Thursday, February 27, 2014

Rasimu ya Pili ya Kanuni za Bunge Maalum hizi hapa; na masuala yanayohitaji kuungwa mkono ni haya:

Itakumbukwa kwamba tarehe 19 Februari 2014 Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum Pandu Kificho aliteua Kamati ya Wajumbe ishirini yenye uwakilishi wa makundi yote yanayounda Bunge Maalum kwa ajili ya kumshauri kuhusu Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalum.

Rasimu ya kwanza ya Bunge Maalum iliandaliwa na Kamati ya Maandalizi chini ya Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (nakala yake niliwapa hapa: http://goo.gl/hEI4aw ).

Kazi ya mjumbe ni kuwakilisha na kuwasilisha; katika kutekeleza wajibu huo, jana 26 Februari 2014 tulikuwa na Semina ya Bunge Maalum kuhusu Rasimu ya Pili ya Kanuni za Bunge Maalum toleo la 2014. 

Katika mjadala wa jana niliunga mkono mapendekezo ya rasimu katika sehemu ya nne kuhusu kupunguzwa kwa mamlaka na madaraka makubwa ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum, tofauti na rasimu ya kwanza; sasa maamuzi ya mwenyekiti hayatakuwa ya mwisho. Mjumbe asiporidhika anaweza kukata rufaa na pia rasimu sasa inapendekeza kwamba mwenyekiti au makamu wanaweza kuondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani.

Niliunga mkono kuruhusiwa kwa utaratibu wa kuwasilisha Taarifa ya Maoni Kinzani (dissenting opionion); hii ni kwa sababu rasimu ya kwanza haikuwa na utaratibu wa uwasilishaji bungeni wa hoja za wabunge, hoja zote ilikuwa ni kamati. Njia pekee ya kuwezesha mawazo mbadala kuweza kufika katika ukumbi wa Bunge kwa ukamilifu ukiondoa michango ya wabunge ni kupitia Taarifa za Maoni Kinzani.

Sunday, February 23, 2014

Pata nakala ya rasimu ya kanuni za Bunge Maalum la Katiba hapa, na shiriki mkutano wa mtandaoni leo tuijadili kutoa maoni na mapendekezo

Ratiba na utaratibu wa Bunge Maalum la Katiba haujatuwezesha kurejea kupata maoni ya mliotutuma au walau kuwekwa utaratibu wa Mwenyekiti wa Muda kuitisha mkutano wa kusikiliza umma/wadau (public/stakeholders hearing) hapa Dodoma.

Nilitoa pendekezo hili kwa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge na kwa wadau; rejea: http://mnyika.blogspot.com/2014/02/kwanini-ni-muhimu-tushirikishe-wananchi.html na http://www.ippmedia.com/frontend/?l=64919

Hata hivyo, mjadala wa bungeni unaanza kesho na hatimaye kanuni kupitishwa kwa kile ambacho vyanzo vyangu vimenidokeza kuwa msimamo wa wenye madaraka ni kwamba “mamlaka ya kujitungia kanuni ni ya bunge maalum lenyewe, kutunga kanuni ni suala la ndani la wajumbe wenyewe”.

Kutokana na ukuu na upekee wa kanuni hizi katika uendeshaji wa Bunge Maalum, ni wazi kasoro katika kanuni zitaacha mianya ya maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. 

Aidha, yapo mambo katika rasimu ya kanuni yanayohusu haki, kinga na maslahi ya wajumbe wa Bunge Maalum ambayo katika mizania ya utawala bora ni vyema katika kuyatunga maoni na mapendekezo ya wadau wengine wa nje ya Bunge la Maalum yakatolewa.

TAARIFA KWA UMMA: SAKATA LA FIDIA YA ENEO LA MLOGANZILA

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika ameendelea kufuatilia kuhusu fidia ya ardhi ya wananchi wa kata ya Kwembe waliohamishwa baada ya kulipwa fidia ya maendelezo pekee kupitisha ujenzi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.

Kwa upande mwingine, Mbunge Mnyika ameendelea pia kuhoji katika mamlaka mbalimbali juu ya kauli za viongozi wa Serikali kutamka kwamba eneo hilo lipo katika Mkoa wa Pwani badala ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam.

Tarehe 19 Januari 2014 Mbunge Mnyika alifika katika kata ya Kwembe na kukutana na wananchi kusikiliza malalamiko yao na mara baada ya mkutano huo alizikutanisha kamati mbili zinazofuatilia suala hilo.

Kufuatia hatua hiyo, Mbunge Mnyika aliwasiliana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwakumbusha kutekeleza ahadi zao za kuupatia ufumbuzi mgogoro huo kufuatia hatua ya mbunge kuhoji suala hilo bungeni kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2011 mpaka 2013. (Baadhi ya rejea kutoka Kumbukumbu Rasmi za Bunge-Hansard zimeambatanishwa).

Saturday, February 22, 2014

Maoni yangu kuhusu matokeo ya kidato cha nne wa mwaka 2013


Maoni yangu kuhusu matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne wa mwaka 2013 yaliyotangazwa na kuelezwa kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 15.17 yamedhihirisha tahadhari niliyotoa kuhusu mabadiliko ya viwango vya ufaulu yaliyotangazwa na Serikali tarehe 30 Oktoba 2013.

Serikali kwa barakoa (veil) ya kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) imeamua kulificha taifa juu ya Matokeo Mabaya ya Sasa (Bad Results of Now). Hivyo, wachambuzi wa masuala ya elimu wanapaswa kutoa takwimu za matokeo yangekuwa namna gani iwapo viwango vya awali vya ufaulu vingetumika ili nchi ijue hali halisi kwa manufaa ya wananchi.

Aidha, natoa mwito kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuweka wazi kwa umma ripoti za uchunguzi zilizoundwa kuwezesha wananchi kuihoji Serikali iwapo kupanda huko kwa ufaulu ni matokeo ya kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunza au ni kiini macho cha mabadiliko ya wigo wa alama na madaraja?

Ukweli ni kuwa hali ya mazingira ya kujifunza na kujifunzia katika shule nyingi za msingi na sekondari hasa za umma sio nzuri kutokana na kutokuwa na vitabu vya kutosha, maabara za kutosha, waalimu wenye sifa wapo wa kutosha na kuboresha maslahi ya waalimu ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa siku nyingi.

Thursday, February 20, 2014

Rasilimali na mchakato wa kuandika Katiba Mpya

Kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini natoa mwito kwa wadau wote wa masuala ya rasilimali kuzingatia kwamba rasimu ya katiba haijazingatia masuala ya msingi kuhusu haki ya wananchi kumiliki na kunufaika na rasilimali za nchi. Hatua hii ni kinyume na mapendekezo niliyoyatoa bungeni tarehe 22 Mei 2013 na maoni yangu niliyoyatoa mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba pamoja na maoni yaliyotolewa na wadau wengine mbalimbali. 

Katika hotuba yangu ya Bungeni nilitaka Serikali isitishe kuendelea kunadi leseni za vitalu vya gesi mpaka kwanza mchakato wa katiba mpya ukamilike na pawepo sera na sheria zitazoongozwa na katiba mpya. Nilieleza kwamba katiba mpya inapaswa kuwa na ibara mahususi ya haki za wananchi kuhusu rasilimali ikiwemo ardhi, madini, gesi, mafuta, maji, misitu na maliasili zingine. Hata hivyo, katika rasimu ya katiba sura ya nne sehemu ya kwanza inayohusu haki za binadamu hakuna haki yeyote iliyotolewa kwa wananchi kuhusu kumiliki na kunufaika na rasilimali. Nitapendekeza kwa Bunge Maalum ibara mahususi kurekebisha udhaifu huo

Kwanini ni muhimu tushirikishe wananchi katika kutunga kanuni za Bunge Maalum

Kwenye kikao cha juzi cha Bunge Maalum nilipendekeza umuhimu wa suala la ushirikishwaji wa wananchi na wadau mbalimbali katika kutengeneza kanuni (Soma hapa: http://goo.gl/b0nQVA) . Wapo wenye mtazamo kwamba kanuni kwa kuwa ni za Bunge Maalum, kuandaa na kupitisha rasimu hiyo ni suala la wajumbe wenyewe pekee; hakuna ulazima wa wadau wala umma kushirikishwa.

Hata hivyo, kwa uzito na unyeti wa kanuni zenyewe na kwa kuzingatia kwamba mjumbe anapaswa kuzingatia maoni ya aliyemtuma ni muhimu umma ujue na kushiriki.

Pia, izingatiwe kwamba Bunge Maalum linapoendelea upo wakati wadau na wananchi wanataka kufuatilia kuhakikisha maoni na maslahi yao yanazingatiwa na wajumbe wao.

Hivyo, ni muhimu kushirikishwa kupata kuwezesha kanuni kuruhusu fursa hiyo. Ni wajulishe tu kwamba rasiu ya Katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. Nitafanya uchambuzi wa vifungu hivyo vibovu na hatimaye nitawasilisha mapendekezo ya maboresho kwa Bunge Maalum.

Wednesday, February 19, 2014

Uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga: CHADEMA yamekea pingamizi CCM!

CHADEMA imemuwekea pingamiza mgombea wa CCM kwamba sio raia wa Tanzania. 

Kazi imeanza!

Mkakato wa Katiba Mpya: Wadau washirikishwe kutunga kanuni Bunge la Katiba

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amesema atawasilisha mapendekezo ya kutaka ratiba ya Bunge Maalumu la Katiba ibadilishwe, ili wadau washirikishwe kwenye mchakato wa kutunga kanuni za Bunge hilo.

Mnyika alisema hayo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.

Alisema ratiba iliyotolewa inaonyesha kwamba baada ya kusomwa kwa tangazo la kuitisha Bunge hilo na uchaguzi wa mwenyekiti wa muda, kazi ya kutunga kanuni itaanza.

Mnyika alisema kanuni ndiyo msingi wa kufikia mwafaka wa kuboresha rasimu ya Katiba badala ya kuchakachua na kwamaba ili zisitungwe kanuni mbovu ipo haja ya wadau wote wanaohusika na mchakato wa Katiba mpya ndani na nje ya Bunge kushiriki. 

“Nakusudia kuwasilisha mapendekezo kwamba ratiba ya Bunge ifanyiwe mabadiliko ili kuwapo na kikao cha kusikiliza umma (Public hearing), juu ya kanuni hizo ili mawazo ya wadau yazingatiwe katika maandaluzi ya kanuni kabla ya Bunge kupitisha azimio la kuridhia kanuni hizo,” alisema Mnyika.

Tafakari ya leo!


Tuwe wepesi wa kusikia si kusema wala kukasirika.

Tuwe watendaji sio wasikiaji tu.

Dini safi ni matendo mema.


-Funzo toka Yak. 1:19-27

Fursa kwa kijana kufanya kazi Ofisi ya Mbunge

Feb 2014 ni mwaka 1 toka nilipowasilisha Bungeni Hoja Binafsi ya kupendekeza Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka kuboresha upatikanaji wa Maji Safi na ushughulikiwaji wa Maji Taka katika jiji la Dar es Salaam. Soma hapa: http://goo.gl/Q770zm Natumia fursa hii kutangaza nafasi ya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini mafanikio na vikwazo kwa kijana wa ndani ya Jimbo la Ubungo (Mwanamke au Mwanaume) aliyetayari kufanya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini hatua za haraka juu ya suala la Maji ndani ya jiji la Dar es Salaam afike Ofisi ya Mbunge, Halmashauri ya Kinondoni.

John J. Mnyika
Mbunge wa Ubungo
19.02.2014

Tuesday, February 18, 2014

Hon. John Mnyika's witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly

IN THE EAST AFRICAN COURT OF JUSTICE
FIRT DIVISION
AT ARUSHA
REFERENCE NO.07 OF 2012
(In the matter of interpretation of Article 50 of the Treaty for the Establishment of the East African Community)
BETWEEN
ANTON CALIST KOMU………………….CLAIMANT
AND
THE HONOURABLE ATTORNEY GENERAL OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA…………………….......RESPONDENT


WITNESS STATEMENT OF JOHN MNYIKA

I, John Mnyika Member of Parliament of the United Republic of Tanzania for Ubungo Constituency, make the following witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly members:

I wrote a letter dated 8th February 2012 with reference no. OMU/BJMT/004/2012 to the Clerk of The Parliament of United Republic of Tanzania requesting amendment  to be  made in the third schedule of the Parliamentary Standing Orders (The East African Legislative Assembly Election Rules).

I made those proposals commensurate with the requirement of sections 3(3)(a) and (b) of the eighth schedule made under standing order 115 of the Parliamentary Standing Orders (2007 Edition).

I requested the Clerk to recall what transpired in the Election of East African Legislative Assembly that was conducted in the Parliament of the United Republic of Tanzania on the 2nd of November 2006. 

In that particular election complains arose and were raised that indicated the need for amendment of the East African Legislative Assembly Election Rules of the Parliament of the United Republic of Tanzania. I also drew to the attention of the Clerk that The East African Assembly had passed the EALA elections Act of 2011.

Monday, February 17, 2014

Mrejesho wa leo Februari 17: Jitihada za kuboresha barabara jimboni Ubungo na mengineyo

1. Barabara ya Goba-Mbezi Louis nawaomba wananchi wenzangu mfuatilie matengenezo yaliyoanza na kutoa mrejesho; lami kidogo nayo itaanza. Tuungane kupendekeza nyongeza bajeti hii

2. Barabara ya Malambamawili-Msigani naombeni tathmini ya matengenezo yaliyofanyika; ujenzi wa lami utaanzia kipande cha Kinyerezi-Kifuru. Kwa hii sasa ni hatua.

3. Barabara ya Bonyokwa-Mavurunza Kimara mwisho; nimewasiliana na Manispaa ya Kinondoni kukumbusha utekelezaji wa ahadi ya matengenezo. Majibu kesho.

4. Barabara ya Matete-Jeshini-Golani haikutengewa fedha KMC, nimewatumia ujumbe TANROADS wakishughilikia Msewe wasogee

5. Barabara ya Mavurunza-Golani-Msewe-Matete hali ya barabara ni tete. Nimewasiliana na diwani Pascal Manota na kumtumia posho ya leo kuweka mafuta grader. Ikiwa unatumia barabara za Mavurunza-Golani-Matete wasiliana na Diwani 0713792966 utuunge mkono sasa; mamlaka zingine nazo tunazifuatilia