia mchakato huo.

Tangu kumalizika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, Chadema imewasha moto wa mabadiliko ya katiba na kufufua mjadala wa kutaka kuandikwa kwa katiba mpya kiasi cha Waziri Pinda kuamua kutoa tamko mwishoni mwa wiki kuwa atamshauri Rais Jakaya Kikwete aunde tume kuchunguza madai hayo.

Miongoni mwa viongozi waliojiunga kwenye mjadala huo wa kutaka katiba mpya ni mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Sinde Warioba na Frederick Sumaye, Jaji Mkuu Agustino Ramadhan na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa ambaye alitahadharisha kuwa bila ya katiba mpya nchi inaweza kuingia kwenye vurugu.

Akizungumza na Mwananchi jana, Mnyika ambaye ni mmoja wa wabunge vijana kwenye Bunge la Kumi, alisema atatimiza ahadi yake katika kipindi cha wiki moja kwa kuwasilisha taarifa kuhusu hoja binafsi ya katiba mpya kwa katibu wa bunge.
"Ibara ya 8 kifungu kwanza cha katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na mapungufu yake inaeleza wazi umuhimu wa wananchi kushirikishwa katika uundwaji wa katiba. Pia Ibara ya 63-(2) nayo inaeleza wazi," alisema Mnyika.
Aliongeza kuwa kama mbunge ana haki ya kuwasilisha hoja binafsi kuhusu katiba mpya na kwamba ni vyema suala la uundwaji wa katiba likarejeshwa mikononi mwa Bunge kwa kuwa ni mhimili wa dola unaofanya kazi kwa niaba ya wananchi.

"Ibara ya 98 ya katiba ndio sehemu pekee inayozungumzia marekebisho ya katiba hivyo ni wakati muafaka suala hili la katiba likapelekwa bungeni ili wananchi wawakilishwe," alifafanua Mnyika.
Mwanasiasa huyo kinda, ambaye pia ni mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chadema, alieleza sababu za kutaka kupeleka hoja hiyo bungeni ni kutaka chombo hicho lipitishe mchakato wa kuundwa kwa katiba mpya.

"Unajua katiba ni sheria na kwa kuwa bungeni ndiko kunakotungwa sheria basi wanaopaswa kutoa mwelekeo wa katiba mpya ni Bunge," aliongeza.
"Pia katiba ni mkataba kati ya wananchi na watawala... ikumbukwe kuwa anayeandika mkataba ni mwenye mali, na hapa mwenye mali ni mwananchi na Bunge lipo kwa ajili ya wananchi. Kutokana na hilo, ipo kila sababu ya suala hili kurudi bungeni."

Lakini Mnyika alipingana na moja ya mapendekezo ya Waziri Pinda ya kuunda tume ya kuangalia mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya.
"Sikubaliani na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu katiba,” Mnyika aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana.
“(Waziri Mkuu) Amesema atamshauri rais kuunda timu itakayoangalia mapendekezo ya tume zilizoundwa na pia kuanzisha utaratibu wa marekebisho ya katiba. Naona kauli yake haijalenga kuwepo kwa katiba mpya, bali inalenga zaidi marekebisho ya katiba."

Mnyika alifafanua kwamba, hoja hiyo ya Pinda ina mwelekeo wa kuchukua suala la katiba mpya mikononi mwa wananchi na kulipeleka kwa kundi fulani.
Waziri Pinda aliwaeleza wahariri wa vyombo vya habari mwishoni mwa wiki kuwa kuna njia mbili za kushughulikia kilio cha wananchi cha katiba mpya, akiitaja ya kwanza kuwa ni kumshauri rais aunde kamati ya watu ambao wataangalie maeneo gani ya kuingiza katika katiba.

Alisema njia ya pili ni rais kuunda timu yake ya kiserikali itakayoangalia mapendekezo ya tume zilizoundwa awali kuangalia marekebisho ya katiba na kuchukua mapendekezo yaliyojirudia yatakayoonekana kufaa kuingia katika katiba.

Lakini Mnyika alipingana na mapendekezo hayo akisema haoni sababu ya kuundwa kwa tume nyingine kwa kuwa tangu nchi ipate uhuru, zimeshaundwa tume nyingi kushughulikia suala la katiba.
Alitoa mfano wa Tume ya Jaji Nyalali ambayo ilipendekezwa kufutwa kwa sheria kadhaa ambazo zinaonekana kukandamiza haki za binadamu na Tume ya Jaji Kisanga, akisema matokeo ya uchunguzi wa vyombo hivyo viwili hayajafanyiwa kazi.

"Kutokana na hoja hii napendekeza kwamba, Bunge liweke mfumo wa tume ya kikatiba pamoja na kupitisha azimio ili nchi ifanye mkutano mkuu wa kikatiba kujadili suala hili na kisha zipigwe kura za maoni," alisema.
Alisisitiza kuwa katika suala la katiba mpya, ni lazima wananchi washirikishwe kwa kuwa sasa Watanzaania wanataka katiba mpya.

"Kwanza, katiba inayotumika hii leo ni ya mwaka 1977, tangu kipindi hicho kuna mabadiliko mengi yameshatokea kama ya kiuchumi, kiteknolojia; pili uundwaji wa katiba hiyo haukuwashirikisha wananchi; tatu katiba hii inakabiliwa na changamoto nyingi, mfano suala la Muungano na Tume ya Uchaguzi," alisema.

Chadema ilionyesha kwa vitendo dhamira yake ya kudai katiba mpya wakati wabunge wake walipoondoka kwenye ukumbi wa Bunge wakati Rais Jakaya Kikwete akianza kutoa hotuba ya ufunguzi. Viongozi wa chama hicho pia walisusia hafla ya kutangazwa kwa matokeo na sherehe za kuapishwa kwa rais na wiki mbili zilizopita hawakuonekana kwenye sherehe za uhuru.

Chanzo: Mwananchi-20/12/2010

MP to table private motion on constitution

Ubungo legislator John Mnyika yesterday said that he plans to table a private motion on the new constitution in the February session of parliament.

Mnyika said this in Dar es Salaam yesterday during a press conference he called, to stress that the public needed a new constitution and not the amendment of the present one as is being proposed by some government leaders.

“I am planning to table a private motion in the February parliamentary session, because the process towards writing a new constitution starts from the parliament,” Mnyika said.

He noted that since the law recognises one of parliament’s functions as making or amending laws, it is reasonable to start in parliament.

“Since members of the parliament are the representatives of people, it is good if the matter starts there. It will come up with the public views on how the new constitution should look,” he said

He cited some of the government constitutional reforms through various commissions which did not meet the public expectations on how the country should be administered and that even some of the good recommendations were left on shelves.

“The government before 1965 formed a committee which collected public views which led to the interim constitution. Unfortunately, it did not meet public expectations,” he said, adding that ineffectiveness of the committee led to the formation of the Thabit Kombo Committee in 1976 from whose findings the constitution was amended in 1977.

He said in 1991, the Nyalali Commission was formed, named after the late Chief Justice Francis Nyalali, who headed it.

The commission’s recommendation that a new constitution be written was ignored, Mnyika said.

In 1998, the Judge Robert Kisanga Commission also among others, called for a new constitution, again without success.

Mnyika however explained that Tanzanians needed new constitution and not amendments arguing there are some challenges currently facing the country which the present basic laws has failed to address.

He mentioned the challenges as the handling of the general elections which he said threatened the national security and the recent amendment of the Zanzibar Constitution, incorporating a national unity government and establishing the sovereignty of the Isles.

Last Friday, Prime Minister Mizengo Pinda said he will advise President Jakaya Kikwete to appoint a team to look into modalities of preparing a new constitution for the country.

The Premier said the matter fell under his docket as head of the Constitution and Parliament Committee, one of the four committees of the cabinet.

Leaders and other high-profile figures from Tanzania’s public and private sectors, pressure groups, political parties, religious leaders and ordinary citizens have been pushing for constitutional reforms, with some calling for a complete overhaul of the current (1977) Constitution.

Kenya's High Commissioner to Tanzania, Mutiso Mutinda, recently advised Tanzania against being as slow in drawing up a new constitution.

He said waiting for over 20 years to come up with a new constitution has taught his country bitter lessons.

Human Rights and Good Governance Commission retired High Court judge Amir Manento was recently quoted as saying Tanzania cannot help drawing up a new constitution. Chief Justice Augustino Ramadhani also joined the constitutional reform debate, urging the government to consider the issue as a fundamental need for the nation.

The Christian Council of Tanzania called upon the government to speed up the process of putting together a new constitution drawing on the people’s views, through research and wisdom of the founders of the nation.

Source-Guardian 20/12/2010

Madai ya katiba mpya sasa yahamia bungeni

Mjadala kuhusu madai ya kutungwa kwa Katiba mpya, huenda sasa ukahamia bungeni, baada ya Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, kutangaza rasmi kusudio la kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuliomba Bunge liazimie kuanzisha haraka mchakato wa suala hilo.

Azimio lingine ambalo amesema anakusudia kuliomba Bunge lipitishe, ni kuweka utaratibu wa kuitisha Mkutano Mkuu wa Kikatiba ili kushirikisha watu wengi kujadili kwa mapana na marefu, kuundwa tume ya kuratibu mchakato wa Katiba mpya na kufanyika kura ya maoni ili kupata mawazo ya pamoja.

Alitangaza kusudio hilo alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

Alisema kusudio lake limezingatia kanuni ya 55 (1) ya Bunge, hivyo ataliwasilisha kwa Katibu wa Bunge ndani ya wiki moja kuanzia sasa ili aweze kuiwasilisha rasmi hoja hiyo katika Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza Februari 8, mwaka huu.

Hata hivyo, alisema changamoto kubwa aliyonayo, ni namna gani wabunge wa vyama vyote, watakubaliana naye ili kwa pamoja Bunge liweze kupitisha azimio la hoja yake binafsi.

Alisema hakuwa na wazo la kuipeleka hoja hiyo katika Mkutano wa Bunge wa Februari, mwaka huu, ingawa tangu mwanzo alikwishakuazimia kuwa angehakikisha anaipeleka ndani ya uhai wa Bunge la sasa.

Mnyika alisema uamuzi wa kuharakisha kuipeleka katika Mkutano wa Bunge ujao, unatokana na kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wiki iliyopita katika mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari ya kutaka yafanyike marekebisho ya Katiba na si kutunga Katiba mpya, kuunda jopo la wataalamu na kwenda kumshauri Rais Jakaya Kikwete.

Alisema kauli hiyo ya Pinda inawapeleka Watanzania kwenye njia mbovu; kwani suala la Katiba si la serikali wala Rais, bali ni la wananchi na pia njia zote hizo, serikali imekwishakuzipitia, lakini zikafeli.

Mnyika alisema sababu ya kwanza iliyomfanya akusudie suala hilo, ni Katiba kuwa sheria mama, kwenye Ibara yake ya 63 Kifungu kidogo cha (1) na cha (2) Ibara ya 98 (1), imetoa mamlaka kwa Bunge kutunga sheria na kubadili Katiba.

“Hivyo, nimeona mahali mwafaka pa kufanya hivyo ni bungeni,” alisema Mnyika.

Alisema sababu ya pili, ni Katiba kuwa mkataba kati ya mtawala na mtawaliwa na kwamba, katika kufikiwa mkataba wowote, mwenye mali ndiye anayepaswa kuanza mchakato.

Kutokana na hali hiyo, alisema katika suala la Katiba, wenye mali ni wananchi, hivyo kwa kuzingatia Ibara 63, ambayo imeipa Bunge mamlaka ya kuisimamia serikali, akiwa mwakilishi wa wananchi, ameona abebe jukumu hilo kwa vile mwananchi mmoja mmoja hawezi kuamua.

Alisema sababu ya tatu, ni uzoefu kuonyesha kuwa tume zote zilizowahi kuundwa na serikali kupitia Rais, hazikuweza kukata kiu ya wananchi ya kuleta mabadiliko ya Katiba na mapendekezo yake kuwekwa kabatini.

Mnyika alisema tume hizo ni kama ile ya Thabiti Kombo iliyoundwa na Rais wa Awamu ya Kwanza, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, mwaka 1976; ya pili ya marehemu Jaji Mkuu wa zamani, Francis Nyalali iliyoundwa na Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mwaka 1991; na ya tatu ya Jaji Mstaafu, Robert Kisanga, iliyoundwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa mwaka 1998.

Alisema maoni ya Tume ya Thabiti Kombo yalipelekwa Halmashauri Kuu (NEC) ya Tanu kisha baadaye yakapelekwa bungeni, ambako yalijadiliwa kwa saa tatu tu na kuipitisha Katiba ya sasa ya mwaka 1977.

Mnyika alisema kitendo cha maoni ya tume hiyo kupelekwa NEC ya Tanu, badala ya Bunge, kinathibitisha kwamba, Katiba iliyopo, ina mawazo ya chama kimoja na ndio maana ina udhaifu mkubwa na imewekewa viraka na kufanyiwa marekebisho mara 14 kwa miaka 33.

“Kuna katiba za baadhi ya nchi zina miaka 50, lakini hazijawahi kufanyiwa marekebisho,” alisema Mnyika.

Alisema mfano mwingine ni mapendekezo ya Tume ya Jaji Kisanga, ambayo kwanza Mkapa aliyeiunda, aliishambulia kuwa ilifanya mambo mengine zaidi, ambayo hakuituma na baadaye akachagua mambo aliyoyataka kwenye mapendekezo ya tume hiyo.

Mambo hayo ni kama suala la mgombea urais kutozidi asilimia 50 ya kura na kumpa rais mamlaka ya kuteua watu 10 kuwa wabunge, lakini yaliyohusu mabadiliko ya Katiba yakatupwa.

Mbunge huyo alisema sababu ya nne ya kudai Katiba mpya, ni kuwapo changamoto mpya zinazoikabili nchi, ambazo alisema Katiba iliyopo imeshindwa kuzitolea majibu.

Baadhi ya changamoto mpya, ambazo alisema Katiba iliyopo imeshindwa kuzitolea majibu, ni uchaguzi kuwa tishio la amani kutokana na kufanyika kwa misingi isiyokuwa huru na haki. Nyingine ni marekebisho ya Katiba ya Zanzibar yaliyofanyika baada ya kufikiwa maridhiano ya kumaliza chuki na uhasama wa kisiasa miongoni mwa Wazanzibari visiwani humo, ambayo alisema baadhi ya vifungu vinapingana dhahiri na Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Changamoto nyingine mpya, alisema ni kupungua kwa utamaduni wa uwajibikaji serikalini, ambako kumesababisha kukithiri kwa ufisadi nchini na hivyo kuhitajika Katiba mpya.

Alisema hakuna ulazima wa kuunda jopo la wataalamu kwa ajili ya kushughulikia Katiba iliyopo kama ilivyotamkwa na Waziri Mkuu Pinda, kwani huko nyuma suala hilo lilifanywa, lakini halikuzaa matunda yaliyotarajiwa na wananchi.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo jopo hilo litaundwa, itakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za walipakodi.

Akijibu swali kwamba, Katiba wanayoidai, wananchi wengi hawaijui, Mnyika alikiri, lakini akasema sababu ya wananchi wengi kutoishika wala kuisoma Katiba iliyopo, ni upatikanaji wake kuwa adimu na ghali.

Hata hivyo, alisema hali hiyo haimaanishi kuwa hawajui udhaifu wa Katiba hiyo, kwani taarifa za tume zilizoundwa na serikali, ni ushahidi tosha kwamba, wanaujua vyema.

Alisema japo wananchi wengi hawaijui Katiba, hoja zao zinathibitisha kuwa wanajua udhaifu wake na kutolea mfano wa namna, ambavyo wamekuwa wakihoji kuhusu haja ya kuwapo tume huru ya uchaguzi.

Mnyika alisema wananchi wametoka kwenye mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini Katiba iliyopo bado inashikilia mawazo ya zamani, huku uundwaji wake ukiwa umefanyika bila kuushirikisha umma.

Katika hatua nyingine, Mnyika, ambaye pia ni Katibu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, amelaani kitendo cha polisi cha kumpiga Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) kwa vile ni kinyume cha sheria, haki za binadamu, utawala bora, Katiba, sheria za Jeshi la Polisi, kinga, haki na madaraka ya Bunge.

Chanzo: Nipashe-20/12/2010

Mnyika kuwasilisha hoja bungeni kuhusu katiba mpya

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Ubungo, Bw. John Mnyika ambaye amedokeza kusudio lake la kuwasilisha hoja bungeni katika mkutano wake wa Februari, mwakani, ili liweke utaratibu wa kuanzishwa, kuratibiwa na kusimamiwa kwa mchakato wa katiba mpya kwa kuzingatia matakwa ya umma

Katika mkutano wake na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Bw. Mnyika alisema ameona kuna haja ya kuwasilisha hoja hiyo mapema kuliko alivyokuwa amepanga awali, baada ya kuona dalili za suala hilo 'kupelekwa katika njia zenye kasoro' ambazo ziliwahi kutumika huko nyuma na matokeo yake kupuuzwa.Bw. Mnyika ambaye pia ni katibu wa Kamati ya Wabunge wa CHADEMA, alisema kuwa itakuwa si sahihi kwa hoja ya katiba mpya kuchukua mkondo wa 'kuundiwa tume au kamati ya rais au jopo la wataalamu washauri,' bali itakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwani vitu kama hivyo viliwahi kuundwa lakini mapendekezo yake yakaishia 'kutupwa kapuni na watawala.' "Zipo sababu kadhaa ambazo zimenisukuma kuona umuhimu wa kulipeleka suala hilo bungeni sasa, ili lichukue mkondo wa bunge, kwanza katiba ni sheria, tofauti yake na sheria zingine yenyewe ni sheria mama.

"Ibara ya 63 (2) na (3) zinaeleza kuwa bunge lina mamlaka ya kutunga sheria pia ibara ya 98 (1) si sheria tu, bunge lina mamlaka ya kufanya mabadiliko ya katiba...hivyo kuna haja ya mjadala huu kuchukua mkondo wa bungeni, ndiyo uende serikalini, kisha urudi bungeni. Lakini pia katiba ni mkataba kati ya watawala na watawaliwa, viongozi na waongozwaji au serikali na wananchi.

"Sasa kama ndivyo hivyo kwenye mkataba wa namna hii ambapo mwenye mali ambaye ni mwananchi anatoa mamlaka ya kusimamiwa mambo yake kwa serikali, lazima yeye awe na kauli kubwa juu ya uendeshwaji wa masuala hayo...ibara ya 8 (1) ya katiba inasema kuwa wananchi ndiyo msingi wa mamlaka yote na madaraka, wajibu wa serikali ni kuleta ustawi kwa niaba yao," alisema Bw. Mnyika na kuongeza;

"Ibara ya 63 (2) inasema kuwa bunge litafanya kazi kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri serikali, hivyo basi bunge na wabunge ambao ndiyo wawakilishi wa wananchi, wanaosimama badala ya wenye mali wanapaswa kujadili na kutoa maelekezo kwa serikali."Sababu ya tatu ni kuwa huu sasa si wakati tena wa kuendelea kuliundia tume au kamati za rais suala hili, imeshafanyika sana huko nyuma na historia inaonesha kuwa hazikutimiza matakwa ya wananchi.

