Tuesday, July 13, 2010

Hongera Kinondoni kwa kushinda Copa Coca Cola U 17

Nawapongeza timu ya vijana(U 17) wa Mkoa wa kimichezo wa Kinondoni kwa kuwa mabingwa wa Copa Coca Cola tarehe 10 Julai 2010.

Mashindano kama haya ya vijana na watoto na yale ya mashuleni kama umishumta na umiseta ni ya muhimu sana katika kujenga oganizesheni ya soka na kuunda timu bora za baadae(dream team).

Ni muhimu sana tukayapa mkazo na kuwekeza pia katika mafunzo na viwanja kuanzia ngazi ya chini kabisa mitaani na kwenye wilaya.


John Mnyika-Mwenyekiti Mkoa wa Kichama wa Kinondoni (CHADEMA)

No comments: