Thursday, March 11, 2010

Heshima ya mwisho kwa Anna Daraja

Leo tarehe 11 Machi 2010 ni siku ambayo marehemu Anna Daraja (Mke wa Balozi Mstaafu Andrew Daraja) amepewa heshima za Mwisho jijini Dar es salaam kabla ya kusafirishwa kwa ajili ya maziko.

Kwa niaba ya Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa ya CHADEMA na niaba yangu binafsi natoa salamu za rambirambi kwa mwanadiplomasia Balozi Daraja, familia yake na wote walioguswa na msiba huo kwa namna moja au nyingine.

Kwa upande mwingine, namkumbuka Mama Daraja kama mkazi mwenzetu ndani ya Halmashauri ya Kinondoni aliyekuwa karibu na jamii ya eneo lake kabla ya mauti kumkuta kwa kuchomwa na kisu nyumbani kwake Kimara Temboni. Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema.

John Mnyika: Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mwenyekiti wa Mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum Dar es salaam (CHADEMA).

No comments: