Wednesday, February 19, 2014

Fursa kwa kijana kufanya kazi Ofisi ya Mbunge

Feb 2014 ni mwaka 1 toka nilipowasilisha Bungeni Hoja Binafsi ya kupendekeza Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka kuboresha upatikanaji wa Maji Safi na ushughulikiwaji wa Maji Taka katika jiji la Dar es Salaam. Soma hapa: http://goo.gl/Q770zm Natumia fursa hii kutangaza nafasi ya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini mafanikio na vikwazo kwa kijana wa ndani ya Jimbo la Ubungo (Mwanamke au Mwanaume) aliyetayari kufanya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini hatua za haraka juu ya suala la Maji ndani ya jiji la Dar es Salaam afike Ofisi ya Mbunge, Halmashauri ya Kinondoni.

John J. Mnyika
Mbunge wa Ubungo
19.02.2014

No comments: