Saturday, April 7, 2012

Rambirambi ya Kanumba na matukio mengine ya leo

Natoa pole kwa wasanii na wapenzi wa tasnia ya filamu nchini kwa kifo cha ghafla cha Steven Kanumba, nimetoka nyumbani kwa marehemu Sinza Jimboni Ubungo kutoa rambirambi; tutaendelea kuwa pamoja kwa kadiri mipango ya mazishi itavyopangwa.


Kwa sasa naelekea kwenye mkutano wa hadhara Manzese Bakhresa saa 10 Jioni, nitatumia fursa hiyo kujibu maswali ya wananchi na pia kupokea masuala ya kuzingatia katika uwakilishi kwenye mkutano wa saba wa bunge utaotarajiwa kuanza tarehe 10 Aprili 2012.

Nawatakia Wazanzibar na Wabara wote heri katika siku ya kumbukumbu ya Mzee Karume. Maslahi ya Umma Kwanza.

No comments: