Monday, July 24, 2017

24 July: Ziara ya Ukaguzi wa Miradi katika Kata zote


Mbunge Wa jimbo la Kibamba Mh John John Mnyika leo tarehe 24/07/2017amefanya ziara ya kukagua miradi iliyofadhiliwa na Mfuko Wa Jimbo katika Kata zote sita zinazounda Ji mbo hilo ambazo ni Kata ya Saranga, Goba, Mbezi, Msigani, Kwembe na Kibamba.

Miradi hiyo ambayo ni vyoo vya Shule ya secondari Mpigimagohe , Kivuko cha Kibungobungo Kibamba, Ofisi ya Selikaliya mtaa Kinzudi Goba, Simtank Shule ya msingi msakuzi pamoja na fedha zilizoelekezwa kwenye vikundi vya ujasiliamali wanawake na vijana kwaajili ya kukuza mitaji yao.

Pia Mhe Mbunge aliwaagiza watumishi Wa Manispaa ya Ubungo kukamilisha miradi ambayo haijakamilika kwa wakati  ili kufikia malengo yaliyo kusudiwa  kupitia fedha za mfuko huo.







No comments: