Thursday, February 20, 2014

Rasilimali na mchakato wa kuandika Katiba Mpya

Kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini natoa mwito kwa wadau wote wa masuala ya rasilimali kuzingatia kwamba rasimu ya katiba haijazingatia masuala ya msingi kuhusu haki ya wananchi kumiliki na kunufaika na rasilimali za nchi. Hatua hii ni kinyume na mapendekezo niliyoyatoa bungeni tarehe 22 Mei 2013 na maoni yangu niliyoyatoa mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba pamoja na maoni yaliyotolewa na wadau wengine mbalimbali. 

Katika hotuba yangu ya Bungeni nilitaka Serikali isitishe kuendelea kunadi leseni za vitalu vya gesi mpaka kwanza mchakato wa katiba mpya ukamilike na pawepo sera na sheria zitazoongozwa na katiba mpya. Nilieleza kwamba katiba mpya inapaswa kuwa na ibara mahususi ya haki za wananchi kuhusu rasilimali ikiwemo ardhi, madini, gesi, mafuta, maji, misitu na maliasili zingine. Hata hivyo, katika rasimu ya katiba sura ya nne sehemu ya kwanza inayohusu haki za binadamu hakuna haki yeyote iliyotolewa kwa wananchi kuhusu kumiliki na kunufaika na rasilimali. Nitapendekeza kwa Bunge Maalum ibara mahususi kurekebisha udhaifu huo

No comments: