Wednesday, November 27, 2013

Taarifa kwa umma kuhusu serikali kupandisha bei ya umeme

Gazeti la Tanzania Daima Toleo na. 3280 la tarehe 26 Novemba 23 limenukuu kauli iliyotolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene wakati akizungumza na kipindi cha Kumepampazuka kilichorushwa na Redio One juu ya Serikali kupandisha bei ya umeme kama Shirika la Umeme (TANESCO) lilivyoomba.

Katika habari hiyo Simbachawene amenukuliwa akisema kwamba endapo kuna mwananchi yeyote atakayeona gharama za umeme ni kubwa ni vema akaamua kuwasha kibatari au akae giza. 

Rais Jakaya Kikwete anapaswa kumwagiza Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospter Muhongo kuwaomba radhi wananchi kwa kauli hiyo iliyotolewa na Naibu Waziri Simbachawene kwa niaba ya wizara anayoiongoza.

Aidha, ni vyema Rais Kikwete kwenye hotuba yake kwa taifa ya mwisho wa mwezi huu akawaeleza wananchi iwapo uamuzi huo wa kupandisha kwa mara nyingine bei ya umeme ndio utekelezaji wa ahadi ya maisha bora aliyoitoa kwa watanzania kuanzia kwenye uchaguzi wa mwaka 2005.

Hii ni kwa sababu kupandisha bei ya umeme kuna athari ya kuchangia katika ongezeko la gharama na ugumu wa maisha kwa kuwa shughuli za uzalishaji na maisha ya kila siku zinategemea kwa kiwango kikubwa nishati.

Thursday, November 21, 2013

Mgao wa umeme na uongo nyuma yake!

Mgawo huu wa umeme ni wa ufisadi wa kimikataba Songosongo/PAT na udhaifu wa Mpango wa Dharura wa Umeme; Bungeni Muhongo alinijibu uongo.

Mgawo wa Umeme ufisadi wa PAT na udhaifu wa ukarabati wa visima ulijulikana toka Julai na Novemba 2011; Prof Muhongo alisema uongo kuficha.

Trilioni 1 ilitumika kuficha uongo wa Prof Muhongo Mgawo wa Umeme kwenye manunuzi ya mafuta mazito; Ufisadi, PAT, visima, gesi umemshinda.

MgawowaUmeme Prof Muhongo alisema uongo mara 2 bungeni; 1. 28 Julai 2012 baada ya kumhoji kwenye hotuba 27 Jul http://mnyika.blogspot.com/2012/07/hotuba-ya-kambi-rasmi-ya-upinzani.html

Uongo wa mara ya 2 wa Prof Muhongo bungeni kuhusu MgawowaUmeme ni wa Mei 23 nilipohoji baada ya hotuba ya 22 Mei: http://mnyika.blogspot.com/2013/05/hotuba-ya-msemaji-wa-kambi-rasmi-ya.html

Halafu kwa maagizo ya IMF/WB wanataka kupandisha bei ya umeme kufidia ufisadi kukodi mitambo ya dharura/ununuzi mafuta na mikataba mibovu.