Wednesday, October 13, 2010

Mnyika kufungua Maadhimisho ya siku ya Nyerere Ubungo

Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo,John Mnyika ambaye pia ni Kaimu Katibu mkuu wa CHADEMA ataongoza wanachama na wapenzi wa chama hicho ktk maadhimisho ya siku ya Nyerere tar14Oktoba.Maadhimisho hayo yatafanyika ktk eneo la Manzese darajani.

Pamoja na hotuba zitakazotolewa Mnyika atazindua rasmi Tawi la Mwl Nyerere ktk mtaa wa Mwongozo.Uzinduzi huo utafuatiwa na ufunguzi wa matawi mengine ktk maeneo mbalimbali na kumalizia na Mkutano wa hadhara ktk mtaa wa Sisi kwa Sisi.

CHADEMA inamuenzi Mwalimu kwa vitendo kwa kupambana na ufisadi ,kutetea rasilimali za taifa na kuhakikisha fursa kwa wote ikiwemo kutoa huduma kama elimu bure.

Mnyika anaendelea na kampeni ambapo tar12 amehutubia kata ya msigani,tar13 amehutubia Kwembe na tar 15 anatarajia kuwa Kimara.

Tuzidi kuwa Pamoja!!

No comments: