Thursday, March 25, 2010

Tamko letu kuhusu ajali ya leo Kata ya Kibamba Wilaya ya Kinondoni

Taarifa kwa Umma: Kwa niaba ya Uongozi wa CHADEMA Mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum ya Dar es salaam; natuma salamu za rambi rambi kwa ndugu, jamaa na marafiki wa wafiwa wote kufuatia ajali mbaya iliyotokea leo asubuhi Kibamba jijini Dar es salaam ikihusisha Lori la Mafuta na Hiece iliyokuwa na abiria.

Aidha tunatoa mwito kwa serikali na vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina kuhusu vyanzo vya ajali za mara kwa mara katika eneo la Kibamba ambazo zimekuwa zikisababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.

Ikumbukwe kuwa mwezi Disemba mwaka 2007 ajali nyingine ilitokea eneo la Kibamba Hospital ikihusisha malori na kusababisha vifo vya watu saba akiwemo mjamzito na wengine 11 kujeruhiwa.

Aidha mwezi Aprili 2008 Bunge jumla ya watu 181 wamepoteza maisha kwa kugongwa na magari kati ya mwaka 2005 hadi mwaka 2007 katika eneo la kuanzia Kibamba mpaka Ubungo kwenye mataa.

Ikumbukwe kuwa Mei 2009 madereva wawili walikufa baada ya magari yao kugongana uso kwa uso huko maeneo hayo hayo ya Kibamba.
Itakumbukwa pia kwamba mwezi Januari 2010 watu 18 walijeruhiwa vibaya katika ajali ya gari iliyotokea katika barabara ya Morogoro eneo la Kibamba Darajani (barabara ina mteremko kuelekea darajani) ambapo magari matano yaligongana kwa pamoja.

Imetolewa tarehe 25 Machi 2010:





John Mnyika-0754694553; mnyika@chadema.or.tz
Mwenyekiti wa Mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum (CHADEMA)





No comments: