Monday, April 9, 2012

Mkutano wa Manzese na masuala ya kuyawasilisha bungeni

Nashukuru wananchi mliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara Manzese Bakhresa; kura mlizopiga za wazi kuwa hata uchaguzi ukirudiwa leo mtanichagua kwa kura nyingi zaidi zimenipa imani ya kuwatumikia kwa nguvu zaidi. 

Asanteni kwa kuchangia 193,000 kwa ajili ya kesi ya kupinga ushindi wetu ikiwa ni ishara ya kuwa mko tayari kuendelea kulinda kura mlizopiga kwa hali na mali. 

Nitafikisha pia ushauri wenu kwa CHADEMA kuhusu umuhimu wa kuharakisha kwenda vijijini, kujijenga ngazi ya chini kwa kuwa na matawi na ofisi na kuanzisha chombo cha habari cha chama.

Mkutano wa Bunge unaanza kesho, nitatimiza wajibu mlionituma wa kuwawakilisha kwa kuwasilisha masuala mliyonieleza: Hoja Binafsi kutaka hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji; Ombi la wazalishaji wadogo na wafanyabiashara ndogondogo kwa ajili ya kuchangia katika kuongeza ajira na kukuza uchumi wa nchi; Swali juu ya hatma ya kupandishwa hadhi kwa barabara kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya pembezoni na kupunguza msongamano. 

Naendelea kukaribisha maoni yenu kuhusu miswada minne ya sheria inayotarajiwa kujadiliwa katika mkutano huu wa bunge. Maslahi ya umma kwanza.

No comments: