Thursday, August 8, 2013

Salamu za Eid-Al-Fitr na kutembelea kata ya Malamba Mawili!

Saa 5 mpaka 8 mchana nitakuwa pamoja na viongozi wenzangu Malamba Mawili (Eneo la Stendi Mwisho). Tutagawa zawadi kwa watoto pamoja na kutoa salamu za Eid-Al-Fitr. Tutasambaza nakala za rasimu ya katiba mpya vijiweni na kwa wawakilishi wa makundi ya kijamii yenye malengo yanayofanana.

Tunaanza muda huo ili kuheshimu wajib wa salaat ya Eid na sunnah ya khutbah asubuhi. Imekuwa ni kawaida kwa siku ya Eid kuwa pia ni wasaa kwa kusikiliza hotuba juu ya wajibu kwa Allah lakini pia kwa binadamu wengine. Ni wakati wa ummah kukumbushwa masuala muhimu katika jamii. Tunamaliza mapema kutoa fursa ya mikusanyiko mingine.

Nitazungumza na umma kuhusu mchakato wa katiba na kutoa pia mrejesho juu ya masuala ya maendeleo ikiwemo juu ya ujenzi/matengenezo ya Barabara ya Kinyerezi-Malamba Mawili Mbezi, kuhusu maji na juu ya masuala mengine muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Kwa wakazi wa maeneo jirani yanayozunguka Malamba Mawili ya Kifuru, King’azi, Msingwa, Msigani na mengineyo mnaweza kuja kujumuika nasi. 

Kwa maelezo zaidi na maelekezo naomba muwasiliane na Ali Makwilo 0715/0784691449.

Eid Mubarak!

No comments: