Tuesday, September 30, 2008

Wanaoeneza ukabila wamefilisika kisiasa


Wosia wa Nyerere na Viti Maalum: Wanaoeneza ukabila wamefilisika kisiasa

Na John Mnyika

Wiki iliyopita nilianza kutoa mtazamo wangu kuhusu suala la ubunge wa viti maalumu. Katika makala yangu iliyopita nilijenga hoja “Viti Maalum:Msekwa na Makamba wapuuzwe Tarime”. Katika mtazamo huo, nilikosoa Sheria yetu ya Uchaguzi ambayo ilitungwa na bunge lililokuwa na wabunge wengi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), chini ya Msekwa kama Spika wa wakati huo. Sheria ambayo inavinyima fursa vyama ya kujua matokeo ya uchaguzi ili kugawa viti hivyo kwa kutoa kipaumbele katika kukubalika kwa chama husika katika maeneo mbalimbali. Hii ni kwa sababu sheria hiyo, ina kifungu kinacholazimisha vyama vya siasa kutangaza wateule wake wa viti maalum kwa kuwasilisha majina Tume ya Uchaguzi kabla ya kura za uchaguzi mkuu kupigwa na matokeo ya ujumla kutangazwa. Dhamira ya sheria hiyo inajichanganya yenyewe, wakati ambapo viti hivyo maalum vinagawiwa kwa vyama kutokana na uwiano wa kura na uwingi ya wabunge wa majimbo, vyama vinalazimika kufanya uteuzi bila kuzingatia uwiano na uwingi huo; hata kama vyama hivyo, vingependa kuweka mambo hayo kama sehemu ya vigezo vyake. Ndio kikwazo kimojawapo ambapo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ilikumbana nacho wakati wa uteuzi wa wabunge wa viti maalum mwaka 2005.

Katika mtazamo wangu wa leo, kama nilivyoahidi wiki iliyopita- nitajikita katika kuchambua masuala badala ya kuwajadili wakina Msekwa na Makamba, na kauli zao za kizushi dhidi ya CHADEMA. Masuala ambayo yameibuliwa katika mijadala mbalimbali kuhusu suala hili pamoja na mambo mengine ni tuhuma za uwepo wa ubaguzi, ukabila na upendeleo katika mgawanyo wa viti hivyo. Lakini masuala mazito zaidi, ni mjadala kuhusu dhana na dhima ya viti maalum hususani vya wanawake katika taifa letu katika muktadha wa mfumo wa uwakilishi wa kidemokrasia nchini.

Kwa kuitwa ‘viti maalum vya wanawake’, hakika tayari nafasi hizi zinabeba sura ya upendeleo kabla hata ya uteuzi wenyewe. Na kwa ujumla, vinaweza kutafsiriwa kuwa ni ‘ubaguzi’ kama tutachukua maana pana zaidi ya maneno hayo. Kwa mantiki hiyo, viti hivyo, vinaweza kuonekana kama ni ‘maalumu’, vya ‘upendeleo’ na kwa ujumla vinagawiwa ‘kibaguzi’ kwa wanawake dhidi ya makundi vingine. Vinapatikana kwa ushindani ‘uliofungwa’ miongoni mwa wanawake wengine. Ni watu wenye mtizamo huu mpana ndio ambao wanamsimamo kuwa viti hivyo ‘vifutwe’. Watetezi wa viti hivi wamekuwa wakijenga hoja wakati wote kuwa viti hivyo ni muhimu, kwa kuwa wanawake wamekuwa wakishindwa kushindana na kushinda majimbo na hivyo kufanya uwakilishi wao kuwa duni. Na wanatoa sababu za kihistoria na sababu za vikwazo vya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kama vikwazo vya wanawake kupata nafasi za ubunge. Katika hali hiyo, watatezi hao wanaamini kama uwepo wa viti maalum, ni tiba na daraja la kuwawezesha wanawake kupata nafasi katika siasa.(Affirmative action). Lakini Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) na Wanaharakati wa Haki za Wanawake(FEMACT) wao wamefanya tathmini ya miaka kumi toka viti maalum viazishwe, wakati wa mapitio ya miaka kumi toka tamko la Beijing na kubaini kwamba viti hivi; havijasadia masuala ya wanawake kupewa kipaumbele katika vyombo vya maamuzi, wala havijasaidia kuwezesha wanawake wengi zaidi kuingia katika siasa na kushinda majimboni. Kwa ujumla, viti hivi vinaonekana kuzua ‘upendeleo’, ‘ubaguzi’ nk miongoni mwa wanawake wenyewe na kunufaisha tabaka la wachache. Wapo wenye mtizamo mkali zaidi, kuwa kwa kutengewa ‘viti maalum’, wanawake wanazidi kusukumwa pembezoni mwa mkondo na mfumo wa uwakilishi. Hivyo, mjadala huu unapaswa kuwa mpana zaidi ili kuhakikisha mfumo wa uwakilishi wa uchaguzi na kisiasa mwaka 2010 na kuendelea unatoa tija inayostahiki kwa makundi yote ya kijamii. Nitajadili suala hilo kwa undani wakati nachangia mtizamo wangu kuhusu mjadala wa uwakilishi wa uwiano mintaarafu 50 kwa 50 ulioibuka katika taifa letu.

Nimeacha leo kuingia kwenye mjadala huo mpana zaidi wa kitaifa kwa wasomaji wa mtazamo wangu wa wiki iliyopita, wamenirudisha katika mjadala wa kuhusu Viti Maalumu ndani ya CHADEMA. Wametaka kujua vigezo na mchakato gani ulitumika, na kama kwa maoni yangu palikuwa na upendeleo na ubaguzi wa kikabila wa kuwapendelea wachaga katika uteuzi huo.

Nasikitika kwamba mijadala ya ukabila na udini na kutazamana kwa vigezo hivyo inaanza kushamiri katika taifa letu. Mijadala ambayo isipojadiliwa kwa umakini wake ni chimbuko la kuteteresha misingi ya undugu, umoja na pengine hata amani katika taifa letu. Katika muktadha wa mjadala huu wa viti maalum, nimekuwa nikosoma mitazamo ya wachambuzi magezetini; wengine wakiandika wabunge wa viti maalum CHADEMA wote ni wachagga, wengine wakiandika watano ni wachagga nk.

Ieleweke wazi, ukabila si uwepo wa makabila; maana kama ukabila ungekuwa ni hali hiyo, basi tusingekuwa na haja ya kujadili suala la ukabila katika nchi yenye makabila takribani120. Ukabila, ni uwepo wa ubaguzi kwa misingi kabila. Neno kabila hapa, kila mtu analijua kwa kuwa analo!

Katika hali hii, wengine tunalazimika kuingia katika mijadala ya kutaja watu na matukio; badala ya mijadala ya masuala. Lakini ni muhimu kwa sasa, katika kukabiliana na uzushi na propaganda zenye kuchochea ukabila. CHADEMA ina wabunge sita wa viti maalamu. Halima Mdee, mpare aliyeteuliwa kutoka Dar es salaam, mkazi wa Jimbo la Ubungo. Maulidah Anna Komu, aliyeteuliwa toka Zanzibar; mzaliwa wa Kwabijokha-Tanzania visiwani. Suzan Lyimo, mchagga aliyeteuliwa toka Dar es salaam akiwakilisha Vyuo Vikuu nchini. Lucy Owenya, mchagga aliyeteuliwa toka Kilimanjaro. Grace Kiwelu, mchagga aliyeteuliwa toka Kilimanjaro. Mhonga Said toka Kigoma. Kati mazingira hayo, tunaona kuna wachagga watatu, wao pamoja na wenzao wengine; wameteuliwa si kwa uchagga wao, ama kwa makabila yao; bali kwa vigezo mbalimbali. Ni katika mazingira kama hayo, wengine hatukutia neno pale ambapo Baraza la kwanza la mawaziri la Kikwete lilijaa wachagga wengi na manaibu wenye asili ya Kilimanjaro. Wala siwashangai wananchi wa mikoa mingine tofauti na Kilimanjaro ambayo wabunge wake wa Viti Maalum wa CCM wana asili ya Kilimanjaro. Kwa sababu naamini, sisi sote ni watanzania!

Katika mchakato wa uteuzi wa mwaka 2005 ulianzia kwenye ngazi ya wilaya zao na baadaye kupitia kwenye Kamati Kuu ya chama. Mchakato huu uliongozwa na vipengele vya Katiba ya CHADEMA toleo la mwaka 2004 ambayo ilikuwa ikitumika wakati huo. Vigezo hivyo vilijikita katika kuangalia sifa za uongozi na mchango wa kila mwombaji katika kutimiza wajibu kwa CHADEMA na taifa. Katika mtizamo wangu wa wiki ijayo, nitachambua vigezo hivyo kwa undani, na kuibua pia masuala ya kitaifa; kwa lengo la kutoa mtazamo wangu katika kuboresha mfumo, vigezo na mchakato uwakilishi wa wanawake na makundi mengine katika taifa.

Jambo moja ambalo watanzania ni vyema wakalifahamu; CHADEMA kama chama kinachokuwa. Mwaka 2006 kilifanya tathamini ya chama, na kuandaa Mpango Mkakati wa chama 2006 mpaka 2010. Na kati ya mambo ambayo chama kiliyatazama ni mfumo wa uteuzi wa wanawake wa viti maalum. Pamoja na mafanikio yaliyopatikana, na mchango mzuri wa wabunge wetu bungeni ikiwemo wa viti maalum, palionekana changamoto- namna kati ya kuwianisha mfumo wa uteuzi kwa vigezo na mfumo wa uteuzi kwa kugombea pekee. Chama kiliona kuna haja ya kuboresha zaidi mfumo wake wa uteuzi wa wabunge hawa, na hivyo, CHADEMA ikabadili katiba yake. Sasa katiba imetoa fursa ya kuanzishwa kwa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA), na pamoja na mambo mengine- BAWACHA ndio itayosimamia uteuzi wa wabunge wa viti maalum mwaka 2010, kupitia ushindani wa wanawake wenyewe. Mambo hayo yote yalifanyika kwa uwazi, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu wa chama uliofanyika Agosti 13 mwaka 2006, wanaCHADEMA waliungana pamoja mbele ya umma kwa kuwa mkutano huo ulikuwa wazi kwa vyombo vya habari. WanaCHADEMA walikubaliana kutazama mbele kwa Tumaini jipya, ikiwemo katika suala hili la uteuzi wa viti maalum. Mjadala huu, unapoendelezwa mwaka 2008, katika sura ya kuituhumu CHADEMA kwa ukabila, katikati ya harakati za CHADEMA za kupambana na ufisadi na kutetea rasilimali za Taifa. Inanikumbusha maneno ya Mwalimu Nyerere, kwamba ukiona watu waanza kutumia dini au kabila kujihalalisha; ujue wamefilisika kisiasa.


0754694553 na http://mnyika.blogspot.com

Monday, September 29, 2008

RAI limekiuka maadili ya uandishi wa habari

C/HQ/ADM/BV/20

19 Agosti, 2008

Mhariri,RAI,Da es salaam.

Ndugu,

Malalamiko juu ya gazeti la RAI kukiuka maadili ya uandishi wa habari na kunichafua

Utakumbuka kwamba tarehe 2 Agosti, 2008 wakati Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe(Mb) akiwasilisha malalamiko ya chama chetu kuhusu jinsi vyombo kadhaa ya habari vilivyoripoti tarehe 1 Agosti, 2008 kuhusu yaliyojiri kwenye msiba wa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wetu na Mbunge wa Tarime, Chacha Zakayo Wangwe; uliibua tuhuma nzito juu yangu. Katika Mkutano huo wa Jukwaa la Wahariri, wewe kama mhariri wa RAI ulinilaumu kuwa mimi ndiye niliyekuwa chanzo cha sintofahamu iliyotokea katika taifa kutokana na msiba huo na kwamba nastahili kubeba lawama kwa yaliyotokea.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Sakina Datoo aliponipa nafasi ya kufafanua kuhusu madai yako; nilikanusha madai yako na nilidokeza kusudio langu la kutafakari na kuchukua hatua zinazostahili kutokana na gazeti la RAI kukiuka maadili ya uandishi wa habari na kunichafua.

Kinyume na madai yako niliweka bayana kwamba kuwa gazeti la RAI ndio lililopotosha na kuudanganya umma, na kuliingiza taifa kwenye hisia tenge kuhusu Kifo cha Chacha Wangwe.

Nikaeleza kuwa gazeti la RAI la alhamisi ya 31 Julai, 2008 lililokuwa na Kichwa cha habari “Wangwe kauwawa” ni moja ya mambo yaliyochochea hisia miongoni mwa wananchi kuhusu ‘kuuwawa’ kwa aliyekuwa kiongozi wetu. Siku hiyo hiyo ya kutoka kwa habari hiyo, ilitokea sintofahamu kwenye msiba Tarime na kupelekea magazeti ya 1 Agosti, 2008 kubeba habari zisizo za kweli kuhusu Mbowe kukaribia kukatwa mapanga nk na kuhusisha kifo hicho na ‘risasi’.

Nilifafanua zaidi kwamba habari hiyo ya ukurasa wa mbele ambacho ilikuwa na kichwa kingine kinachosema “Wataka Polisi iwabane Mnyika na Mallya”, ililenga kujenga hisia kwa wasomaji za kunihusisha na kifo cha Wangwe. Hii ilidhihirika wazi kwa kuwa pamoja na kichwa cha habari kutaka polisi wanihoji, ndani ya habari yenyewe hakukuwa mahali popote ambapo chanzo chochote kimesema nihojiwe na polisi.

Hata aya za ndani za habari yenyewe zilionyesha wazi kukiuka maadili ya uandishi wa habari. Mathalani aya ya kwanza na ya pili za habari hiyo, ambazo zinaeleza kuwa msimamo wa “wazawa wa Tarime” kwamba “chacha ameuwawa’ ulichochewa na kauli zangu; nilikuhoji mbele ya Jukwaa la Wahariri kwanini Habari yenyewe haitaji kauli yangu iliyolalamikiwa na ‘wazawa’ hao. Pia katika habari husika haielezewi popote wazawa hao kutamka bayana kuhusisha kauli zao na msimamo wangu.

Katika habari hiyo, paliwekwa aya, ambayo inataja kwamba msimamo wa Dr Slaa ulikuwa ni kutaka uchunguzi ufanyike wakati mimi nilitoa taarifa kwamba vyombo vya habari kuwa kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA. Mara baada ya maneno ya habari hiyo, gazeti la RAI likaongezea maswali yafuatayo: “Kwanini Mnyika akimbie kutoa kauli hii? Je, Mnyika ni polisi kutangaza mazingira ya kifo cha Wangwe?Je, Mnyika alikuwepo eneo la tukio?, Je, Ni kinga ipi anayotaka kuweka Mnyika?”

Kutokana na habari hiyo kuongezewa maswali hayo ni dhahiri kuwa maswali hayo yaliongezwa na gazeti la RAI kuibua hisia kwa msomaji za kunihusisha na kifo cha Wangwe.

Gazeti la RAI limekiuka maadili ya uandishi wa habari kwa kushindwa kunihoji na kunipa haki ya kutoa majibu; na katika kipindi chote cha msiba huo gazeti la RAI halikuwahi kufanya mahojiano ya moja kwa moja na mimi kuhusu maswali na masuala ambayo wameandika kwenye toleo hilo yanayonigusa moja kwa moja.

Nikakueleza wewe kama Mhariri wa RAI mbele ya Jukwaa la Wahariri kwamba sisi kama CHADEMA tunafanya kazi kama timu kwa kwamba tulipozipokea tu taarifa za msiba tumekuwa tukibadilishana mawazo na kutoa misimamo ya pamoja. Nikakujulisha kwamba Jumanne 29 Julai, 2008 waandishi wa habari walinifuata ofisini kutaka kujua jinsi CHADEMA tulivyopokea msiba huo.

Waandishi wengi walifika baada ya kikao cha sekretariati ya chama ambacho mimi kama kaimu katibu mkuu(wakati huo), nilikuwa Mwenyekiti wa Kikao. Niliwajulisha waandishi hao jinsi ambayo wamekipokea kifo hicho kwa mshtuko na masikitiko makubwa na kwamba tutaendelea kumkumbuka Chacha kama kiongozi jasiri aliyesimamia yale aliyoyaamini na kuwaeleza taratibu za maombolezo ikiwemo bendera kupepea nusu mlingoti na kufungua daftari la maombolezo.

Baada ya kuhitimisha kutoa taarifa hiyo, kwa nyakati tofauti Mwandishi wa Habari wa Mtanzania, na wa TBC1 waliuliza maswali. Wakati yule wa Mtanzania akiuliza swali kwamba habari za mitaani zinasema kwamba CHADEMA ndio ‘imemuua’ Chacha nini kauli ya chama kuhusu suala hilo? Yule wa TBC1 aliuliza kama kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA? Wote wawili niliwaeleza kwamba CHADEMA haihusiki na kifo hicho wala hakihusiani na mgogoro ndani ya chama chetu, na kwamba taarifa za awali tulizokuwa tumezipokea toka kwa Kamanda wa Polisi ni kwamba kifo hicho kimetokana na ajali. Nilisisitiza kuwa waandishi wasianze kuitazama CHADEMA badala yake vyombo vya ulinzi na usalama ndio vinawajibu wa kutoa taarifa kamili.

Huu ndio uliokuwa msimamo wa pamoja ambao ulitolewa pia na viongozi wengine wa CHADEMA siku hiyo akiwemo Katibu Mkuu, Dr Slaa. Hata viongozi wa kiserikali akiwemo Spika wa Bunge na Rais wa nchi katika salamu zao na taarifa walieleza kwamba kifo hicho kimetokana na ajali.

Katika Mkutano huo wa Jukwaa la Wahariri nilikuhoji wewe kama Mhariri wa RAI kwamba ni kwanini kati ya watu wote walionukuu taarifa ya polisi kuwa kifo hicho kimetokana na ajali hawakuandikwa na RAI kwamba wamekurupuka kujikinga; na ni kwanini gazeti la RAI halikuandika wahojiwe na polisi kama nilivyoandikwa mimi?

Nilikueleza masikitiko yangu kuwa pamoja na kuwa Jumatano ya tarehe 30 Julai, 2008 mimi mwenyewe nilimwandikia Barua Mkuu wa Polisi(IGP) kutaka uchunguzi wa utata wa mazingira ya ajali uliotokana na kauli tofauti tofauti ambazo zilitolewa na Deus Mallya ukilinganisha na watoto wa marehemu kuhusiana na ajali hiyo; gazeti la RAI halikuitumia kabisa barua hiyo ambayo nilipeleka nakala kwa vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo kwa njia ya mtandao na vyombo vingi vya habari vilitoa habari hiyo.

Kwa mtiririko wa mambo ya mwelekeo wa habari hiyo, nilikueleza wazi wewe kama Mhariri wa RAI mbele ya Jukwaa la Wahariri kwamba, habari hiyo ililenga kunichafua jina langu na kunihusisha na kifo cha Chacha Wangwe.

Nimeshangazwa kwamba hata baada ya kutoa maelezo hayo kwako, mbele ya wahariri wenzako; gazeti lako katika matoleo yake yaliyofuata mpaka leo, halijafanya tendo la kiungwana la kurekebisha upotoshaji na upungufu nilioueleza.

Kutokana na hali hiyo, nakuandikia barua rasmi ya malalamiko na kukutaka ufanye yafuatayo katika toleo lako la RAI la tarehe 21 Agosti, 2008:

Gazeti lako liwaombe radhi watanzania kwa kukiuka maadili ya uandishi wa habari; kwa kuandika habari isiyokuwa na ukweli, isiyo sahihi, iliyoegemea upande mmoja, yenye mwelekeo wa uchochezi, yenye kuleta majonzi nk.

Gazeti lako liniombe radhi kwa kunichafua na kunihusisha na “kuuwawa kwa Chacha Wangwe”; liniombe radhi ukurasa wa mbele kwa kiwango na uzito ule ule ambao upotoshoji, uchafuzi na ukiukwaji wa maadili ulifanyika katika toleo lililotoka tarehe 31 Julai, 2008.

Kwa kuwa Vichwa vya Habari vya toleo hilo vilisomwa na vyombo vingine vya habari hususani redio na televisheni siku hiyo, napeleka nakala ya malalamiko yangu kwao ili waweze kuyatoa kwa uzito ule ule ambao ambao walisambaza habari hiyo iliyonichafulia jina langu.

Kadhalika, napeleka nakala ya malalamiko haya kwa menejimenti ya Kampuni ya New Habari Corporation wamiliki wa gazeti la RAI na Imprint Limited wachapishaji wa gazeti kwa ajili ya hatua ambazo wataona zinastahili kuchukuliwa.

Aidha napeleka ya barua hii kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari(MCT) na Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa taarifa yao.

Natarajia gazeti lako litatoa ushirikiano wa haraka katika kulinda maadili ya uandishi wa habari nchini kwa kuyafanyia kazi malalamiko yangu.

Wako katika demokrasia na maendeleo.
John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana
C/HQ/ADM/BV/20

19 Agosti, 2008

Mhariri,RAI,Da es salaam.

Ndugu,

Malalamiko juu ya gazeti la RAI kukiuka maadili ya uandishi wa habari na kunichafua

Utakumbuka kwamba tarehe 2 Agosti, 2008 wakati Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe(Mb) akiwasilisha malalamiko ya chama chetu kuhusu jinsi vyombo kadhaa ya habari vilivyoripoti tarehe 1 Agosti, 2008 kuhusu yaliyojiri kwenye msiba wa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wetu na Mbunge wa Tarime, Chacha Zakayo Wangwe; uliibua tuhuma nzito juu yangu. Katika Mkutano huo wa Jukwaa la Wahariri, wewe kama mhariri wa RAI ulinilaumu kuwa mimi ndiye niliyekuwa chanzo cha sintofahamu iliyotokea katika taifa kutokana na msiba huo na kwamba nastahili kubeba lawama kwa yaliyotokea.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Sakina Datoo aliponipa nafasi ya kufafanua kuhusu madai yako; nilikanusha madai yako na nilidokeza kusudio langu la kutafakari na kuchukua hatua zinazostahili kutokana na gazeti la RAI kukiuka maadili ya uandishi wa habari na kunichafua.

Kinyume na madai yako niliweka bayana kwamba kuwa gazeti la RAI ndio lililopotosha na kuudanganya umma, na kuliingiza taifa kwenye hisia tenge kuhusu Kifo cha Chacha Wangwe.

Nikaeleza kuwa gazeti la RAI la alhamisi ya 31 Julai, 2008 lililokuwa na Kichwa cha habari “Wangwe kauwawa” ni moja ya mambo yaliyochochea hisia miongoni mwa wananchi kuhusu ‘kuuwawa’ kwa aliyekuwa kiongozi wetu. Siku hiyo hiyo ya kutoka kwa habari hiyo, ilitokea sintofahamu kwenye msiba Tarime na kupelekea magazeti ya 1 Agosti, 2008 kubeba habari zisizo za kweli kuhusu Mbowe kukaribia kukatwa mapanga nk na kuhusisha kifo hicho na ‘risasi’.

Nilifafanua zaidi kwamba habari hiyo ya ukurasa wa mbele ambacho ilikuwa na kichwa kingine kinachosema “Wataka Polisi iwabane Mnyika na Mallya”, ililenga kujenga hisia kwa wasomaji za kunihusisha na kifo cha Wangwe. Hii ilidhihirika wazi kwa kuwa pamoja na kichwa cha habari kutaka polisi wanihoji, ndani ya habari yenyewe hakukuwa mahali popote ambapo chanzo chochote kimesema nihojiwe na polisi.

Hata aya za ndani za habari yenyewe zilionyesha wazi kukiuka maadili ya uandishi wa habari. Mathalani aya ya kwanza na ya pili za habari hiyo, ambazo zinaeleza kuwa msimamo wa “wazawa wa Tarime” kwamba “chacha ameuwawa’ ulichochewa na kauli zangu; nilikuhoji mbele ya Jukwaa la Wahariri kwanini Habari yenyewe haitaji kauli yangu iliyolalamikiwa na ‘wazawa’ hao. Pia katika habari husika haielezewi popote wazawa hao kutamka bayana kuhusisha kauli zao na msimamo wangu.

Katika habari hiyo, paliwekwa aya, ambayo inataja kwamba msimamo wa Dr Slaa ulikuwa ni kutaka uchunguzi ufanyike wakati mimi nilitoa taarifa kwamba vyombo vya habari kuwa kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA. Mara baada ya maneno ya habari hiyo, gazeti la RAI likaongezea maswali yafuatayo: “Kwanini Mnyika akimbie kutoa kauli hii? Je, Mnyika ni polisi kutangaza mazingira ya kifo cha Wangwe?Je, Mnyika alikuwepo eneo la tukio?, Je, Ni kinga ipi anayotaka kuweka Mnyika?”

Kutokana na habari hiyo kuongezewa maswali hayo ni dhahiri kuwa maswali hayo yaliongezwa na gazeti la RAI kuibua hisia kwa msomaji za kunihusisha na kifo cha Wangwe.

Gazeti la RAI limekiuka maadili ya uandishi wa habari kwa kushindwa kunihoji na kunipa haki ya kutoa majibu; na katika kipindi chote cha msiba huo gazeti la RAI halikuwahi kufanya mahojiano ya moja kwa moja na mimi kuhusu maswali na masuala ambayo wameandika kwenye toleo hilo yanayonigusa moja kwa moja.

Nikakueleza wewe kama Mhariri wa RAI mbele ya Jukwaa la Wahariri kwamba sisi kama CHADEMA tunafanya kazi kama timu kwa kwamba tulipozipokea tu taarifa za msiba tumekuwa tukibadilishana mawazo na kutoa misimamo ya pamoja. Nikakujulisha kwamba Jumanne 29 Julai, 2008 waandishi wa habari walinifuata ofisini kutaka kujua jinsi CHADEMA tulivyopokea msiba huo.

Waandishi wengi walifika baada ya kikao cha sekretariati ya chama ambacho mimi kama kaimu katibu mkuu(wakati huo), nilikuwa Mwenyekiti wa Kikao. Niliwajulisha waandishi hao jinsi ambayo wamekipokea kifo hicho kwa mshtuko na masikitiko makubwa na kwamba tutaendelea kumkumbuka Chacha kama kiongozi jasiri aliyesimamia yale aliyoyaamini na kuwaeleza taratibu za maombolezo ikiwemo bendera kupepea nusu mlingoti na kufungua daftari la maombolezo.

Baada ya kuhitimisha kutoa taarifa hiyo, kwa nyakati tofauti Mwandishi wa Habari wa Mtanzania, na wa TBC1 waliuliza maswali. Wakati yule wa Mtanzania akiuliza swali kwamba habari za mitaani zinasema kwamba CHADEMA ndio ‘imemuua’ Chacha nini kauli ya chama kuhusu suala hilo? Yule wa TBC1 aliuliza kama kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA? Wote wawili niliwaeleza kwamba CHADEMA haihusiki na kifo hicho wala hakihusiani na mgogoro ndani ya chama chetu, na kwamba taarifa za awali tulizokuwa tumezipokea toka kwa Kamanda wa Polisi ni kwamba kifo hicho kimetokana na ajali. Nilisisitiza kuwa waandishi wasianze kuitazama CHADEMA badala yake vyombo vya ulinzi na usalama ndio vinawajibu wa kutoa taarifa kamili.

Huu ndio uliokuwa msimamo wa pamoja ambao ulitolewa pia na viongozi wengine wa CHADEMA siku hiyo akiwemo Katibu Mkuu, Dr Slaa. Hata viongozi wa kiserikali akiwemo Spika wa Bunge na Rais wa nchi katika salamu zao na taarifa walieleza kwamba kifo hicho kimetokana na ajali.

Katika Mkutano huo wa Jukwaa la Wahariri nilikuhoji wewe kama Mhariri wa RAI kwamba ni kwanini kati ya watu wote walionukuu taarifa ya polisi kuwa kifo hicho kimetokana na ajali hawakuandikwa na RAI kwamba wamekurupuka kujikinga; na ni kwanini gazeti la RAI halikuandika wahojiwe na polisi kama nilivyoandikwa mimi?

Nilikueleza masikitiko yangu kuwa pamoja na kuwa Jumatano ya tarehe 30 Julai, 2008 mimi mwenyewe nilimwandikia Barua Mkuu wa Polisi(IGP) kutaka uchunguzi wa utata wa mazingira ya ajali uliotokana na kauli tofauti tofauti ambazo zilitolewa na Deus Mallya ukilinganisha na watoto wa marehemu kuhusiana na ajali hiyo; gazeti la RAI halikuitumia kabisa barua hiyo ambayo nilipeleka nakala kwa vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo kwa njia ya mtandao na vyombo vingi vya habari vilitoa habari hiyo.

Kwa mtiririko wa mambo ya mwelekeo wa habari hiyo, nilikueleza wazi wewe kama Mhariri wa RAI mbele ya Jukwaa la Wahariri kwamba, habari hiyo ililenga kunichafua jina langu na kunihusisha na kifo cha Chacha Wangwe.

Nimeshangazwa kwamba hata baada ya kutoa maelezo hayo kwako, mbele ya wahariri wenzako; gazeti lako katika matoleo yake yaliyofuata mpaka leo, halijafanya tendo la kiungwana la kurekebisha upotoshaji na upungufu nilioueleza.

Kutokana na hali hiyo, nakuandikia barua rasmi ya malalamiko na kukutaka ufanye yafuatayo katika toleo lako la RAI la tarehe 21 Agosti, 2008:

Gazeti lako liwaombe radhi watanzania kwa kukiuka maadili ya uandishi wa habari; kwa kuandika habari isiyokuwa na ukweli, isiyo sahihi, iliyoegemea upande mmoja, yenye mwelekeo wa uchochezi, yenye kuleta majonzi nk.

Gazeti lako liniombe radhi kwa kunichafua na kunihusisha na “kuuwawa kwa Chacha Wangwe”; liniombe radhi ukurasa wa mbele kwa kiwango na uzito ule ule ambao upotoshoji, uchafuzi na ukiukwaji wa maadili ulifanyika katika toleo lililotoka tarehe 31 Julai, 2008.

Kwa kuwa Vichwa vya Habari vya toleo hilo vilisomwa na vyombo vingine vya habari hususani redio na televisheni siku hiyo, napeleka nakala ya malalamiko yangu kwao ili waweze kuyatoa kwa uzito ule ule ambao ambao walisambaza habari hiyo iliyonichafulia jina langu.

Kadhalika, napeleka nakala ya malalamiko haya kwa menejimenti ya Kampuni ya New Habari Corporation wamiliki wa gazeti la RAI na Imprint Limited wachapishaji wa gazeti kwa ajili ya hatua ambazo wataona zinastahili kuchukuliwa.

Aidha napeleka ya barua hii kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari(MCT) na Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa taarifa yao.

Natarajia gazeti lako litatoa ushirikiano wa haraka katika kulinda maadili ya uandishi wa habari nchini kwa kuyafanyia kazi malalamiko yangu.

Wako katika demokrasia na maendeleo.
John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana

Thursday, September 25, 2008

Toka Ubungo-Mwito wa kuchukua hatua

Hii imetolewa na Katibu wa CHADEMA Jimbo la Ubungo. Nathibitisha kuwa nitakuwepo kwenye mkutano huo:



25 Septemba, 2008

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
HATUJARIDHIKA NA HATUA ZA SERIKALI KUHUSU KERO ZA WANANCHI

Fedha zilizolipwa Dowans zirudishwe, wahusika wapelekwe mahakamani

Serikali itoe tamko kuhusu madai ya Wafanyakazi kiwanda cha Urafiki ufisadi na maslahi/mishahara duni

Ulipaji wa Fidia Luguruni bado una mapungufu, Serikali itangaze hatua zilizofikiwa kutokana na orodha ya mafisadi ardhi aliyopewa Waziri Magufuli.

Mkutano wa Hadhara kueleza haya kufanyika Kimara 27 Septemba, 2008

Kuzindua kipeperushi cha “Mwito wa Kuchukua Hatua”

Taarifa inatolewa kwa umma kwamba CHADEMA Wilaya ya Kinondoni Jimbo la Ubungo inakusudia kufanya mkutano wa hadhara siku ya Jumamosi tarehe 27 Septemba, 2008 kuanzia saa 9 alasiri katika Kata ya Kimara, Dar es salaam uwanja wa Kimara Matangini Stendi ya Mabasi. Mpaka sasa Mbunge wa Viti Maalum Suzan Lyimo, Mkurugenzi wa Vijana, John Mnyika na Afisa Mwandamizi wa Habari, David Kafulila wamethibitisha kuhudhuria na kuhutubia katika Mkutano huo wa hadhara.

Kama sehemu ya mchakato wa mkutano ya mchakato wa Hadhara na Maandamano, kesho ijumaa 26 Septemba, 2008; Mwenyekiti wa Kamati ya Msukumo Jimbo la Ubungo-Joseph Maserere atazindua kipeperushi maalum cha kutoa mwito kwa wananchi kushiriki kwenye maandamano hayo. Kipeperushi hicho kitakuwa maadhui ya kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za Taifa. Uzinduzi huo utafanyika katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Ubungo iliyopo Kimara eneo la KONA.

Mkutano huu umepangwa mahususi wa kutoa shinikizo kwa serikali kuhusu masuala mbalimbali yanayowakabili wananchi wa Jimbo la Ubungo na Wilaya ya Kinondoni kwa ujumla kama yalivyojadiliwa na kuazimiwa katika Kongamano la Maendeleo Ubungo lililofanyika Ukumbi wa Kilato, Kimara Jumamosi tarehe 14 Juni, 2008. Mgeni rasmi katika Kongamano hilo alikuwa Mh. Zitto Kabwe(Mb), Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA. Katika Kongamano hilo wananchi kutoka kata mbalimbali za jimbo la Ubungo na maeneo ya jirani katika mkoa wa Dar es salaam walijadili kuhusu kero mbalimbali zinazowakabili wakazi na kufikia maazimio mbalimbali. Taarifa ya kufanya mkutano huo imeshatolewa kwa Serikali za Mitaa, Kata na Polisi na hapajatolewa na pingamizi lolote. Awali mkutano huo ilikuwa ufanyike tarehe 3 Agosti, 2008 lakini uliahirishwa kutokana na msiba wa kitaifa wa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wetu, na Mbunge wa Tarime, Chacha Zakayo Wangwe.

Kongamano hilo lilijadili bajeti ya halmashauri ya Kinondoni 2008/09 na kubaini kwamba bajeti hiyo imeshindwa kukabiliana na kero nyingi za msingi za wakazi, hivyo Kongamano likaazimia kwamba bajeti hiyo ifanyiwe uchambuzi zaidi na ukweli kuhusu bajeti hiyo uweze kusambazwa kwa wakazi wengi zaidi ili waweze kuiwajibisha serikali. Kati ya mambo yaliyojadiliwa katika Kongamano hilo ni pamoja na kuongezeka kwa bei ya umeme kunakochangiwa na mikataba mibovu katika sekta hiyo. Kwa kuwa kampuni ya Dowans iliyorithi mkataba feki wa Richmond ipo katika jimbo la Ubungo, wakazi wa jimbo hilo walioshiriki Kongamano waliazimia mkataba huo uvunjwe, malipo ya milioni 152 yasitishwe, fedha zilizokwishalipwa zirejeshwe, mitambo iondolewe, watendaji wa serikali waliohusika wachukuliwe hatua ikiwemo kupelekwa mahakamani kama sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu suala hilo baada ya ripoti ya Kamati Tuele ya Bunge. Kadhalika Kongamano lilijadili kuhusu migororo mbalimbali ya ardhi na kuweka hadharani tuhuma za ufisadi katika ulipaji wa fidia kwa wananchi wa Eneo la Luguruni Kata ya Kibamba mkoani Dar es salaam. Kongamano liliazimia kuwa serikali iwachukulie hatua watuhumiwa wote wa ufisadi huo na kufanya upya mchakato wa tathmini na ulipaji fidia ili kuhakikisha wananchi wanalipwa haki yao ili kupitisha utekelezaji wa mradi wa maendeleo ya mji katika eneo hilo. Pia Kongamano lilijadili kuhusu haki za wafanyakazi katika wilaya ya Kinondoni hususani jimbo la Ubungo, na katika Kongamano hilo tuhuma za ufisadi katika uuzaji wa nyumba za wafanyakazi, ukodishaji kibiashara badala ya makazi wa maghorofa ya wafanyakazi na mishahara/maslahi duni ya Wafanyakazi wa Kiwanda cha Nguo cha Urafiki ziliwekwa bayana na kujadiliwa. Kongamano liliazimia kuwa kiwanda hicho ni Ubia kati ya serikali ya Tanzania na watu wa China, serikali izifanyie kazi tuhuma hizo na kutoa kauli. Ili kuishinikiza serikali kushughulikia kero hizo Kongamano liliazimia kwamba maandamano ya wananchi yaandaliwe na hivyo Kongamano liliunda Kamati ya Kuandaa Maandamano hayo.

Tarehe 20 Julai, 2008 katika ofisi za CHADEMA jimbo la Ubungo, Kamati ya Kongamano ilikutana na viongozi wa Wilaya ya Kinondoni na Jimbo la Ubungo chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano, John Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Vijana Taifa kutathmini hatua ambazo serikali imechukua baada ya Kongamano hilo. Pamoja na serikali kutangaza kusitisha mkataba na Dowans, Kikao kilibaini kuwa serikali haijavunja mkataba husika. Bali ilifanya usanii. Hii ni kwa sababu mkataba wa awali uliingiwa Agosti 2006 kwa miaka miwili hivyo, mkataba huo muda wake wa kuisha ni Agosti 2008. Hivyo, kwa kuwa serikali imetangaza kusitisha mkataba kuanzia Agosti, 2008 maana yake ni kwamba serikali itakachositisha ni kuendelezwa kwa mkataba mpya; ndio maana mpaka sasa serikali imeendelea kulipa milioni 152 kwa kampuni ya Dowans. Kadhalika, pamoja na Waziri wa Viwanda, Mh. Mary Nagu kutembelea kiwanda cha urafiki siku chache baada ya Kongamano hakujibu madai ya msingi ya wafanyakazi kuhusu tuhuma za ufisadi na/ama matumizi mabaya ya madaraka katika uuzaji na ukodishaji nyumba za wafanyakazi wala kushughulikia tatizo la mishahara na maslahi duni ya wafanyakazi. Kwa upande mwingine, mara baada ya Kongamano serikali ilianza kufanya uthamini upya kuhusu fidia za wananchi wa eneo la Luguruni lakini mchakato huo bado una mapungufu mbalimbali ikiwemo kutokushirikishwa kikamilifu kwa wananchi, kutokutangazwa kwa kiwango cha fidia kwa mujibu wa bei ya soko, na kutokuelezwa kwa hatua zilizochukuliwa baada ya aliyekuwa Waziri wa Ardhi Mh. John Magufuli kukabidhiwa orodha ya watuhumiwa wa ufisadi katika ulipaji wa fidia katika eneo hilo ambao unahusisha fedha za umma shilingi bilioni tatu. Kwa upande mwingine, pamoja na Meya wa Kinondoni, Mh. Salum Londa kutoa kauli ya kumjibu Mgeni Rasmi wa Kongamano, Mh. Zitto Kabwe, majibu yake hayakujibu mapungufu ya bajeti ya wilaya yake yaliyojadiliwa na wananchi na wala hakujibu hoja ya msingi ya mgeni rasmi ya kutaka aeleze umma ni kwanini bajeti ya wilaya hiyo iliwasilishwa na yeye Meya badala ya Mkurugenzi mtendaji. Suala hili ni la muhimu kwa sababu linahusisha dhana nzima ya mgawanyo wa madaraka(kati madiwani na utendaji) na kuhakikisha uwajibikaji kama sehemu ya mihimili muhimu ya uwajibikaji. Hivyo Kamati ya Maandamano pamoja na Viongozi wa wilaya ya Kinondoni na Jimbo la Ubungo kwa pamoja walikubaliana siku hiyo kwamba kabla ya kufanya maandamano paandaliwe Mkutano wa Hadhara wa tarehe 3 Agosti 2008( ambao sasa utafanyika Jumamosi tarehe 27 Septemba, 2008) katika Kata ya Kimara kuzungumza na Wananchi kwa kina kuhusu masuala hayo ili kuunganisha nguvu ya umma katika maandamano ambayo yatapangwa kufanyika baadaye. Mambo mengine ambayo yaliyokubaliwa kuzungumzwa katika mkutano huo wa hadhara ni pamoja na kupanda kwa gharama za maisha ikiwemo nishati, chakula, nauli nk na haja ya kujenga matatu katika barabara kuu ya Morogoro kupunguza kugongwa kwa wananchi kama ilivyo katika maeneo mengine ya barabara hiyo.

Katika hatua nyingine; tunapenda kuutarifu umma kuwa Jumapili 21 Septemba, 2008 ambayo ilikuwa ni Siku ya Amani na Duniani na pia ni Siku ya Michezo Tanzania; CHADEMA Jimbo Ubungo iliadhimisha siku hiyo kwa kukabidhi Mpira kwa Jumuia ya Waganga wa Tiba Asilia Mburahati. Mpira huo ulikabidhiwa na Kaimu Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Ubungo, Martin Mng’ong’o kwa niaba ya Mkurugenzi wa Vijana, Bwana John Mnyika. Mpira huo ulitolewa na Bwana Mnyika kama sehemu ya kutimiza ahadi yake ya kuchangia vifaa vya michezo kwa jumuia hiyo. Itakumbukwa kwamba katika Kongamano la Juni 14, 2008 Jumuia hiyo ilishiriki, na kutoa mwito kwa umma kuwapatia mpira kwa ajili ya kushiriki kukuza michezo.

Akituma salamu za mshikamano katika kuadhimisha siku hiyo, Bwana Mnyika alisema “ Mpira huo ni ishara ya kwamba kila mdau ana wajibu wa kuunga mkono jitihada za kuboresha michezo. Hata hivyo, pamoja na kuwa na vifaa kuna haja ya kuongeza jitihada za kupata viwanja vya michezo. Hivyo, natoa rai kwa serikali itumie maadhimisho ya mwaka huu ya Siku ya Michezo Tanzania. Kutafakari kurudisha kwa umma viwanja vya michezo na maeneo mengine ya wazi ambayo yamejengwa kiholela katika jimbo la Ubungo na maeneo mengine ya mijiji ili kutumika kuweka misingi mizuri ya oganizesheni ya soka. Hii ijumuishe pia kurudisha kwenye halmashauri ama vyama vya michezo, viwanja vya michezo ambavyo vimehodhiwa na CCM vilivyojengwa na michango ya watanzania wote bila kujali itikadi kabla ya mfumo wa vyama vingi kuanza”. CHADEMA Jimbo la Ubungo imefarijika kuwa katika siku hiyo hiyo, ujumbe wa Waziri wa michezo nchini uligusia suala hilo hilo ambalo lilitolewa mwito na Mkurugenzi wa Vijana. Hivyo, tunatarajia hatua za haraka zitachukuliwa kurekebisha hali hiyo.

Wenu katika ujenzi wa Taifa,

Michael Aweda-0754583330
Katibu wa CHADEMA
Jimbo la Ubungo na Wilaya ya Kinondoni

Tuesday, September 23, 2008

Ujumbe wa Wazi kwa IGP Mwema

Ndugu IGP MwemaLeo vijana wako msafara wa magari takribani ishirini wamefanya patrol Tarime na kukamata zaidi ya vijana hamsini kwa sababu za kisiasa. Na wengine wamekamata mpaka pikipiki na mali zao nyingine. Vijana wako, wanaolipwa mishahara kwa kodi zetu watanzania, wanakubali kutumika kisiasa kwa kuwa tu wanapata chakula toka kwa tajiri anayeitwa Zakaria ambaye pia anagombea udiwani kwa CCM Tarime. Naandikia ujumbe huu wa wazi uchukue hatua za haraka. Nami siku chache zijazo naelekea huko huko Tarime. Mtukamate wote mujaze mahabusu na magereza yote huko. Uchaguzi utakapokishwa, dhana nzima ya polisi jamii ambayo umekuwa ukihubiri itakuwa umepotea.
Wako katika ujenzi wa Taifa
John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana-Taifa
0754694553

Msekwa na Makamba wapuuzwe Tarime


Viti Maalum: Msekwa na Makamba wapuuzwe Tarime

Na John Mnyika

Mama yangu aliwahi kuniasa kwamba uongo ukisemwa sana huaminika kuwa ukweli. Lakini baba yangu aliwahi kunieleza pia kuwa siku ukweli ukijitokeza uongo huweza kutahayari, kujificha na wakati mwingine kutoweka. Tutafakari! Hii ni mara yangu ya kwanza kuandika makala ya mtizamo wangu kuhusu suala la viti maalum. Mjadala huu ulikuwa mkali, mwaka 2006 mwanzoni. Mashambulizi yakielekezwa kwa CHADEMA. Wakati huo, nikiwa nauguza majeraha ya ushiriki wangu katika uchaguzi wa 2005 kama mgombea ubunge katika Jimbo la Ubungo.

Halafu ukazuka tena mwaka 2007 mwanzoni; kwa ari, nguvu na kasi mpya wakati huo ukipigiwa debe na makada wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wao Bwana Yusuph Makamba, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum kwa kuteuliwa na Rais Kikwete. Ukanyamaza kidogo, na ukarudi tena, wakati wa Uchaguzi wa kuziba pengo la Makamu Mwenyekiti CHADEMA, hii ilikuwa mwishoni mwa mwaka 2007.

Mjadala ukanyamaza tena. Ukaibuka tena 2008 baada ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, kusimamishwa na Kamati Kuu kutumikia nafasi hiyo na kubaki akiitumika CHADEMA akiwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara na Mbunge wa Tarime. Akashika kasi zaidi baada ya Kamanda Chacha kufariki dunia Julai 28, Mungu amlaze mahali pema. Safari hii, ukipigiwa upatu zaidi kwa mara nyingine na Makada wa CCM na wachambuzi wachache hata kufikia hatua ya wanaCCM kusambaza kile walichokiita- Waraka wa Marehemu aliyekuwa kiongozi wa CHADEMA! Katikati ya mjadala huo ambao kitovu kilikuwa CHADEMA palijitokeza pia mijadala mingine ya viti maalumu ambayo haikushika kasi sana. Ule uliotokana na ripoti ya wanaharakati kuhusu miaka kumi ya viti maalum Tanzania. Ule wa kuziba, kiti ya marehemu Amina Chifupa- Mungu amlaze mahali pema. Na ule ulioshikiwa bango hata na Rais Kikwete, kuhusu uwiono wa hamsini kwa hamsini(50-50) bungeni. Nitaeleza sababu katika makala zangu zijazo!

Lakini kilichonisikuma leo, kujitokeza kutoa mtizamo wangu kuhusu suala hili; ni kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mzee Pius Msekwa kuwa wanaTarime wainyime kura CHADEMA kwakuwa haina shukrani! Kwamba Mbowe alipewa kura elfu thelathini Tarime, lakini CHADEMA ikafanya ubaguzi na kuacha kuteua Mbunge wa viti maalum mwanamke kutoka Jimbo hilo. Ukistajaabu ya Musa!

Awali uongo kama huu ulikuwa ukisemwa na watu wa jamii ya Mzee Makamba, ambao walifikia hatua ya kutangaza kwamba CHADEMA ni chama cha wachagga. Eti makao makuu ya CHADEMA imejaa wachagga! Wakati Makamba na wenzake wakitoa kauli hizo, kati ya wakurugenzi wa CHADEMA tisa miaka hiyo ya 2005/07 Mchagga alikuwa mmoja tu, Antoni Komu. Huku wasukuma tukiwa wengi zaidi. Baadaye wakaongezeka wachagga wawili, walioteuliwa si kwa uchagga wao wao, bali uwezo wao na utumishi wao; John Mrema aliyekuwa Waziri Mkuu Chuo Kikuu cha Dar es salam, mara baada ya kuhitimu kwake akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri. Na Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Rasilimali. Hata hivyo, makao makuu ya CHADEMA imeendelea kuwa na wasukuma wengi zaidi. Kwa bahati mbaya, mwaka 2008 propaganda za kikabila zikaendelea kufanywa zaidi, ikafikia hatua hata sisi wasukuma wengine, kubatizwa kabila na kuitwa wachagga. Huku CHADEMA ikiwa na dereva mmoja tu mchagga kati ya madereva wote wa CHADEMA wanaozunguka nchini kufanya kazi za kisiasa, nikashangaa kusoma kwamba madereva wote CHADEMA ni wachagga. Na vyombo vya habari, vichangia kueneza uzushi, ukabila na ubaguzi dhidi ya wachagga. Hakuna mchambuzi aliyekwenda mbali zaidi, kuchunguza na kujua kwamba mtu kama John Mnyika wa CHADEMA ni msukuma aliyezaliwa na familia ya Dalali, ni Mjukuu wa Masalu wa ukoo wa “Inkhamba”! Tuyaache hayo, turudi kwenye mtizamo wangu wa leo.

Wangeendelea kusema wakina Makamba, ningeendelea kunyamaza! Lakini sasa, wamejiingiza katika athari za Lucifer, hata wazee tunaowaheshimu, kama Mzee Msekwa. Kweli sasa CCM imekuwa kokoro. Vijana kama sisi, wanasiasa wa kizazi kipya; kwa kweli hatustahili hata kufungua gidamu za viatu vya kina Mzee Msekwa. Lakini sasa kwa kisingizio cha siasa, wazee wetu hawa wamejishusha na kufikia hatua sasa wanatusukuma kuwapandia vichwani.

Mzee Msekwa niliyemsoma mimi katika vitabu vya historia ya nchi yetu kama mwanasiasa mkongwe na mweledi wa masuala ya kisheria; siamini kama kauli aliyoitoa Tarime amekosea. Nionavyo mimi ni kuwa amedhamiria kupotosha kwa malengo ya kisiasa.

Huyo Mzee Msekwa, aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyepitisha Sheria ya Uchaguzi yenye kuvilazimisha vyama kupeleka Orodha ya majina ya Wateule wake wa Viti Maalum kabla ya kura za Uchaguzi Mkuu kupigwa. Leo anaibuka na kusema uwongo kuwa CHADEMA ilikuwa inajua kuwa Mbowe amepewa kura elfu thelathini Tarime, lakini bado CHADEMA ikaamua kuwanyima wananchi wa Tarime kiti hata kimoja cha Wabunge wa Viti Maalum. Yeye anajua, kuwa CHADEMA ililazimishwa na Sheria kufanya uteuzi kabla ya kujua matokeo, na ikumbukwe kwamba mwaka 2000, CHADEMA haikufanya vizuri Tarime kama ilivyokuja kufanya maajabu Mwaka 2005. Wakati CHADEMA inajua matokeo iliyoyapata Tarime, tayari uteuzi wa Viti Maalum ulishafanyika. Msekwa analijua hilo, mintaarafu mjadala ndani ya CCM na UVCCM kuziba nafasi ya Amina Chifupa aliyekuwa akiwakilisha Vijana; nafasi yake ikaja kuzibwa na Dr Ishengoma wa UWT kwa kuwa tayari CCM nayo ilishalazimishwa kisheria kufanya uteuzi toka kabla ya matokeo ya uchaguzi 2005 na majina yalikuwa Tume ya Uchaguzi(NEC) tayari. Nitaendelea na mjadala huu, nitaachana na wakina Msekwa na Makamba na kujikita katika kujadili hoja kuhusu viti maalumu Tanzania; mpaka kieleweke. Ila ninachoweza kusema kwa sasa, wana Tarime; wapuuzeni watu ambao wako tayari kusema chochote ama kufanya chochote kwa sababu ya uchaguzi. Watu hawa hugueza uchaguzi kuwa uchafuzi, na demokrasia kuwa domo-ghasia!

Mwandishi ni mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia 0754694553 na http://mnyika.blogspot.com

Viti Maalumu:Msekwa na Makamba Wapuuzwe Tarime


Viti Maalum: Msekwa na Makamba wapuuzwe Tarime

Na John Mnyika

Mama yangu aliwahi kuniasa kwamba uongo ukisemwa sana huaminika kuwa ukweli. Lakini baba yangu aliwahi kunieleza pia kuwa siku ukweli ukijitokeza uongo huweza kutahayari, kujificha na wakati mwingine kutoweka. Tutafakari! Hii ni mara yangu ya kwanza kuandika makala ya mtizamo wangu kuhusu suala la viti maalum. Mjadala huu ulikuwa mkali, mwaka 2006 mwanzoni. Mashambulizi yakielekezwa kwa CHADEMA. Wakati huo, nikiwa nauguza majeraha ya ushiriki wangu katika uchaguzi wa 2005 kama mgombea ubunge katika Jimbo la Ubungo.

Halafu ukazuka tena mwaka 2007 mwanzoni; kwa ari, nguvu na kasi mpya wakati huo ukipigiwa debe na makada wa CCM wakiongozwa na Katibu Mkuu wao Bwana Yusuph Makamba, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum kwa kuteuliwa na Rais Kikwete. Ukanyamaza kidogo, na ukarudi tena, wakati wa Uchaguzi wa kuziba pengo la Makamu Mwenyekiti CHADEMA, hii ilikuwa mwishoni mwa mwaka 2007.

Mjadala ukanyamaza tena. Ukaibuka tena 2008 baada ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, kusimamishwa na Kamati Kuu kutumikia nafasi hiyo na kubaki akiitumika CHADEMA akiwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara na Mbunge wa Tarime. Akashika kasi zaidi baada ya Kamanda Chacha kufariki dunia Julai 28, Mungu amlaze mahali pema. Safari hii, ukipigiwa upatu zaidi kwa mara nyingine na Makada wa CCM na wachambuzi wachache hata kufikia hatua ya wanaCCM kusambaza kile walichokiita- Waraka wa Marehemu aliyekuwa kiongozi wa CHADEMA! Katikati ya mjadala huo ambao kitovu kilikuwa CHADEMA palijitokeza pia mijadala mingine ya viti maalumu ambayo haikushika kasi sana. Ule uliotokana na ripoti ya wanaharakati kuhusu miaka kumi ya viti maalum Tanzania. Ule wa kuziba, kiti ya marehemu Amina Chifupa- Mungu amlaze mahali pema. Na ule ulioshikiwa bango hata na Rais Kikwete, kuhusu uwiono wa hamsini kwa hamsini(50-50) bungeni. Nitaeleza sababu katika makala zangu zijazo!

Lakini kilichonisikuma leo, kujitokeza kutoa mtizamo wangu kuhusu suala hili; ni kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mzee Pius Msekwa kuwa wanaTarime wainyime kura CHADEMA kwakuwa haina shukrani! Kwamba Mbowe alipewa kura elfu thelathini Tarime, lakini CHADEMA ikafanya ubaguzi na kuacha kuteua Mbunge wa viti maalum mwanamke kutoka Jimbo hilo. Ukistajaabu ya Musa!

Awali uongo kama huu ulikuwa ukisemwa na watu wa jamii ya Mzee Makamba, ambao walifikia hatua ya kutangaza kwamba CHADEMA ni chama cha wachagga. Eti makao makuu ya CHADEMA imejaa wachagga! Wakati Makamba na wenzake wakitoa kauli hizo, kati ya wakurugenzi wa CHADEMA tisa miaka hiyo ya 2005/07 Mchagga alikuwa mmoja tu, Antoni Komu. Huku wasukuma tukiwa wengi zaidi. Baadaye wakaongezeka wachagga wawili, walioteuliwa si kwa uchagga wao wao, bali uwezo wao na utumishi wao; John Mrema aliyekuwa Waziri Mkuu Chuo Kikuu cha Dar es salam, mara baada ya kuhitimu kwake akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri. Na Mbunge wa Viti Maalum, Suzan Lyimo akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Rasilimali. Hata hivyo, makao makuu ya CHADEMA imeendelea kuwa na wasukuma wengi zaidi. Kwa bahati mbaya, mwaka 2008 propaganda za kikabila zikaendelea kufanywa zaidi, ikafikia hatua hata sisi wasukuma wengine, kubatizwa kabila na kuitwa wachagga. Huku CHADEMA ikiwa na dereva mmoja tu mchagga kati ya madereva wote wa CHADEMA wanaozunguka nchini kufanya kazi za kisiasa, nikashangaa kusoma kwamba madereva wote CHADEMA ni wachagga. Na vyombo vya habari, vichangia kueneza uzushi, ukabila na ubaguzi dhidi ya wachagga. Hakuna mchambuzi aliyekwenda mbali zaidi, kuchunguza na kujua kwamba mtu kama John Mnyika wa CHADEMA ni msukuma aliyezaliwa na familia ya Dalali, ni Mjukuu wa Masalu wa ukoo wa “Inkhamba”! Tuyaache hayo, turudi kwenye mtizamo wangu wa leo.

Wangeendelea kusema wakina Makamba, ningeendelea kunyamaza! Lakini sasa, wamejiingiza katika athari za Lucifer, hata wazee tunaowaheshimu, kama Mzee Msekwa. Kweli sasa CCM imekuwa kokoro. Vijana kama sisi, wanasiasa wa kizazi kipya; kwa kweli hatustahili hata kufungua gidamu za viatu vya kina Mzee Msekwa. Lakini sasa kwa kisingizio cha siasa, wazee wetu hawa wamejishusha na kufikia hatua sasa wanatusukuma kuwapandia vichwani.

Mzee Msekwa niliyemsoma mimi katika vitabu vya historia ya nchi yetu kama mwanasiasa mkongwe na mweledi wa masuala ya kisheria; siamini kama kauli aliyoitoa Tarime amekosea. Nionavyo mimi ni kuwa amedhamiria kupotosha kwa malengo ya kisiasa.

Huyo Mzee Msekwa, aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyepitisha Sheria ya Uchaguzi yenye kuvilazimisha vyama kupeleka Orodha ya majina ya Wateule wake wa Viti Maalum kabla ya kura za Uchaguzi Mkuu kupigwa. Leo anaibuka na kusema uwongo kuwa CHADEMA ilikuwa inajua kuwa Mbowe amepewa kura elfu thelathini Tarime, lakini bado CHADEMA ikaamua kuwanyima wananchi wa Tarime kiti hata kimoja cha Wabunge wa Viti Maalum. Yeye anajua, kuwa CHADEMA ililazimishwa na Sheria kufanya uteuzi kabla ya kujua matokeo, na ikumbukwe kwamba mwaka 2000, CHADEMA haikufanya vizuri Tarime kama ilivyokuja kufanya maajabu Mwaka 2005. Wakati CHADEMA inajua matokeo iliyoyapata Tarime, tayari uteuzi wa Viti Maalum ulishafanyika. Msekwa analijua hilo, mintaarafu mjadala ndani ya CCM na UVCCM kuziba nafasi ya Amina Chifupa aliyekuwa akiwakilisha Vijana; nafasi yake ikaja kuzibwa na Dr Ishengoma wa UWT kwa kuwa tayari CCM nayo ilishalazimishwa kisheria kufanya uteuzi toka kabla ya matokeo ya uchaguzi 2005 na majina yalikuwa Tume ya Uchaguzi(NEC) tayari. Nitaendelea na mjadala huu, nitaachana na wakina Msekwa na Makamba na kujikita katika kujadili hoja kuhusu viti maalumu Tanzania; mpaka kieleweke. Ila ninachoweza kusema kwa sasa, wana Tarime; wapuuzeni watu ambao wako tayari kusema chochote ama kufanya chochote kwa sababu ya uchaguzi. Watu hawa hugueza uchaguzi kuwa uchafuzi, na demokrasia kuwa domo-ghasia!

Mwandishi ni mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia 0754694553 na http://mnyika.blogspot.com

Monday, September 8, 2008

Undumilakuwili wa UVCCM

Baada ya waandishi kadhaa kuniomba nitoe maoni kuhusu suala la Nape kuchufukuzwa unachama wa UVCCM niliwaandikia ifuatavyo:

“Awali ya yote nianze kwa kusema kwamba si kawaida yangu kutoa maoni kuhusu masuala ya kawaida ya kiutendaji ndani ya vyama vingine. Hata hivyo, nalazimika kulitolea maoni suala hili kwa kuwa lina mwelekeo wa kuvuka mipaka ya CCM na kugusa maslahi ya vijana wengi nchini na watanzania kwa ujumla. Hii ni kwa sababu, mosi- asili ya mjadala ni Jengo linaloitwa na UVCCM ambalo kimsingi ni jengo liliopaswa kuwa la vijana wote bila kujali itikadi. Pili, uamuzi umechukuliwa wakati ambapo tayari mjadala wa kitaifa ukiwa umeibuka kuhusu tuhuma za ufisadi katika mkataba wa Jengo hilo. Na tatu kauli za Makamba, Kingunge nk ambazo zinaibua mjadala kuhusu aina ya ushiriki wa vijana katika siasa ndani ya chama chao na hata katika taifa kwa ujumla.

Si lengo la maoni yangu kutetea aina yoyote ya ukiukwaji wa maadili na nidhamu ndani ya chama chochote cha siasa iwe ni kwa kusema uwongo, kutokutumia vikao wala kwa kutokuwa na uwajibikaji wa pamoja. Na wala sina nia ya kujiingiza katika mijadala ya makundi yaliyomo ndani ya CCM. Mimi ni mwanachama wa CHADEMA, chama cha demokrasia na maendeleo. Rangi nyeupe katika bendera yetu inawakilisha ukweli, uwazi na uadilifu; hivyo wakati wote hii ndio misingi ambayo wanachama wa Baraza la Vijana wa CHADEMA(BAVICHA) tunasimamia na tuko tayari kuhakikisha misingi hii inasimamiwa popote pale bila kujali itikadi.
Bwana Nape amesimamishwa kwa tuhuma za kusema uwongo, kuhusu mchakato wa Mkataba wa Jengo la UVCCM. Mimi binafsi nimeona nakala ya makubaliano ya mradi wa Jengo ambayo yanamaudhui ya kimkataba. Na kwa maoni yangu, naungana na Bwana Nape makubaliano hayo ni bomu na kwamba yana sura ya mkataba mbovu kama mikataba mingine ambayo Viongozi wa chama chake ikiwemo waliomo katika serikali wamekuwa wakiingia kwenye sekta mbalimbali nchini ikiwemo madini. Na kwa ujumla kuingia makubaliano hayo ni ufisadi na kuendelea kuwaibia vijana wa Tanzania ambao kimsingi jengo lile ni lao kwa kuwa lilijengwa na kodi za watanzania wote bila kujali itikikadi wakati wa mfumo wa chama kimoja na kuporwa na UVCCM baada ya kuanza kwa mfumo wa vyama vingi. Katika mazingira hayo, kwa maoni yangu badala ya vikao vya UVCCM na CCM ya chama hicho kuendelea kujadili mradi huo, wanapaswa kupitisha azimio la kurudisha jengo hilo serikalini ili litumiwe na vijana wote bila kujali itikadi. Inasikitisha kwamba wakati Idara ya Vijana ya Serikali ikiwa kwenye jengo dogo na bovu, huku vikundi na taasisi nyingi za vijana zikiwa hazina ofisi; UVCCM wanaendelea kung’an’gania mikataba na makubaliano mabovu kuhusu mradi wa Jengo hilo.

Bwana Nape amesimamishwa akiwa ameibua mjadala wa ufisadi ndani ya UVCCM, hali ambayo inabua maswali kuhusu dhamira ya CCM katika vita dhidi ya ufisadi. Nirudie tena, kuna haja ya kutofautisha madai ya uwongo dhidi ya ukweli. Na nimesema wazi kuwa ni kweli kuwa uporaji wa jengo la UVCCM toka kwa wananchi na makubaliano hayo yaliyosainiwa baada ya uporaji huo, ni ukweli wa ufisadi ambao haupaswi kufumbiwa macho na wapenda demokrasia na maendeleo. Lakini kinachosikitisha zaidi ni kuwa Baraza Kuu la UVCCM limekaa katika kipindi ambacho Orodha ya Mafisadi imetolewa na mjadala wa ufisadi umeshamiri katika taifa letu, badala ya UVCCM kutoka na Azimio la kutaka watuhumiwa wa ufisadi kama wakina Lowassa, Chenge nk kuvuliwa uanachama katika chama hicho au walau kuvuliwa nafasi za uongozi kama walivyopendekeza kwa Kamati Kuu kuhusu Bwana Nape. Uamuzi huu wa UVCCM umeendeleza vitendo vya jumuia hiyo kutumika kuwalinda na kuwasafisha mafisadi. Kama hali hii haitabadilika, wasiwasi wa watanzania mbalimbali kuwa chama hicho kinageuka kuwa chama cha mafisadi utazidi kushamiri na hatma ya taifa itakuwa mashakani kama chama kilicho madarakani kwa wakati huu kitakuwa kinaelea vijana wake katika malezi, fikra na maamuzi ya utamaduni wa ufisadi.
Kwa maoni yangu, uamuzi wa UVCCM ni shinikizo toka katika kundi la kina Kingunge, Lowassa, Makamba na Nchimbi ndani ya chama hicho; kwa kuzingatia kauli ambazo viongozi hao wamezitoa kuhusu mradi wa jengo hilo na/ama Bwana Nape. Kauli za Wazee wa chama hicho kama Makamba, Kingunge nk kuwataka vijana wa chama hicho wawe wapole inatishia uhuru, udadisi na ushiriki makini wa vijana katika medani ya siasa. Kauli hizo zinapingana kabisa na dhamira ya Mwalimu Nyerere na misingi ya zamani ya ushiriki wa vijana wakati huo chini ya TANU Youth League(TYL) ambapo vijana walikuwa mstari wa mbele kuhoji. Ni dhahiri kuwa wanasiasa hao wamepitwa na wakati. Lakini kauli zao zinadhihirisha wazi kuwa vijana wadadisi na wapenda mabadiliko hawapaswi kuwa wala kujiunga katika UVCCM. BAVICHA inawakaribisha vijana wote wenye moyo wa uadilifu na kutetea rasilimali za taifa kujiunga na CHADEMA ili kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi na kuleta maendeleo nchini. Aidha kusimamishwa kwa Bwana Nape kumetanguliwa na kauli ya Mzee Kingunge ya hivi karibuni(ambayo hakuitoa ndani ya vikao vya chama chake, lakini hakuitwa kuhojiwa na kuadhibiwa kwa kutoa kauli nje ya vikao kama Bwana Nape); ya kuwakemea wanaokosoa chama hicho na viongozi wake dhidi ya ufisadi. Kusimamishwa kwa Bwana Nape kunapaswa kuwa mwito wa kuamka(wake up call) kwa wapuliza filimbi wote(whirstle blowers) ndani ya chama hicho na serikali juu ya ufisadi ikiwemo baadhi ya wabunge kuwa wanaweza kuchukuliwa hatua; hivyo, ni wakati sasa wa kuchukua hatua zinazovuka mipaka ya CCM. CCM imeanza kujidhihirisha wazi kuwa kina uongozi wenye kulinda ufisadi. Haki za binadamu ndani ya CCM zinalindwa zaidi kwa mafisadi lakini inapokuja suala la kukemea ufisadi wanaokemea haki zao hazilindwi kikamilifu.

Tunapenda kuwakumbusha UVCCM na watanzania kauli ambayo CHADEMA tuliitoa mwaka 2005 kuwa ‘Mabadiliko ya Kweli, hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale, eti kwa Ari, Nguvu na Kasi mpya. Kwa falsafa ya chukua chako mapema(ccm), Tanzania yenye neema haiwezekani.’
Maoni yametolewa 8/9/2008:

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana
0754694553

PS: Nimeandika kwa haraka, utafanya uhariri kama kuna makosa ya uchapaji, unaweza pia kushauri itolewe kama makala




Wednesday, September 3, 2008

SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASSA

Siku chache zilizopita. Nilitoa taarifa hii kwa vyombo vya habari. Hata hivyo, kwa sababu ambazo sizifahamu, habari hii haikutoka katika magazeti mengi ya kila siku. Pengine inaweza ikawa ni njia iliyotumika kufikisha ujumbe(barua pepe) lakini kuna uwezekano mkubwa sababu ikawa ni kuwa Lowassa hakutajwa kuchukuliwa hatua kama hizi ambazo nimezieleza hapa katika yale Maazimio 23 ya Bunge. Yeye aliambiwa tu atakafakari na kuchukua maamuzi ambayo ataona yanafaa. Yeye akaamua kujiuzulu. Lakini bado siridhiki sana na sababu hii kwa kuwa maazimio hayo 23 hayajasema Karamagi na Msabaha wachunguzwe kuhusu Rushwa kama serikali ilivyoamua. Kama imeamualiwa na Serikali hawa wachunguzwe, kwanini serikali haikumjumuisha na Lowassa? Hii inafanya niamini kwamba bado msimamo huu hapa chini ni mwafaka:

TAARIFA KWA UMMA

SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASSA

  • Ni mmoja wa mizizi ya ufisadi wa Richmond
  • Akamatwe, ahojiwiwe na achukuliwe hatua za kisheria.

Tarehe 25 Februari, 2008 Vijana wa CHADEMA tulitoa taarifa kwa umma tukikemea jitihada zilizokuwa zikiendelea za Lowassa kujisafisha na kusafishwa na tukahimiza achukuliwe hatua za haraka kutokana na tuhuma za ufisadi na/ama matumizi ya madaraka katika kashfa ya RICHMOND. Pamoja na taarifa yetu hiyo kwa umma katika kipindi chote ambacho Serikali ilipewa na Bunge kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu suala hilo hatua tulizopendekeza hazikuchuliwa. Aidha tumefadhaishwa zaidi na Taarifa ambayo Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo ameiwasilisha Bungeni Alhamisi 28 Agosti, 2008 pamoja na kutaja hatua ambazo zimechukuliwa kuhusu watuhumiwa wengine ikiwemo kuandikiwa Barua za kujieleza na/ama kuanza kuchunguzwa na vyombo vya dola/usalama; Waziri Mkuu hakueleza hatua ambazo zimeaanza kuchukuliwa dhidi ya Bwana Lowassa.

Tunatambua kuwa Waziri Mkuu katika taarifa yake ameeleza kuhusu hatua ambazo serikali imeanza kuchukua ikiwemo za marekebisho ya Sheria ama mifumo ya uwajibikaji, ikiwemo ile ya manunuzi. Hata hivyo, tungependa kuweka bayana kwamba matatizo ya msingi ya taifa letu hayasababishwi na mapungufu katika sheria pekee, ila kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na kulegea kwa misingi ya utawala wa sheria na uwajibikaji miongoni mwa viongozi. Hivyo, tunapenda kuwajulisha Watanzania kuwa kama watuhumiwa wa ufisadi hawatachukuliwa hatua mapema, misingi ya utawala wa sheria itazidi kutetereka na matokeo yake ni kuwa mageuzi yoyote katika mifumo ya kiutawala hayatatekelezwa kikamilifu. Kwa ujumla tunaamini kwamba utamaduni huu wa kulindana katika serikali unatoa mfano mbaya kwa vijana wa kitanzania kuhusu uongozi na utawala bora.

Tungependa kusisitiza kuwa Bwana Lowassa, akiwa Waziri Mkuu wa nchi yetu wakati huo alikuwa mmoja wa mizizi mikuu ya ufisadi wa RICHMOND. Hivyo, tunaona kuwa Taarifa ya Utekelezaji ya Waziri Mkuu Pinda imejikita katika kushughulikia matokeo badala ya mzizi wa tatizo lenyewe na hivyo kama hali hii ikiendelea itaporomosha nidhamu na uwajibikaji katika taifa letu. Tunaamini kwamba kama Bwana Lowassa aliyekuwa kinara wa Serikali wakati huo, ataweza kuchukuliwa hatua kikamilifu basi itakuwa rahisi kwa waliokuwa chini yake kuweza kuchukuliwa hatua za haraka na hatimaye kurejesha maadili katika utawala. Lakini kama Serikali itaendelea kumlinda Bwana Lowassa na kuwatoa kafara maafisa wa chini, bado haitakuwa imetekeleza kikamilifu dhana ya uwajibikaji na utawala wa Sheria. Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na mawaziri wenzake kadhaa ni hatua ndogo sana katika kashfa iliyohusisha uvunjaji wa Sheria za nchi yetu, mazingira ya ufisadi na hasara kubwa kwa taifa.

Sisi tunaona kutotajwa kikamilifu kwa hatua zilizochuliwa juu ya Bwana Lowassa ni mwendelezo wajitihada za miezi ya karibuni za Bwana Lowassa(Mb) kupita akijitetea kuanzia katika hotuba yake alipokwenda Jimboni Monduli na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari na hata mahojiano yake maalumu na Televeshioni ya Taifa(TVT).

Aidha, taarifa ya Waziri Mkuu Pinda imeakisi uamuzi wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu Bwana Edward Lowassa kujitokeza miezi ya karibuni kujitetea kuhusu kuhusika kwake katika kashfa ya Richmond ambayo kwa ujumla ni ishara ya unafiki wa kisiasa. Itakumbukwa kuwa baada ya Kamati Teule kuwasilisha taarifa yake, Bwana Lowassa alipata nafasi bungeni takribani mara mbili kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni wakati akiwa Waziri kuzungumzia suala hili lakini hakutoa utetezi ambao Mwezi Februari alijaribu kuutoa kwa umma. Waziri Mkuu Pinda inabidi auleze Umma kama uamuzi wa kumtomtaja katika Taarifa yake ya utekelezaji kuhusu hatua ambazo amechuliwa ni ishara kuwa serikali imekubaliana na utetezi wa Bwana Lowassa.

Itakumbukwa kuwa Vijana wa CHADEMA tulieleza wazi kwamba katika kujitetea kwake mwezi Mei, Bwana Lowassa alithibitisha wazi uzembe na matumizi mabaya ya madaraka ambayo aliyafanya alipokuwa Waziri Mkuu wakati wa sakata zima la Richmond. Hivyo, tunarudia kutoa mwito kwa vyombo vya dola kuweza kumkamata, kumhoji na kumchukulia hatua za kisheria dhidi ya uzembe na matumizi hayo mabaya ya madaraka kwa mujibu wa sheria za nchi yetu. Badala ya Bwana Lowassa kuendelea kupita akijitetea kuwa Kamati Teule haikumuita kuweza kujieleza; vyombo vya dola vimkamate akatoe maelezo yake panapohusika. Vyombo vya dola vimekuwa vikiwakamata raia wa kawaida wenye taarifa za uhalifu kuweza kuisadia polisi, inashangaza Bwana Lowassa amejieleza wazi kuwa alikuwa anafahamu uhalifu uliokuwa ukitendeka lakini bado yuko nje akijitetea na pia Taarifa za kiserikali zikielekea kumlinda. Tunaamini akikamatwa yeye, atawezesha watuhumiwa wakuu wa kashfa ya Richmond kuweza kupatikana. Tulieza wazi katika tamko letu na Mwezi Februari kuwa , jitahada zozote za kumlinda na kumtetea zingeweza kuathiri mwekekeo wa hatua ambazo zitanatarajia kupendekezwa na Kamati ya Waziri Mkuu mpya Mheshimiwa Mizengo Pinda. Kutokana na Taarifa ya Waziri Mkuu Pinda aliyowasilisha Bungeni Alhamisi tarehe 28 Agosti, 2008 ni wazi kuwa kuna kila dalili kuwa mwelekeo huo umeanza kuathiriwa, hivyo tunarudia tena kutaka Bwana Lowassa achukuliwe hatua kabla ya Bunge la Mwezi Novemba, 2008.

Bwana Lowassa akiwa Waziri Mkuu amethibitisha kwamba maneno yake mwenyewe kuwa alikiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995 na Sheria ya Makosa ya Udhibiti wa Uhujumu wa Uchumi wa nchi ya Mwaka 1984.

Bwana Lowassa alikiri kwamba alikuwa anafahamu kwamba Richmond ni kampuni ya kitapeli, lakini katika kipindi chote cha uongozi wake aliinyamazia hali hii na kwa kiasi kikubwa aliitetea kampuni hiyo mbele ya macho ya umma. Wakati wa Viongozi mbalimbali wa upinzani walipoweka bayana kwamba Richmond ni kampuni isiyo na uwezo, serikali ilitetea kampuni hiyo. Vyombo mbalimbali vya habari vilimtuhumu Bwana Lowassa mwaka 2006 na 2007 kama kiongozi wa Shughuli za serikali bungeni, kwamba alishiriki ‘kuwaziba midomo’ wabunge wa CCM wasijadili suala hili. Pia, ni Bwana Lowassa huyo huyo, alinukuliwa akiwa Arusha akiwataka watanzania wasiijadili kampuni ya Richmond baada ya mvua kuanza kunyesha. Kama Bwana Lowassa wakati wote huo alijua kama ni kampuni ya kitapeli kama anavyojaribu alivyojaribu kujitetea, uamuzi wake wa kuwaasa watanzania wasiijadili ulikuwa ni wa kulinda ufisadi ambao aliufahamu. Inashangaza pia ni Lowassa huyo huyo alisema alijua kuwa Richmond ni kampuni ya kitapeli; ni Lowassa huyo huyo alisema kwamba alishauriwa vibaya na watumishi wa umma aliowataja kuhusu uwezo wa Richmond; Ni Lowassa huyo huyo aliyesema kwamba alijua kuwa TANESCO chini ya Menejimenti ya Net Group Solution walitaka kuhujumu mchakato wa tenda na hivyo ‘kuwanyang’anya’. Lakini ni Lowassa huyo huyo aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye angeweza kuviagiza vyombo vya dola kumwezesha kuthibitisha ‘utapeli wa Richmond’; hivyo, maelezo ya sasa yanayotolewa kuhusu ushiriki wake yanaonyesha kuwa sasa kuna mwelekeo wa kumlinda.

Tunaendelea kushangazwa na Serikali na Bwana Lowassa kutumia utetezi wake kueleza tu nia yake ya kutaka mkataba wa Richmond usitishwe; nia ambayo kama ni kweli alikuwa na uwezo wa kuitekeleza na hakuitekeleza. Tunaitaka Serikali na Bwana Lowassa kuweka bayana ni kwa vipi Richmond ilipewa tenda hiyo na kwa shinikizo la nani. Bwana Lowassa anakwepa kuyazungumzia haya kwa kuwa anajua kabisa kwamba ni yeye aliyetumia madaraka yake vibaya alipokuwa Waziri Mkuu kwa kukiuka Sheria na Taratibu za Ununuzi kwa ‘kupora’ mchakato uliokuwa ukiendeshwa na TANESCO, ‘kuunda kamati yake’ na kuzisukuma mamlaka za ununuzi hali iliyopelekea Richmond kupewa tenda ili hali haikuwa na uwezo uliotakiwa. Ni uzembe huu ambao umelisababishia hasara taifa kwa kulipa shilingi milioni 152 kila siku kwa kampuni ya Dowans iliyohamishiwa mkataba wa kitapeli wa Richmond; na takribani bilioni 172 kwa ujumla ambazo taifa linawajibika kuzilipa kutokana na kukodisha mitambo hiyo. Hvyo tunarudia tena rai yetu ya kutaka fedha zilizozilipwa kizembe mpaka sasa kurejesghwa serikalini. Kwa vyovyote vile, jitihada za Bwana Lowassa za kuhamasisha ujenzi wa Sekondari Kata, na utumishi wake kama Waziri Mkuu katika kipindi cha miaka miwili, haviwezi kuzidi hasara aliyosababisha katika uchumi wetu kipindi chote tulichokosa umeme wa dharura na wala hailingani na hasara ambayo tunaendelea kuilipa kila siku iendayo kwa Mungu. Maamuzi haya ya Bwana Lowassa yanaendelea kuwaumiza wananchi wote ikiwemo wa Jimbo lake la Monduli ambao wanataabika kwa mzigo wa gharama za umeme.

Tunarudia tena kumkumbusha Rais Kikwete kwamba Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma inamtaka Rais kuhakikisha kwamba taratibu zinatengenezwa zitakazojenga maadili na kuongeza imani ya wananchi kwa uadilifu wa viongozi wa umma na katika taratibu za utoaji maamuzi ndani ya Serikali na katika sekta ya umma. Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma vile vile imeweka kanuni zinazotakiwa kuongoza utendaji wa viongozi wa umma: kwamba wanapokuwa madarakani, viongozi wa umma watakuwa waadilifu, wenye huruma, utulivu, umakini na watakaoendeleza viwango vya juu vya maadili ili kujenga na kuendeleza imani ya umma kwa uadilifu wa Serikali. Kuhusiana na utoaji wa maamuzi, viongozi wa umma watatekeleza wajibu wao kufuatana na sheria na kwa maslahi ya umma. Hivyo, taarifa ya Waziri Mkuu Pinda kutokueleza bayana hatua ambazo Bwana Lowassa ameshachukuliwa au atachukuliwa ni ishara kuwa kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa wakati akizungumza na Wazee wa CCM mkoani Dar es Salaam kwamba Bwana Lowassa amepata tu ‘ajali ya kisiasa’, na kumsifu kwa utumishi wake imechangia kumlinda mhusika huyu mkubwa katika sakata zima la RICHMOND. Vijana wa CHADEMA tulitarajia kuwa, baada ya Bwana Lowassa kukiri mwenyewe hadharani kuhusu uzembe wake na matumizi mabaya ya madaraka Rais Kikwete angelekeza hatua za kuchukuliwa dhidi yake badala ya kuendelea kumpamba kama “shujaa wa uwajibikaji’, kinyume na hayo tutaamini kwamba serikali yake inaendeshwa kwa ‘ubia wa kulindana’. Aidha tunarudia kutoa rai kwamba Rais Kikwete kuwafukuza kazi watumishi wote wa umma waandamizi ambao wametajwa na Bwana Lowassa kushiriki uzembe na matumizi mabaya ya madaraka; watumishi ambao walitajwa pia na Kamati Teule ya Bunge lakini mpaka sasa wanaendelea kutumikia nafasi zao mbalimbali. Kwa kuwa Waziri Mkuu Pinda ameshatangaza kwamba kwa wale wateule wa Rais, Kamati yake imeshapeleka suala zima kwake, tunategemea Rais atachukua hatua za haraka ili kuonyesha mfano kwa viongozi wengine wa chini yake wanaotarajiwa kuchukua hatua kwa watumishi wa chini.

Kadhalika tunapenda kuvikumbusha tena vyombo vya dola kwamba Sheria ya Udhibiti wa Makosa ya Kuhujumu Uchumi ya mwaka 1984 inatamka makosa yafuatayo kuwa baadhi ya makosa ya kuhujumu uchumi ni pamoja na yale yote yenye kusababisha hasara kwa mamlaka ya Serikali. Pia Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007 inatamka kuwa ubadhirifu na/au ufujaji wa mali ya umma unaofanywa na watumishi wa umma na Matumizi mabaya ya madaraka kwa ajili ya manufaa binafsi, ni sehemu ya ufisadi. Bwana Lowassa alithibitisha kwamba maneno yake kwamba wapo viongozi waandamizi wa Serikali ambao amewataja kwa majina wamefanya maamuzi ya kifisadi, kitendo chake cha kunyamazia ufisadi huo- kinafanya iwe vigumu kwa yeye kutenganishwa na tuhuma za ufisadi zilizomo katika mchakato mzima wa kupewa tenda kwa kampuni ya Richmond na mambo yote yaliyotokea baada ya Mkataba huo kuhamishiwa kwa kampuni ya Dowans.

Aidha tumefadhaishwa na Taarifa ya Waziri Mkuu Pindi kwamba kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na Baadhi ya Mawaziri ilikuwa ni ishara ya hatua ambazo serikali imechukua kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu suala husika. Tunarudia kukumbusha kwamba toka sakata la Richmond lilipoanza zaidi ya mwaka mmoja uliopita tulimtaka Bwana Lowassa kujiuzulu kulinda heshima yake lakini alikaidi na kuitetea kampuni ya Richmond. Uamuzi wa yeye kujiuzulu baada ya kashfa yote kuwa hadharani, umesaidia tu kuilinda serikali ya CCM lakini katu hauwezi kumpatia heshima ya uwajibikaji na wala hakuwezi kuwa ishara ya kwamba Maazimio ya Bunge yameshatekelezwa.

Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), kwa taarifa hii tunarudia kukemea jitihada zozote za kumlinda na kumtangaza Lowassa kuwa shujaa katika taifa letu kwani hali hii ikiachwa kuendelea inatoa mfano mbaya kwa vijana wa Tanzania. Tusingependa kwa namna yoyote katika taifa letu, mtuhumiwa wa ufisadi aliyetajwa pia katika orodha ya mafisadi(list of shame) kulindwa na kuenziwa kama shujaa wa Taifa letu kwani ni kuharibu maana nzima ya ushujaa katika uwajibikaji.

“Inasikitisha kwamba vijana wezi wadogo wadogo wakijazana magerezani. Vijana wamachinga kuendelea kukosa mitaji na maeneo ya kufanyia biashara; wanafunzi wa elimu ya juu wakipandishiwa ada na wengine kukosa mikopo- huku fedha za walipa kodi zikiendelea kuteketea kwa ufisadi na watuhumiwa wa ufisadi wakiendelea kutamba hadharani. Hali hii ikiachwa, itaharibu utawala wa sheria na kuleta matabaka katika taifa letu. Vijana tusingependa kuona nchi yetu inatumbukia kwenye migawanyiko kwa sababu ya kuwalinda watu wachache kwa kisingizio cha haki za binadamu”

Imetolewa tarehe 31 Agosti 2008 safirini Kenya na:

John Mnyika

Mkurugenzi wa Vijana

0754694553