Monday, January 6, 2014

Kauli kuhusu Uongo wa Waziri Profesa Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ametoa kauli za uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 ndani na nje ya Bunge kuhusu utafiti na uendelezaji wa gesi asilia.

Waziri Muhongo alijibu uongo kwamba hafanyi kazi kwa vyombo vya habari nilipohoji kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge ya kuanzia Novemba 2011 ya kushughulikia ufisadi uliothibitika katika mapato ya mauzo ya gesi na udhaifu mwingine uliobanishwa.

Aidha, Waziri Muhongo aliahidi uongo alipounda alipounda kamati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) na kuahidi kwamba kamati hiyo itafanya mapitio ya mikataba na kuandaa ripoti itakayowezesha mikataba mibovu ya utafiti wa mafuta na gesi asili kufanyiwa marekebisho. Hata hivyo, Wizara ya Nishati na Madini baadaye iliyoa taarifa kwamba matokeo ya ripoti hiyo hayatatumika kwa ajili ya mikataba iliyopita bali mikataba ijayo.

Pia, Waziri Muhongo aliahidi kwamba kungekuwa na uwazi kuhusu ripoti hiyo; hata hivyo mara baada ya kamati kumkabidhi ripoti ameamua kuifanya kuwa siri hata baada ya kuomba kupewa nakala ya ripoti hiyo kwa mujibu wa masharti ya sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge.

Mwaka huu wa 2014 nitatoa kwa umma maelezo ya uongo wa Waziri Muhongo mfululizo kuanzia sasa mpaka atakapoomba radhi kwa umma na kuchukua hatua zinazostahili kuhakikisha maslahi ya nchi na matakwa ya wananchi yanazingatiwa kuhusu utafiti na uendelezaji wa gesi asilia.

Katika kauli itayofuata nitaeleza uongo wa Waziri Muhongo kuhusu zabuni ya nne ya kunadi vitalu vya utafiti wa gesi asilia ambao ameueleza kwa nyakati mbalimbali bungeni, katika Kongamano juu ya Rasilimali lililoandaliwa na UDASA katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na kupitia taarifa kwa umma ilivyotolewa kwenye vyombo vya habari tarehe 30 Disemba 2014.

Imetolewa na:
John Mnyika (Mb)
6/1/2014
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini

1 comment:

Anonymous said...

Mimi si mkazi wa DSM lakini nimeishi DSM nikiwa chuo, mawazo yako ni mazuri lakini yamejikita haswa kwenye jimbo lako kuliko maeneo mengine. nasauri hivi:-
1. Kigamboni iwe Wilaya- Manispaa
Nimependekeza Kigamboni kwa sababu ya kijiographia

2. Tegeta iwe Wilaya - Manispaa
Kwa sababu ya upatikanaji wa huduma za kiutawala, Wnanchi wa Bunju kuja kupata huduma Magomeni kwangu naona sio huduma bali ni kero hivyo wasogezewe at list Tegeta isitoshe hivi saasa watu wengi wapo huko na mahitaji ya huduma yanahitajika.

3. Kibamba iwe Wilaya - Manspaa
hii itasaidia badala watu wote kuelekea Uande mmoja wakati wa asubuhi na jioni sasa wataelekea Kibamba kufuata huduma hivyo kupunguza foleni, pia Kibamba kuna maeneo yanayofaa ujenzi wa Maofisi

Nihayo tu kwa leo