Monday, August 27, 2012

Tunapaswa kuendelea kushiriki vuguvugu la mabadiliko!


Nimetoka kwenye kikao cha RCC. Itachukua muda  kwa uozo aliouanika kwenye UDA, kituo cha mabasi Ubungo, soko la Karikoo, fidia ya wahanga wa mabomu Gongo la Mboto, EAMTCO kushughulikiwa!

Nchi hii ina uozo sehemu nyingi hali inayohitaji mabadiliko ya utawala ili kuharakisha maendeleo. Kadiri tunavyojifungia DSM na kuleta maendeleo kidogo mjini, huku vijijini wakididimia kwenye umaskini ndivyo watu wengi hukimbilia DSM na vijana kukosa ajira na miundo mbinu ya maji, barabara na mengine mengi kuzidiwa DSM. Hatimaye DSM nayo itaendelea kuwa jiji lenye kero. Kwa hiyo, tunao wajibu pamoja na kuisimamia serikali kwa maendeleo ya DSM, tuna wajibu pia wa kuunganisha nguvu kuwezesha vuguvugu la mabadiliko vijijini. Leo naelekea Morogoro, kesho nitakuwa Iringa na kesho kutwa nitarejea DSM kuendelea na kazi za maendeleo jimboni Ubungo kwa mwezi mzima wa Septemba.

Maslahi ya Umma Kwanza.

John John Mnyika
Jimboni Ubungo
27 Agosti, 2012

No comments: