Thursday, April 21, 2011

Mbunge atoa rambirambi vifo vya watoto

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vifo vya watoto watano vilivyotokea jana tarehe 19 Aprili na leo tarehe 20 Aprili 2011 kutokana na ajali ya kuangukiwa na ukuta katika eneo la Matosa Kimara B, Dar es salaam.

Marehemu hao walikuwa ni wanafunzi wa Shule ya Chekechea ya Nia na walifikwa na mauti hayo kwa kuangukiwa na ukuta wa nyumba jirani na shule yao; watoto wanne walifariki papo hapo jana wakati mmoja amefia hospitali leo.

Mbunge Mnyika ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu wote na kuwatakia moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Aidha kufuatia msiba huo, Mnyika ameahirisha kushiriki katika vikao vya Kamati za Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni vinavyoendelea leo kwa ajili ya kushiriki maziko ya watoto hao.

Mnyika ameomba taasisi za masuala ya haki za watoto na wadau wengine kujumuika na familia za marehemu kuwafariji katika majonzi.

Kwa upande mwingine, ametoa mwito kwa serikali kufanya uchunguzi wa mazingira ya ajali na kuchukua hatua zinazostahili.

Chanzo: Ofisi ya Mbunge Ubungo

No comments: