Saturday, September 27, 2014

TAARIFA KWA UMMA

Katika Mkutano wa 14 Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.

Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa kwenye kamati zinazohusika;  Nne, ni upi wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Katika Mkutano wa 14 Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa kwenye kamati zinazohusika;  Nne, ni upi wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Ofisi ya Jimbo la Ubungo inawakumbusha vijana na wadau wote wa maendeleo yao kwamba kutokuwepo kwa chombo kinachowaunganisha vijana wote bila kujadili itikadi kufuatilia masuala ya maendeleo ya vijana  kunafanya Wizara mbalimbali za kisekta kutokuzingatia masuala yaliyokipaumbele kwa maendeleo ya vijana.
Mathalani, katika Mkutano huu wa Bunge katika Fungu la 65 la Wizara ya Kazi na Ajira Kitabu cha Nne Cha Miradi ya Maendeleo Kifungu cha 2002, pamoja na wabunge na vijana kupewa matumaini kwamba zimepitishwa bilioni tatu kwa ajili ya mikopo na mitaji kwa vijana ukweli ni kwamba fedha hizo zimepangiwa matumizi ambayo kusipokuwa na chombo cha kuyafuatilia kutakuwa na udhaifu, ufisadi na ubadhirifu kama ilivyojitokeza katika fedha za mifuko ya maendeleo ya vijana  kati ya mwaka 1993/1994 mpaka 2013/2014.
Kwa mujibu wa Kasma za Kifungu hicho cha 2002 cha Bajeti iliyopitishwa ya Fungu 65 Wizara ya Kazi na Ajira, fedha hizo zinazopaswa kuwa za mikopo na mitaji kwa vijana zitatumika milioni 700 kwa ajili ya kulipia utaalamu elekezi (consultancy fees) kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa vijana 200 tu; milioni 150 zitatumika kununulia magari Wizarani, milioni 60 zitatumika kwenye matangazo na orodha ndefu nyingine ya  matumizi yasiyo ya lazima ambayo kutokana na ufinyu wa muda sitaendelea kuyataja.
Aidha, katika mjadala wa bajeti hiyo wabunge waliweka bayana kwamba kiwango kinachotengwa katika Mifuko ya Maendeleo ya Vijana iwe ni kwa Serikali Kuu na hata Halmashauri ni kidogo ukilinganisha na uwezo wa nchi, mahitaji ya vijana na mafungu mengine yasiyo na matumizi muhimu yanavyotengewa fedha nyingi katika baadhi ya Wizara.
Hivyo, ili Baraza la Vijana la Taifa na Benki ya Vijana ambavyo ni vyombo muhimu kwa maendeleo ya vijana viweze kuanzishwa kwa wakati, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inamkumbusha Spika wa Bunge kuelekeza muswada binafsi uliokwisha wasilishwa kwa Bunge kwa kamati zinazohusika kwa ajili ya kuanza  kuujadili. Suala hili ni muhimu likapata majibu ya mapema ili muswada huo uweze kuwasilishwa Bungeni katika Mkutano wa 16 wa Bunge unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba mwaka 2014.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inatoa mwito pia kwa vijana na wadau wa maendeleo ya vijana kuingilia kati suala hili na kuisimamia Serikali kwa kuzingatia kwamba katika majumuisho ya Bajeti ya Wizara yenye dhamana ya vijana kwa mwaka 2013/2014 tarehe 21 Mei 2013 mkutano wa 11 kikao cha 30; Serikali ilitumia kisingizio kwamba ‘ni bunge la bajeti’ kukwepa kuwasilishwa kwa muswda Bunge. Hata hivyo, ahadi ya Serikali ya kuwasilisha muswada haikutekelezwa kwenye mikutano mitatu uliyofuatia ya 12, 13, 14 na 15; hivyo mkutano huu wa 16 ni muafaka kuwezesha maamuzi kufanyika kwa ajili ya maendeleo ya vijana nchini.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inaukumbusha umma kwamba Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa  Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007; hata hivyo Serikali imekuwa ikiwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera tajwa yanatekelezwa pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo ya vijana nchini.
Imetolewa tarehe 24 Septemba 2014 na:

Aziz Himbuka
Katibu wa Mbunge

Jimbo la Ubungo

Monday, September 8, 2014

Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) yakabidhiwa Komputa na Kasiki (safe) na Mbunge Mnyika

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika akikabidhi kompyuta na Kasiki (Safe) kwa Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) ikiwa ni sehemu ya milioni 10 za CDCF tulizotenga kwenye kuchochea vijana na wanawake kujiajiri.

Uzinduzi wa rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake,vijana na wenye ulemavu


John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo Akizindua rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake, vijana na wenye ulemavu katika uongozi uliofanywa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)

Monday, September 1, 2014

Mnyika akabidhi vyerahani kutimiza ahadi ya ajira kwa wanawake


Mnyika akibidhi vyerehani na mashine kudarizi kwa VICOBA viwili vya wanawake Kimara na Matete ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya kutoa vifaa vya kuwawezesha kujiajiri vyenye thamani ya jumla ya milioni 10 kwa vikundi mbalimbali jimboni kutoka katika CDCF;

(Kutoka kushoto Diwani Manota, anayekabidhiwa ni Mwenyekiti wa Kikundi na anayeshuhudia ni Mtendaji wa Kata)

Rais Kikwete, Waziri wa Maji Prof Maghembe na Bodi mpya ya DAWASCO

Tarehe 13 Agosti 2014 Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe alizindua Bodi mpya ya Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASCO) na kutoa kauli mbalimbali mbele ya vyombo vya habari ambazo zinaendeleza udhaifu ule ule badala ya kuchukua hatua za haraka kunusuru wananchi katika shida kubwa ya upatikanaji wa maji.

Ni suala lililo wazi kwamba kuzindua bodi mpya ya DAWASCO pekee haitoshi, kwa kuzingatia kuwa majukumu makuu ya kuwezesha hatua za haraka yapo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASA) ambayo nayo inahitaji bodi mpya.

Natoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kuvunja bodi iliyopo ya DAWASA na kuunda bodi mpya. Aidha, namkumbusha Rais Kikwete kuitisha kikao ikulu pamoja na DAWASCO, DAWASA na Wizara ya Maji kama alivyoahidi mbele ya wananchi mwezi Machi mwaka 2013.