"Iliundwa tume ya chama, enzi zile za chama kimoja, wakati wa Mwalimu Nyerere mwaka 1976, maarufu kwa jina la Tume ya Thabit Kombo, ndiyo iliyokuja na mapendekezo ya katiba hii mbovu tuliyonayo, yenyewe ilipeleka mapendekezo straight foward (moja kwa moja) kwa Halmashauri Kuu ya chama wakati huo, kisha bunge likayajadili kwa saa tatu na kupitisha.

Bw. Mnyika aliongeza kuwa kila 'joto' la mjadala wa katiba mpya linapopanda, watawala walioko madarakani wamekuwa wakijaribu kuuzima au kupindisha hoja kwa kuunda tume, kamati au jopo na kisha kuishia 'kuweka viraka' badala ya kufanya kulingana na matakwa ya wananchi.

"Ukiacha hiyo Tume ya Thabit Kombo, mwaka 1983 kulikuwa na joto kubwa la mjadala juu ya katiba hii ya mwaka 1977 ambao ndio mjadala wa katiba mpya ulizaliwa kabisa, serikali ikaamua kufanya marekebisho madogo na kuingiza haki za binadamu mwaka 1984...mwaka 1991 ikaundwa Tume ya Nyalali juu ya mfumo wa vyama vingi, lakini kwa jinsi ilivyokusanya maoni ikaona kuna umuhimu wa kuwa na katiba mpya.Bw. Mnyika alisema kuwa mapendekezo hayo ya Tume ya Nyalali juu ya kuandikwa upya kwa katiba na juu ya sheria 40 mbovu yalipuuzwa, isipokuwa lile la kuruhusu mfumo wa vyama vingi kwa sababu ilikuwa ni tume ya rais na yeye kwa mujibu halazimiki kusikiliza ushauri wa mtu yeyote.

"Mwaka 1998 pia ikaundwa tume nyingine ya rais, Tume ya Jaji Kisanga, Tume ya White Paper, tume ya serikali nyingine badala ya tume ya wananchi, rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa alipuuza ushauri wa katiba mpya, tena akaibeza kuwa ilifanya zaidi ya ilichokuwa imeagizwa kufanya, badala yake serikali ikachukua mapendekezo ya rais kuwa na mamlaka ya kuteua wabunge 10 na lile la kuondoa ulazima wa mshindi wa urais kushinda kwa asilimia zaidi ya asilimia 50 ya kura zote.

"Marekebisho hayo ya mwaka 2000 kwa maoni yangu yakaturudisha nyuma zaidi badala ya kwenda mbele...suala la kuunda tume, mbali ya kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma, lakini pia si njia mwafaka kwa sababu rais kwa mujibu wa ibara ya 37 (1) halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote...lakini pia hii si hoja ya rais wala serikali ni hoja ya wananchi," alisema Bw. Mnyika.

Alisema kuwa kwa hoja yake hiyo ambayo atakuwa ameikamilisha ndani ya juma moja, kisha kuiwasilisha siku moja kabla ya kuanza kwa mkutano wa bunge unaotarajia kujadili hoja hiyo kama zinavyosema kanuni za bunge, ataliomba bunge lianzishe mchakato huo kwa kuisimamia na kuishauri serikali juu ya njia sahihi, na baadaye serikali iitishe mkutano mkuu wa taifa wa kikatiba.

"Kisha kuundwe tume ya kisheria itakayojumuisha watu mbalimbali, si jopo la wataalamu tu, kuratibu maoni ya Watanzania kwani katiba ni mali ya wananchi si ya wataalamu pekee, baada ya hapo ifuatie kura ya maoni itakayojumuisha wananchi wote kufikia mwafaka wa kitaifa juu ya suala hilo.

Alisema kuwa pamoja na kuwa alikuwa na sababu zingine nyingi za kutaka kuwasilisha hoja hiyo ndani ya miaka mitano bungeni, lakini moja ya sababu zilizomfanya aamue kuipeleka katika bunge la Februari, mwakani ni pamoja na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambaye alisema juma lililopita kuwa atamshauri Rais Jakaya Kikwete aunde jopo la wataalamu kisha watoe mapendekezo ya marekebisho ya katiba lakini si kuandika katiba mpya.

Alisema sababu zingine ni pamoja na kukumbana na swali la mahitaji ya katiba mpya na Tume ya Taifa ya Uchaguzi iliyo huru katika karibu kila mkutano wake wakati wa kampeni za uchaguzi, ambapo alikuwa akiahidi kuwa atakapopewa nafasi ataitumia kuwasilisha hoja bungeni ili mchakato uanze kwa manufaa ya Watanzania, hivyo kuwa hoja ya wapiga kura wake.

Chanzo: Majira-20/12/2010

Saturday, December 18, 2010

Mnyika atoa asilimia 20 ya mshahara kuchangia elimu

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amesema ameanza kutekeleza ahadi yake ya kutenga asilimia 20 ya mshahara wake kwa ajili ya Mfuko wa Elimu katika jimbo hilo.

Akizungumza katika kongamano la Vijana Wasomi wa Vyuo Vikuu jana lililofanyika katika ukumbi wa River Side Dar es Salaam, alisema kwa kuwa wakati wa kampeni alitoa ahadi hiyo, ameona ni vyama akaanza nayo kwa kuwa ina manufaa kwa kukuza elimu na kuwa na wasomi wengi nchini.

Mnyika aliwashukuru vijana pamoja na wananchi kwa ujumla kwa kumuunga mkono ambapo aliwaahidi kufanya kazi na hata wasiomuunga mkono wakati wa uchaguzi lengo likiwa kuiinua Ubungo.

“Uchaguzi umekwisha nawashukuru kwa kuniunga mkono nitafanya kazi na wote, ninyi na hata ambao hawakuniunga mkono nawaomba wananchi wote wazee na rika zote pamoja na watendaji wote wa serikali na viongozi wa vyama mbalimbali tushirikiane pamoja katika kuutumikia umma na kuwezesha maendeleo,” alisema Mnyika.

Alisema wananchi wa Ubungo mwenye tatizo au ushauri ofisi ya mbunge imeanza kufanya kazi na iko ndani ya jengo la Wilaya ya Kinondoni, lakini pia atafungua ofisi ya ziada ambayo itakuwa inashughulika na kutoa elimu kwa vijana, wanawake na makundi mengine ya kijamii.

Katika kongamano hilo wataalamu vijana waliwasilisha mada mbalimbali za namna ya kutekeleza mipango ya kushughulikia masuala yanayowagusa wananchi katika sekta za elimu, ajira, maji, miundombinu, usalama, uwajibikaji, ardhi na afya.

Chanzo: Tanzania Daima (Asha Bani)

Friday, December 17, 2010

Pigo kubwa la Kuondokewa na Jabari la Muziki


Ndugu zangu wanamuziki nchini, wakazi wenzangu wa Kata ya Sinza, wanajimbo zima la Ubungo na Taifa zima kwa ujumla. Kama nilivyosema hapo awali-Napenda kutoa rambi rambi zangu za dhati kwa kuondokewa na jabali katika tansia ya muziki nchini, Hayati Dr. Remmy Ongala. Ni vyema tukatumisha kile alichokuwa anatufunza kupitia tungo zake. Na kuendelea kupatumia jina la "Kwa Remmy" eneo lile la Sinza kama tufanyavyo sasa.

Sunday, December 5, 2010

Uzinduzi wa Mabweni Shule ya Kings


Tayari kazi imeanza ya kushiriki kikamilifu pamoja na wananchi na wadau mbalimbali katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa Jimbo la Ubungo na Taifa zima kwa ujumla. Nimeshiriki kuzindua rasmi ujenzi wa mabweni ya shule ya Kings. Kuboresha elimu kwa maslahi ya umma mzima inawezekana. Tushiriki sote kwa kadiri ya nafasi na michango yetu.Shime sasa!!