Wednesday, November 19, 2008

Ya ukraine yarejea Urusi




Tafadhali tazama mwisho wa ujumbe huu, usome tuhuma na malalamiko ya Wanafunzi wa Tanzania walioko nchini Russia kuhusu Ubalozi wa Tanzania nchini humo, Bodi ya Mikopo na serikali kwa ujumla. Tuhuma na malalamiko hayo yamewasilishwa kwetu Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) na Rais wa .Umoja wa Wanafunzi wa Kitanzania(Patrice Lumumba University, Moscow), Bwana Boniphace Kanyathare.

Naomba muyachambue na kuchapa kama habari au makala ili umma wa watanzania uweze kufahamu malalamiko yao. BAVICHA tutafanya ufuatiliaji wa malalamiko hayo na kutoa tamko la kina siku chache zijazo.

Lakini, katika habari za kesho; pamoja na uchambuzi wa malalamiko hayo, mnaweza kuninukuu ifuatavyo:

TAARIFA KWA UMMA

· Naitaka bodi ya Mikopo hapa nchini ieleze wazi kwa umma fedha ambazo imeshapeleka mpaka sasa na fedha ambazo iliwajibika kuzipeleka ikiwemo kutaja majina ya wanafunzi waliostahili kupokea fedha hizo. Na ifanye utaratibu wa kupeleka fedha zilizobaki haraka iwezekanavyo ili kuokoa hatma ya vijana hawa.
· Nalaani vitendo vya unyanyasaji na uvunjaji wa haki za binadamu waliofanyiwa vijana hawa nchini Urusi vikihamasishwa, kushuhudiwa na kushabikiwa na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Urusi. Tunamtaka Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Jaka Mwambi atoe kauli ya haraka kueleza kadhia hiyo. Bwana Mwambi yuko nchini Urusi kwa gharama za kodi ya watanzania wote bila kujali itikadi kwa lengo la kutumikia umma na kuwakilisha maslahi ya watanzania nchini humo. Tulitarajia awe balozi mzuri wa kuhakikisha vijana hawa wanasikilizwa na kusaidiwa baadala ya kunyanyaswa. Tunamtaka Balozi afungue mara moja ukumbi wa majadiliano na vijana hao ili kulipatia ufumbuzi wa haraka suala lao. Serikali ichukue hatua za kinadhamu kwa maofisa watakaobainika kusababisha hali hii.
· Kwa kuwa vitendo kama hivi vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara(rejea tatizo la wanafunzi wa kitanzania waliokwama nchini Ukraine); ni wazi kwamba kuna tatizo la kimfumo ambao serikali ya CCM imeshindwa kulipatia ufumbuzi wa kudumu. Pia pamekuwepo na tuhuma za ufisadi katika mchakato wa malipo ya wanafunzi wa kitanzania wanaosoma nje ya nchi. Kuna haja ya wadau kuunganisha nguvu katika kulitafakari na kulipatia ufumbuzi tatizo la kuchelewa ama kupunjwa kwa malipo ya watanzania wanaosoma nje ya nchi. Aidha tunaitaka serikali ieleze kwa umma marekebisho yaliyofanyika toka ahadi za Rais Kikwete na viongozi wenzake wa serikali walizozitoa kuhusu kuboresha mfumo wa kupeleka vijana watanzania nje ya nchi kwa ajili ya masomo.
· Aidha serikali iliwahi kutoa tamko la kutaka kupunguza idadi ya watanzania wanaopelekwa kusoma nje ya nchi; wakati serikali imetoa tamko hilo, bado na ndani ya nchi mfumo wa elimu ya juu nao umekuwa ukiathiriwa na migomo na migogoro ya mara kwa mara inayosababishwa na sera mbovu ya ubebaji wa gharama za elimu ya juu(cost bearing). Serikali imekuwa ikiwaghilibu raia wake kuwa sera hii ni ya uchangiaji(cost sharing) wakati ambapo wanafunzi wamekuwa wakipewa mikopo ambayo wanajibika kuilipa baada ya masomo yao; lakini kibaya zaidi wanashindwa kupatika mikopo hiyo kwa asilimia mia moja na hivyo wengine kushindwa kumudu gharama za elimu ya juu. Wakati fedha za taifa letu zikiwa zinafujwa kupitia matumizi ya anasa ya serikali na ufisadi wa mabilioni unaofanywa kwenye kodi za wananchi; ni aibu kwa serikali hiyo hiyo kushindwa kugharamia elimu, ni aibu zaidi kwa serikali kushindwa hata kukopesha wanafunzi wa asilimia mia moja.


Tunataka watanzania waelewe kwamba taifa linahitaji mabadiliko makubwa katika mfumo wa elimu yetu. Kama kungekuwa na sera bora na mfumo mzuri wa kugharamia elimu ya watanzania, vijana watanzania wangeweza kusoma popote pale iwe ndani ya nchi au nje ya nchi bila kulazimika kufanya maandamano na migomo ya mara kwa mara yenye kuathiti hatma ya elimu yao. CHADEMA kikiwa ni chama mbadala kiko tayari kuwaongoza watanzania kufikia hatma hiyo.

Imetolewa 16 Novemba, 2008:




John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
Na Kaimu Mkurugenzi Masuala ya Kimataifa
0754694553

MATATIZO YALIYOPEREKEA VIJANA WAKITANZANIA WANAOSOMA CHUOKIKUU CHA URAFIKI (PATRICE LUMUMBA-MOSCOW-RUSSIA) KUANDAMANA KWA SIKU YA TATUMFULULIZO NJE YA UBALOZI WA TANZANIA MOSCOW
Ndugu zangu watanzania, leo kwa mara nyingine nimeamua kuwaelezea kiundani matatizo yanayotukabili watoto wenu tulioletwa na serikali yetu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kusoma mjini Moscow Russia,matatizo haya yameperekea baadhi ya wanafunzi kushindwa kuendelea na masomo yao,na wengine kushindwa kukamilisha taratibu za awali ili waweze kuanza masomo.
Matatizo yetu yamegawanyika katika makundi yafuatayo
a).Wanafunzi wafuatao mpakasasa hawajaletewa fedha zao za kujikimu pamoja na ada .
1. BROWN ELIAS LEKULE – mwaka wa tatu
2. BONIPHACE ELPHACE KANYATHARE – mwaka wa tatu
3. ALLY MOHAMED LUSESA – mwaka wa pili
4. JACKSON JACKOB TEMU – mwaka wa kwanza
5. MUHAYA SAMWELI CHITIMBO – mwaka wa kwanza
6. KINANASY R. SEIF – mwaka wa kwanza
7. MARIA F. MAJIJI – mwaka wa pili
8. IS-HACK S. IS-HAK – mwaka wa kwanza
9. NICHOLAUS MBILINYI – mwaka wa kwanza
10. ANDULILE FRANCIS MWAIGWISA – mwaka wa kwanza
11. ANDREW MASHAMBA – mwaka wa tatu
12. MICHAEL MBASHA – mwaka wa pili
13. ABDALLAH MOHAMED OTHMAN ELNOFELY – mwaka wa kwanza
Wanafunzi hawa baadhi wapo kozi ya tatu na baadhi wapo kozi ya kwanza, wenzao wote wamepata fedha, wamezipata mwezi wa tisa mwishoni na wengine mwezi wa kumi mwishoni kwa maandamano,fedha walizozipata wanafunzi wa mwaka wa kwanza zilikuwa na mapungufu mengi sana kwani kwa hesabu za kawaida naomba uangalie mfano huu.
Kwa wanafunzi wanaosoma kozi ya “international relationship” wanapaswa kupatiwa fedha zifuatazo kwa mwaka
Tuition fees-4800 us.dollors
Health insurance-250 us.dollors
Meals and accommodation-5400 us dollors
Total amount -10450 us dollors
Kwa baadhi ya wanafunzi wanaosoma kozi hiyo ya “international relation” wametumiwa fedha zifuatazo
1.FATUMA RASHID MOHAMMED-9843 US dollars
2.ISAACK ALOIS ISANZU-7713 US dolars
Ikumbukwe kuwa hawa wanafunzi wote wanasoma kozi moja na wapo darasa moja , lakini wameletewa fedha pungufu na pia ni kiwango tofauti kwa kila mmoja. Mimi kama rais wa watanzania wanaosoma chuoni hapa, niliomba mchanganuo wa fedha hizo kutoka ubalozini lakini maafisa wa ubalozi wakasema hawajaletewa kutoka bodi, tulipo wasiliana moja kwa moja na bodi wakasema wametuma ubalozini , na jitihada hizo za kuupata mchanganuo huo mpaka sasa zimegonga mwamba. Kutokana na hali hii, kuna baadhi ya wanafunzi waliopata fedha ambao mpaka sasa wameshindwa kulipa ada kufuatia ukweli kwamba fedha walizotumiwa ni pungufu. Wanafunzi wapatao 80 wakiwemo mwaka wa kwanza, wa pili na watatu wanakumbwa na tatizo hilo.
B . Mnamo tarehe 29.10.2008 wanafunzi wapya kutoka Tanzania wapatao 28 waliwasili chuoni kutoka Tanzania na ilipofika tarehe 05.11.2008 kundi lapili la wanafunzi wapya kutoka Tanzania wapatao 34 nao waliwasili kutoka Tanzania, wanafunzi wa kundi la kwanza (28) na lapili (34), waliambiwa fedha zao tayari watazikuta urusi (ubalozini), lakini baada ya kufika uongozi wa wanafunzi uliwasiliana na uongozi wa ubalozi ili kujua mustakabali wa fedha zao lakini tulijibiwa kuwa hakukuwa na fedha zao mpaka wenzao waliobaki nyumbani ambao hawajapata barua za mwaliko watakapofika hapa Urusi ndipo fedha zao kwa pamoja zitatumwa ubalozini . Kulingana na taratibu za uhamiaji hapa Urusi, suala hili linaweza kuchukua mwezi mmoja ujao.
Baada ya uongozi kupata majibu hayo tuliamua kuwafahamisha vijana na baada ya vijana kutoridhika na majibu hayo walichagua wawakilishi walioandamana na baadhi ya viongozi kwenda ubalozini ili wapate maelekezo zaidi,
Siku ya tarehe 13.11.2008 ujumbe huo ulienda ubalozini ili kujua mustakabali wa fedha zao walipofika ubalozini, afisa mmoja wa ubalozi, akaamua kupigasimu kwa Mkurugegenzi wa Wizara ya Elimu , Prof Shao, vijana wakiwa wanasikiliza kupitia loud speaker ya simu ya Afisa huyo (Dismas Kajogoo), ndipo waliposhangazwa na maneno ya mkurugenzi wa wizara ya elimu kwa kusema kuwa hautambui ujio wa wanafunzi hao wala hajui kama wapo huku Urusi. Vijana walisikitishwa sana na kauli za afisa huyo wa serikali. Baada ya hapo akawaambia kuwa wafungue accounts ndipo fedha zao ziweze kutumwa , huo ulikuwa uamuzi wa kushangaza ,kwani ikumbukwe kuwa ili mwanafunzi mpya hapa Urusi aweze kufungua account katika benki yoyote ile urusi, ni lazima awe amesajiliwa nchini urusi (amekamilisha taratibu za kiuhamiaji) . Kutokana na ukweli kuwa vijana hawa toka wafike urusi wanamuda usiozidi wiki tatu,na hawajafanyiwa usajili huo kwani ili waweze kusajiliwa ni lazima wafanyiwe uchunguzi wa afya ambao unachukua wikimbili na nusu, baada ya hapo kuna gharama ambazo wanapaswa kulipia ili waweze kukamilisha usajili , na baada ya kukamilisha mambo hayo, usajili hupatikana baada ya mwezi mmoja na nusu au zaidi. Kutokana na mlolongo huo wa usajili nilioufafanua, ni dhahili kwamba zoezi la kufungua accounts linahitaji muda usiopungua miezi mitatu. Hii inamaanisha kwamba vijana hao wakae bila fedha kwa kipindi chote hicho(miezi mitatu na kuendelea). Ikumbukwe kuwa, vijana hao hawana fedha za kujikimu, fedha za mabweni, fedha za medical insurance, na fedha za ada. Pia, ni ukweli kwamba vijana wengi wametoka familia za kimaskini kama yangu na hawakuja na fedha zozote.
Baada ya uongozi wa ubalozi kuona vijana hao hawaridhishwi na majibu hayo ukaahidi kuwakopesha kila mmoja kiasi cha dola za kimarekani 150. Lakini kwa hali halisi fedha hizo ni ndogo sana hapa urusi na haziwezi kukidhi matatizo yao, kwani mwanafunzi mmoja ili aweze kukidhi mahitaji niliyoyataja, anatakiwa apewe dola za kimarekani 5400 kwa mwaka kwa ajili ya kujikimu tu. Wawakilishi hao waliamua kuwarudishia wenzao taarifa, ili waamue cha kufanya kwa pamoja.
Siku hiyo baada ya vijana kumaliza kikao chao ,mimi kama rais wa wanafunzi ambaye pia sijapata fedha za mkopo wangu toka Bodi, nilikwenda ubalozini pamoja na ujumbe wa vijana 13 (wa mwaka wa kwanza wa pili na watatu)ambao pia hawajapata fedha ili kujua mustakabali wa fedha zetu. Kama ilivyokawaida ya ubalozi, tulizuiliwa kuingia ili kuongea na viongozi wa ubalozi , tulikaa nje kwenye baridi kuanzia saa sita mchana mpaka saa kumi na moja jioni ndipo mimi rais nikaruhusiwa kuingia ubalozini, peke yangu na wanafunzi wenzangu wakaendelea kupigwa na baridi kali nje ya ubalozi wanchi yetu tuipendayo, mpaka saa tatu usiku hali zao zilipokuwa mbaya ndipo wakaamua kuondoka, nilipo fika ndani bahati nzuri kiongozi mmoja aliyeingia na vijana wale alibaki ndani na alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi ambao hawajapata fedha, hivyo tukawa waathirika wawili ,tukajaribu kuzungumza na uongozi wa ubalozi kutaka kujua watatusaidia vipi ili tuweze kuendelea na masomo yetu kwa manufaa ya taifa letu,lakini majibu tuliyopewa na viongozi hao wa ubalozi yalikuwa ya kukatisha tamaa na kusisitiza kuwa wao hawahusiki na matatizo yetu na wakasema tunawabebesha mzigo wasiostahili kwani eti wao siyo serikali. Maneno haya yalitolewa na Afisa wa ubalozi bwana Dismas Kajogoo ambaye alizidi kusisitiza bila uoga kwamba, “Serikali ni kikwete na aliounda nao baraza la mawaziri”. Ndugu zangu nguvu ziliniishia na nikashindwa kujua , taifa letu linaelekea wapi? Naje tutaishi vipi ughaibuni bila kuwa na fedha za kujikimu achilia mbali za kulipia ada ya shule pamoja na mabweni? Ikumbukwe kuwa miezi miwili na nusu imeshapita tangu tulipopaswa kupata fedha na mpaka sasa maishayetu yamekuwa ya kusuasua. Baada ya kutathmini pamoja na kiongozi mwenzangu ndipo tulipo amua kukaa ubalozini na kuomba kukutana na balozi ili kujaribu kumsihi afikirie namna ya kuweza kuwasaidia wanafunzi wote wenye matatizo ya fedha lakini ombi letu lilipuuzwa na wakatuacha kwenye chumba cha mkutano ubalozini bila kutusikiliza. kutokana na ukweli kuwa hatukuwa na namna nyingine ya kuweza kuishi tuliamua kulala kwenye viti ubalozini kwa nidhamu ya hali yajuu kwa taifa letu bila kumsumbua mtu yeyote, mpaka asubuhi ya tarehe 14.11.2008 bila kula chochote, ilipofika asubuhi wanafunzi wenzetu walipopata taarifa kuwa mimi rais wao na kiongozi mwingine tulilala ubalozini wanafunzi wapatao 90 ambao hawajapata fedha zao wakiwemo wale wapya wakaandamana wote kuja ubalozini ili waweze waweze kujua hatima ya fedha zao.Mimi pamoja na kiongozi mwenzangu, tuliendelea kukaa ndani ya ubalozi kwenye ukumbi wa mikutano mpaka saa saba mchana, huku wenzetu 90 wakiwa wanapigwa na baridi nje bila kufunguliwa mlango. Mimi na mwenzangu kule ndani tulishangaa kuona maaskari wapatao 11 wakiingia ndani tulikokuwa na kuanza ghafla kutukaba kama majambazi au wahalifu na kutuburuza huku wakituchania nguo zetu na kutukanyagia simu zetu za mikononi mbele ya watumishi wa ubalozi akiwemo Balozi Jaka Mwambi, mpaka nje ya ubalozi ambapo wengine walibaki wakitulinda na wengine wakarudi ndani ya ubalozi , baada ya muda mfupi walitoka na kutukamata tena na kutuingiza ndani ya gari kwa nguvu huku wakituelekezea bunduki kama majambazi mpaka kituoni ,tukaingizwa kwenye selo na kufungiwa kwa muda wa masaa matano bila kuhojiwa., Wakati tupo ndani ya selo wenzetu waliobaki pale nje ubalozini walianza kufanya jitihada za kuwashawishi maaskari watuachie lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda. Baadae mkuu wa kituo alikuja na kupokea maelezo kutoka kwetu ndani ya selo na akasema suala hilo la sisi kukamatwa ndani ya ubalozi wetu lilifanyika kimakosa. Mkuu huyo wa kituo cha polisi alitutaka radhi na akaendelea kufafanua kwamba, maaskari wake waliokuwa lindoni ubalozini siku hiyo walipokea agizo la maandishi lililotiwa sahihi na Afisa wa ubalozi bwana Dismas Kajogoo, akiagiza askari hao watukamate na kututoa ndani ya ubalozi wetu. Baada ya hapo, tuliachiwa huru na majeraha yetu tuliyoyapata wakati askari hao walipotukaba ubalozi.
Mpaka naandika maelezo haya bado wanafunzi wapatao 100 tunaendelea na maandamano mpaka tutakapo pata fedha zetu na balozi Jaka mwambi ametutumia taarifa kuwa kuanzia sasa hawashughuliki na maswala ya wanafunzi mpaka uongozi wa wanafunzi ubadilishwe, na wawekwe watu ambao hawawezi kudai haki zao wala kusimamia utekelezaji wa mkataba kati ya serikali yetu na serikali ya urusi mfano.
1) 1. MKATABA HUO UNASEMA KWA KILA WANAFUNZI WAWILI WANAOSOMESHWA NA SERIKALI YA TANZANIA, SERIKALI YA URUSI(CHUO) HUTOA NAFASI KWA MTU WA TATU KUSOMA BURE. LAKINI KWA WANAFUNZI WALIOFIKA HAPA CHUONI MWAKA 2007/2008 AMBAO WALIKUWA 78 NA BAADAYE KUBAKI 76 NI WANAFUNZI 17 TU NDIO WALIOPEWA NAFASI HIZO. HII NI KINYUME NA MKATABA HUO KWANI WALIOSTAHILI KUPATA UDHAMINI WA CHUO NI 24. KATIKA KUFUATILIA SWALA HILO UONGOZI WA WANAFUNZI ULIGUNDUA KUWA KATIBU WA UBALOZI BWANA MBAROUK N. MBAROUK KWA KUSHIRIKIANA NA AFISA MMOJA WA CHUO WANATUMIA NAFASI HIZO ZA WALALA HOI KWA MANUFAA YAO. HII INAMAANISHA KUWA, MWAKA ULIOPITA NAFASI 7 HAZIJULIKANI ZIMEKWENDA WAPI. UONGOZI WA WANAFUNZI UMEJARIBU KUFUATILIA SUALA HILI LAKINI MIMI BINAFSI KAMA RAIS WA UMOJA WETU PAMOJA NA MAKAMU KATIBU TULIKUMBANA NA VITISHO VYA KUFUKUZWA CHUO KUTOKA KWA AFISA WA CHUO (MRUSI) ANAYESHUGHULIKIA SUALA HILO, SUALA HILI NI VYEMA SERIKALI YETU IKALICHUNGUZA UPYA NA KWA MAKINI KWANI KUNA KILA DALILI ZA UFISADI. MAAFISA HAO WA UBALOZI HAWANA UCHUNGU NA NCHI YETU KWANI KUPATIKANA KWA NAFASI HIZO KUNGEPUNGUZA MALIPO YA FEDHA ZA ADA KWA WATU HAO, NA FEDHA HIZO ZINGEWEZA KUTUMIKA KUWASOMESHA WATOTO WA MASKINI AMBAO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE WAMEKOSA NAFASI ZA KUSOMA.
2) PILI UMEZUKA MTINDO CHUONI WA KUWALAZIMISHA WANAFUNZI KUSOMA LUGHA KWA MUDA WA MIAKA MIWILI KINYUME NA MKATABA UNAOSEMA WAZI KWAMBA MWANAFUNZI ANAPASWA KUSOMA LUGHA KWA MWAKA MMOJA TU. BILA SABABU ZA MSINGI. NA KATIKA HILI KUNA MKONO WA MOJA KWA MOJA WA KATIBU WA UBALOZI BWANA MBAROUK N. MBAROUK . AFISA HUYO HUFAIDIKA NA UVUNJWAJI WA MKATABA HUO KWANI, MWANAFUNZI ANAPOSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI, HULIPIWA ADA NUSU KWA ULE MWAKA WA KWANZA WA LUGHA. IKUMBUKWE KUWA KILA MWAKA SERIKALI HUTUMA ADA YA MWAKA MZIMA KWA KILA MWANAFUZI, HIVYO NI DHAHIRI KWAMBA NUSU YA ADA INAYOBAKI HUMNUFAISHA AFISA HUYO WA UBALOZI. TUNAOMBA SERIKALI IFANYE UCHUNGUZI WA KINA KWANI DOCUMENTS ZA USHAHIDI WA MALIPO HAYO TUNAZO, NA MOJA YA NYARAKA HIZO TUMEAMBATANISHA NA TAARIFA HII. MAJINA YALIYOWEKEWA TIKI NI YA WANAFUNZI WALIOLAZIMISHWA KUSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI NA KULIPIWA ADA NUSU MWAKA. HUU NI UBADHILIFU WA HALI YA JUU KWA FEDHA ZA WANAFUNZI NA NI UDANGANYIFU KWA TAIFA. MIMI KAMA RAIS WA UMOJA WETU WA WANAFUNZI SITA RUHUSU LITOKEE KWANI NINAIPENDA NCHI YANGU NA NINAWAPENDA WANAFUNZI WENZANGU NA HILI SUALA LA KUSOMA LUGHA MIAKA MIWILI INABIDI LIISHE ,ILI MAFISADI WASIPATE MWANYA ,KWANI SISI TULIOKUJA 2005 KUNA BAADHI YA WANAFUNZI WALICHELEWA KUJA KWANI WALIFIKA URUSI JANUARI BADALA YA SEPTEMBER NA WALISOMA LUGHA KWA MUDA WA MIEZI MITANO BADALA YA MIEZI KUMI BILA KURUDIA MWAKA NA KWA SASA WAPO KOZI YA TATU. KUWALAZIMISHA WANAFUNZI KUSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI ILI UBALOZI UNUFAIKE NA FEDHA ZA ADA,NI MPANGO MCHAFU UNAORUDISHA NYUMA MAENDELEO YA TAIFA ILI KUWAFAIDISHA WACHACHE.
NDUGU ZANGU WATANZANIA PAMOJA NA YOTE AMBAYO VIONGOZI WA UBALOZI WAMEFANYA ILI KUWEZA KUFICHA MAOVU HAYO MPAKA SASA WAMESHINDWA, NA KWASASA LENGOLAO WANAWATUMIA BAADHI YA WANAFUNZI WENZETU KWA KUWAPA RUSHWA ILI KUWEZA KUTUONDOA KWENYE UONGOZI , PAMOJA NA VITISHO MBALIMBALI KUTOKA CHUONI ILI TUSISIMAMIE HAKI ZETU, LAKINI HATURUDI NYUMA TUNAAMINI KWA DHATI KUWA TANZANIA INAHITAJI MABADILIKO NA MABADILIKO TUTAYALETA WENYEWE VIJANA HIVYO NAOMBA NITUMIE NAFASI HII KUWAOMBA VIJANA WENZANGU ,TUSIMAME IMARA ILI TUWEZE KUIOKOA NCHI YETU HUUNDIO WAKATI WETU.
BAADHI YETU WANASHINDWA KUSIMAMIA UKWELI KWA KUOGOPA KUWA FAMILIA WANAZOTOKA NI MASKINI , NAOMBA NIWAHAKIKISHIE KUWA FAMILIA ZETU MASKINI TUTAWEZA KUZIKOMBOA KWA KUSIMAMA IMARA NA KUTETEA KILE KILICHO CHEMA MBELE ZA MUNGU, NA SIYO VINGINEVYO , SINTORUDINYUMA NA UKWELI LAZIMA UFAHAMIKE ILI HAKI IWEZE KUTENDEKA MIMI KAMA RAIS WA UMOJA WA WANAFUNZI WA KITANZANIA KATIKA CHUOKIKUU CHA PATRICE LUMUMBA MOSCOW, NAOMBA KWAPAMOJA TUUKEMEE UBADHILIFU ILI TAIFA LETU LIWEZE KUSIMAMA IMARA.
TUNAENDELEA NA MGOMO WA AMANI MPAKA MATATIZO YETU YATAKAPO PATA SULUHISHO,KWANI KWA NJIA YA MAZUNGUMZO TUMEJARIBU LAKINI KILA MARA TUMEKUWA TUKIFUNGIWA NJE YA UBALOZI KWENYE BARIDI KALI BILA KURUHUSIWA KUZUNGUMZA NAO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
BONIPHACE ELPHACE KANYATHARE
RAIS WA UMOJA WA WANAFUNZI WA KITANZANIA
(PATRICE-LUMUMBA UNIVERSITY). MOSCOW.RUSSIA



Sunday, November 9, 2008

Taifa lenye utamaduni wa ufisadi

Leo niwapatie mchango wangu nilioutoa hapa kwenye mjadala unaoendelea kuhusu ufisadi: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/20024-ccm-yafanya-maamuzi-mazito-kamati-kuu-22.html#post319258

"Muda mrefu sijachangia JF, ile hii post imenigusa sana.Maudhui yake yamehitimisha kile ambacho nimewahi kukisema na kukiandikia mara kadhaa kwamba nchi yetu imeingia katika 'utamaduni wa ufisadi'. Ambapo ile dhana ya kila 'mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake'(ongezea mahali pake)- soma 'kazini kwake', imekuwa ni jambo la kawaida katika maisha ya watanzania.Hili ndio tatizo na msingi ambalo kama taifa tunapaswa kulishughulikia kurejesha MAADILI na UWAJIBIKAJI.Wazee wetu wanatuambia enzi za miaka ya awali ya Mwalimu ufisadi hakuwa umeshika kazi na kupenya katika mishipa ya wananchi na viongozi kama ilivyo sasa.Swali la kujiuliza- ni kwa vipi tumefika hapa? Na tunarudi vipi katika misingi iliyokuwepo awali?Wengine wanasema ni kwa sababu ya mabadiliko ya kiuchumi kuelekea uchumi wa soko ambao wengine wanajenga hoja kuwa unaambatana na ubinafsi na kutaka kujilimbikizia. Wao wanaamini kwamba ujamaa ungekuwa suluhu ya kuendelea kuwa na maadili.Wengine waamini kuporomoka kwa uchumi kulikoleta hali ngumu ya maisha na hatimaye mishahara kushuka ukilinganisha na gharama za maisha kumepunguzia wananchi uwezo wa kununua na hatimaye sasa wafanyakazi wengine kugeuka wala rushwa mahali pao na watoa rushwa kwa wengine. Hawa wanajaribu kuelezea rushwa ndogo ndogo(petty corruption). Ukiwauliza ni kwa vipi matajiri wakubwa na viongozi wakuu wa serikali wenye mishahara mizuri na maslahi mazuri nao wanapokea na kutoa rushwa kubwa kubwa(grand corruption), wanakosa majibu mazuri.Katika kukubiliana na rushwa, wapo waomini kwamba tukiweka sheria kali na kujenga taasisi zenye nguvu, rushwa itaondoka. Lakini wanasahau kwamba sheria zinapaswa kusimamiwa na watu, taasisi nazo zinasimamiwa na watu. Kama ukiwa na taifa lenye utamaduni wa ufisadi, sheria hata ziwe nzuri haziwezi kusimamiwa(rejea kauli ya rais kwamba watakaorudisha fedha za EPA watasamehewa- nimeijadili kidogo hapa: JJ: Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika ); mnakumbuka pia mfano(rejea hapa:TAKURU inalinda na kutetea Rushwa? ) wa Taasisi ya TAKUKURU(wakati huo TAKURU) ilivyoisafisha RICHMOND na mchakato wake.Wengine wanasema basi tuanzie kwa kuweka viongozi waadilifu, halafu wao kwa maneno na matendo yao watasimamia utawala wa sheria na uwajibikaji wa taasisi hizo. Lakini uchaguzi kwenye taifa lenye utamaduni wa ufisadi mara nyingi huzaa viongozi mafisadi. Wananchi mafisadi huchagua viongozi mafisadi.Kwa hiyo hili suala la ufisadi, ni kama hadithi ya kuku na yai- ni mjadala unaozunguka kusema kwamba kipi kilianza.Kwa maoni yangu, sababu zote kila moja kwa nafasi yake inachangia katika utamaduni wa ufisadi. Ujamaa wa dola(naita ujamaa wa dola kwa kuwa nina mtazamo tofauti sana kuhusu uzuri na udhaifu wa ujamaa mfululizo wa uchambuzi wangu kuhusu hoja hii upo hapa: Tanzania, CHADEMA, CCM na mjadala wa falsafa na itikadi; Lipi ni jibu? ) ,ulizaa urasimu wa bidhaa na huduma ambao ulichangia katika baadhi ya wananchi kuanza kuweka pemebeni misingi ya maadili na uwajibikaji na kujiingiza katika utamaduni wa ufisadi. Viongozi waliochaguliwa baadaye walikuja tu kuchochea utamaduni wa ufisadi ambao tayari ilishaanza. Utadamuni ambao ulijengwa pia kwa raia kuweka mawazo yao yote kwa dola na serikali. Kushuka kwa hali ya maisha na kupungua kwa uwezo wa kununua kulikoambana na mishahara duni kuliongeza tu huu utamadauni wa ufisadi. Halafu ndipo tukaingia katika mduara ya ufisadi(the cycle of corruption); kwamba chama tawala na vingozi wake wanalinda ufisadi, wananchi nao wanazidi kuwa mafisadi katika mahali pao pa kazi na uchaguzi ukija mafisadi wengi zaidi wanachaguliwa; mzunguko unaoendelea. Sasa changamoto ni kuvunja huu mduara.Kwa bahati njema, si raia wote ni mafisadi. Si viongozi wote ni mafisadi. Bado kuna tabaka la watu wachache ambao si mafisadi. Hatua za haraka zinahitajika kuchukuliwa na tabaka hilo kuliokoa taifa. Uzoefu unaonyesha kwamba utamaduni wa ufisadi huwa ukikomaa una kawaida ya ama kuangusha dola au kuazaa taifa lenye matabaka kati ya walionacho na wasionacho na lenye vurugu za kijamii. Tunapaswa tusifike huko kama taifa.Kama ambavyo takaba la watu wachache liliamini kwamba mkoloni anaweza kutoka katikati ya tabaka la waliowengi waliomini kama mkoloni hawezi kushindika na kwamba kutawaliwa ni jambo la kawada na kwamba waafrika wameumbwa kutawaliwa; ndivyo inavyopasa kuwa kwenye suala hili la ufisadi.Suluhisho ni kurudi kwa umma. Hao waadilifu wachache kwenda kwa wananchi kutoa elimu ya uraia, wananchi wakaunga mkono kwamba ufisadi wao ndio kaburi lao; kwamba ufisadi wa watawala ni jeneza tu la kuwabeba na kuwazika. Kwamba ufisadi unawaathiri zaidi wao wenyewe. Wananchi wakaelewa uhusiano kati ya maisha yao kuwa mabaya, huduma za kijamii kuwa mbovu na ufisadi. Wananchi wakajua kwamba ufisadi ni dhambi si ya kuliathiri taifa tu bali kujiathiri mtu mwenyewe. Hapo ndio wananchi watachukua hatua kwa nguvu ya umma. Tararibu tutajenga taifa lenye utamaduni wa maadili ambao mimi huwa napenda kuuita utamaduni wa uwajibikaji. (Niliwahi kugusia kidogo hii dhana hapa: 45th Anniversary: My greetings to you and reflections with Mwalimu Nyerere). Katika taifa la namna hiyo, viongozi wanamachaguo matatu; ama kukubaliana na sauti ya umma na wao kuanza kusimamia uwajibikaji(Rais Kikwete kuunda kamati ya bomani na Bunge kuunda Kamati ya Richmond ni matokeo ya umma kuanza kuchukua hatua baada ya Hoja ya Zitto kuhusu Buzwagi na hoja ya Dr Slaa kuhusu BOT. Kupelekwa kwa kesi za EPA ni matokeo ya yaliyojiri baada ya Kutajwa kwa Orodha ya Mafisadi); ama watawala kunyamaza(na wakati mwingine kugeuka madikteta) na kuruhusu kuzuka kwa utamaduni wa hukumu ya ujmma(mob justice) ambao unaweza kuwa na faida katika usalama wa taifa ama unaweza kutishia utangamano wa umma(unaweza kuwa na mifano ya hivi karibuni) ama wananchi kuvuta subira na kusubiri kuchukua hatua wakati wa chaguzi(kuondoa madarakani utawala na watawala waolinda ufisadi).Lakini hatua hii inapaswa kwenda sambamba na umma kutaka hatua zichukuliwe ili kuboresha pia maeneo mengine mathalani suala la mishahara na usimamizi wa taasisi za uwajibikaji.Hii ni njia ya amani kuelekea maadili na uwajibikaji. Njia nyingine ni kikundi cha watu wachache kujitwalia madaraka ama kwa sanduku la kura lakini mara nyingi kwa mapinduzi na kujivika dhima ya kulitoa taifa kutoka katika utamaduni wa ufisadi na kuelekea katika maadili na uwajibikaji. Hawa huitwa madikteta wakarimu!(mifano imewahi kutokea katiika mataifa mengine). Hawa huweka adhabu kali dhidi ya aina zote za ufisadi na huzisimamia adhabu hizo na hatimaye kujenga hofu katika taifa kwa mafisadi na hiyo watu kuacha ufisadi si kwa kuelewa au kwa kupenda; bali kwa hofu! Tatizo la msingi la njia hiyo ni kuwa linaanzia kwenye njia yenyewe na hivyo baada ya muda fulani watawala hao hao wenyewe hugeuka kuwa mafisadi kwa kujilimbikizia kutokana na mamlaka makubwa wanayokuwa nayo ama huishia kukataa kutoka madarakani na hatimaye kuzua tena utadamuni wa ufisadi.Hivyo, nawapongeza Dr Slaa na Zitto kwa njia mliyoamua kuipitia. Mabadiliko huanzia kwa mtu mwenyewe, naamini kwa kukataa kwako umemuambukiza huyo mzee utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji. Majaribu ni mengi lakini hakuna sababu ya kukata tamaa. Uovu hushamiri wema unapokata tamaa.Lakini tukumbuke pia rushwa kubwa kubwa katika mataifa ya Afrika inachangiwa pia na mataifa ya nje hususani kupitia makampuni makubwa(MNC). Nilikuwa napitia sheria za nchi mbalimbali, mataifa mengi yanakataza ndani ya nchi zao mashirika yao kutoa chochote kupata zabuni lakini mataifa hayo hayo yametunga sheria ambazo zinaruhusu mataifa yao kuwahonga viongozi wa kifrika katika kupata zabuni. Hivyo uhusiano wa kimataifa umejengwa katika misingi ya utadamuni wa ufisadi uliojificha katika vivuli vya commission nk.Jambo moja lazima tuamue, kama tunataka maendeleo ya taifa letu-hatuna jinsi zaidi ya kuendeleza utamaduni wa uwajibikaji. Ambapo kila mtu atawajibika kwa nafasi yake na atakayeshindwa kuwajibika atawajibishwa. Umaskini wetu umechangia katika ufisadi, lakini umaskini wetu sio chanzo kikuu cha ufisadi huu. Hivyo, lazima tufikiri zaidi na kuendelea kuchukua hatua.BTW 1: Thread inahusu Kamati Kuu ya CCM, mod aidha badilisheni heading au hii michango kuhusu ufisadi ianzishwe thread yake.BTW 2: Zitto, mpe hongera Chachage Jr.BTW 3: Unaweza kuwa ulishawahi kuwa fisadi, ama ulishawahi kuwa fisadi lakini kama kuna chochote kinaweza kukugusa katika mjadala huu, unaweza kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Kwenye kitabu kitakatifu kimojawapo kuna hadhithi ya Saul ambaye alikuwa anachinja watu wa dini, baadaye akaongoka na kuwa Paulo mweneza dini.BTW 4: Kwa fisadi yoyote anayesoma hapa-aelewe kwamba ufisadi ni uuaji wa taifa na wananchi walio wengi. Ni ubatili, sawa na kufukuza upepo! Ni raha ya muda fulani na karaha ya muda mrefu.Nawakatika mjadala mwema mpaka panapo majaliwa"

Friday, November 7, 2008

TUBADILI MFUMO WA UCHAGUZI KUPATA UONGOZI BORA

TUBADILI MFUMO WA UCHAGUZI KUPATA UONGOZI BORA
Na John Mnyika

Makala yangu ya leo inajikita katika eneo moja tu: “Mfumo wa Uchaguzi Tanzania”. Mfumo ni roho ya uchaguzi na chaguzi ndio msingi wa Siasa. Kama siasa(nikimaanisha siasa safi) ni hitaji muhimu la maendeleo kama alivyowahi kusema hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere; basi uendeshwaji wa uchaguzi(kwa maana ya uchaguzi huru na haki); ndio njia ya kulipata hitaji hili. Uendeshwaji wa uchaguzi huru na haki hutupatia pia hitaji lingine la msingi kwa maendeleo- yaani “Uongozi Bora”.

Wakati suala la mfumo wa uchaguzi limeshawekewa sheria zinazosimamia kwa karibu katika nchi zilizoendelea ambapo demokrasia ya mfumo wa vyama vingi imekuwepo kwa miaka mingi; katika nchi zenye demokrasia changa bado tunaendelea kujiuliza maswali na kuibua masuala kwa lengo kupata mifumo ambayo itakidhi mahitaji yetu.

Shabaha ya makala hii ni kuchochea mjadala ambao utawezesha mapitio ya katiba na sheria zinazotawala siasa Tanzania katika muktadha wa mfumo wa uchaguzi na kuhamasisha marejeo ama mabadiliko yanayostahili. Ni lazima tuhakikishe tunaendelea kuwa na “uchaguzi” badala ya “uchafuzi”.

Mfumo wa uchaguzi unaotumika sasa

Mfumo unatotumika Tanzania ni Mfumo wa Wengi Wape; hata hivyo kuna Viti Maalumu vya Wanawake katika ngazi ya Ubunge na Udiwani ambavyo vinagawanywa kwa misingi ya uwiano. Mfumo wa Wengi Wape (Plurality-Majority) ni mfumo ambao hutumia wilaya/jimbo za/la uchaguzi na mgombea anachaguliwa kuwakilisha wilaya/jimbo husika. Tawi la mfumo huu linaloitwa kwa Kiingereza First-Past-the-Post (FPTP) ndilo lililo maarufu sana na hutumika katika nchi nyingi zilizo katika Jumuiya ya madola. Katika mfumo huu vyama huteua wagombea na kuwadhamini katika majimbo. Mgombea anaeshinda kwa kura nyingi kuliko wenzake hata kama hazifikii nusu ndio huwa amechaguliwa na kunyakua kiti kinachogombewa. Mfumo huu unatumika nchini Uingereza, India, Kenya na Tanzania.Mfumo huu pia hupelekea kuwa na chama kimoja chenye uwezo wa kuunda serikali peke yake bila ya kuhitaji vyama vingine na kuwa na mseto. Mfumo huu husaidia wananchi kuchagua watu na sio vyama vya siasa na hivo mpiga kura anaweza kutathmini utendaji wa mbunge au mwakilishi badala ya utendaji wa chama fulani. Mfumo huu ni rahisi kuutumia na unaeleweka miongoni mwa wananchi, wagombea huwa wachache na hata uhesabuji wa kura unakuwa ni rahisi. Mfumo wa wengi wape hupelekea kuminya nafasi za wanawake kuchaguliwa kuingia bungeni. Kwa tamaduni za nchi za kiafrika kwamba mwanamke hawezi kushindana na mwanaume na pia gharama kubwa za uchaguzi katika majimbo, wanawake wanaochaguliwa kuingia bungeni wanakuwa ni wachache sana. Mfumo huu huua ukuaji wa vyama na hivyo nchi kukosa vyama makini. Hii ni kwa sababu, badala ya vyama kufanya kampeni kwa kutumia sera zao, hutumia majina ya watu ambao ni wagombea wao. Hivyo basi mfumo huu hupelekea vyama kubaki dhaifu na kushindwa kushindana na kutotoa mbadala. Vyama katika mfumo wa wengi wape huwa vigumu sana kuwajibika kwa wananchi kwani badala ya kurekebihsa sera zao vyama hubadili wagombea tu na kuwalaghai wananchi na kushinda tena. Maoni ya wananchi yanakuwa hayaheshimiki na nchi inakosa maendeleo kwa sababu ya demokrasia duni inayosababishwa na mfumo wa wengi wape.
Marekekebisho yanayotaka kufanywa na wanaCCM

Katika mtandao wa www.jamiiforums.com pamezuka mjadala kutokana na marekebisho yanayotarajiwa kusukumwa na wanaCCM kuhusu suala la mfumo wa uchaguzi. Marekebisho hayo yameshadokezwa pia na vyombo kadhaa vya habari. Mmoja wa wachangiaji katika mjadala huo ametoa mchango ambao ni nimeona na vyema nikaukuu kama ulivyo kabla ya kutoa uchambuzi wangu.

Nanukuu: “CCM imebuni kete mpya ya kuizidi CHADEMA na kupunguza nguvu ya upinzani bungeni. Katika mkakati huo mpya ambao umeshapata baraka ya kamati kuu ya chama hicho ukisubiri kupitishwa na NEC hivi karibuni, katiba ya nchi itafanyiwa marekebisho kuweza kutekeleza mkakati huo. Chini ya marekebisho hayo, wabunge wa viti maalum hawatapatikana kwa kuteuliwa na vyama bali watagombea kupitia wilaya ambazo ndizo zitakazo kuwa majimbo ya wanawake pekee. Chini ya mfumo huo mpya, patakuwa na majimbo ya kawaida 232 ambayo yatagombewa na watu wote kwa kama ilivyo utaratibu wa sasa. Kwa upande mwingine viti maalum vya wanawake pekee 75 vitaondolewa na badala yake wanawake watagombea wenyewe kwenye wilaya 130 za Tanzania. Kwa hali hiyo, kutakuwa na ongezeko la wabunge ambalo litalazimisha taifa kupanua tena ukumbi wa bunge na pia bajeti ya matumizi ya wabunge ya mishahara na posho itabidi iongeze kwa zaidi ya bilioni 50. Kwa idadi hiyo ya wabunge, Tanzania itaingia katika kundi la nchi zenye wabunge wengi zaidi.Mkakati huo umebuniwa kupunguza nguvu za kambi ya upinzani hususani CHADEMA ambayo imepata kutokana na kupata wabunge wengi wa viti maalum kutokana na idadi ya kura ambazo chama hicho na vingine vya upinzani vimeokoteza nchi nzima.Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 CHADEMA ilipata wabunge watano tu wa kuchaguliwa lakini ikapata wabunge wa viti maalum sita kutokana na kura ambazo chama hicho kilipata katika uchaguzi. Kama viti maalum vingetolewa kwa idadi ya viti ambavyo chama kimepata chama hicho kingepata kiti maalum kimoja au viwili tu.“Unajua tumeweka sheria inayoisaidia CHADEMA, hawa chini ya Operesheni Sangara hata kama tukitumia nguvu kushinda majimbo bado watapata zaidi ya asilimia 20-40 ya kura katika majimbo mbalimbali hali itayofanya wapate kati ya wabunge 15 mpaka 30 wa viti maalum mwaka 2010. Lazima tutafute njia ya kuwadhibiti mapema kwa kubadili sheria”, alinukuliwa mmoja wa wajumbe wa Kamati kuu ya chama hicho.Timu ya kuandaa mpango huo iliundwa miezi michache iliyopita baada ya kujitokeza fursa ya marekebisho hayo kutokana na Rais Kikwete kutoa ahadi kupitia hotuba yake ya kuongeza uwakilishi wa wanawake bungeni kuwa 50 kwa 50.Timu hiyo ilifanikiwa kushawishi wajumbe wa kamati kuu ya chama hicho kuweka pembeni mapendekezo mengine ya Kamati ya Dr Ghalib Billal ambayo iliundwa baadaye kuchambua kuhusu suala hilo.Kamati hiyo ilikuja na mapendekezo mbalimbali ikiwemo kupanua idadi ya wanawake katika uwakilishi wa uwiano kuwa na orodha yenye uwiano wa majina kijinsia. Aidha pendekezo lingine la kamati hiyo lilitaka uchaguzi uhusishe wagombea wawili mwanamke na mwanaume katika majimbo ya uchaguzi na kupunguza majimbo ya sasa.Mfumo huu mpya unatarajiwa kupata upinzani mkali toka kwa makundi ya kijamii mathalani walemavu na asasi za kiraia.“Unajua mfumo wa sasa wa viti maalum, unatoa fursa ya uwakilishi wa makundi maalum ya wanawake. Kwa mfano, mimi nimechaguliwa kuwakilisha kundi la walemavu. Lakini kwa marekebisho hayo yanayopendekezwa, nitatakiwa nikagombee katika jimbo la uchaguzi. Tunaweza tukapoteza kabisa uwakilishi wa makundi mbalimbali bungeni”, alisema mbunge mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake.Chini ya mfumo mpya hakutakuwa na viti maalum vya makundi kama vijana, walemavu, wawikilishi wa elimu ya juu na mashirika yasiyo ya kiserikali ambavyo vimekuwa vikitengwa na vyama kutokana na uwingi wa viti ambavyo chama kimepata.Makubaliano hayo ya Kamati Kuu yanatarajiwa kuzua mjadala mkali katika kikao cha NEC kutoka kwa wabunge wa majimbo kuhusu hadhi yao katika mfumo mpya.“Inabidi tuelezwe wazi, kati ya wabunge wa wilaya, na wabunge wa majimbo. Ni nani watakuwa na hadhi na mamlaka zaidi chini ya marekebisho hayo”, alisema mbunge machachari wa kanda ya ziwa akitoa maoni yake kuhusu uamuzi wa NEC.Chini ya mapendekezo hayo, mathalani wilaya kama Ilala yenye majimbo mawili ya Ukonga na Ilala itakuwa na wabunge watatu; Mbunge wa Wilaya ya Ilala ambaye atakuwa ni Mwanamke na Wabunge wawili wa majimbo ya Ilala na Ukonga ambao watakuwa ni wa jinsia yoyote.Hata hivyo, ili kupunguza mjadala katika jamii kuhusu mkakati huo, tayari Mkuu wa Mawasiliano amekabidhiwa jukumu la kuundaa umma kukubaliana na marekebisho hayo kupitia propaganda za vyombo vya habari.Kama sehemu ya propaganda hizo imekubaliwa kwamba habari maalum zitolewe na vyombo vya habari kabla zikieleza kwamba marekebisho hayo yanalenga kuundoa migogoro katika vyama vya siasa inayotokana na upendeleo katika uteuzi wa viti maalum kwa kuweka mfumo huu mpya ambao utafanya wanawake washindane wenyewe kwa wenyewe.Habari hizo zitaeleza kwamba CHADEMA ni mfano dhahiri wa migogoro hiyo ya upendeleo wa viti maalum ambayo serikali ya CCM inalenga kuindoa kwa kufanya marekebisho hayo ya katiba ya nchi na sheria za uchaguzi katika upatikanaji wa wabunge wa viti maalum.Changamoto kubwa kwa serikali inatabaki kutumiza ahadi ya kuwa na wabunge kwenye uwiano wa 50 kwa 50 kati ya wanawake na wanaume, ahadi ambayo mfumo huu mpya hauwezi kuitekeleza badala yake mfumo huo umeondoa mfumo wa kuthamini kura ambao umekuwa ukitumika katika nchi mbalimbali” Mwisho wa kunuu.

Mabadiliko yanayostahili kufanywa

Katika mazingira ya majadiliano niliyoyanukuu hapo juu, ni wazi suala hili sasa linahitaji mjadala mkubwa wa umma kwa sababu mabadiliko ya katiba na sheria za nchi si hodi ya chama chochote cha siasa au kikundi cha watu wachache; ni suala la maslahi na matakwa ya umma. Mjadala huo umegusia suala la uteuzi wa viti maalumu katika CHADEMA hoja ambayo nimewahi kuiandikia makala mbili mfululizo kama sehemu ya kuchambua vigezo vilivyotumika; makala hizi zinapatikana kupitia mtandao wa http://mnyika.blogspot.com.

Makala ya leo inalenga zaidi kutoa maoni yangu ya kutokubaliana na marekebisho hayo hapo juu ambayo yameanza kujadiliwa. Kwa maoni yangu mfumo wa Uchaguzi urekebishwe na kuruhusu mfumo mchanyato wa uwiano wa kura na mfumo wa “first-past-the-post” badala ya mifumo hiyo iliyotangulia. Mfumo wetu wa uchaguzi unataka Wabunge na Madiwani kupatikana kutoka katika majimbo na kata tu. Marekebisho yanayopendekezwa yanaturudisha nyuma zaidi. Kwa mfumo wa sasa wabunge wanawake hupatikana kwa uwiano wa kura za Wabunge nchi nzima na Madiwani wa wanawake kutokana na uwiano wa viti vya udiwani ambao kila chama kimepata. Lakini Wabunge Wanawake hawana mamlaka ya kisheria kwa eneo maalumu. Kwa sasa ni rahisi kusema kuwa wanatoka mikoani, lakini hii ni kwa sababu tuna chama kimoja kikubwa na hivyo kupata kura za kuenea mikoa yote. Huko mbele, tena na hawa wagombea binafsi, itatokea mikoa ambayo haitapata wabunge wanawake kwa sababu kura hazitotosha kwa chama kimoja kugawa wabunge kila mkoa. Umefikia wakati sasa kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa uchaguzi ili kuingiza uwakilishi wa uwiano. Kama nchi tutafakari mambo yafuatayo yanayohusu mabadiliko ya mfumo wa kisiasa wa nchi yetu: Mosi; Wabunge wa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi watokane na Halmashauri za Wilaya za sasa. Mfano, badala ya Wilaya ya Manispaa ya Kinondoni kuwa na Wabunge watatu, iwe na Mbunge mmoja tu. Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji ndio iwe Jimbo la Uchaguzi. Katika ngazi hii wagombea wasio na vyama waruhusiwe pamoja na wale wenye vyama. Kwa hali ya sasa tutapata Wabunge takribani 130 kutoka kundi hili. Idadi yao itaongezeka kutokana na kuongezeka kwa Halmashauri zitakazoundwa pindi mahitaji yanapotokea. Ikumbukwe kwamba katika ngazi ya chini kitovu cha mamlaka ni halmashauri, ambao ni msingi pia hata katika upangaji wa bajeti taifa.

Haitakuwa tena kazi ya Tume za Uchaguzi kuunda Majimbo ya uchaguzi bali vile vigezo vya kuunda Halmashauri (Baraza la Madiwani) vilivyopo kisheria (Local Government Authorities Acts) ndio vitatumika. Pili; Wabunge kati ya 150 na 200 watokane na kura za uwiano (idadi tofauti inaweza kupendekezwa). Vyama vya siasa vitapata viti kutokana na uwiano wa kura ambao kila chama kimepata katika Mkoa.

Chama cha siasa ni lazima kiwe kimepata kwanza asilimia tano ya kura zote zilizopigwa katika Mkoa husika ili kigawiwe viti. Kwa hiyo kila chama kitatengeneza orodha ya wagombea wake kwa kila Mkoa na kuipeleka Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Orodha hii iwe katika hali ambayo kama jina la kwanza ni Mwanaume la pili awe Mwanamke, hali kadhalika kama jina la kwanza ni Mwanamke katika orodha la pili liwe la mwanaume. Mikoa itapata idadi ya Wabunge kutokana na vigezo maalumu, mfano idadi ya watu n.k. Kwa mapendekezo haya tuna uhakika wa kuwa na Wabunge wanawake zaidi ya theluthi moja katika Bunge. Lakini pia tutakuwa na uhakika kwamba kila Mkoa utakuwa na Mbunge au Wabunge wanawake. Ama kwa lengo la kuongeza idadi kubwa ya wanawake kuelekea uwiano wa hamsini kwa hamsini(50-50), robo tatu ya wabunge wa uwiano inaweza kuwa ni orodha ya wanawake na robo ikabaki kwa ajili ya wanaume. Lengo la kuwa na orodha ni kuwezesha pia vyama kutumia orodha hiyo kuhakikisha uwakilishi wa makundi ya kijamii mathalani walemavu, vijana na viongozi muhimu wa kijamii ambao ni muhimu kuwepo bungeni.

Mabadiliko haya ya mfumo wetu wa Uchaguzi yana faida nyingi sana. Moja ya faida ni kuvigeuza vyama vyetu vya siasa kutoka katika kushindanisha watu tu, bali pia kushindanisha sera. Kwa sababu wananchi watakuwa wanapiga kura mbili. Kura moja ya chama na kura nyingine ya ama diwani au Mbunge na Rais. Kura ya chama ndio itatufanya kupata wabunge wa uwiano. Wala hatutatumia mfumo mmoja kuzalisha mfumo mwingine. Bali kila mfumo utazalisha Wabunge kuunda Bunge letu. Sisi hatutokuwa wa kwanza kufuata mfumo huu wa uwiano-Msumbiji, Afrika ya Kusini, Ujerumani, Uswidi na hata India.

Vyama vikianza kushindanisha sera tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana kama nchi katika kuimarisha mfumo wa demokrasia na kwa kweli hatutokuwa na wasiwasi wa vyama kudhoofika kutokana na wagombea Binafsi kuruhusiwa. Demokrasia ndani ya vyama itaimarika kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi itahakikisha vyama vinapata wawakilishi wake katika Orodha ya Mikoa kidemokrasia. Tubadili mfumo wa uchaguzi tupate viongozi bora!

Wednesday, November 5, 2008

Obama-Tumaini la Mabadiliko ya kweli








Nafurahi ikulu nyeupe imepata Rais mweusi. Ndoto ya Martin Luther King ya kutaka Wamarekani wahukumiane sio kwa rangi bali kwa tabia na uwezo imetimia kwa Obama. Changamoto kwa Rais mteule ni kusimamia mabadiliko aliyoahidi. Pamoja na kuwa Marekani ni Marekani na misingi ya sera zake inajulikana; kupumzishwa kwa Republican na kuingia wa Democrat kunaleta tumaini jipya katika siasa za nchi yao na dunia kwa ujumla. Nawapongeza vijana wa Marekani kwa kuwa mstari wa mbele kufanya kampeni za kisasa zenye hamasa na zilizochangia Barack kushinda. Mwaka 2005 kama ilivyokuwa kwa Obama sasa, CHADEMA tulikuwa na kauli mbiu ya kutaka mabadiliko ya kweli, na wakati huo mimi nikiwa mgombea ubunge jimbo la Ubungo nilisimamia siasa za kizazi kipya kama njia ya kuleta maisha mapya; jambo kubwa ambalo watanzania hususani vijana wanapaswa kujifunza kutoka kampeni za Obama ni kuwa wakala wa mabadiliko wanayotaka kuyaona 2010 na kuendelea. Ni muhimu kwa raia kuunga mkono wagombea na vyama wazi kwa hali na mali kwa siasa safi za sera.



John Mnyika

Kaimu Mkurugenzi wa Mahusiano ya Kimataifa na

Mkurugenzi wa Vijana


Nimesoma hii hotuba ya Obama ya kukubali kuchaguliwa; baadhi ya maudhui niliwahi kuyaandika huko nyuma katika makala hii: http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_15.html


na mengine niliyahubiri sana katika kampeni zangu za uchaguzi mwaka 2005.



"If there is anyone out there who still doubts that America is a place where all things are possible, who still wonders if the dream of our founders is alive in our time, who still questions the power of our democracy, tonight is your answer.It's the answer told by lines that stretched around schools and churches in numbers this nation has never seen, by people who waited three hours and four hours, many for the very first time in their lives, because they believed that this time must be different, that their voice could be that difference. It's the answer spoken by young and old, rich and poor, Democrat and Republican, black, white, Latino, Asian, Native American, gay, straight, disabled and not disabled - Americans who sent a message to the world that we have never been a collection of Red States and Blue States: we are, and always will be, the United States of America.It's the answer that led those who have been told for so long by so many to be cynical, and fearful, and doubtful of what we can achieve to put their hands on the arc of history and bend it once more toward the hope of a better day.It's been a long time coming, but tonight, because of what we did on this day, in this election, at this defining moment, change has come to America.'Unyeilding support'I just received a very gracious call from Senator McCain. He fought long and hard in this campaign, and he’s fought even longer and harder for the country he loves. He has endured sacrifices for America that most of us cannot begin to imagine, and we are better off for the service rendered by this brave and selfless leader. I congratulate him and Governor Palin for all they have achieved, and I look forward to working with them to renew this nation's promise in the months ahead.I want to thank my partner in this journey, a man who campaigned from his heart and spoke for the men and women he grew up with on the streets of Scranton and rode with on that train home to Delaware, the vice president-elect of the United States, Joe Biden. I would not be standing here tonight without the unyielding support of my best friend for the last sixteen years, the rock of our family and the love of my life, our nation’s next First Lady, Michelle Obama. Sasha and Malia, I love you both so much, and you have earned the new puppy that's coming with us to the White House. And while she's no longer with us, I know my grandmother is watching, along with the family that made me who I am. I miss them tonight, and know that my debt to them is beyond measure.To my campaign manager David Plouffe, my chief strategist David Axelrod, and the best campaign team ever assembled in the history of politics - you made this happen, and I am forever grateful for what you’ve sacrificed to get it done.But above all, I will never forget who this victory truly belongs to - it belongs to you.I was never the likeliest candidate for this office. We didn’t start with much money or many endorsements. Our campaign was not hatched in the halls of Washington - it began in the backyards of Des Moines and the living rooms of Concord and the front porches of Charleston. 'Task ahead'It was built by working men and women who dug into what little savings they had to give five dollars and ten dollars and twenty dollars to this cause. It grew strength from the young people who rejected the myth of their generation's apathy, who left their homes and their families for jobs that offered little pay and less sleep, from the not-so-young people who braved the bitter cold and scorching heat to knock on the doors of perfect strangers, from the millions of Americans who volunteered, and organized, and proved that more than two centuries later, a government of the people, by the people and for the people has not perished from this Earth. This is your victory. I know you didn't do this just to win an election and I know you didn't do it for me. You did it because you understand the enormity of the task that lies ahead. For even as we celebrate tonight, we know the challenges that tomorrow will bring are the greatest of our lifetime - two wars, a planet in peril, the worst financial crisis in a century. Even as we stand here tonight, we know there are brave Americans waking up in the deserts of Iraq and the mountains of Afghanistan to risk their lives for us. There are mothers and fathers who will lie awake after their children fall asleep and wonder how they'll make the mortgage, or pay their doctor's bills, or save enough for college. There is new energy to harness and new jobs to be created; new schools to build and threats to meet and alliances to repair.The road ahead will be long. Our climb will be steep. We may not get there in one year or even one term, but America - I have never been more hopeful than I am tonight that we will get there. I promise you - we as a people will get there. There will be setbacks and false starts. There are many who won’t agree with every decision or policy I make as President, and we know that government can’t solve every problem. But I will always be honest with you about the challenges we face. I will listen to you, especially when we disagree.And above all, I will ask you join in the work of remaking this nation the only way it's been done in America for 221 years – block by block, brick by brick, calloused hand by calloused hand. 'Spirit of patriotism'What began twenty-one months ago in the depths of winter must not end on this autumn night. This victory alone is not the change we seek – it is only the chance for us to make that change. And that cannot happen if we go back to the way things were. It cannot happen without you.So let us summon a new spirit of patriotism; of service and responsibility where each of us resolves to pitch in and work harder and look after not only ourselves, but each other. Let us remember that if this financial crisis taught us anything, it’s that we cannot have a thriving Wall Street while Main Street suffers – in this country, we rise or fall as one nation, as one people.Let us resist the temptation to fall back on the same partisanship and pettiness and immaturity that has poisoned our politics for so long. Let us remember that it was a man from this state who first carried the banner of the Republican Party to the White House – a party founded on the values of self-reliance, individual liberty, and national unity.Those are values we all share, and while the Democratic Party has won a great victory tonight, we do so with a measure of humility and determination to heal the divides that have held back our progress. As Lincoln said to a nation far more divided than ours, "We are not enemies, but friends ... though passion may have strained it must not break our bonds of affection." And to those Americans whose support I have yet to earn – I may not have won your vote, but I hear your voices, I need your help, and I will be your President too. And to all those watching tonight from beyond our shores, from parliaments and palaces to those who are huddled around radios in the forgotten corners of our world – our stories are singular, but our destiny is shared, and a new dawn of American leadership is at hand.'Peace and security'To those who would tear this world down – we will defeat you. To those who seek peace and security – we support you. And to all those who have wondered if America’s beacon still burns as bright – tonight we proved once more that the true strength of our nation comes not from our the might of our arms or the scale of our wealth, but from the enduring power of our ideals: democracy, liberty, opportunity, and unyielding hope. For that is the true genius of America – that America can change. Our union can be perfected. And what we have already achieved gives us hope for what we can and must achieve tomorrow. This election had many firsts and many stories that will be told for generations. But one that’s on my mind tonight is about a woman who cast her ballot in Atlanta. She’s a lot like the millions of others who stood in line to make their voice heard in this election except for one thing – Ann Nixon Cooper is 106 years old. She was born just a generation past slavery; a time when there were no cars on the road or planes in the sky; when someone like her couldn’t vote for two reasons – because she was a woman and because of the color of her skin.And tonight, I think about all that she's seen throughout her century in America – the heartache and the hope; the struggle and the progress; the times we were told that we can’t, and the people who pressed on with that American creed: Yes we can. 'Common purpose'At a time when women’s voices were silenced and their hopes dismissed, she lived to see them stand up and speak out and reach for the ballot. Yes we can. When there was despair in the dust bowl and depression across the land, she saw a nation conquer fear itself with a New Deal, new jobs and a new sense of common purpose. Yes we can. When the bombs fell on our harbor and tyranny threatened the world, she was there to witness a generation rise to greatness and a democracy was saved. Yes we can. She was there for the buses in Montgomery, the hoses in Birmingham, a bridge in Selma, and a preacher from Atlanta who told a people that “We Shall Overcome.” Yes we can. 'Fundamental truth'A man touched down on the moon, a wall came down in Berlin, a world was connected by our own science and imagination.And this year, in this election, she touched her finger to a screen, and cast her vote, because after 106 years in America, through the best of times and the darkest of hours, she knows how America can change. Yes we can. America, we have come so far. We have seen so much. But there is so much more to do. So tonight, let us ask ourselves – if our children should live to see the next century; if my daughters should be so lucky to live as long as Ann Nixon Cooper, what change will they see? What progress will we have made? This is our chance to answer that call. This is our moment. This is our time – to put our people back to work and open doors of opportunity for our kids; to restore prosperity and promote the cause of peace, to reclaim the American Dream and reaffirm that fundamental truth – that out of many, we are one, that while we breathe, we hope, and where we are met with cynicism, and doubt, and those who tell us that we can't, we will respond with that timeless creed that sums up the spirit of a people:

Saturday, November 1, 2008

Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika




Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika

Ni saa sita na ushee usiku. Siku mpya imeanza, ni Novemba Mosi; ni siku ya vijana Afrika. Najaribu kutafakari maudhui ya siku hii ya pekee kwa vijana Afrika kama ilivyopitishwa na umoja wa Afrika. Natafakari ujumbe wa mwaka huu “Maadili chanya ya kiafrika, amani na mshikamano”. Tafakari yangu inanirudisha nyuma katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja wa Afrika aliyoitoa usiku wa Oktoba 31 mwaka 2008. Mwangi wa maneno ya Rais wa nchi yangu unarindima katika kichwa changu na kunikosesha usingizi. Si kwa uzito wa maneno bali kwa hofu yangu juu ya madhara ya wepesi wa maneno yenyewe kwa mwelekeo wa taifa.

Nagutuka; nagundua natafakari ubatili, najihisi kama afukuzaye upepo. Haraka nachukua moja ya vitabu vitakatifu, najaribu kutafuta maneno ya kupoza hisia zinazoniandama. Napekua pekua bila kujua nini hasa natafuta kusoma, nakutana na kisa cha Mfalme Nebukadneza. Napata shauku ya kurudia kisa chake nilichokikariri nilipokuwa mtoto, nakutana na maneno ‘mene mene na tekel’. Najikumbusha maana yake; ‘ufalme wake umepimwa na umeonekana haufai’!

Natabasamu kwa uchungu. Ni kama nimeona kidole kikiandika maandishi hayo katika ukuta wa taifa letu. Naukumbuka mjadala ulioibuliwa na Katibu wa Itikadi wa CCM, John Chiligati, ambaye pia ni Waziri katika serikali ya Rais Kikwete wa kubeza na kutweza wenye kuhoji uwezo wa Rais Kikwete. Nakumbuka kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwamba nchi imekwama Rais Kikwete ameelemewa. Nakumbuka maneno ya Mbowe akitangaza kwamba Rais Kikwete ameshindwa kuliongoza taifa na hivyo kuna haja ya watanzania kutompa kura yeye na chama chake katika uchaguzi wa mwaka 2010. Nakumbuka maneno ya Waziri Mkuu na Jaji mstaafu Joseph Warioba kwamba nchi si shwari. Mene mene na tekel!

Napata nguvu ya kuamka na kuandika; Rais Kikwete amenidhihirishia mimi niliye mdogo, ambaye sistahili hata kufungua kidamu za viatu vyake kwamba anaipeleka nchi harijojo. Katiba ya nchi yetu inatamka kwamba kila mtu anastahili heshima lakini katika medani ya uongozi; heshima ya mtawala inalindwa kwa maneno na matendo yake. Namheshimu Rais Kikwete lakini maneno na matendo yake, yanastahili kukosolewa. Hakika hotuba ya Rais wetu imenidhihirishia pia kuwa hata wale washauri na wasaidizi wake waliopo pale Ikulu na serikalini wanapaswa kutuambia watanzania kwanini kodi zetu zitumike kuendelea kuwalipa mishahara kama wanashindwa kutimiza wajibu wa kulinda heshima ya taasisi ya Urais. Nakabiliwa na mtanziko bado, kati ya kuandika vile ninavyoamini na kuonekana kwamba sinaheshima kwa Amiri Jeshi mkuu. Ama kusema ukweli, nikiamini kwamba Rais aliye kioo cha taifa letu atachukua hatua za haraka kujirekebisha na kurekebisha hali ya mambo inavyokwenda katika taifa letu. Rais Kikwete aliwahi kusema kwamba alikuwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu Nyerere; hivyo naamini amesoma waraka wake wa ‘tujisahihishe’. Kutenda kosa si kosa, kosa kurudia kosa.

Kadiri hotuba ya Rais ilivyokuwa ikicheleweshwa ndipo matumaini yalipozidi kwamba pengine kulikuwa na mambo mazito ambayo mkuu wa nchi alikuwa akiyaandaa. Shauku ya kukosa hotuba za Rais kwa mwezi wa Septemba tofauti ya utaratibu ambao Rais amejiwekea ikazimwa kwa hotuba ambayo kimaudhui inafafana na hotuba ambayo tayari Rais alishaitoa Bungeni mwezi Agosti na kauli zake zilizofuatia katika ziara zake. Nikajiuliza; yamfaa nini mwanadamu kusema kama hana cha kusema?.

Rais wangu alionekana kuelemewa na mambo moyoni, haiba yake imegubikwa na uchovu pengine kutokana na ziara nyingi ama ni msongo wa mawazo au ni tatizo la macho yangu la kuona yasiyopaswa kuonekana. Rais alikuwa akihutubia kwa kutazama huko na kule kama vile palikuwa na nguvu za giza pembeni zikimzinga asitoe mwanga kwa taifa letu analoliongoza. Wanasaikolojia wanajua, jinsi ujumbe unavyotolewa unaweza kusema mengi kuliko hata ujumbe wenyewe.

Rais akaanza kwa kugusa suala tete la Tanzania kujiunga na OIC. Moja kwa moja akawaasa watanzania wasiuendeleze mjadala huo. Mjadala ambao umeendelezwa na serikali yake yenyewe, mjadala ambao yeye mwenyewe katika hotuba yake ameweka bayana kwamba serikali inauendeleza. Nikashangaa! Lakini nikashangaa zaidi kwa Rais Kikwete kutofautina wazi wazi na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Benard Membe ambaye Rais Kikwete amemuita kuwa ndio ana dhamana ya suala hilo. Wakati Rais anasema kwamba utafiti wa suala hilo bado haujakamilishwa na Waziri Membe, waziri mwenyewe wakati anahutubia bunge Agosti 22 mwaka huu huu alitangaza kwamba wizara yake imeshakamilisha utafiti. Nani mkweli kati yao Mungu ndio ajuaye. Lakini Mwalimu Nyerere, katika kitabu cha Uongozi wetu na hatma ya Tanzania, alizungumza vizuri kuhusu serikali. Mwalimu aliweka wazi, mkusanyiko wa mawaziri wasiokuwa na dira ya pamoja na uwajibikaji wa pamoja, wanabaki kuwa serikali kwa mujibu wa sheria tu. Lakini kimaadili na kimantiki; hakuna serikali! Rais anataka kila mtu akae kimya aiachie Wizara imalize kazi yake, kama vile wizara ni chombo kisikokuwepo Tanzania kisichowajibika kufanya kazi kwa kuzingatia hisia na matakwa ya watanzania. Kwa mtindo huu wa funika kombe, Rais Kikwete anazidi kuligawa taifa chini kwa chini; ni kama kujaribu kufunika moshi na kujifariji kuwa hakuna moto.

Liliamshwa la mpasuko Zanzibar; likajadiliwa, likakwamishwa. Liliibuliwa na mahakama ya kadhi; likakolezwa, likafunikwa. Likaibuliwa la mafisadi; likavumishwa, likatulizwa. Limeibuka la OIC; likachochewa, limefutikwa. Uongozi wa kuahirisha matatizo badala ya kuyatatua! Haya na mengine ni mabomu ya wakati.

Zoezi la kutumia visingizio kuahirisha matatizo likaendelea katika suala la walimu pia. Nilitaraji walau kwa mara hii Rais awaombe radhi walimu kwa ahadi yake aliyoitoa awali ambayo haikutimizwa katika tarehe ambayo aliitaja mwenyewe. Kwa kuwa sakata hili liko mahakamani; niishie hapa, nivute subira. Walimu waendelee tu kusota kwa sababu ya udhaifu wa serikali wa kutoweka kumbukumbu vizuri za waliofariki na zile za kutambua stahiki za kila Mwalimu. Serikali isiyoweza kuwatambua wafanyakazi wake inaweza kweli kuwakumbuka wananchi wa kawaida?

Ndipo Rais alipohamia kwenye changamoto ya hali ya uchumi ya dunia na hasa wa mfumo wa fedha unaozikabili nchi zilizoendelea. Kilichonishangaza ni Rais kutumia muda mrefu kuhutubia yale yale ambayo aliyasema kwa taifa Katika hotuba yake ya Tanga wakati wa sherehe za kuzima Mwenge na maadhimisho ya miaka tisa ya kifo cha, hayati Mwalimu Julius Nyerere. Halafu Rais katika kutafuta suluhisho la suala hilo, hoja kuu aliyoitoa ni kukaribisha wazo la Rais George Bush wa Marekani la kuitisha mkutano maalum wa kimataifa wa kuzungumzia tatizo la kifedha la kimataifa!. Utegemezi wa mawazo toka Washington ndio unaotufanya tusahau kulinda mihimili ya kiuchumi ambayo awamu zilizopita za utawala wa nchi yetu zilijaribu kuiweka. Kubwa zaidi, nilitarajia Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kuwaeleza watanzania ni jinsi gani anakusudia kuziunganisha nchi zingine za Afrika kuhakisha nafasi ya Afrika inahakikishwa. Badala yake Rais Kikwete ameishia kulalamika tu kwamba “kwa bahati mbaya afrika imesahaulika katika mkutano huo”. Rais Kikwete walau angetumia nafasi hiyo kueleza mikakati ya bara la Afrika hususani ile ya kuunganisha jumuia mbalimbali za kiuchumi iliyojadiliwa nchini Uganda ambapo yeye alishiriki kama sehemu ya ujenzi wa nguvu ya kiuchumi ya bara letu. Uthabiti na ueledi kama huo ungekuwa ni zawadi nzuri kwa vijana wa Tanzania wakati wanaungana na wenzao kuadhimisha siku ya vijana Afrika.

