Friday, January 23, 2009

Mpishi na Mafiga Matatu

Mpishi yoyote makini hulenga kuhakikisha mafiga yanamwezesha kupika. Mpishi makini huangalia mafiga yanayowezesha chungu kukaa vizuri, chakula kisimwagike, kiive, apakuwe, kiliwe. Mpishi makini hana lengo la kuhakikisha mafiga yako sawa sawa lakini mbinu ni kuhakikisha yapo sawa. Nia ni kuona chungu hakipinduki. Maendeleo ni chungu cha chakula, kiongozi ni figa, kura ni Mpishi. Mpishi makini hachunguzi figa kwa rangi, anaangalia figa lililo sawa ambalo litawezesha chungu kukaa vizuri. Mpiga kura makini anapaswa kuchangua kiongozi bora ili apate maendeleo. Kikwete anakiri kabisa kuwa mafiga yake ni mabovu. Vipi amlazimishe Mpishi kuyapikia? Ndio maana nasema nakubaliana na hoja ya mafiga matatu kama zana ya kukibeba chungu cha maendeleo. Mpishi makini akikosa mafiga bora ndani ya nyumba yake anatoka kwenda kutafuta na akikosa huazima kwa jirani. Upinzani umeanzishwa kutoa viongozi mbadala,haya ni mafiga bora yanayopaswa kuchaguliwa. Tukiendelea kuyaacha mafiga yale yale ambayo tunaona ni mabovu, chungu hakitakaa, kitamwagika na tutalala na njaa ya maendeleo. Tutaendelea kukosa viongozi wenye kuwajibika na kuhamasisha nguvu za kutatua kero za wananchi.

No comments: