Monday, August 27, 2012

Nape amezidi kuibua vioja!!


Leo Nape Nnauye amekwepa kujibu hoja ameibua vioja. Kwa kuwa amekataa kuomba radhi, CHADEMA kitamburuza mahakamani kwani madai yake ya uongo kwa CHADEMA imepata mabilioni toka nje hayawezi kuwa na ushahidi wa ukweli. Nape na CCM wajibu hoja kwa kuwa Dr. Slaa alitaja mpaka namba ya silaha, CCM ilipaswa kueleza iliingiaje nchini na suala ambalo Nape hajui kwa hiyo tunasubiri jibu la Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete. CCM huwa wanatoa madai ya uongo dhidi ya CHADEMA ushahidi ni hukumu ya kesi ya Igunga ambapo ilithibitika Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama alizusha kuwa CHADEMA imeingiza magaidi toka nje ya nchi. Kati ya CHADEMA na CCM ni chama kipi kimepoteza mvuto jibu wanatoa wananchi wanavyounga mkono vuguvugu la mabadiliko (M4C) kwa hali na mali kwa kiwango cha CCM kufanya siasa chafu.

Baada ya Dr.Slaa kufichua silaha za CCM, leo wametumia za polisi Morogoro. Umma umeweka hofu pembeni, mkutano umejaa name naelekea huko tukawavue magamba. Peopleeee……..ss!!!

John John Mnyika
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi
27 Agosti, 2012

1 comment:

MathiasLyamunda said...

Peeeeeeeeoplesss.....
Hakuna cha kutuzuia mbele yutasonga daima! Kawafungueni macho wana morogoro!