Thursday, July 31, 2014

Kuhusu uongozi mpya wa wilaya ya CHADEMA Ubungo

Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine (wa kanza kushoto) akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
UONGOZI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya kichama Ubungo unatarajiwa kujulikana Agosti 3, 2014 baada ya uchaguzi wa ngazi za chini katika wilaya hiyo kukamilika. 

Mbali na viongozi wa wilaya hiyo kujulikana siku hiyo, pia chama hicho kimeeleza kuwa, kimejiandaa vema kuwadhibiti mamluki wasijipenyeze katika uongozi huo. 

Hayo yalibainishwa na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine, wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi wa ngazi za msingi, matawi na kata. 

Nafasi zitakazowaniwa ni ya mwenyekiti, katibu, katibu mwenezi na mhazini na kwamba, kwa ngazi ya mabaraza ni vijana, wazee na wanawake. 

Monday, July 28, 2014

Mnyika ataka matengenezo ya barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni yaharakishwe

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika amemtumia mjumbe Meya wa Manispaa ya Kinondoni kutaka afuatilie kwa karibu matengenezo ya Barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni (Barabara ya Mlandizi) kuharakishwa.

Mbunge amechukua hatua hiyo baada ya kupita katika barabara hiyo kuanzia maeneo ya Sinza Kijiweni-Mtogole hadi Makanya na kubaini kwamba bado ukarabati haujaanza na hali ya barabara ni mbaya.

Mnyika amewasiliana pia na Mkurugenzi wa Halmashauri kutaka Ofisi yake itoe taarifa kupitia vyombo vya habari tarehe ngapi matengenezo hayo yataanza na lini yanatarajiwa kumalizika.

Mnyika amekumbusha kwamba pamoja na kero ambazo wananchi wanapata hivi sasa Serikali inapaswa kutambua kwamba barabara hiyo ni muhimu katika kupunguza msongamano kwenye Barabara ya Morogoro na inapaswa kupewa kipaumbele wakati huu ambapo ujenzi wa mradi wa mabasi ya haraka (DART) unaendelea na hivyo kuhitajika kwa barabara mbadala.

Sunday, July 20, 2014

Mkutano wa naibu waziri wa maji waingia dosari katika kata ya Goba.


Mnyika amnusuru Waziri Makala

16 Julai, 2014 Na Abdallah Khamis

Naibu Waziri wa Maji, Amos MakalaMBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemnusuru Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala asiendelee kuzomewa na wananchi wakati wa  ziara yake ya ukaguzi wa miundombinu ya maji jimboni humo.
Mapema wanachama wa CCM wakiwa na bendera zao, walionekana kupangwa ili kumzomea Mnyika ambaye hata hivyo hakuwajali, badala yake aliendelea kuhutubia mkutano huku Makala akionekana kufurahishwa na hali hiyo.
Mnyika alieleza jinsi alivyowapigania wakazi wa Kimara Mavurunza na maeneo mbalimbali ya jiji kupata maji pasipo kujali itikadi zao za vyama.
Alisema ziara hiyo ya naibu waziri ni matokeo yake ya kumbana Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, pamoja na watendaji wa Kampuni ya kusambaza maji ya Dawasa kuhakikisha maji yanapatikana kwa wakazi wa Dar es Salaam.

CCM,Chadema wafanya vurugu ziara ya Makalla, Mnyika

Na Mary Geofrey 16th July 2014
Print
Ujumbe ulioongozana na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ukiwa ndani ya tenki la maji lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi jana.
Wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana walifanya vurugu katika ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla na Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika ya kukagua miradi ya maji katika jimbo hilo.

Mbali na kukagua miradi ya maji, Makalla na Mnyika alitumia ziara hiyo pamoja na kuzungumza na wananchi juu ya mipango na mikakati ya serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa maji jimboni humo.

Vurugu hizo zilianza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mavurunza, Kata ya Kimara, baada ya Mnyika kusimama na kutaka kuzungumza na wananchi kuhusu ujio wa Makalla pamoja na juhudi alizozifanya za kuhakikisha maji yanapatikana.

Baada ya Mnyika kusimama wafuasi wa CCM walianza kumshambulia kwa maneno ya kumtaka kuwa muda wake wa kukaa katika jimbo hilo umekwisha na kwamba, hana kazi nyingine anayofanya zaidi ya kutoa hoja bungeni na kuomba mwongozo wa Spika.

Waziri anusurika kichapo


Imeandikwa na Sharifa Marira

*Aondolewa chini ya ulinzi baada Chadema, CCM kuzusha vurugu

*Ni baada ya kudaiwa kuingiza u-CCM katika ziara ya kiserikali


KITENDO cha Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, kumkaribisha Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge, kusalimia wananchi kwenye mkutano wa kiserikali, jana kilizua balaa na kulazimisha nguvu za dola kuingilia kati kumnusuru mteule huyo wa Rais.

Tafrani hiyo ilizuka jana mchana huko Goba, wakati Makalla, ambaye yupo kwenye ziara ya siku nne kukagua miradi ya maji jijini Dar es Salaam, alipokuwa katika mkutano wa mwisho wa hadhara kwa siku hiyo.

Kitendo cha kada wa CCM, Madenge, kuitwa jukwaani, hakikuwapendeza wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwapo kwenye mkutano huo, kwa madai kuwa huo haukuwa mkutano wa kisiasa, ndipo wanachama hao walipokumbana na wenzao wa CCM na kuzusha vurugu kubwa zilizodumu kwa takriban dakika 30.

Habari Picha: Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Jimbo la Ubungo

ZIARA KATA YA KIBAMBA







Tukikagua ujenzi wa tanki la maji katika kata ya Kibamba


John Mnyika, Mbunge wa Ubungo akaiwa amebebwa na wafuasi wa chama chake wakati akiingia eneo la mkutano Kibamba




Diwani wa Kata ya Kibamba akizungumza jambo la Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla


Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia wananchi wa kata ya Kibamba


Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo wakiondoka katika eneo la tanki-Kibamba

ZIARA KATA YA KIMARA


Naibu Waziri wa Maji Amos Makalla, akimsikiliza kiongozi wa ujenzi wa Tanki la maji lililopo Kimara jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika.


Tanki hili litavunjwa na kujengwa jipya





Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza na vyombo vya habari katika ziara hiyo ya kukagua miradi ya maji kata zilizopo Jimboni Ubungo

MKUTANO NA WANANCHI KATIKA UWANJA WA SEKONDARI YA MAVURUNZA


Diwani wa Kimara Pacal Manota, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Sekondari ya Mavurunza


Askari Polisi akiwambeleleza wanaCCM kusikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa meza kuu katika mkutano uliofanyika uwanja wa Sekondari Mavurunza


Wakutanapo Chadema na CCM 


John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza katika mkutano huo na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla uwanja wa Sekondari Mavurunza





Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akizungumza katika mkutano wa hadhara








Katika hati hati ya kutaka kunusuru fujo zilizoanza kutokea katikati ya mkutano wa hadhara







Ujumbe wa wananchi kwa njia ya mabango





Polisi akijaribu kuwasihi wanaCCM kutulia ili mkutano uweze kuendelea


WanaCCM na WanaCHADEMA akutanapo


Ujumbe katika mabango












Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika tukijaribu kuwasihi wananchi toka katika pande zote za vyama kutulia ili mkutano uweze kuendelea









Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akijaribu kuwatuliza Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota














Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu. Huku Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akiendelea kuwasihi Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota


Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu


Shukrani kwa picha: Blogu ya Mzuka Kamili (www.mzukakamili-mzuka.blogspot.com)



Tuesday, July 8, 2014

Mnyika adai kutishiwa maisha

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amewaomba wapiga kura wake kumuombea kila siku kutokana na madai kuwa amekuwa akiwindwa na watu wanaotishia uhai wake.
Mnyika alitoa kauli hiyo juzi jioni katika eneo la Mbezi mjini Dar es Salaam, wakati akihutubia mkutano wa hadhara.
“Nimekuwa nikizungumza mambo mengi ninapokuwa bungeni Dodoma, hasa ninapowatetea wananchi na wapiga kura wangu, lakini kuna watu hawafurahishwi kabisa…sasa wamefikia hatua ya kunitishia maisha yangu.

Tuesday, July 1, 2014

Maghembe awasilisha nyaraka za kuhusu Mnyika

Na Mary Geofrey

Prof. Jumanne Maghembe, Waziri wa Maji
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, amepokea barua kutoka kwa Katibu wa Bunge ikimjulisha kwamba Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, hatimaye amewasilisha nyaraka na ripoti za utekelezaji wa miradi ya maji katika Jiji la Dar es Salaam.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Katibu Msaidizi wa Mnyika, Aziz Himbuka, inasema kuwa taarifa hiyo imepelekwa katika Ofisi ya Mshauri Mkuu wa Mambo ya Sheria wa Bunge ili iweze kusomwa na hatua zitakazohitajika zichukuliwe.

Alisema Mnyika ataanza kazi ya kuzipitia taarifa hizo katika Ofisi Kuu ya Bunge Dodoma na baada ya kazi hiyo atarejea kuanza ziara ya kikazi jimboni kwake kuanzia mwanzoni mwa mwezi huu (Julai), 2014.

Mnyika anatarajia kufanya ziara katika kata zote 14, ambayo pamoja na mambo mengine atakagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ya maji.