Kama ilivyotarajiwa na wengi Rais Kikwete akagusia suala la mauji ya Maalbino, ikiwa ni siku chache toka alizungumze suala hilo kwa kina Oktoba 19, 2008. Mara hii Rais akiwataka wananchi watoe kwa siri taarifa za watu wanaojihusisha na vitendo hivyo. Binafsi nilitarajia badala ya kutaka orodha mpya, Rais Kikwete kama alitaka kuzungumzia tena suala hili, angeueleza umma wa watanzania orodha za mwanzo za watuhumiwa wa mauaji ya maalbino ambazo ziliwasilishwa kwa vyombo vya dola ikiwemo kwa kufuatilia mtandao ulioanikwa na mwandishi wa habari wa BBC, Vicky Ntetema. Lakini haya mambo ya Rais Kikwete kutaka orodha za siri hayakuanza leo, aliwahi kutaka orodha ya watuhumiwa wa biashara ya madawa ya kulevya, akapatiwa; kimyaaa. Zikafuata orodha nyingine mbalimbali; hakuna hatua zinazoeleweka. Ndipo ikafuata ile orodha ambayo kwa ushujaa wa Dr Wilbroad Slaa(Mb) na viongozi wenzake wa upinzani waliamua kuitoa orodha hiyo hadharani kabisa pale Uwanja wa Temeke Mwembe Yanga. Orodha ya Mafisadi(list of shame) ikawekwa hadharani; hasara ya ufisadi uliotajwa inasababisha vifo vya watanzania wengi zaidi kila siku mpaka leo.

Kama kila siku wakina mama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma bora za kujifungua. Kama kila siku watanzania masikini wanakufa kwa kushindwa kuweza kununua dawa za kutibu malaria. Kama helikopta mbovu zinanunuliwa na kuua. Kama watoto wanakufa kwenye kumbi za disco kwa kukoseshwa hewa. Basi mafisadi ni sawa wauaji! Taifa linazidi kugawanyika, kati ya tabaka lenye kufa taratibu kwa kunyonywa kwa ufisadi na tabaka lililojifungia kwenye pepo ya akaunti za vijisenti mpaka nje ya nchi.

Rais Kikwete akaendelea kuikwepa Orodha ya Mafisadi kwa ukamilifu wake, akaendelea kuzungumzia suala la EPA tu. Akaendelea kukwepa kusema chochote kuhusu Meremeta, Tangold, Deep Green na ufisadi mwingine ambao kwa ujumla wake ni mara kumi ya bilioni 133 za EPA.

Lakini hata kwenye EPA kwenyewe, Rais Kikwete katika hotuba yake ameendelea kukwepa kuchukua uamuzi; amepalilia mche wa mbegu ya ubaguzi katika utawala wa sheria ambayo aliipanda Agosti 21 mwaka 2008 kupitia hotuba yake bungeni.

Rais Kikwete ameendelea kuliganya taifa kwa kuwalinda mafisadi na kugeuza suala lao kuwa la madai badala ya jinai.

Katika hotuba yake Rais Kikwete anatoa pongezi kwa Kamati ya Mwanasheria Mkuu “kwa kazi nzuri iliyofanya ambayo mbali na kubaini namna ya tuhuma za uhalifu zilivyofanywa, pia ilibaini wahusika na kuwabana kiasi cha kufanikiwa kurejeshwa kwa fedha ambazo vinginevyo zingepotea kabisa. “

Kama Rais Kikwete mwenyewe anakiri kwa maneno yake mwenyewe kwamba kamati yake imebaini uhalifu na wahalifu sasa ni vipi Rais huyu huyu anawapa msamaha wahalifu kabla ya kufikishwa mahakamani? Anawapa msamaha huu kwa sheria ya nchi gani? Maana Katiba ya nchi na sheria ambazo Rais ameapa kuvilinda vinampa mamlaka chini ya utaratibu maalum wa kusamehe watu kwa sababu Fulani Fulani baada ya kushtakiwa na kuhukumiwa(clemance/parole). Hakika Rais Kikwete amekiuka katiba kwa kuendesha nchi kwa ubaguzi na kuvunja sheria za nchi kwa kulinda wahalifu. Kwa mantiki hii, na vijana wezi nao wakirudisha mali za wizi nao waachiwe huru tu ili tujenge taifa la misamaha ili wajumuike na hao mafisadi walioghushi nyaraka na kuhujumu uchumi wa taifa. Milango ya magereza na ifunguliwe ili majambazi waachiwe huru, na milango ya mahakama ifungwe ili wezi wasishitakiwe tena; ili tujenge taifa lisilo na utawala wa sheria, linaoendeshwa kwa kanuni za mwituni. Mene mene na tekel!

Namsikiliza Rais wangu kwa mara nyingine akitaja kiwango cha fedha kilichorudishwa bila kuwa na hakika. Kwa mara nyingine akitoa maagizo ya kufungua mashtaka kwa watu ambao hawajarudisha fedha; maagizo ambayo aliyayatoa siku nyingi. Kwa yale makampuni mengine tisa yaliyofisadi bilioni 40 Rais ndio kwanza ‘anakusudia’ kuwataka polisi waendelee na uchunguzi. Na kati ya hayo ipo ile kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota takribani bilioni 30 ambazo nyingine zimeelezwa na vyanzo mbalimbali kuwa zilitumika kwenye kampeni za uchaguzi zilizomweka yeye na chama chake cha CCM madarakani. Rais Kikwete amekosa uthubutu na uthabiti wa kuwataja hadharani maswahiba wake na kuwachukulia hatua. Mene mene na tekel.
Rais Kikwete amemalizia hotuba yake kwa kutusihi watanzania tujiepushe na mambo yanayoweza kutugawa na kupandikiza mbegu za chuki miongoni mwetu na badala yake tuimarishe maelewano, mshikamano na umoja wa kitaifa. Misingi ambayo yeye mwenyewe ameibomoa kwa maneno na matendo yake. Ukiona wananchi wanazomea viongozi, wanarusha mawe, wanalala barabarani ujue migawanyiko imeshapandikiza mbegu ya chuki na kukata tamaa. Vitabu vitakatifu vinaeleza kwamba amani ni tunda la haki. Maelewano tunayopaswa kuyaimarisha ni yale ya kutambua asili na matitizo yanayolikabili taifa letu na kuelewana suluhu tunayohitaji. Mshikamano tunapaswa kuuimarisha ni wa kuunganisha nguvu ya umma katika kuleta mabadiliko tunayoyahitaji. Umoja wa kuimarisha ni unaojengwa kwa misingi ya uadilifu na fikra mbadala zenye kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa.

Daima tukumbuke; mabadiliko ya kweli katika taifa letu hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale kwa ari, nguvu na kasi mpya. Kwa falsafa ya chukua chako mapema(ccm), Tanzania yenye neema haiwezekani. Ni wakati wa kusimama na kujitambulisha; ama upande wa kuliunganisha taifa ama kuligawa, historia itakuhumu kwa kadiri ya maamuzi yako ya leo. Mene mene na tekel. Tuombe ulinzi wa Mungu tuvuke salama!

John Mnyika
Novemba Mosi, 2008-Mwanza, Tanzania

Friday, October 31, 2008

“VIJANA TUFIKIRI NA KUUNGANA KUKOMBOA AFRIKA”



TAARIFA KWA UMMA

SALAMU ZA MSHIKAMANO KATIKA SIKU YA VIJANA AFRIKA

“VIJANA TUFIKIRI NA KUUNGANA KUKOMBOA AFRIKA”

Novemba Mosi ni siku ya Vijana Afrika. Siku hii imepitishwa na Umoja wa Afrika kama siku maalum ya kuadhimisha na kutafakari mchango wa vijana katika maendeleo ya bara letu kiuchumi, kisiasa na katika nyanja mbalimbali za jamii. Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA(BAVICHA), napenda kuungana na vijana wote barani Afrika katika kuadhimisha siku hii.

Kama sehemu ya maadhimisho hayo, vijana wa CHADEMA wamepanga kufanya mkutano na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama Novemba Mosi ili kuzungumzia hali ya siasa, uchumi na kijamii katika bara la Afrika katika muktadha wa changamoto zinazowakabili vijana na fursa ambazo zinaweza kutumika.

Nachukua fursa hii kutoa salamu za mshikamano kwa vijana wote kuungana kuitumia siku hii kutafakari nafasi na wajibu wa vijana katika kuleta demokrasia na maendeleo katika bara la Afrika.

“Vijana wa zamani kama Mwalimu Nyerere, Nkurumah Mandela na wengineo walitumia ujana wao kupambana na ukoloni, na kuleta uhuru katika mataifa yao. Ni wajibu wa vijana wa sasa kuwa mstari wa mbele katika kukabiliana na ushindani wa kibeberu unaoliathiri bara la Afrika nyuma ya kivuli cha utandawazi. Vijana wanaweza kutekeleza wajibu huu vizuri kama watathubutu kufikiri na kufikiri kuthubutu kuunganisha nguvu bila kujali mipaka ya nchi, hali au itikadi”

Bara la Afrika ni bara ambalo limejaliwa rasilimali, lakini rasilimali hizi zimegeuzwa na watawala kuwa laana(resource curse) yenye kuchochea vita na kuongezeka masikini kwa wananchi walio wengi hususani vijana.

Tunachukua fursa hii kuwataka vijana wa Afrika badala ya kuelekeza nguvu zao kutumika katika vita na migogoro ya wenyewe kwa wenyewe watumie nguvu hizo kupambana na ufisadi, kutetea rasilimali na kuleta mabadiliko katika mataifa yao kupitia fikra mbadala.

Nafasi ya vijana kuleta ukombozi katika bara ni kubwa kama vijana watatumbua kwamba bara la Afrika lina uwingi mkubwa wa vijana kuliko makundi rika mengine; na kwamba vijana wakijitazama na kutazamwa kama suluhisho badala ya tatizo wanaweza kutoa mchango mkubwa zaidi katika maendeleo ya bara letu.

Ni vyema, waunda sera na watoa maamuzi barani Afrika wakatambua uwepo wa ongezeko kubwa la idadi ya vijana(youth population bulge) na kwamba wachukulie hali hii kuwa ni fursa badala ya tatizo. Bila hali hii kutambuliwa rasmi na kuundiwa sera na mikakati, matatizo yanayowakabili vijana mathalani ongezeko la ukosefu wa ajira, upungufu wa fursa za kielimu, mmomonyoko wa maadili, ongezeko la matumizi ya madawa ya kulevya na kusambaa kwa ugonjwa wa VVU/UKIMWI miongoni mwa vijana yatazidi kushamiri.

Changamoto ya ongezeko la vijana Afrika inaathiri zaidi miji mikubwa katika Afrika kutokana na kasi ya vijana kutoka vijijini kukimbilia mijini kutafuta fursa za maisha. Hivyo, katika kuadhimisha siku ya vijana Afrika kwa mwaka huu, mkazo uwekwe katika kuhamasisha uwepo wa mazingira ya kuboresha sekta zinazogusa vijana wengi Afrika hususani kwa kuboresha kilimo. Pia, sekta za rasilimali Afrika mathalani uchimbaji madini na mafuta ziwekewe mazingira ya kutoa ajira kwa vijana walio wengi badala za sekta hizo kutawaliwa na makampuni makubwa ya kigeni. Hata pale sekta hizo zinapotawaliwa na uchimbaji mkubwa mkazo uwekwe kuhakikisha muunganiko wa mbele na nyuma(forward and backward linkage) na sekta nyingine za kiuchumi.

Ili kuhakisha kwamba nguvu ya umma ndio inakuwa msingi wa uongozi katika Afrika, vijana wachukue hatua za kulinda demokrasia Afrika ambayo imeanza kutetereshwa na utadamuni ambao unaoendelea katika bara hili wa kung’ang’ania madaraka. Utamaduni huu unachukua sura ya baadhi ya nchi kutawaliwa kijeshi lakini pia unachukua sura ya ung’ang’anizi wa madaraka hata baada ya chaguzi kutaka vingenevyo kwa kutumia mwanya wa uundaji wa serikali za mseto ama za umoja wa kitaifa kama njia ya kuepusha migogoro.

Mwisho, ili kuwa na muongozo wa pamoja katika kuwezesha vijana kutimiza wajibu wao katika bara la Afrika, tunatoa rai kwa serikali za Afrika ambazo hazijaridhia bado Mkataba ya Vijana wa Afrika(African Youth Charter) ulipitishwa na viongozi wa umoja wa Afrika mwaka 2006 mjini Banjul nchini Gambia kufanya hivyo mara moja. “Na katika hili, namtaka Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika aonyesha mfano mzuri kwa wenzake kama kweli wamedhamiria kuweka mstari wa mbele kushughulikia masuala ya vijana. Inashangaza kwamba mpaka pamoja na Rais Kikwete kusaini mkataba huo mwaka 2006 akiwa mjini Banjul, mpaka sasa mkataba huo haujaridhiwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kila mwaka, kuanzia wakati huo mpaka sasa, Wizara inayohusika na masuala ya vijana imekuwa ikitoa kauli kwamba mkataba huo utaridhiwa ‘kikao kijacho cha bunge’. Hata hivyo vikao vingi vimepita bila mkataba huo kuridhiwa; wakati sasa umefika wa Rais Kikwete kama Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri kuiwajibisha hadharani wizara inayohusika kwa kuchelewa kutimiza wajibu huu muhimu wa maendeleo ya vijana wa Tanzania na Afrika kwa ujumla”

Ujumbe huu umetolewa Mwanza-Tanzania 31 Oktoba 2008 na:

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa

Monday, October 27, 2008

Salamu za Mshikamano kuunga mkono Maandamano ya Wadau wa Habari

Salamu za Mshikamano kuunga mkono Maandamano ya Wadau wa Habari

Ndugu Wahariri

Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) tukiwa ni sehemu ya wadau wa sekta ya habari nchini, tunaunga mkono maandamano ya amani mliyoitisha ya kupinga hatua ya serikali kulifungia gazeti la MwahaHALISI.

Tunawapongeza wahariri kwa mshikamano wenu katika kipindi hiki cha majaribu; endeleeni kusimama pamoja, ni umoja wenu ndio utakaokuwa kinga ya pamoja dhidi mtu au chombo chombo chochote kinachoingilia uhuru wenu. Mshikamano wenu ni ishara ya kushindwa kwa mkakati wa ‘wagawe uwatawale’ na imani kwamba umoja ni nguvu. Wahariri wote hawapaswi kukaa kimya kuhusu kufungiwa kwa MwanaHALISI kwa kuwa leo ni kwa gazeti hilo, kesho itakuwa kwa gazeti lingine; hivyo ni vyema kuungana pamoja kulinda uhuru, taaluma na sekta ya habari nchini.

Kwetu sisi hatua hiyo ya serikali tunaitafsiri zaidi ya kufungia gazeti la MwanaHALISI; ni hatua ya kufungia uhuru wa kusambaza habari na uhuru wa kupokea habari. Hivyo hatua hiyo ni kinyume cha haki za binadamu, kinyume cha utawala bora na ni kikwazo kwa demokrasia na maendeleo. Hakika serikali na viongozi wake wamevuka mstari wa kukubali kukosolewa na sasa wameamua kuanza kufungia uhuru wa fikra mbadala.

Hatua ya Waziri mwenye dhamana na sekta ya habari kugeuka mlalamikaji, mwendesha mashtaka na mfungaji ni mwelekeo mbovu wa kupuuza taasisi za kusimamia uwajibikaji na haki. Uamuzi uliofanywa na serikali hauna tofauti na unaofanywa na raia wanaojichukulia sheria mikononi(mob justice). Kwa serikali inayoheshimu misingi ya asili ya haki, tulitarajia chombo chochote cha habari, kikivunja sheria ama kukiuka maadili dhidi ya serikali, viongozi wake ama watu binafsi mashtaka ama malalamiko yangepelekwa kwa taasisi zinazohusika mathalani Baraza la Habari(MCT) ama Mahakama.

Hatua ya serikali kufungia gazeti la MwanaHALISI pamoja na kuwa imechukuliwa kwa mujibu wa sheria iliyopo, imekiuka misingi ya asili ya utawala wa sheria. Kwani kulikuwa na sheria nyingine nzuri ambazo serikali ingeweza kutumia kupitia mahakama lakini ikaamua kuchagua kutumia sheria mbaya kwa kutumia mamlaka ya Waziri. Itakumbukwa kwamba wadau wa sekta ya habari na hata serikali yenyewe imekuwa ikikiri kwamba Sheria hiyo iliyotumiwa ni sheria mbovu inayohitaji kufutwa ama kufanyiwa marekebisho makubwa ikiwemo kupunguza mamlaka makubwa ya viongozi wa serikali dhidi ya vyombo vya habari. Sheria yoyote inayotambulika kuwa mbovu katika jamii yoyote, inapoteza uhalali wa kihaki(legitimacy) miongoni mwa umma na hivyo kuendelea kuitumia ni kuteteresha misingi ya utawala wa sheria na kutoa mfano mbaya kwa vijana nchini na wananchi kwa ujumla. Hivyo, tunachukua fursa hii kuitaka serikali kuharakisha mchakato wa kupitisha sheria ya vyombo habari na sheria ya uhuru wa taarifa.

Aidha tumeshangazwa na uamuzi wa serikali kufanya maamuzi yake kwa ubaguzi kwa kulichukulia hatua gazeti la MwanaHALISI na kukwepa kuyachukulia hatua magazeti mengine ambayo yameandika habari inayoshabihiana na maudhui ya habari iliyoandikwa na gazeti hilo. Kwa muda mrefu sasa, habari za uwepo wa viongozi ama makundi ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) yenye kupanga ‘kumng’oa’ Rais Jakaya Kikwete miongoni mwa wanaotarajiwa kugombea urais kupitia chama hicho mwaka 2010 zimeandikwa na magazeti mbalimbali. Hatua hii ya kibaguzi inaibua maswali kuhusu dhamira ya serikali kulifungia gazeti hilo wakati huu ambapo mchango wa gazeti hilo na mengine yaliyo mstari wa mbele kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za taifa unahitajika kwa kiasi kikubwa. Hata baada ya kulifungia gazeti la MwanaHALISI, habari za aina hiyo zimeendelea kuandikwa ikiwemo na vyombo vya habari vya nje; mathalani tarehe 24 Oktoba, 2008 kutoka Ufaransa gazeti la Africa Intelligence inayomtaja Rostam Aziz kukusanya fedha kwa ajili ya kufadhili kundi lake katika uchaguzi huo. Katika muktadha huo, serikali inapaswa kulifungia gazeti la MwanaHALISI mara moja, kama imeonyesha wazi kushindwa kuyachukulia hatua magazeti mengine.

Kadhalika kwa mtiririko wa matukio katika taifa letu, kuna mwelekeo wa Serikali na CCM kuminya maoni yenye kumkosoa au kumgusa Rais Kikwete. Mjadala wa Rais Kikwete ‘kung’olewa’ katika uchaguzi mwaka 2010 unaelekea kuichukiza kwa kiasi kikubwa Serikali na CCM. Gazeti la MwanaHALISI liliandika habari ya namna hiyo, likafungiwa na Serikali. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe akiwa katika ‘Operesheni Sangara’, alitoa hoja hiyo na matokeo yake CCM ikaibuka na kujibu kwa vitisho na vioja. Vijana wa Tanzania wangependa kupata mfano uongozi bora wenye kukubali kukosolewa na kukubali mabadiliko badala ya uongozi legelege wenye kuendeleza udikitekta wa kimawazo na hivyo kuminya fikra huru. Si dhambi kwa CHADEMA ama mtu yoyote kutaka kuiondoa CCM ama kiongozi wake yoyote madarakani mwaka 2010 kupitia njia za kidemokrasia.

Mwisho, tunatoa mwito kwa watanzania wote kusoma alama za nyakati na kuunga mkono harakati hizi za wahariri na wadau wa sekta ya habari kutetea uhuru wa kweli katika taifa letu. Jamii itambue kwamba kitisho cha uhuru na haki kwa mtu Fulani au mahali Fulani ni tishio kwa watu wote na mahali pote. Yanayofanywa kwa vyombo vya habari, yanaweza pia kufanywa kwa watetezi wengine kwani hivi karibuni taifa limeshuhudia Asasi ya HAKIELIMU ikitishiwa kutokana na jitihada zake za kuhamasisha mabadiliko ya fikra katika sekta ya elimu na kupiga vita ufisadi unaoathiri sekta hiyo. Tuko katika kipindi cha majaribu; kuibuka kwa mijadala yenye kuchochea mgawanyiko/ubaguzi, kuongezeka kwa matabaka na malalamiko juu ya hali za maisha. Katika wakati huu ambapo misingi ya nchi yetu iliyopo katika Ngao ya Taifa ya Uhuru na Umoja inapotikiswa ni wakati wa kuunganisha “Nguvu ya Umma” kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa kwa kuhamasisha maadili, fikra mbadala na mabadiliko ya kweli. Kuunga mkono maandamano ya wadau wa sekta ya habari ni sehemu ya azma hiyo. Mshikamano, daima; pamoja, tutashinda!

Wasalaam,

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
Mwanza, Tanzania-28/10/2008





Tuesday, October 21, 2008

Ngawaiya: Nguvu ya Umma ilishinda yote Tarime

Ngawaiya: Nguvu ya Umma ilishinda yote Tarime

Na John Mnyika

Makala ya mtizamo wa Thomas Ngawaiya aliyejitambulisha kama Mkurugenzi wa Taasisi ya Utawala Bora na Maendeleo (CEGODETA) ya 21 Oktoba, 2008 si ya kupitwa bila kutolewa mtizamo mbadala.

Kwa mtizamo wake, Bwana Ngawaiya amejenga hoja za ‘vioja’ kadhaa: Mosi, amepotosha umma kuwa CHADEMA ilishikilia halmashauri ya Tarime kuanzia mwaka 2005. Pili, amepotosha zaidi umma kuwa viongozi wa CHADEMA wanakataza wananchi wasilipe kodi. Tatu, amedanganya umma kuwa kutokana na kukataza huko, Tarime imekosa maendeleo na kwamba miradi ya shule katika wilaya hiyo imeshindwa kutekelezwa na sasa shule hizo zimekuwa magofu. Nne, ameibua kioja kingine kwa hoja yake kuwa viongozi wa CHADEMA wanasera ya kutaka biashara zipitie njia za panya. Tano, ametoa mtazamo wake kuwa mapigano ya koo Tarime yanaletwa na mababa wa vita(war lords) kwa lengo la kujipatia fedha. Mwisho, ameibua uzushi wa kuhusisha CHADEMA na hoja ya wananchi kuhusu mbolea ya ruzuku tani 6,000 iliyopelekwa msimu uliopita kutowafikia walengwa.

Nitaacha kwa muda mjadala wa viti maalum, niliouchangia kwa wiki kadhaa sasa ili nipate fursa ya kuzijibu hoja hizi za Bwana Ngawaiya. Awali ya yote, ni vyema ikazingatiwa kuwa mwandishi wa mtazamo huu, amewahi kuwa Mbunge na kwa maana nyingine amewahi pia kuwa diwani; hivyo anaelewa utendaji wa halmashauri na pia wa serikali kwa ujumla wake kupitia uwajibikaji ambao unafanyika bungeni.

Hivyo, naamini upotoshaji huo wa hoja sita hapo juu, kama nitavyoeleza ameufanya si kwa kutokujua-bali kwa kudhamiria, kwa lengo la kuendeleza kile ambacho niliwahi kukiita; propaganda chafu!

Huko nyuma, niliwahi kuandika kwamba katika sanaa na sayansi ya siasa na maendeleo, kuna aina tatu za propaganda; propaganda nyeupe, huu ni ukweli ambao mimi hupenda kuuita propaganda safi, ni mfumo wa kusambaza ukweli kwa lengo la kujenga imani na kukubalika. Aina ya pili ni propaganda za kijivu, ambapo mwenezi au msambazaji huchanganya ukweli na uwongo katika sura ambayo kwa uchambuzi wa kawaida si rahisi kujulikana. Aina ya tatu, ni propaganda nyeusi ambayo huhusisha mahubiri ya uwongo. Unaotolewa kishujaa na kwa uwazi, katika hali ambayo, kama mtu haufahamu ukweli basi huweza kuamini uwongo kuwa ukweli na ukweli ukageuzwa kuwa uwongo.

Naandika makala haya, nikiwa nimerejea toka Tarime ambapo nimepata wasaa wa kuzunguka maeneo mbalimbali ya jimbo hilo na kuzungumza na wananchi. Kama ilivyoada ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo, iliendeleza zile zile mbinu zake za zamani za kutumia maadui, ujinga, umasikini, maradhi na ufisadi katika kutafuta madaraka kwa nguvu!

Nimeshuhudia, CCM ikijaribu kutumia umasikini wa watanzania kwa kufanya uchaguzi kuwa gulio la kura- kwa kugawa fedha taslimu wazi wazi, kununua kadi za kura, kugawa mavazi ili kutafuta ridhaa ya kuongoza. Nimeshuhudia, CCM ikitumia ujinga, kutafuta madaraka, ikijaribu kumwaga propaganda chafu badala ya sera safi ili kutafuta madaraka. Hakika mkakati huu, ulihusisha makada wa upotoshaji, mmojawao akiwa Bwana Thomas Ngawaiya. Katika mikutano yake, alikuwa akihubiri hizo hoja sita hapo juu, akijaribu kupotosha kila hali mtizamo na hatimaye msimamo wa wananchi wa Tarime. Katika kundi hilo, wapo pia makada wengine ambao kampeni zao hazikuwa na lingine zaidi ya kusingizia, mimi na viongozi wengine katika CHADEMA pamoja na watu wengine wa pembeni- kwamba tumemuua kwa ‘kumchoma na kisu na kumpiga na nyundo kichwani’ hayati Chacha Zakayo Wangwe(Apumzike kwa Amani). Nimeshuhudia, CCM wakijaribu kutumia maradhi ikiwemo kufadhili na kutuma vikundi vya kiharamia vyenye silaha kuwazuru wananchi ili kujenga mazingira ya hofu na vitisho kwa lengo la kupata madaraka. Katika kundi hili, nilishuhudia pia Askari polisi, waliotumwa kufanya operesheni demokrasia wakiwa wa kwanza kuanzisha ghasia ili kupata sababu ya kuwapiga wananchi, kutukamata na wakati huo huo kufanya vitendo vya uwizi na unyang’anyi. Nilishuhudia CCM, ikiwatumia maadui hawa watatu-ujinga, umasikini na maradhi kwa kumtumia vizuri adui namba nne aliyetangazwa na Mwalimu Nyerere-adui ufisadi! Haya ndiyo niliyoyashuhudia Tarime, chama kinachotawala, kikitumia kila aina ya ufisadi, kikifadhiliwa na fedha za mafisadi ili kushinda uchaguzi. Moyoni, nikasema wakishinda hawa, hakuna uadilifu utakaokuwepo zaidi ya kuendeleza ufisadi Tarime, kwa ari, nguvu na kasi mpya. Hivyo, Tarime ilikuwa mpambano kati ya mafisadi na umma.

Katikati ya mazingira hayo hayo ya kukatisha tamaa, nikashuhudia Tumaini Jipya. Nikashiriki katika kampeni ambazo ziliongozwa na maneno ya Mwalimu Nyerere kwamba ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Nikashuhudia falsafa ya CHADEMA, ya Nguvu ya Umma ikiwa katika maneno na vitendo-katika uhalisia kwenye maisha ya wananchi. Nikashuhudia: uwongo ukikabiliwa kwa ukweli; vitisho vikikutana na msimamo wenye amani. Wananchi wakasimamia haki na maendeleo kwa nguvu ya umma. Hakuna mabomu ya machozi, vipigo, risasi, rumande, mapanga ya maharamia yaliyoweza kuzima dhamira ya kuchagua viongozi wao na nguvu ya umma iliyohamasishwa miongoni mwa wananchi wa Tarime. Hakuna uwongo na propaganda chafu ulioweza kuushinda ukweli; hakika, wapiga kura waliufahamu ukweli na ukweli ukawapa uhuru wa kuchagua viongozi waliowataka. Kuna mengi niliyoyashuhudia Tarime, ambayo pekee yanaweza kuandikiwa mfululizo wa makala kadhaa, hususani hatua kwa hatua yaliyotokea tulipokamatwa na taathira yake katika siku zilizofuatia. Kwa ujumla kampeni zile zilijaa huzuni na furaha, huku vijana wakiwa mstari wa mbele kuandika historia. Vituko vya kampeni zile, navyo vinaweza kujaza kurasa.

Ukweli uliposambaa na kukabiliana na uwongo, hata CCM iliamua kuiga mikakati ya kampeni za kisayansi ikiwemo kutumia helikopta; kile chama kilichokuwa kikibeza matumizi ya helikopta kuwa ni anasa, nacho kikaleta helikopta mbili. Hata hivyo, kwa nguvu ya ukweli, wale wananchi waliokuwa wakibezwa kuwa ni ‘wahuni’ wanaokwenda kwenye mikutano ya Mbowe ‘kushangaa helikopta’ wakawazomea wao na helikopta yao! Helikopta za CCM zikawa karaha badala ya raha.

Bila kujiuliza ni kwanini yote haya yanayokea, CCM ikaendeleza kampeni za kuwatumia makada wake kusambaza propaganda chafu ikiwemo hizo sita hapo juu zilizokuwa zikipigiwa upatu na Bwana Thomas Ngawaiya.

Ukweli katika vichwa vya wananchi ulikuwa ukizijibu hoja hizo sita moja baada ya nyingine, na hukumu ya hoja hizo za uwongo ikiwa ni katika sanduku la kura. Sasa naona wameanza kuhamishia hoja hizo kwenye makala za magazeti ili kuwapotosha watanzania wa maeneo mengine ya nchi.

Wakati Ngawaiya na wenzake wakisema kuwa CHADEMA imeshikilia halmashauri toka mwaka 2005, wananchi walikuwa wakiwapuuza kwa kuwa wanajua ukweli kuwa mwaka 2005 CHADEMA ilishinda Ubunge na udiwani katika maeneo kata kadhaa; halmashauri ilikuwa chini ya CCM. Kwa taarifa ya Bwana Ngawaiya na wenzake, CHADEMA ilipata halmashuri ya Tarime mwaka 2007 baada ya Halmashauri ya awali kugawanywa kuwa mbili za Rorya na Tarime.

Wakati Bwana Ngawaiya na wenzake wasema kwamba viongozi wa CHADEMA wamewakataza wananchi kulipa kodi na hivyo kukwamisha maendeleo, wananchi wa Tarime walikuwa wanawapuuza. Kwa kuwa wanajua ukweli kuwa hakuna kiongozi aliyekataza wananchi wasilipe kodi. Wananchi wanaelewa wazi hoja ya Wabunge wa CHADEMA akiwemo marehemu Chacha Wangwe ilikuwa ni nini. Lakini inasikitisha kwamba Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo na Utawala Bora katika mtizamo wake gazetini anashindwa kabisa kuelewa tofauti kati ya michango na kodi. Kwa taarifa ya Bwana Ngawaiya, hakuna kiongozi wa CHADEMA aliyekataza wananchi wasilipe kodi. Kodi ni lazima, na kukataza mtu kulipa kodi ama kuzuia kodi kukusanywa ni kosa la jinai. Kwa hiyo Bwana Ngawaiya anataka kusema kuwa viongozi wa CHADEMA wamekuwa wakivunja sheria na serikali ya CCM chini ya Amiri Jeshi Mkuu Rais wa nchi ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho amekuwa akikaa kimya wakati wote? Wananchi wa Tarime wanajua kuwa wanalipa kodi kila wanaponunua bidhaa kama sukari na nyinginezo. Wanajua kabisa kuwa wote wanalipa kodi, tena kodi nyingi sana. Viongozi wa CHADEMA wametoa somo kuhusu kodi mpaka kimeeeleweka. Wafanyakazi Tarime wanajua kuwa wanalipa kodi. Suala la msingi kule, ni je, kodi zetu zinatumikaje, na nini mgawo unaobaki kwenye halmashauri kutokana na kodi hizo ikiwemo kodi zinazolipwa na Makampuni ya madini yaliyopo katika halmashauri hiyo? Je, haziwanufaishi mafisadi na tabaka la matajiri wachache? Na hapo ndipo inapozaliwa hoja ya michango, ambayo pengine ndiyo ambayo Ngawaiya alitaka kuizungumzia. Ni kweli, viongozi wa CHADEMA wamekuwa wakikataza wananchi kulipa michango, bila kwanza kuelezwa na kuridhika kwamba kodi wanazolipa hazitoshelezi kufanya maendeleo. Na pili, kupewa taarifa za mapato na matumizi ya michango iliyotangulia. Na tatu; wamewakataza wananchi kukataa kulipa michango kama michango hiyo inakusanywa kwa njia ambazo zinavunja haki za binadamu ikiwemo kupora mali za raia. Sasa kwa CCM na makada wake, ambao wamekubali serikali yao ilee ufisadi, itumie kodi za wananchi katika matumizi makubwa ya anasa; somo hili ni mwiba mchungu hususani katika uchaguzi!

Na hapo ndipo wanapozua vioja vingine, kwamba eti kutokana na uamuzi huo Tarime imekosa maendeleo. Ngawaiya na wenzake, wanashindwa kujua kabisa kuwa kwa miaka zaidi ya arobaini toka uhuru wa Tanzania, halmashuri ya Tarime imekuwa chini ya CCM ikikusanya kodi na kutoza michango lukuki bila maendeleo yanayokusudiwa. Wanajua kuwa Halmashauri zilizotangulia kuchukuliwa na CHADEMA kama Karatu zilionyesha njia kwa kufuta michango ya manyanyaso lakini bado zikaweza kuleta maendeleo kwenye sekta za maji, elimu nk. Bahati nzuri, wananchi wa Tarime katika uchaguzi ule, walikuwa na rekodi za kulinganisha. Tuweke pembeni rekodi ya utawala wa giza wa CCM wa zaidi ya miaka 40 toka uhuru, wananchi walikuwa na fursa ya kulinganisha mwaka mmoja na nusu toka CCM ichukue halmashuri hiyo mwaka 2005 na mwaka mmoja toka CHADEMA ikuchukue halmashuri hiyo mwaka 2007. Na tofauti ilikuwa bayana. Wakati CCM kwa muda mrefu ikiwa inapokea mamilioni ya kodi toka kwenye migodi iliyomo kwenye halmashuri hiyo na mamilioni hayo kuishia kutumika kifisadi na mengine kutumika kwenye matumizi ya anasa ya posho za wakubwa katika halmashauri;CHADEMA ilifanya tofauti. Kwa muda mchache wa uongozi wa CHADEMA, Charles Mwera akiwa Mwenyekiti wa Halmashuri; CHADEMA ilipiisha utaratibu wa kwamba katika milioni 260 zinazopatikana toka migodini, milioni 140 zitumike kulipia elimu ya watoto wa Tarime kwa wastani wa milioni saba kwa kila kata. Hii ni sera ya CHADEMA ambayo imeanza kutekelezwa katika kata zote zenye madiwani wa CHADEMA, huko watoto wote waliopata nafasi ya kusoma Tarime wanasomeshwa bure na halmashauri yao. Kwa bahati mbaya, katika kata chache za madiwani wa CCM, wamekataa utaratibu huu na hivyo kukwamisha maendeleo ya vijana na watoto katika kata hizo! Hawa ndio wakina Ngawaiya wanaoamini kwamba ili tuendelee ni lazima wananchi wachangishwe kwa wingi zaidi na ni lazima kwenda kuomba omba nje ya nchi. Huu ndio utawala bora na maendeleo wanayohubiri.

Bwana Ngawaiya inaelekea haielewi hali halisi ya Tarime, inaelekea aliishia kwenye majukwaa ya kisiasa alipokuwa kule na hakupata fursa ya kutembelea shule zilizojengwa Tarime toka mwaka 2005 mpaka sasa ndio maana amezuka na kioja kuwa ‘shule zimetelekezwa na kuwa magofu’! Badala ya kuinyooshea kidole Tarime, ambayo imeonyesha mfano wa kuwa halmashuri pekee nchini ambayo wanafunzi wanasomeshwa bure, azitazame halmashuri zilizo chini ya chama chake CCM katika mkoa huo huo wa Mara. Aende Bunda akaone shule ambazo hazina vyoo, binafsi nafahamu shule sita katika wilaya hiyo ambazo hazina huduma hiyo muhimu kwa mwanadamu. Aende Wilaya ya Mugumu chini ya utawala wa miaka zaidi ya arobaini ya CCM hakuna barabara ya Lami, halafu alinganishe na Tarime iliyochini ya CHADEMA. Halafu apitie mahesabu ya halmashuri hizo kwenye taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG), aione zilivyojaa hati chafu. Halafu arudi Tarime, akatazame; baada ya miaka mingi ya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma yaliyopelekea hati chafu katika wilaya hiyo, wananchi wakaamua kuichagua CHADEMA kuongoza halmashauri. Na katika kipindi kifupi, cha kuwa chini ya CHADEMA, halmashauri ikaongozwa kwa uadilifu na kupata hati safi. Ngawaiya na wenzake wafahamu kuwa rangi nyeupe katika bendera ya CHADEMA haipo kama urembo, ni nembo ya kwamba chama hicho kinasimami uwazi, ukweli na uadilifu katika uongozi wake kwa kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa.

Katika mtizamo wake Bwana Ngawaiya anasema kwamba viongozi wa CHADEMA wanatetea biashara huria na kutaka biashara zipitie njia za panya. Hapa ndipo sanaa na sayansi ya propaganda majivu inapotumika kupotosha umma. Wananchi wa Tarime na watanzania, wanajua kabisa kuwa ni kweli CHADEMA chini ya itiakadi yake ya mrengo wa kati inaungana mkono soko huria bila kupora mamlaka ya umma katika sekta nyeti. Lakini CHADEMA imetamka bayana katika katiba yake kuwa haiungi mkono soko holela. Na wakati wote, nimekuwa nikisema kwamba serikali ya CCM inayoamini katika ujamaa wa dola kumiliki njia za uzalishaji mali, imerukia sera ya soko huria bila kuwa na misingi ya utekelezaji wake kupitia yale Maamuzi ya Zanzibar yaliyozika Azimio la Arusha. Matokeo yake, wameipeleka nchi katika soko holela! Ieleweke wazi, chini ya mfumo wa chama cha kina Ngawaiya, ambacho kinadhodhi mamlaka ya mambo mengi katika serikali kuu tofauti na mfumo wa majimbo ambao CHADEMA inaupigia upatu, udhaifu katika mipaka ya Tarime unafanywa na serikali ya CCM na si halmashauri ya wilaya ya Tarime iliyoko chini ya CHADEMA. Ikumbukwe kwamba, uhamiaji na askari walioko mipakani, wanapokea maagizo na maelekezo toka serikali kuu ambayo kwa sasa iko chini ya CCM. Matokeo ya mifumo mibovu ya serikali hiyo, ni kufanya mipaka kuwa na njia chache za kiserikali hali inayopelekea wananchi kutengeneza njia nyingine za panya. Serikali ya CCM inashindwa kusimamia mipaka ya nchi, na hata katika njia rasmi kama za Sirari katika wilaya ya Tarime, napo kuna udhaifu mkubwa! Lilipojitokeza suala la uhaba wa mchele nchini Kenya, ambapo wafanyabishara walikuwa wakipitisha na kuuza katika nchi hiyo kwa bei ya juu kupitia njia za panya; serikali ya CCM badala ya kukabiliana na chanzo cha tatizo, ikaanza kukimbizana na matokeo. Ikaamua kuweka kizuizi cha barabarani katika eneo la Kirumi; mpakani mwa wilaya ya Musoma na Tarime. Matokeo yake, ili kudhibiti mchele kwenda Kenya serikali ikaamua kudhibiti mchele kwenda Tarime!. Watanzania wakaanza kunyimwa haki ya kula wali kwa uhuru kwa sababu ya wakenya. Hapo ndipo Marehemu Wangwe, akiwa mbunge anayewakilisha sauti ya tabaka la chini, akaibua suala hilo bungeni. Serikali ya CCM badala ya kushughulika na mzizi wa tatizo, wameendelea na utamaduni wao wa kushughulikia matunda; sasa wamehamishia kizuizi hicho eneo la Rubana, mpakani mwa Bunda na Mwanza.

Bwana Ngawaiya ameenda mbele zaidi kwa kuwaita viongozi wa koo zinazokinzana huko Tarime kuwa ni mababa wa vita(war lords) wanapogiana kutafuta fedha. Ni hoja za kutokujua historia ya migogoro ya koo kama hizo ndizo zilizofanya makada wa CCM wakina Ngawaiya, Makamba na wengineo kunyimwa kura katika maeneo hayo. Bahati nzuri, Mbunge Mteule Charles Mwera, katika ilani yake ya uchaguzi akigombea ubunge mwaka huu, ameeleza bayana asili ya matatizo ya koo hizo kuwa ni migogoro ya ardhi. Na ameweka wazi dhamira yake na ya chama anachotoka ya kuhakikisha kwamba panakuwa na mipaka na upatanisho. Ni muhimu sasa akapewa ushirikiamo na asasi zote za haki za binadamu na za utawala bora kutekeleza azima hiyo.

Bwana Ngawaiya amemalizia mtazamo wake kwa kuibua uzushi wa kuhusisha CHADEMA na hoja ya wananchi kuhusu mbolea ya ruzuku tani 6,000 iliyopelekwa msimu uliopita kutowafikia walengwa. Bila kujijua ameibua kashfa kwa chama chake na serikali yake. Lakini pia, ameibua mjadala mkubwa zaidi kwa kuwa huko Kilimanjaro, kwa miaka kadhaa kati ya wafanyabiashara ambao wamekuwa wakitajwa tajwa katika kashfa za ruzuku za wakulima yeye ni mmoja wao. Bahati nzuri, wananchi wa wilaya ya Tarime na watanzania wa maeneo mengi wanafahamu kwamba makala wa kusambaza mbolea hizi wanateuliwa kutoka serikali kuu moja kwa moja. Matokeo ya serikali kuu kuhodhi mamlaka hayo, ni kuwepo kwa tuhuma za ufisadi katika uteuzi wa baadhi ya mawakala ambao wengine wameshindwa kufikisha mbolea hizo kwa wananchi na wengine wamepandisha bei tofauti ya dhamira ya mpango wa mbolea ya ruzuku. Halmashauri za CHADEMA, na wabunge wake, wamekwisha anza harakati za kufichua ufisadi na/ama matumizi mabaya ya madaraka katika eneo hilo mpaka kieleweke! Bwana Ngawaiya ameyasema yote hayo, kujenga hoja kwamba Tarime hawakufanya chaguo bora; hii ni baada ya wananchi wa huko kudhihirisha kuwa ‘sauti ya watu ni sauti ya Mungu’. Nguvu ya umma ilishinda yote Tarime.

Thursday, October 2, 2008

Salam za rambi rambi za Vifo vya Watoto Tabora

TAARIFA KWA UMMA

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA VIFO VYA WATOTO TABORA

Vijana wa CHADEMA tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watoto na vijana wenzetu wadogo vilivyotokea wakati wa Sikuu ya Iddi mkoani Tabora Oktoba Mosi, 2008.

Kutokana na msiba huo mzito, kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) natuma salamu za pole kwa familia za marehemu wote na kuwaomba wawe na utulivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Aidha tunalitaka Jeshi la Polisi mkoani Tabora kuwajibika kwa uzembe wa kuruhusu watoto chini ya miaka kumi nane kuweza kuingia kwa wingi katika ukumbi wa muziki. Tunaamini kwamba Jeshi la Polisi, lina wajibu wa kusimamia sheria nchini zinazokataza watoto wa umri mdogo kuwepo katika mabaa na vilabu.

Ni vyema vyombo vya dola vikaendelea kuwashikilia wamiliki na waendeshaji wa ukumbi huo ili kuwezesha uchunguzi uweze kufanyika kwa uhuru na kwa ukamilifu na matokeo yake kuwekwa hadharani na hatua zinazostahili ikiwemo za kisheria kuchukuliwa.

Pamoja na kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa ajali hiyo imetokana na watoto kuingizwa katika ukumbi kwa wingi kupindukia; tunatoa mwito kwa timu iliyoundwa kuchunguza ajali hiyo kufanya kazi yake kwa undani na kwa uwazi ikiwemo kuchunguza ujenzi wa jengo hilo linalomilikiwa na asasi ya umma(NSSF) kama lilijengwa kwa ajili ya kumbi za burudani zenye kuweza kukabiliana na ajali kama hiyo iliyojitokeza.

Mwisho, uongozi wa vijana wa CHADEMA Mkoani Tabora utaelekezwa kushiriki maziko kuwakilisha BAVICHA pindi taratibu za maziko zitakapotangazwa.

Imetolewa 2 Oktoba, 2008:



John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
0754694553