Tuesday, December 4, 2012

Kuchangia kukuza soka-Mburahati Queens


Mbunge wa jimbo la Ubungo, John Mnyika akikabidhi sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo, Shuka, Godoro na Chandarua pamoja na fedha taslimu kiasi cha sh. laki saba kwa Makamu Mwenyekiti wa timu ya soka ya Wanawake ya Mburahati Queens, Ridhwan Mkasa kwa ajili ya kuisaidi timu hiyo.

Na Elizabeth John

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (Chadema ) amelitaka Shilikisho la saka Tanzania (TFF) kutoa mchanganuo kwa dola 250 za Marekani zinazotolewa na Shirikisho la soka Duniani (FIFA) kila mwaka kwa ajili ya kuendeleza soka nchini.

Mnyika aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati alipokabidhi msaada wa shilingi milion 1.5 pamoja na godoro moja likijumuishwa kwenye fedha hizo kwa timu ya mpira wa miguu ya Wanawake ya Mburahati Queens.

“TFF inaulazima wa kutoa ufafanuzi kuhusu fedha hizo ambazo zinatolewa kwaajili ya kukuza soka la vijana na wanawake, wanatakiwa kuchanganua kwa kiwango ambacho kulitumika kuanzia Juni mwaka jana hadi Juni mwaka huu na matumizi yaliyoanza kutumika Julai yanatakiwa yaelekeze ni kiasi gani kimetengwa kwaajili ya vijana na wanawake,” alisema Mnyika.

Mburahati Queens ilipewa msaada huo baada ya timu hiyo kutembelea bungeni mjini Dodoma kwaajili ya kuhamasisha upatikanaji wa Katiba mpya.

Mnyika alisema shilingi laki tano zilichangwa na wabunge viti maalumu na kukabidhiwa kwake na Waziri kivuli wa Habari Utamaduni na Michezo Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ katika kikao kilichopita.

Pia baada ya kurudi kutoka bengeni katika kikao kilichopita Mnyika alikusanya michango mingine kwa wadau wengine na michezo na hadi kufikia kiwango kicho.

Mnyika aliuomba uongozi wa timu hiyo kuandaa mchezo mwingine wa kuwahamisisha wananchi wa Jimbo la Ubungo kujitokeza kutoa maoni yao kwa wajumbe wa tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya.

“Kutokana na Kamati ya Katiba kufika katika Jimbo letu mnatakiwa kujitahidi kuandaa mchezo wa kirafiki ili kuhamisisha wananchi kujitokeza katika utoaji wa maoni ya Katiba Mpya,” alisema Mnyika.

Chanzo: http://francisdande.blogspot.com/2012/12/mnyika-aipiga-tafu-mbiurahati-queens.html

No comments: