Saturday, March 24, 2012

Katizo la umeme DSM, maeneo yatakayokatizwa Jimbo la Ubungo

Jumapili tarehe 25 Machi kutakuwa na katizo la umeme kwenye baadhi ya maeneo ya DSM kuanzia saa 2 Asubuhi mpaka  10 jioni.
Kwa Jimbo la Ubungo katizo litahusu maeneo yafuatayo: Sinza, Goba, Ubungo Kisiwani, Mabibo Jeshini,  Makuburi (External, Barabara ya Mandela, Mabibo Hosteli, Kibangu).
Hivyo usishike waya wowote uliokatika badala yake toa taarifa kwa ofisi za kanda za TANESCO Kinondoni Kaskazini (Mikocheni):0716768584; 0784768584 au Kinondoni Kaskazini (Magomeni): 0768985100; 0784271461; 0784078837 au 0788379696.
Sababu zilizotajwa na TANESCO: Kuunga line ya msongo mkubwa wa 132kV katika kituo cha kupoozea umeme Ubungo na Kufunga LBS kwenye njia ya FZ3-1&2 na U1 ili kurahisisha uzimaji wa line wakati inapopata hitilafu na kurahisisha kugundua eneo la hitilafu kwa urahisi na haraka. Maslahi ya Umma Kwanza.

No comments: