Monday, July 24, 2017

24 July: Ziara ya Ukaguzi wa Miradi katika Kata zote


Mbunge Wa jimbo la Kibamba Mh John John Mnyika leo tarehe 24/07/2017amefanya ziara ya kukagua miradi iliyofadhiliwa na Mfuko Wa Jimbo katika Kata zote sita zinazounda Ji mbo hilo ambazo ni Kata ya Saranga, Goba, Mbezi, Msigani, Kwembe na Kibamba.

Miradi hiyo ambayo ni vyoo vya Shule ya secondari Mpigimagohe , Kivuko cha Kibungobungo Kibamba, Ofisi ya Selikaliya mtaa Kinzudi Goba, Simtank Shule ya msingi msakuzi pamoja na fedha zilizoelekezwa kwenye vikundi vya ujasiliamali wanawake na vijana kwaajili ya kukuza mitaji yao.

Pia Mhe Mbunge aliwaagiza watumishi Wa Manispaa ya Ubungo kukamilisha miradi ambayo haijakamilika kwa wakati  ili kufikia malengo yaliyo kusudiwa  kupitia fedha za mfuko huo.







Tuesday, July 18, 2017

Matengenezo ya haraka ya miundo mbinu-Kata ya Saranga

Jana Julai 17 Nilitembelea Kata ya Saranga na kujionea hali duni ya miundombinu ya barabara ambazo zimeharibika vibaya sana.

Kwa hatua ya awali nimekwishafanya mawasiliano na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo na Mkurugenzi wa Dawasco ili nao watembelee na kutuma watendaji kufanya matengenezo kwa haraka.

Nimetoa mwito, maeneo yote mabovu yawekwe kifusi lakini kwa hatua ya kudumu yawekwe slabu za zege kama ilivyofanyika kwenye baadhi ya maeneo kwenye barabara hiyo.

Muhimu: 
Ziara ktk kata zingine tano ndani ya Jimbo letu la Kibamba zinakuja!

John John Mnyika,
Mbunge wa Kibamba,
Julai 18, 2017

Mazishi ya Mzee Mchungaji Mwasiwelwa




Jana, Julai 16 niliungana na wananchi wenzangu wa King'ong'o na kwingineko kumpumzisha Mzee wetu, Mch. Mwasiwelwa-Baba wa Mwenezi wetu, Perfect.

Mwenyezi Mungu amjalie pumziko la milele. Aipe pia faraja na utulivu familia na wote ambao wameguswa na kuondokewa kwa Mzee wetu.

John John Mnyika,
Mbunge wa Kibamba,
Julai 18, 2017

Uzinduzi wa albamu mbili za Baraka Mwaijande katika Kanisa la KKKT Usharika wa Temboni

Mkuu wa Jimbo, Mch.Mwangomola na Mchungaji wa Usharika wa Temboni, Mch.Lusekelo 

Baraka na Mkewe

Kwaya ya vijana
Nikiwa na Paul Clement


Jumapili Julai 16: Nilibahatika kualikwa kushiriki uzinduzi wa albamu mbili za kumsifu Mungu za kijana Baraka Mwaijande katika Kanisa la KKKT Usharika wa Temboni , Jimbo la Magharibi-Dayosisi ya Mashariki na Pwani [ndani ya Jimbo letu la Kibamba].

Nilifurahi na kufarijika sana kushuhudia  vijana wakitumia vipaji vyao kumsifu Mungu.

Baraka pia alinigusa kiupekee sana kwa ndoto yake ya kujenga kituo cha kuhudumia watoto yatima. Anafanya harambee kutekeleza azma hii. Tumuunge mkono. Kwa wenye kutamani kusikia kazi zake mbili za kumsifu Mungu au kumuunga mkono wawasiliane nae moja kwa moja: 0715-189 911

Paul Clement, alinigusa sana na wimbo wake “Amenifanyia Amani”! Hakika ana kipaji cha kipekee.

Nimefurahi pia kuwa na Baba Wachungaji, Mkuu wa Jimbo-Mch. Mwangomola, na Mkuu wa Usharika-Mch. Lusekelo na wachungaji wengine.


Naamini kila mmoja anaweza kuwa chachu ya kuiboresha jamii yetu kwa kutumia vipaji/talanta tulizopewa na MUNGU vyema.

John John Mnyika,
Mbunge wa Kibamba,
Julai 17, 2017