Tuesday, March 3, 2009

Richmond, Dowans and Operesheni Safisha Mafisadi

Richmond, Dowans na Operesheni Safisha Mafisadi

Na John Mnyika

Kwa muda wa wiki mbili nimekuwa kikifuatilia na kutafakari mjadala unaoendelea kuhusu ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya Dowans mintaarafu hofu ya taifa kukumbwa na tatizo la uhaba wa umeme. Aidha katika kipindi hicho nimekwepa kuandika hadharani mawazo yangu kuhusu suala hilo. Katika kipindi chote hicho nimekuwa nikizungumza na walio katika korido za mamlaka na maamuzi kueleza mawazo yangu. Nikiamini kwamba waliouanzisha mjadala huu, watauhitimisha kwa kuzingatia mahitaji ya taifa na hisia za umma. Badala yake mjadala huu, kama moto wa nyikani, umeendelea kushika kasi na kuchukua sura mbalimbali.

Pamoja na kuwa na uhuru wangu, kama mtanzania; natambua kwamba kwa upande mwingine sehemu ya uhuru huo imeshikiliwa na taasisi ambazo mimi ni sehemu ya uongozi. Bahati njema, taasisi hizo bado hazijatoa misimamo yao. Kati ya taasisi hizo, ni CHADEMA. Bahati nzuri zaidi ni kuwa chama hiki kimejitambulisha kuwa ni cha demokrasia, kinachotoa fursa ya uhuru wa mawazo. Ndio maana, mwaka 2007 ulipozuka mjadala baada ya Rais Kikwete Kamati ya kupitia sheria, sera na mikataba ya madini, maarufu kama Kamati ya Bomani, umma ulishuhudia mjadala mkali baina ya viongozi wa CHADEMA. Mjadala huo ulichangiwa na dhamira ya kuundwa kwa kamati hiyo, muundo na uteuzi wa Mbunge kupitia CHADEMA, Zitto Kabwe katika kamati hiyo. Mjadala huo ulioibua mambo kadha wa kadha ya msingi ulihitimishwa kwa msimamo wa pamoja wa chama uliobeba fikra mbadala.

Kwa mara ya kwanza nilizungumza kuhusu hili suala la Richmond mwaka 2006, wakati huo serikali ilikuwa ni kwanza imeweka dhamira ya kununua mitambo hiyo. Wakati huo, tukiwa kwenye kongamano la vijana tuliweka msimamo wetu bayana kuwa Richmond ni kampuni ya kitapeli, na mchakato mzima wa tenda umegubikwa na ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka. Serikili na CCM wakati huo ilikanusha, na kwa ujumla onyo letu lilionekana kuwa ni ‘kelele za mlango’, ‘uzushi’ na ‘upinzani wa maslahi ya taifa’. Kwa kuwa ukweli ni mmoja na haugawanyiki, ni hoja hoja zile zile baadaye zikaja kubebwa na Kamati Teule ya Bunge, maarufu kama Kamati ya Mwakyembe na baadaye kubarikiwa na maazimio ya Bunge.

Lakini ‘geuka nyuma’ hii ya Bunge na serikali inayoongozwa na CCM haikuja hivi hivi. Ni baada ya heka heka za vyama vya upinzani, vyombo vya habari na wadau wengine. Ni baada ya kuanza kwa ‘uasi wa umma’ kulikofuatiwa baada ya kupitishwa kwa ‘udikteta wa uwingi’; bajeti iliyoongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi, kuzimwa kwa hoja Buzwagi iliyowasilishwa na Zitto; kuwekewa mizengwe kwa hoja ya ufisadi wa Benki Kuu(BOT) iliyokuwa iwasilishwe na Dr Slaa; na kwa ujumla, hotuba mbalimbali za kambi ya upinzani za wakati huo zilizozungumza suala la Richmond ikiwemo ile bajeti mbadala. Nguvu hiyo ya umma iliunganishwa na ziara ya ushirikiano wa upinzani, iliyoratibiwa na kufadhaliwa na CHADEMA, ambayo ilianzia uwanja wa Jangwani kwenye mapokezi ya Zitto Kabwe baada ya kusimamishwa na kuhitimishiwa Mwembe Yanga, ambapo Orodha ya Mafisadi ilisomwa na Dr Slaa. Hiyo ilikuwa ni Septemba 15 mwaka 2007. Toka wakati huo, mpaka wakati huu; taifa haliko kama lilivyokuwa. Tulizoea kwamba tabaka tishio kwa uhai wa taifa, ni kupatuka kwa pengo kati ya matajiri na masikini. Lakini sasa mstari umechorwa katika taifa, kati ya mafisadi na waadilifu; baina ya maisha ya ufisadi na utamaduni wa ufisadi. Mawaziri wa Serikali na makada wa CCM nao wakaanza ziara za ‘kuelezea uzuri wa bajeti’,ambazo kwa muda mwingi zaidi zilihusisha kujibu hoja za ufisadi-kuanzia Richmond, Benki Kuu(EPA, Majengo pacha nk), Buzwagi, Rada; orodha ni ndefu. Wakaambulia ‘uasi’ na ‘upinzani’ toka kwa umma, ulioambatana na ‘zomea zomea’ katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Neno ‘ufisadi’ likawa msamiati wa kila kaya, na mafisadi wakatambulika rasmi kuwa ni maadui wa taifa.

Pima joto za vyombo vya dola na vile vya ushushushu zikaona bayana kwamba uwepo wa serikali madarakani upo mashakani. Namna pekee ya kutokea ikawa ni kusikilizwa kwa sauti ya wengi; kama isemavyo, sauti ya watu; sauti ya Mungu. Kamati ya Bomani ikaundwa, Kamati Teule ya kuchunguza suala la Richmond ikaundwa; Ofisi ya Rais ikatoa tamko kuhusu EPA iliofuatia kuundwa kwa Kamati. Kadiri nguvu ya umma, ilivyokuwa ikishinda mtandao wa mafisadi na kuilazimisha serikali kuanza kuchukua hatua ndivyo ambayo mafisadi nao wakaanza kuchukua hatua. Vita baridi ikazuka katika taifa letu, vita ambayo inaendelea mpaka hivi leo.

Mafisadi, mawakala na vibaraka wao nao wakarudi mezani kujipanga upya. Wakaja na mikakati mipya. Mkakati wa awali ukawa kukanusha madai yote na kutishia kwenda mahakamani, mkakati huo ukashindwa. Mkakati ukafuata wa kuwachafua vinara wa kupinga ufisadi, nao ukashindwa. Hatimaye kamati husika zikamaliza kazi yake. Kutokana na taarifa ya Kamati mojawapo, Waziri Mkuu akalazimika kujiuzulu; baraza la mawaziri likavunjika lenyewe kwa kitendo hicho. Matokeo ya Kamati hizo ni baadhi ya watuhumiwa kupelekwa mahakamani. Kwa bahati mbaya, wakati yote hayo yanafanyika mihimili ya ufisadi huo iliyojikita katika mfumo wa chama kinachotawala na kwenye dola yenyewe; bado iko barabarani inapanga mikakati mipya kila kukicha.

Mara baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Lowassa kujiuzulu, wengine tulijitokeza hadharani na kutaka yeye na maswahiba wake wakamatwe na kufunguliwa mashtaka. Na wakati huo tulionya kuhusu mkakati wa mafisadi kujisafisha na wasiwasi wa mafisadi kuligawa taifa. Toka tuseme hayo, mpaka leo wakina Lowassa na watuhimiwa wengine wa matumizi mabaya ya madaraka wako barabarani wakati wenzao wakina Mramba na Yona wako mahakamani. Tulionya kuhusu kutikishwa kwa utawala wa sheria na mifumo ya haki, wakati ulipotolewa msamaha kwa wezi wa fedha za EPA waliorejesha fedha zao, hata wachache waliokacha kurejesha fedha walipopelekwa mahakamani tuliendelea kupaza sauti kutaka mafisadi halisi wa Kagoda wapelekwe mahakamani.

Matokeo ya mafisadi kuendelea kutamba barabarani badala ya kuwa mahakamani ni kupata fursa ya kupanga na kutekeleza mikakati. Ukitafakari kinachoendelea hivi sasa, inaonyesha bayana kwamba iko Operesheni Safisha Mafisadi (OSAMA) katika taifa letu. Mkakati ule ule uliotumiwa na wanamtandao, wa kumwingiza Rais Kikwete madarakani wa kumsafishia mteule wao njia na kujenga matumaini mapya, huku wakichafua wapinzani wao wote-wa nje na ndani ya chama chao ndio ambao unaendelea hivi sasa.

Baada ya kushindwa OSAMA ya kupita majimboni kujisafisha; sasa OSAMA mpya ikabuniwa. Mikakati hiyo ikahusisha pia kuanzishwa kwa wimbi la magazeti ya uchafuzi na utetezi. Mikakati hiyo ikahusishwa kuzushwa kwa mijadala mingine yenye kuligawa taifa ili kuondoa fikra za taifa katika mjadala wa ufisadi. Mkakati huu ukahusisha mpaka baadhi ya watu wa kada mbalimbali kufadhiliwa kufanya ziara za kusafisha mafisadi, na kushambulia wenye kupinga ufisadi. Hapa ninapoandika makala hii, mikutano ya hadhara inaendelea katika baadhi ya mikoa nchini ikiwa na ajenda hiyo. Mafisadi wenyewe sasa wako nyuma ya barokoa, wakiendesha mambo kwa mbali kwa kutumia vibwebwezo (remote control) walilichezesha taifa na baadhi ya viongozi wake, kuanzia wa kisiasa mpaka wa dini; ngoma wasizozielewa.

Pamoja na kuwa na orodha ndefu ya kashfa ya za ufisadi katika taifa letu, bado Mkataba wa Richmond, na kujiuzulu wa Lowassa ni matukio yaliyopiga muhuri kwenye mioyo ya watanzania. Kwa wataalamu wa OSAMA, ushindi na kubadili nyoyo za wananchi katika suala hili, ni hatua moja kubwa katika ujio wao mpya na kutezwa harakati zote zilizokwishafanyika mpaka hivi sasa.

Baada ya mkakati wa kumsafisha Lowassa, mlango unaonekana kwa sasa ni kupitia kuibariki mitambo ya Dowans. Fungua za kuingilia mlango huo ni kuinuua mitambo hiyo. Wakati mzuri wa kufanya hivyo, ni kipindi ambacho taifa lina hofu ya uhaba wa umeme siku za usoni. Ili Dowans na maswahiba wake waonekane kuwa ni wakombozi wa Taifa!

Kwa yoyote aliyewahi kusoma kitabu cha Confession of the Economic Hitman (ungamo la kuwadi wa kiuchumi- kwa tafsiri yangu), wanaweza kupata picha la mfumo wa kifisadi unavyoweza kufanya kazi katika suala kama hili.

Makuwadi hao wakajifunika katika kivuli cha maslahi ya taifa na nia njema ya kulinasua taifa kwenye shaka ya kukumbwa na baa la uhaba wa umeme, wakaenda katika Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, ambayo mwenyekiti wake ni Mbunge Zitto Kabwe. Wakamwaga takwimu na maelezo yao, kwa ustadi na ushawishi mkubwa. Mdadisi yoyote wa mambo akichambua wajumbe wanaounda kamati hiyo, kwa kuangalia michango yao bungeni- hususani michango yao wakati wa mjadala wa Bunge kuhusu ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu Richmond unaweza kubashiri kilichojiri na kitakachojiri. Wapo wabunge wa jamii ya Zitto Kabwe, wao wakati wote wanachotazama ni nguvu ya hoja na kutazama ukweli na daima wamekuwa wakitanguliza zaidi maslahi ya taifa pengine hata kuliko maslahi ya vyama vyao. Hawa walishawishiwa na TANESCO kwa hoja, na hivyo kuanza kuhoji maamuzi ya Kamati zingine za bunge kuhusu suala hilo hilo. Lakini hawakutaka kufanya maamuzi ya mwisho, wametaka kamati zikutune ili ukweli uweze kujulikana. Kundi hili, wakipata muda wa kutafakari ukweli wa ziada na kupata taarifa sahihi, hubadili msimamo wao.

Halafu wako wabunge jamii ya Peter Selukamba, ambao msimamo wao wa kutetea ya mfumo wa utawala na wakati mwingine kuwatetea watuhumiwa wa ufisadi pamoja na ufisadi wao inajulikana bayana. Katika ya kundi hili, wapo wanaonufaika na ufisadi na wapo pia mawakala wa ufisadi. Hawa ni wazi watamshinikiza zaidi Mwenyekiti wa Kamati ili matakwa yao yatimie. Ni katika ule usemi kwamba katika siasa, hakuna rafiki wala audui wa kudumu; kuna maslahi ya kudumu.

Halafu kuna kundi la wabunge wengine wachache, ambao wao kwa kawaida yao hawana kawaida ya kuchotwa na yanayowasilishwa; wanakwenda mbali zaidi. Wao walishafanya maamuzi, na hawaoni haja ya kamati hizo kukutana. Kwao wao, kwa kusikiliza maelezo ya TANESCO na kupitia taarifa za Kamati nyingine, wameshaweka misimamo yao moyoni- kununua mitambo ya Dowans, hapana!. Hakika suala hili litaendelea kuigawa kamati husika, sitashangaa wakiendelea kupingana hadharani, na katika maeneo mengine wajumbe wakiwa na mgawanyiko wa namna hii wanaweza kupigiana kura za kutokuwa na imani.

Inawezekana mimi si mtu mwafaka kuchambua ama kutoa mawazo kuhusu suala hili kwa kuwa msimamo wangu kuhusu suala hili tayari unajulikana. Lakini naandika makala haya kuchochea mjadala zaidi na hatimaye taifa liweze kufanya maamuzi kwa kuzingatia fikra mbadala. Naandika makala hii kutaka wabunge wetu na serikali wasikilize sauti ya umma

Eneo ambalo kampuni ya Richmond ilikuwa iweke mitambo yake, lipo ndani ya jimbo la Ubungo. Ni eneo hilo hilo ambalo kampuni ya Dowans imeweka mitambo yake. Katika jiografia ya Dar es salaam mitambo ya Dowans iko pembeni ya Makao Makuu ya TANESCO ukipita tu mataa ya Ubungo. Kwa kuzingatia mazingira hayo, mwaka 2008 tuliitisha Kongamano la Wakazi wa Ubungo, kujadili masuala mbalimbali ya wananchi katika sekta za ardhi, umeme na wafanyakazi. Katika suala la umeme, mjadala kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Kamati ya Bunge kuhusu Richmond ulichukua nafasi kubwa kwa kurejea tatizo la bei kubwa na uhaba wa umeme nchini. Mimi nilikuwa Mwenyekiti wa kongamano hilo. Kama wakazi wa jimbo hilo, tuliazimia kwamba kwa kuwa imethibitika kwamba mkataba na Richmond ulikuwa batili, hata mkataba wa mrithi wa mkataba batili yaani Dowans nao unapaswa kutafakariwa ubatili wake. Hivyo, tuliazimia mitambo ya Dowans itaifishwe na serikali, iuzwe kufidiwa gharama za fedha ambazo serikali imeshalipa mpaka sasa kwa Richmond/Dowans. Ilibainika pia kwamba tayari kwenye mchakato huo, serikali ilikwishalipa takribani bilioni 30; ziada ya yale malipo ya milioni 152 kwa siku ambayo yalikuwa yakitolewa. Fedha hizo ni nyingi kiasi cha kutoa shilingi milioni moja kwa kila mkazi mtu mzima wa kata ya Ubungo. Ama ni sawa na kununua mitambo kamili ya umeme kwani kwa taarifa mbalimbali mitambo kama hiyo inapatikana kwa bei ya dola milioni 14. Baada ya Kongamano hilo, azimio hilo pamoja na maazimio mengine yalisambazwa kwa umma kupitia mikutano ya hadhara, na kukabaliana kwamba Oktoba 14, 2008 pangefanyika maandamano ya wakazi wa Ubungo kushinikiza utekelezaji wa matakwa hayo ya umma.

CHADEMA jimbo la Ubungo ikaratibu maandamano ya wakazi, kuelekea kwenye kampuni za Dowans na TANESCO ambazo ziko jirani; lakini polisi walikataa kutoa kibali cha maandamano hayo. Sababu pekee ambayo ilitolewa ni kuwa Oktoba 14 ni siku ya Nyerere, hivyo vyama havipaswi kufanya maandamano ya siku hiyo kukumbuka mchango wa Baba wa Taifa katika kupiga vita ufisadi. Badala yake, polisi ikaelekeza watanzania wote wakashiriki pamoja katika uwanja ambao serikali imeandaa maadhimisho!

Baadaye ikafutiwa na taarifa ya Waziri Mkuu Pinda kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge na kupelekwa kwa mtuhumiwa mmojawapo wa Richmond mahakamani. Sambamba na hilo, mjadala wa ununuzi wa mitambo hiyo ukashika kasi, mwanzoni ukibebwa na Waziri wa Nishati, Bwana Ngeleja na kupingwa na Kamati husika chini ya Uenyekiti wa Shelukindo; sasa umeibukia kwenye kamati ya Zitto.

Pamoja na suala la uhalali wa mitambo ya Dowans ukirejea ubatili wa mitambo wa Mkataba wa Richmond. Liko pia suala la umiliki wa kampuni ya Dowans!. Kamati ya Bunge. Kamati ya Mwakyembe ilijulisha bunge kuwa ilitaarifiwa nje ya kiapo kuwa Richmond ni mradi wa kina Lowassa na Rostam Aziz. Pamoja na kuwa kwenye majumuisho yake, Kamati ilikwepa kutaja moja kwa moja mmiliki wa Richmond. Lakini mfuatiliaji yoyote anaweza kuthibitisha uhusiano wa karibu kati ya Lowassa na Rostam Aziz na makampuni ya Richmond na ile ya Dowans, ukirejea kutajwa kwa kampuni ya Caspian. Mduara huu wa tuhuma za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka pekee, unaweza kubatilisha azma ya kununua mitambo toka kampuni hiyo. Pengine kamati zote tatu, ile teule na hizi za kudumu zingeingia kwa undani kuhusu suala hili na kupendekeza hatua timilifu leo taifa lisingekuwa linayubishwa kama penduli! Hoja wala isingekuwa uhalali au uharamu wa kununua mitambo chakavu kwa kurejea sheria ya manunuzi ya umma; hoja ingekuwa ni ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na uhujumu wa uchumi wa taifa.

Wataalamu wa OSAMA, wamefanikiwa kuzifunika hoja hizi kwa hoja tamu ya matazimio ya uhaba wa umeme na haja ya kutanguliza maslahi ya taifa katika mjadala huu. Nakubaliana na Zitto kwamba nchi iko na litaendelea kuwa mashakani kutokana na uhaba wa umeme, na kwamba tunahitaji suluhu ya kitaifa. Lakini ili tupate suluhu hiyo, tupanue wigo wa fikra zetu. Tuichambue asili ya tatizo lenyewe, ukosefu wa maono, sera na mipango ya muda mrefu katika sekta ya umeme chini ya utawala wa CCM, na ombwe la dhamira ya kisiasa ya kutekeleza hata ile miradi iliyopo tayari. Tatizo hili linakuzwa zaidi na uzembe na ufisadi wa kutumia tatizo la umeme kama kivuli cha kujinufaisha. Tumeona hivyo katika IPTL, Kiwira, RICHMOND na tutaendelea kuona hivyo katika Dowans. Katika hili, ni muhimu kwa Zitto na Kamati yake kujinasua na mtego wa kisiasa. Kama ni kutetea maslahi ya taifa, ni umma upi huo wanaoutetea kama umma wenyewe umeshatamka kwamba hautaki mitambo ya Dowans na kwamba Richmond ni ufisadi? Kamati za bunge zitumie muda mrefu zaidi kujadili mbinu za kulinasua taifa katika suala hili, badala ya kutumia kodi zetu na muda wa watanzania kujadili Dowans pekee. Kwa bahati mbaya, taifa limeingizwa katika mizengwe hii na TANESCO. Mwaka 2001, ripoti za kiserikali zilikwisha tabiri kuhusu upungufu wa umeme mwaka 2006 na hata mwaka 2009; lakini miaka mitano baadaye watawala hawakuongoza taifa kujiandaa badala yake wahujumu uchumi wa taifa kupitia kashfa ya Richmond mwaka 2006. Watawala hao, bado wako nyuma ya pazia wakisuka mipango ya kurejea- na makuwadi wao wako bado kwenye korido za Mamlaka za Wizara ya Nishati na hata TANESCO yenyewe wakiendelea kuwa mawakala wa hujuma kwa watanzania. Wanajipenyeza kila mahali na kufanya kila jitihada za kutoa taarifa za uwongo za kuwahadaa wabunge wetu kubariki maamuzi tenge ya serikali. Sasa tuko mwaka 2009, hata baada ya watawala kukumbushwa Februari 2008 kuhusu haja ya kujiandaa na dharura ya umeme bado leo Machi 2009, mwaka mmoja baadaye na miaka takribani nane toka tahadhari ya awali tunalazimishwa kuamini kwamba hii ni dharura ya hali ya juu. Hali Kama hii inafanya wengine tuamini kwamba kuna kikundi cha watu, kinaacha matatizo ya taifa kuweka mianya ya dharura ili kuhalalisha kupitishwa kwa sheria na kupitishwa kwa zabuni kwenya mazingira yanayowawezesha kutimiza malengo yao ya kiuchumi na kisisiasa. Ndio maana, wakati taarifa zikiwa zinaonyesha kwamba katika ya mikoa itayokumbwa na uhaba wa umeme ni Mwanza ambapo kuna mitambo ya umeme ambayo muda wake wa kukodishwa imeisha. Pamoja na utata wa bei na mikataba ya mitambo hiyo, bado hatusikii ikijadiliwa kununuliwa au kukodishwa tena kama ambavyo Dowans inavyopigiwa upatu na TANESCO. Historia ya Taifa letu itufundishe, wataalamu kama Chenge ndio ambao walitumia nafasi zao akiwa mwanasheria mkuu wa serikali kulisukuma taifa katika mikataba kanyaboya ikiwemo katika ununuzi wa RADA. Sasa kama watalaamu kama Dr Idrissa Rashid wamekwishatajwa kwamba walipewa mlungula katika mgao wa rushwa ya RADA ni vyema tukautazama kwa jicho la mashaka utamu wa takwimu na maelezo wanayotupatia kuhalalisha manunuzi makubwa mengine.

Kwangu mimi hoja kuu sio bei ya mitambo ya Dowans. Maana najua pamoja na kuwa bei ya bilioni 30 inayotajwa inakaribia mara mbili ya bei ya kawaida. Bado maajabu yanaweza kufanywa na Dowans ya kupunguza bei zaidi kwa sababu mbili. Kwanza kiuchumi, tayari walishatunufaika na malipo ya awali ambayo yalikwishafanyika. Hivyo, wanaweza kuiuza mitambo hiyo kwa bei ya kutupa. Pili; kisiasa, serikali kununua mitambo ya Dowans ni jambo lenye maslahi makubwa kwa walionyuma ya kampuni hiyo, na wote wanaozongwa na “Mzimu wa Richmond”. Hivyo, kundi hilo linaweza kuwa tayari hata kuitoa mitambo hiyo bure kwa kuwa uamuzi wowote wa kuisafisha kampuni ya Dowans ni mtaji muhimu kwa OSAMA. Kwa OSAMA ununuzi wa mitambo hiyo, sio tu bezo kwa harakati dhidi ya Richmond/Dowans bali utakuwa pia mzigo wa taswira hasi ya kisiasa kwa wote watakaoendelea kupigia debe ununuzi huo.

Jambo lingine ninalokubaliana na Zitto ni kuwa kuna makundi ndani ya CCM. Sasa tunalazimishwa kuamini kwamba makundi hayo yametokana na vita dhidi ya ufisadi, na kwamba makundi hayo ni kati ya kundi la mafisadi na kundi la ‘waadilifu’. Na kwamba CCM sio chafu, ila kuna baadhi ya wanachama wake ndio wachafu!. Kadiri mahubiri haya mapya, ambayo sasa yameanza kutengezewa majukwaa na ziara- ya kujilindia majimbo katika uchaguzi ujao, ndivyo ambayo taifa litatoka katika mstari thabiti ambao taifa lilianza kuuchora nje ya mipaka ya vyama. Makundi ya CCM yapo, yakitokana na sababu mbalimbali; lakini kubwa zaidi ikiwa ni migogoro ya kimaslahi na kimadaraka. Lakini mwisho wa siku, utawala ni utawala. Ndio maana wengine tulihoji, nguvu na makeke yaliyotumika wakati wa mjadala wa Richmond Bungeni lakini nje ya hapo nguvu hiyo imethibitika kuwa ni ya soda. Ukisikiliza kauli mbili za Dr Mwakyembe za hivi karibuni, ile ya kutamka kwamba wananchi kumnyima kura Kikwete mwaka 2010 ni kuwapa ushindi mafisadi; na ile ya wiki hii ya kwamba kauli za Zitto kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge kuhusu Dowans ni sehemu ya Operesheni Sangara. Ukitafakari sana kauli hizi, mtiririko wa matukio na masuala yanayojadiliwa; unaweza kupata taswira ya mambo yaliyokatika akili za wanasiasa wetu.

Tukiacha mijadala ya watu na matukio inayoendelea hivi sasa, kuna masuala mawili yanapaswa kujadiliwa na hatua za haraka kuchukuliwa kila moja kwa peke yake na kwa uzito wake. Mosi, jitihada pana za haraka zifanyike za kutafuta umeme wa kufidia pengo linalotarajiwa, nje ya mjadala wa ununuzi wa mitambo ya Dowans. Kwa hakika, Mkurugenzi wa TANESCO, Dr Iddrissa Rashid ameshindwa kuishauri serikali vizuri katika hili. Kwa uzembe huu, na matumizi mabaya ya madaraka yaliyofanyika hapo nyuma, sio mwelekeo bora wa TANESCO chini yake. Pamoja na kufikiria dharura, kamati za bunge ziisimamie serikali kutekeleza mipango ya muda mrefu; ya sera zenye maono katika sekta ya umeme. Ni aibu kwa taifa lenye rasilimali kama Tanzania kuwa na uhaba wa umeme. Pili; turejeshe utamaduni wa uwajibikaji na uadilufu kwa kuchukua hatua kamili dhidi ya wahusika wa Richmond, na kufunua pazia linalofunika kampuni ya Dowans. Kesi ya Gire mmoja, huku wakina Gire mwingine, Lowassa, Rostam nk wako uraiani ni kuendelea kuahirisha matatizo. Suala hili liende sambamba na kuendeleza mijadala mingine kama ile ya Kagoda, Meremeta, Deep Green nk. Mizizi ya Operesheni Safisha Mafisadi ni lazima ikatwe kwanza, ama sivyo tutaendelea kutumbukizwa kwenye mijadala yenye kupunguza imani na heshima baina ya watanzania wenyewe kwa wenyewe.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kupitia 0754694553, mnyika@chadema.net na http://mnyika.blogspot.com




Friday, January 23, 2009

Expose on salient issues in students politic



Prologue

The whistle marking the beginning of elections processes at the University of Dar es salaam (UDSM) has recently been blown. With the position the UDSM students famously known as intellectuals at the Hill had, have, or at least ought to occupy in the society these processes should not pass without raising the eyebrows of many. Consequently the hub of this commentary is the UDSM students’ organization believed to be the spring of national leadership. The writer exposes salient issues on students politic and attempts to fill the ideological vacuum in the UDSM student community
Concerned Students Should reform UDSM politic

Past decade experienced notable students’ struggles in the country. The use of the coercive instruments of the state like the police and the unanimous closure of the University continues to characterize the reaction of the Government towards students’ struggles. University of Dar es salaam normally referred to as the Hill, experiences students’ struggles since its inception in early 1960s. The well-documented incidences like the 1966 National Service Demonstration and the 1978 Struggle against the salaries hike of the MPs are well known to the activists of the past and present.

It may be recalled that one of the first actions of the independent government was the establishment of the University College of Dar es salaam as part of the University of East Africa.
As could have been expected, no sooner had the new college been opened than the students formed their organs of representation. One such student organization, which was formed in order to take care of students’ affairs, interests and problems, was the University College of Dar es salaam Student Union (USUD).

USUD, which was an elitist and a petty bourgeois student organization was established in October 1961 and changed its name to DUSO in 1970 following the establishment of the University of Dar es salaam. During USUD tenure, there established in 1964 the National Union of Tanzania Students (NAUTS), which organized the demonstration against the conditions for compulsory National Service Programme by the Government. The service was to include the students completing their high school or institutions of higher learning. It was proposed that the duration of the service to be two years and the salaries of the students to be cut by 40% in eighteen months of service.

During DUSO’s time there were also massive student struggles which involved the militant student organization USARF that was established by Yoweri Museveni (Current President of Uganda) and other activists like Walter Rodney, Issa Shivji and Horace Campbell. DUSO was banned in 1978 following the demonstration by students against the move by the members of parliament to hike their salaries while the country was in a deep economic crisis. Students were not only badly beaten by the Police but also sent home by Lorries. This is the major incident for which students stood for the issue that was not affecting them directly.

Following the 1978 student struggles the government placed all the activities of the students under the party youth wing. Therefore, Muungano wa Wanafunzi Tanzania (MUWATA) was established and operated under Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM). The following years were largely silent of any students’ struggles besides the fact that students struggled to get rid of MUWATA.They were successful in early 1990 when MUWATA was abandoned following the wave of multipartism. Hence, The Dar Es Salaam University’s Student Organization (DARUSO-Mlimani) was established as a sole students’ organization at the University of Dar es salaam as recognized by the University of Dar es salaam Act No. 12 of 1970.

The establishment of DARUSO revived the students’ activism at the hill. Although the struggles were rampant, they followed the social-economic changes that were taking place in the country. Most of the struggles were characterized by bread- and-butter politics. Students were largely struggling for students’ welfare issues like the allowances and the likes. Majority of the students have turned into petty bourgeoisies hence progressive ideas are very limited.

The DARUSO constitution recalls that diligent students’ organization had improved to great extent a cordial relationship based on mutual understanding between the students of the University of Dar es salaam and other stakeholders/beneficiaries. DARUSO was meant to enhance academic prosperity, good governance, democracy and human rights observance. However, for the past few years this organization has been betraying its just course. DARUSO is plagued with corruption and misuse of funds; lack of transparency and accountability; conflicts among its leaders; increasing gap between its leaders and the common students; tribalism and other forms of discrimination, puppetism and individualism. The root causes of all these menace are known to be poor management and poor leadership. As a result the students have lost trust and interest over DARUSO and its processes.
This calls for a movement of concerned students to make progressive change in the students’ community through a holistic reform process. This reform process will enhance academic prosperity, good governance, democracy and human rights observance through promoting good leadership and social responsibility.

Trust, confidence, partnership, tripartite and mutually between the government, DARUSO and UDSM administration should be restored. Dialogue should be promoted at all levels in collaboration with other actors such as The Tanzania Students Networking Programme (TSNP). Every problem should be solved through negotiations, protest should not be entertained. This may be used if all the means of solving matters amicably have been exhausted.

Democratization is needed to address the academic problems of students. For instance, students should be involved in academic planning fully and encouraged to make useful inputs in the development of academic curricula. In 1984, for the first time since independence, the Constitution of the United Republic of Tanzania was amended to include a Bill of Rights. The Constitution provided for the right to education and the right to opinion and expression which include academic freedom. But rights are not simply given; they are won. And even when won, they cannot endure unless protected, nurtured and continuously defended against encroachment and curtailment.

Concerning the students’ welfare the era of the government to cover all the costs and other amenities has gone. The forerunners of student activism have struggled to resist cost sharing but they failed. A new approach is needed to ensure that in the implementation of these programs does not affect the welfare of the poor students. This should include massive sensitization of the student community and ensure that safety nets such as the education fund are operating. The stringent conditions of the international Shylocks have begun to put a squeeze on education in a dramatic fashion. Tanzania, like the rest of the African continent, finds itself entangled in a web of socio-economic crises. As budgetary allocations for education become minuscule, education is threatening to become the preserve of a minority of the wealthy and influential in our society.

This new outlook is to involve promoting self-realization among students and enabling the students to understand their responsibility in the community. As People's free and independent existence is in question, they are beginning to question the existence of unfree and right-less policies. Students, as academicians, intellectuals and purveyors of knowledge, have a human obligation and a social responsibility towards the People's Struggle for Rights, Freedom, Social Transformation and Human Emancipation. The participation of students in the struggle of the people is inseparably linked with the struggle for the autonomy of institutions of higher education and the freedom to pursue knowledge without let, hindrance and interference from persons in authority.

Society needs to see a well-coordinated, networked, knowledgeable and committed students’ community in which students freely and actively participate in issues pertaining to their welfare and that of the whole society. The concerned students should come up and reform the UDSM student politic.

The author of this article-Mnyika, J.J. is a youth activist.


Epilogue:
This article was written early 2005(by then the author was non partisan) but it can be circulated and serve as food for thought early 2009 and beyond. A series of events have happened since then in student body politic, with both positive and negative trends. Of recent the university was closed and DARUSO top leadership are not part of the students who have been so far re-admitted.( DARUSO has been technically disbanded due to leadership vacuum- unlikely DUSO which was legally disbanded). The demonstration organized by TSNP against cost sharing policy and solidarity call for unconditionally readmission of all students has been technically banned by the police. (By mere reason that TSNP has said its an organization while it is a company limited by guarantee!. So according to Commander Kova, TSNP that submitted permit application letter is legally inexistent. Although he recognizes that there is a company registered in BRELA No.42386 called Tanzania Students Networking Programme).

Mpishi na Mafiga Matatu

Mpishi yoyote makini hulenga kuhakikisha mafiga yanamwezesha kupika. Mpishi makini huangalia mafiga yanayowezesha chungu kukaa vizuri, chakula kisimwagike, kiive, apakuwe, kiliwe. Mpishi makini hana lengo la kuhakikisha mafiga yako sawa sawa lakini mbinu ni kuhakikisha yapo sawa. Nia ni kuona chungu hakipinduki. Maendeleo ni chungu cha chakula, kiongozi ni figa, kura ni Mpishi. Mpishi makini hachunguzi figa kwa rangi, anaangalia figa lililo sawa ambalo litawezesha chungu kukaa vizuri. Mpiga kura makini anapaswa kuchangua kiongozi bora ili apate maendeleo. Kikwete anakiri kabisa kuwa mafiga yake ni mabovu. Vipi amlazimishe Mpishi kuyapikia? Ndio maana nasema nakubaliana na hoja ya mafiga matatu kama zana ya kukibeba chungu cha maendeleo. Mpishi makini akikosa mafiga bora ndani ya nyumba yake anatoka kwenda kutafuta na akikosa huazima kwa jirani. Upinzani umeanzishwa kutoa viongozi mbadala,haya ni mafiga bora yanayopaswa kuchaguliwa. Tukiendelea kuyaacha mafiga yale yale ambayo tunaona ni mabovu, chungu hakitakaa, kitamwagika na tutalala na njaa ya maendeleo. Tutaendelea kukosa viongozi wenye kuwajibika na kuhamasisha nguvu za kutatua kero za wananchi.

Nukuu ya Leo

Chama kimoja hakiwezi kuwa mama wa wote na wala hakiwezi kabisa kuwa mama wa yote

(John Mnyika, 2005. Kutoka: http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_5.html)

Tuesday, January 20, 2009

Ni wakati wa vitendo si sherehe

Salaam

Awali ya yote nakutakia mwaka mpya wenye upendo, furaha na mafanikio. Kwa mwezi mmoja nimekuwa safarini Mbeya kuanzia Disemba 9 mpaka Disemba 12, kuna mang'amuzi mengi kutokana na safari hiyo ambayo niyaandika wakati mwingine. Lakini kwa leo, napenda kukushirikisha Hotuba ya Obama wakati wa kuapishwa kwake:

Barack Obama has been sworn in as the 44th US president. Here is his inauguration speech in full. "My fellow citizens: I stand here today humbled by the task before us, grateful for the trust you have bestowed, mindful of the sacrifices borne by our ancestors. I thank President Bush for his service to our nation, as well as the generosity and cooperation he has shown throughout this transition. Forty-four Americans have now taken the presidential oath. The words have been spoken during rising tides of prosperity and the still waters of peace. Yet, every so often the oath is taken amidst gathering clouds and raging storms. At these moments, America has carried on not simply because of the skill or vision of those in high office, but because We the People have remained faithful to the ideals of our forbearers, and true to our founding documents. So it has been. So it must be with this generation of Americans. That we are in the midst of crisis is now well understood. Our nation is at war, against a far-reaching network of violence and hatred. Our economy is badly weakened, a consequence of greed and irresponsibility on the part of some, but also our collective failure to make hard choices and prepare the nation for a new age. Homes have been lost; jobs shed; businesses shuttered. Our health care is too costly; our schools fail too many; and each day brings further evidence that the ways we use energy strengthen our adversaries and threaten our planet. These are the indicators of crisis, subject to data and statistics. Less measurable but no less profound is a sapping of confidence across our land - a nagging fear that America's decline is inevitable, and that the next generation must lower its sights. Today I say to you that the challenges we face are real. They are serious and they are many. They will not be met easily or in a short span of time. But know this, America - they will be met. On this day, we gather because we have chosen hope over fear, unity of purpose over conflict and discord. On this day, we come to proclaim an end to the petty grievances and false promises, the recriminations and worn out dogmas, that for far too long have strangled our politics. We remain a young nation, but in the words of scripture, the time has come to set aside childish things. The time has come to reaffirm our enduring spirit; to choose our better history; to carry forward that precious gift, that noble idea, passed on from generation to generation: the God-given promise that all are equal, all are free, and all deserve a chance to pursue their full measure of happiness. In reaffirming the greatness of our nation, we understand that greatness is never a given. It must be earned. Our journey has never been one of short-cuts or settling for less. It has not been the path for the faint-hearted - for those who prefer leisure over work, or seek only the pleasures of riches and fame. Rather, it has been the risk-takers, the doers, the makers of things - some celebrated but more often men and women obscure in their labour, who have carried us up the long, rugged path towards prosperity and freedom. For us, they packed up their few worldly possessions and travelled across oceans in search of a new life. For us, they toiled in sweatshops and settled the West; endured the lash of the whip and plowed the hard earth. For us, they fought and died, in places like Concord and Gettysburg; Normandy and Khe Sahn. Time and again these men and women struggled and sacrificed and worked till their hands were raw so that we might live a better life. They saw America as bigger than the sum of our individual ambitions; greater than all the differences of birth or wealth or faction. This is the journey we continue today. We remain the most prosperous, powerful nation on earth. Our workers are no less productive than when this crisis began. Our minds are no less inventive, our goods and services no less needed than they were last week or last month or last year. Our capacity remains undiminished. But our time of standing pat, of protecting narrow interests and putting off unpleasant decisions - that time has surely passed. Starting today, we must pick ourselves up, dust ourselves off, and begin again the work of remaking America. For everywhere we look, there is work to be done. The state of the economy calls for action, bold and swift, and we will act - not only to create new jobs, but to lay a new foundation for growth. We will build the roads and bridges, the electric grids and digital lines that feed our commerce and bind us together. We will restore science to its rightful place, and wield technology's wonders to raise health care's quality and lower its cost. We will harness the sun and the winds and the soil to fuel our cars and run our factories. And we will transform our schools and colleges and universities to meet the demands of a new age. All this we can do. All this we will do. Now, there are some who question the scale of our ambitions - who suggest that our system cannot tolerate too many big plans. Their memories are short. For they have forgotten what this country has already done; what free men and women can achieve when imagination is joined to common purpose, and necessity to courage. What the cynics fail to understand is that the ground has shifted beneath them - that the stale political arguments that have consumed us for so long no longer apply. The question we ask today is not whether our government is too big or too small, but whether it works - whether it helps families find jobs at a decent wage, care they can afford, a retirement that is dignified. Where the answer is yes, we intend to move forward. Where the answer is no, programs will end. And those of us who manage the public's dollars will be held to account - to spend wisely, reform bad habits, and do our business in the light of day - because only then can we restore the vital trust between a people and their government. Nor is the question before us whether the market is a force for good or ill. Its power to generate wealth and expand freedom is unmatched, but this crisis has reminded us that without a watchful eye, the market can spin out of control - that a nation cannot prosper long when it favours only the prosperous. The success of our economy has always depended not just on the size of our gross domestic product, but on the reach of our prosperity; on the ability to extend opportunity to every willing heart - not out of charity, but because it is the surest route to our common good. As for our common defence, we reject as false the choice between our safety and our ideals. Our founding fathers, faced with perils we can scarcely imagine, drafted a charter to assure the rule of law and the rights of man, a charter expanded by the blood of generations. Those ideals still light the world, and we will not give them up for expedience's sake. And so to all other peoples and governments who are watching today, from the grandest capitals to the small village where my father was born: know that America is a friend of each nation and every man, woman, and child who seeks a future of peace and dignity, and we are ready to lead once more. Recall that earlier generations faced down fascism and communism not just with missiles and tanks, but with the sturdy alliances and enduring convictions. They understood that our power alone cannot protect us, nor does it entitle us to do as we please. Instead, they knew that our power grows through its prudent use; our security emanates from the justness of our cause, the force of our example, the tempering qualities of humility and restraint. We are the keepers of this legacy. Guided by these principles once more, we can meet those new threats that demand even greater effort - even greater cooperation and understanding between nations. We will begin to responsibly leave Iraq to its people, and forge a hard-earned peace in Afghanistan. With old friends and former foes, we will work tirelessly to lessen the nuclear threat, and roll back the spectre of a warming planet. We will not apologize for our way of life, nor will we waver in its defence, and for those who seek to advance their aims by inducing terror and slaughtering innocents, we say to you now that our spirit is stronger and cannot be broken; you cannot outlast us, and we will defeat you. For we know that our patchwork heritage is a strength, not a weakness. We are a nation of Christians and Muslims, Jews and Hindus - and non-believers. We are shaped by every language and culture, drawn from every end of this earth; and because we have tasted the bitter swill of civil war and segregation, and emerged from that dark chapter stronger and more united, we cannot help but believe that the old hatreds shall someday pass; that the lines of tribe shall soon dissolve; that as the world grows smaller, our common humanity shall reveal itself; and that America must play its role in ushering in a new era of peace. To the Muslim world, we seek a new way forward, based on mutual interest and mutual respect. To those leaders around the globe who seek to sow conflict, or blame their society's ills on the West - know that your people will judge you on what you can build, not what you destroy. To those who cling to power through corruption and deceit and the silencing of dissent, know that you are on the wrong side of history; but that we will extend a hand if you are willing to unclench your fist. To the people of poor nations, we pledge to work alongside you to make your farms flourish and let clean waters flow; to nourish starved bodies and feed hungry minds. And to those nations like ours that enjoy relative plenty, we say we can no longer afford indifference to suffering outside our borders; nor can we consume the world's resources without regard to effect. For the world has changed, and we must change with it. As we consider the road that unfolds before us, we remember with humble gratitude those brave Americans who, at this very hour, patrol far-off deserts and distant mountains. They have something to tell us, just as the fallen heroes who lie in Arlington whisper through the ages. We honour them not only because they are guardians of our liberty, but because they embody the spirit of service; a willingness to find meaning in something greater than themselves. And yet, at this moment - a moment that will define a generation - it is precisely this spirit that must inhabit us all. For as much as government can do and must do, it is ultimately the faith and determination of the American people upon which this nation relies. It is the kindness to take in a stranger when the levees break, the selflessness of workers who would rather cut their hours than see a friend lose their job which sees us through our darkest hours. It is the firefighter's courage to storm a stairway filled with smoke, but also a parent's willingness to nurture a child, that finally decides our fate. Our challenges may be new. The instruments with which we meet them may be new. But those values upon which our success depends - honesty and hard work, courage and fair play, tolerance and curiosity, loyalty and patriotism - these things are old. These things are true. They have been the quiet force of progress throughout our history. What is demanded then is a return to these truths. What is required of us now is a new era of responsibility - a recognition, on the part of every American, that we have duties to ourselves, our nation, and the world, duties that we do not grudgingly accept but rather seize gladly, firm in the knowledge that there is nothing so satisfying to the spirit, so defining of our character, than giving our all to a difficult task. This is the price and the promise of citizenship. This is the source of our confidence - the knowledge that God calls on us to shape an uncertain destiny. This is the meaning of our liberty and our creed - why men and women and children of every race and every faith can join in celebration across this magnificent mall, and why a man whose father less than 60 years ago might not have been served at a local restaurant can now stand before you to take a most sacred oath. So let us mark this day with remembrance, of who we are and how far we have travelled. In the year of America's birth, in the coldest of months, a small band of patriots huddled by dying campfires on the shores of an icy river. The capital was abandoned. The enemy was advancing. The snow was stained with blood. At a moment when the outcome of our revolution was most in doubt, the father of our nation ordered these words be read to the people: "Let it be told to the future world...that in the depth of winter, when nothing but hope and virtue could survive...that the city and the country, alarmed at one common danger, came forth to meet [it]." America. In the face of our common dangers, in this winter of our hardship, let us remember these timeless words. With hope and virtue, let us brave once more the icy currents, and endure what storms may come. Let it be said by our children's children that when we were tested we refused to let this journey end, that we did not turn back nor did we falter; and with eyes fixed on the horizon and God's grace upon us, we carried forth that great gift of freedom and delivered it safely to future generations. Thank you. God bless you. And God bless the United States of America."

Wednesday, November 19, 2008

Ya ukraine yarejea Urusi




Tafadhali tazama mwisho wa ujumbe huu, usome tuhuma na malalamiko ya Wanafunzi wa Tanzania walioko nchini Russia kuhusu Ubalozi wa Tanzania nchini humo, Bodi ya Mikopo na serikali kwa ujumla. Tuhuma na malalamiko hayo yamewasilishwa kwetu Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) na Rais wa .Umoja wa Wanafunzi wa Kitanzania(Patrice Lumumba University, Moscow), Bwana Boniphace Kanyathare.

Naomba muyachambue na kuchapa kama habari au makala ili umma wa watanzania uweze kufahamu malalamiko yao. BAVICHA tutafanya ufuatiliaji wa malalamiko hayo na kutoa tamko la kina siku chache zijazo.

Lakini, katika habari za kesho; pamoja na uchambuzi wa malalamiko hayo, mnaweza kuninukuu ifuatavyo:

TAARIFA KWA UMMA

· Naitaka bodi ya Mikopo hapa nchini ieleze wazi kwa umma fedha ambazo imeshapeleka mpaka sasa na fedha ambazo iliwajibika kuzipeleka ikiwemo kutaja majina ya wanafunzi waliostahili kupokea fedha hizo. Na ifanye utaratibu wa kupeleka fedha zilizobaki haraka iwezekanavyo ili kuokoa hatma ya vijana hawa.
· Nalaani vitendo vya unyanyasaji na uvunjaji wa haki za binadamu waliofanyiwa vijana hawa nchini Urusi vikihamasishwa, kushuhudiwa na kushabikiwa na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Urusi. Tunamtaka Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Jaka Mwambi atoe kauli ya haraka kueleza kadhia hiyo. Bwana Mwambi yuko nchini Urusi kwa gharama za kodi ya watanzania wote bila kujali itikadi kwa lengo la kutumikia umma na kuwakilisha maslahi ya watanzania nchini humo. Tulitarajia awe balozi mzuri wa kuhakikisha vijana hawa wanasikilizwa na kusaidiwa baadala ya kunyanyaswa. Tunamtaka Balozi afungue mara moja ukumbi wa majadiliano na vijana hao ili kulipatia ufumbuzi wa haraka suala lao. Serikali ichukue hatua za kinadhamu kwa maofisa watakaobainika kusababisha hali hii.
· Kwa kuwa vitendo kama hivi vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara(rejea tatizo la wanafunzi wa kitanzania waliokwama nchini Ukraine); ni wazi kwamba kuna tatizo la kimfumo ambao serikali ya CCM imeshindwa kulipatia ufumbuzi wa kudumu. Pia pamekuwepo na tuhuma za ufisadi katika mchakato wa malipo ya wanafunzi wa kitanzania wanaosoma nje ya nchi. Kuna haja ya wadau kuunganisha nguvu katika kulitafakari na kulipatia ufumbuzi tatizo la kuchelewa ama kupunjwa kwa malipo ya watanzania wanaosoma nje ya nchi. Aidha tunaitaka serikali ieleze kwa umma marekebisho yaliyofanyika toka ahadi za Rais Kikwete na viongozi wenzake wa serikali walizozitoa kuhusu kuboresha mfumo wa kupeleka vijana watanzania nje ya nchi kwa ajili ya masomo.
· Aidha serikali iliwahi kutoa tamko la kutaka kupunguza idadi ya watanzania wanaopelekwa kusoma nje ya nchi; wakati serikali imetoa tamko hilo, bado na ndani ya nchi mfumo wa elimu ya juu nao umekuwa ukiathiriwa na migomo na migogoro ya mara kwa mara inayosababishwa na sera mbovu ya ubebaji wa gharama za elimu ya juu(cost bearing). Serikali imekuwa ikiwaghilibu raia wake kuwa sera hii ni ya uchangiaji(cost sharing) wakati ambapo wanafunzi wamekuwa wakipewa mikopo ambayo wanajibika kuilipa baada ya masomo yao; lakini kibaya zaidi wanashindwa kupatika mikopo hiyo kwa asilimia mia moja na hivyo wengine kushindwa kumudu gharama za elimu ya juu. Wakati fedha za taifa letu zikiwa zinafujwa kupitia matumizi ya anasa ya serikali na ufisadi wa mabilioni unaofanywa kwenye kodi za wananchi; ni aibu kwa serikali hiyo hiyo kushindwa kugharamia elimu, ni aibu zaidi kwa serikali kushindwa hata kukopesha wanafunzi wa asilimia mia moja.


Tunataka watanzania waelewe kwamba taifa linahitaji mabadiliko makubwa katika mfumo wa elimu yetu. Kama kungekuwa na sera bora na mfumo mzuri wa kugharamia elimu ya watanzania, vijana watanzania wangeweza kusoma popote pale iwe ndani ya nchi au nje ya nchi bila kulazimika kufanya maandamano na migomo ya mara kwa mara yenye kuathiti hatma ya elimu yao. CHADEMA kikiwa ni chama mbadala kiko tayari kuwaongoza watanzania kufikia hatma hiyo.

Imetolewa 16 Novemba, 2008:




John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
Na Kaimu Mkurugenzi Masuala ya Kimataifa
0754694553

MATATIZO YALIYOPEREKEA VIJANA WAKITANZANIA WANAOSOMA CHUOKIKUU CHA URAFIKI (PATRICE LUMUMBA-MOSCOW-RUSSIA) KUANDAMANA KWA SIKU YA TATUMFULULIZO NJE YA UBALOZI WA TANZANIA MOSCOW
Ndugu zangu watanzania, leo kwa mara nyingine nimeamua kuwaelezea kiundani matatizo yanayotukabili watoto wenu tulioletwa na serikali yetu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kusoma mjini Moscow Russia,matatizo haya yameperekea baadhi ya wanafunzi kushindwa kuendelea na masomo yao,na wengine kushindwa kukamilisha taratibu za awali ili waweze kuanza masomo.
Matatizo yetu yamegawanyika katika makundi yafuatayo
a).Wanafunzi wafuatao mpakasasa hawajaletewa fedha zao za kujikimu pamoja na ada .
1. BROWN ELIAS LEKULE – mwaka wa tatu
2. BONIPHACE ELPHACE KANYATHARE – mwaka wa tatu
3. ALLY MOHAMED LUSESA – mwaka wa pili
4. JACKSON JACKOB TEMU – mwaka wa kwanza
5. MUHAYA SAMWELI CHITIMBO – mwaka wa kwanza
6. KINANASY R. SEIF – mwaka wa kwanza
7. MARIA F. MAJIJI – mwaka wa pili
8. IS-HACK S. IS-HAK – mwaka wa kwanza
9. NICHOLAUS MBILINYI – mwaka wa kwanza
10. ANDULILE FRANCIS MWAIGWISA – mwaka wa kwanza
11. ANDREW MASHAMBA – mwaka wa tatu
12. MICHAEL MBASHA – mwaka wa pili
13. ABDALLAH MOHAMED OTHMAN ELNOFELY – mwaka wa kwanza
Wanafunzi hawa baadhi wapo kozi ya tatu na baadhi wapo kozi ya kwanza, wenzao wote wamepata fedha, wamezipata mwezi wa tisa mwishoni na wengine mwezi wa kumi mwishoni kwa maandamano,fedha walizozipata wanafunzi wa mwaka wa kwanza zilikuwa na mapungufu mengi sana kwani kwa hesabu za kawaida naomba uangalie mfano huu.
Kwa wanafunzi wanaosoma kozi ya “international relationship” wanapaswa kupatiwa fedha zifuatazo kwa mwaka
Tuition fees-4800 us.dollors
Health insurance-250 us.dollors
Meals and accommodation-5400 us dollors
Total amount -10450 us dollors
Kwa baadhi ya wanafunzi wanaosoma kozi hiyo ya “international relation” wametumiwa fedha zifuatazo
1.FATUMA RASHID MOHAMMED-9843 US dollars
2.ISAACK ALOIS ISANZU-7713 US dolars
Ikumbukwe kuwa hawa wanafunzi wote wanasoma kozi moja na wapo darasa moja , lakini wameletewa fedha pungufu na pia ni kiwango tofauti kwa kila mmoja. Mimi kama rais wa watanzania wanaosoma chuoni hapa, niliomba mchanganuo wa fedha hizo kutoka ubalozini lakini maafisa wa ubalozi wakasema hawajaletewa kutoka bodi, tulipo wasiliana moja kwa moja na bodi wakasema wametuma ubalozini , na jitihada hizo za kuupata mchanganuo huo mpaka sasa zimegonga mwamba. Kutokana na hali hii, kuna baadhi ya wanafunzi waliopata fedha ambao mpaka sasa wameshindwa kulipa ada kufuatia ukweli kwamba fedha walizotumiwa ni pungufu. Wanafunzi wapatao 80 wakiwemo mwaka wa kwanza, wa pili na watatu wanakumbwa na tatizo hilo.
B . Mnamo tarehe 29.10.2008 wanafunzi wapya kutoka Tanzania wapatao 28 waliwasili chuoni kutoka Tanzania na ilipofika tarehe 05.11.2008 kundi lapili la wanafunzi wapya kutoka Tanzania wapatao 34 nao waliwasili kutoka Tanzania, wanafunzi wa kundi la kwanza (28) na lapili (34), waliambiwa fedha zao tayari watazikuta urusi (ubalozini), lakini baada ya kufika uongozi wa wanafunzi uliwasiliana na uongozi wa ubalozi ili kujua mustakabali wa fedha zao lakini tulijibiwa kuwa hakukuwa na fedha zao mpaka wenzao waliobaki nyumbani ambao hawajapata barua za mwaliko watakapofika hapa Urusi ndipo fedha zao kwa pamoja zitatumwa ubalozini . Kulingana na taratibu za uhamiaji hapa Urusi, suala hili linaweza kuchukua mwezi mmoja ujao.
Baada ya uongozi kupata majibu hayo tuliamua kuwafahamisha vijana na baada ya vijana kutoridhika na majibu hayo walichagua wawakilishi walioandamana na baadhi ya viongozi kwenda ubalozini ili wapate maelekezo zaidi,
Siku ya tarehe 13.11.2008 ujumbe huo ulienda ubalozini ili kujua mustakabali wa fedha zao walipofika ubalozini, afisa mmoja wa ubalozi, akaamua kupigasimu kwa Mkurugegenzi wa Wizara ya Elimu , Prof Shao, vijana wakiwa wanasikiliza kupitia loud speaker ya simu ya Afisa huyo (Dismas Kajogoo), ndipo waliposhangazwa na maneno ya mkurugenzi wa wizara ya elimu kwa kusema kuwa hautambui ujio wa wanafunzi hao wala hajui kama wapo huku Urusi. Vijana walisikitishwa sana na kauli za afisa huyo wa serikali. Baada ya hapo akawaambia kuwa wafungue accounts ndipo fedha zao ziweze kutumwa , huo ulikuwa uamuzi wa kushangaza ,kwani ikumbukwe kuwa ili mwanafunzi mpya hapa Urusi aweze kufungua account katika benki yoyote ile urusi, ni lazima awe amesajiliwa nchini urusi (amekamilisha taratibu za kiuhamiaji) . Kutokana na ukweli kuwa vijana hawa toka wafike urusi wanamuda usiozidi wiki tatu,na hawajafanyiwa usajili huo kwani ili waweze kusajiliwa ni lazima wafanyiwe uchunguzi wa afya ambao unachukua wikimbili na nusu, baada ya hapo kuna gharama ambazo wanapaswa kulipia ili waweze kukamilisha usajili , na baada ya kukamilisha mambo hayo, usajili hupatikana baada ya mwezi mmoja na nusu au zaidi. Kutokana na mlolongo huo wa usajili nilioufafanua, ni dhahili kwamba zoezi la kufungua accounts linahitaji muda usiopungua miezi mitatu. Hii inamaanisha kwamba vijana hao wakae bila fedha kwa kipindi chote hicho(miezi mitatu na kuendelea). Ikumbukwe kuwa, vijana hao hawana fedha za kujikimu, fedha za mabweni, fedha za medical insurance, na fedha za ada. Pia, ni ukweli kwamba vijana wengi wametoka familia za kimaskini kama yangu na hawakuja na fedha zozote.
Baada ya uongozi wa ubalozi kuona vijana hao hawaridhishwi na majibu hayo ukaahidi kuwakopesha kila mmoja kiasi cha dola za kimarekani 150. Lakini kwa hali halisi fedha hizo ni ndogo sana hapa urusi na haziwezi kukidhi matatizo yao, kwani mwanafunzi mmoja ili aweze kukidhi mahitaji niliyoyataja, anatakiwa apewe dola za kimarekani 5400 kwa mwaka kwa ajili ya kujikimu tu. Wawakilishi hao waliamua kuwarudishia wenzao taarifa, ili waamue cha kufanya kwa pamoja.
Siku hiyo baada ya vijana kumaliza kikao chao ,mimi kama rais wa wanafunzi ambaye pia sijapata fedha za mkopo wangu toka Bodi, nilikwenda ubalozini pamoja na ujumbe wa vijana 13 (wa mwaka wa kwanza wa pili na watatu)ambao pia hawajapata fedha ili kujua mustakabali wa fedha zetu. Kama ilivyokawaida ya ubalozi, tulizuiliwa kuingia ili kuongea na viongozi wa ubalozi , tulikaa nje kwenye baridi kuanzia saa sita mchana mpaka saa kumi na moja jioni ndipo mimi rais nikaruhusiwa kuingia ubalozini, peke yangu na wanafunzi wenzangu wakaendelea kupigwa na baridi kali nje ya ubalozi wanchi yetu tuipendayo, mpaka saa tatu usiku hali zao zilipokuwa mbaya ndipo wakaamua kuondoka, nilipo fika ndani bahati nzuri kiongozi mmoja aliyeingia na vijana wale alibaki ndani na alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi ambao hawajapata fedha, hivyo tukawa waathirika wawili ,tukajaribu kuzungumza na uongozi wa ubalozi kutaka kujua watatusaidia vipi ili tuweze kuendelea na masomo yetu kwa manufaa ya taifa letu,lakini majibu tuliyopewa na viongozi hao wa ubalozi yalikuwa ya kukatisha tamaa na kusisitiza kuwa wao hawahusiki na matatizo yetu na wakasema tunawabebesha mzigo wasiostahili kwani eti wao siyo serikali. Maneno haya yalitolewa na Afisa wa ubalozi bwana Dismas Kajogoo ambaye alizidi kusisitiza bila uoga kwamba, “Serikali ni kikwete na aliounda nao baraza la mawaziri”. Ndugu zangu nguvu ziliniishia na nikashindwa kujua , taifa letu linaelekea wapi? Naje tutaishi vipi ughaibuni bila kuwa na fedha za kujikimu achilia mbali za kulipia ada ya shule pamoja na mabweni? Ikumbukwe kuwa miezi miwili na nusu imeshapita tangu tulipopaswa kupata fedha na mpaka sasa maishayetu yamekuwa ya kusuasua. Baada ya kutathmini pamoja na kiongozi mwenzangu ndipo tulipo amua kukaa ubalozini na kuomba kukutana na balozi ili kujaribu kumsihi afikirie namna ya kuweza kuwasaidia wanafunzi wote wenye matatizo ya fedha lakini ombi letu lilipuuzwa na wakatuacha kwenye chumba cha mkutano ubalozini bila kutusikiliza. kutokana na ukweli kuwa hatukuwa na namna nyingine ya kuweza kuishi tuliamua kulala kwenye viti ubalozini kwa nidhamu ya hali yajuu kwa taifa letu bila kumsumbua mtu yeyote, mpaka asubuhi ya tarehe 14.11.2008 bila kula chochote, ilipofika asubuhi wanafunzi wenzetu walipopata taarifa kuwa mimi rais wao na kiongozi mwingine tulilala ubalozini wanafunzi wapatao 90 ambao hawajapata fedha zao wakiwemo wale wapya wakaandamana wote kuja ubalozini ili waweze waweze kujua hatima ya fedha zao.Mimi pamoja na kiongozi mwenzangu, tuliendelea kukaa ndani ya ubalozi kwenye ukumbi wa mikutano mpaka saa saba mchana, huku wenzetu 90 wakiwa wanapigwa na baridi nje bila kufunguliwa mlango. Mimi na mwenzangu kule ndani tulishangaa kuona maaskari wapatao 11 wakiingia ndani tulikokuwa na kuanza ghafla kutukaba kama majambazi au wahalifu na kutuburuza huku wakituchania nguo zetu na kutukanyagia simu zetu za mikononi mbele ya watumishi wa ubalozi akiwemo Balozi Jaka Mwambi, mpaka nje ya ubalozi ambapo wengine walibaki wakitulinda na wengine wakarudi ndani ya ubalozi , baada ya muda mfupi walitoka na kutukamata tena na kutuingiza ndani ya gari kwa nguvu huku wakituelekezea bunduki kama majambazi mpaka kituoni ,tukaingizwa kwenye selo na kufungiwa kwa muda wa masaa matano bila kuhojiwa., Wakati tupo ndani ya selo wenzetu waliobaki pale nje ubalozini walianza kufanya jitihada za kuwashawishi maaskari watuachie lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda. Baadae mkuu wa kituo alikuja na kupokea maelezo kutoka kwetu ndani ya selo na akasema suala hilo la sisi kukamatwa ndani ya ubalozi wetu lilifanyika kimakosa. Mkuu huyo wa kituo cha polisi alitutaka radhi na akaendelea kufafanua kwamba, maaskari wake waliokuwa lindoni ubalozini siku hiyo walipokea agizo la maandishi lililotiwa sahihi na Afisa wa ubalozi bwana Dismas Kajogoo, akiagiza askari hao watukamate na kututoa ndani ya ubalozi wetu. Baada ya hapo, tuliachiwa huru na majeraha yetu tuliyoyapata wakati askari hao walipotukaba ubalozi.
Mpaka naandika maelezo haya bado wanafunzi wapatao 100 tunaendelea na maandamano mpaka tutakapo pata fedha zetu na balozi Jaka mwambi ametutumia taarifa kuwa kuanzia sasa hawashughuliki na maswala ya wanafunzi mpaka uongozi wa wanafunzi ubadilishwe, na wawekwe watu ambao hawawezi kudai haki zao wala kusimamia utekelezaji wa mkataba kati ya serikali yetu na serikali ya urusi mfano.
1) 1. MKATABA HUO UNASEMA KWA KILA WANAFUNZI WAWILI WANAOSOMESHWA NA SERIKALI YA TANZANIA, SERIKALI YA URUSI(CHUO) HUTOA NAFASI KWA MTU WA TATU KUSOMA BURE. LAKINI KWA WANAFUNZI WALIOFIKA HAPA CHUONI MWAKA 2007/2008 AMBAO WALIKUWA 78 NA BAADAYE KUBAKI 76 NI WANAFUNZI 17 TU NDIO WALIOPEWA NAFASI HIZO. HII NI KINYUME NA MKATABA HUO KWANI WALIOSTAHILI KUPATA UDHAMINI WA CHUO NI 24. KATIKA KUFUATILIA SWALA HILO UONGOZI WA WANAFUNZI ULIGUNDUA KUWA KATIBU WA UBALOZI BWANA MBAROUK N. MBAROUK KWA KUSHIRIKIANA NA AFISA MMOJA WA CHUO WANATUMIA NAFASI HIZO ZA WALALA HOI KWA MANUFAA YAO. HII INAMAANISHA KUWA, MWAKA ULIOPITA NAFASI 7 HAZIJULIKANI ZIMEKWENDA WAPI. UONGOZI WA WANAFUNZI UMEJARIBU KUFUATILIA SUALA HILI LAKINI MIMI BINAFSI KAMA RAIS WA UMOJA WETU PAMOJA NA MAKAMU KATIBU TULIKUMBANA NA VITISHO VYA KUFUKUZWA CHUO KUTOKA KWA AFISA WA CHUO (MRUSI) ANAYESHUGHULIKIA SUALA HILO, SUALA HILI NI VYEMA SERIKALI YETU IKALICHUNGUZA UPYA NA KWA MAKINI KWANI KUNA KILA DALILI ZA UFISADI. MAAFISA HAO WA UBALOZI HAWANA UCHUNGU NA NCHI YETU KWANI KUPATIKANA KWA NAFASI HIZO KUNGEPUNGUZA MALIPO YA FEDHA ZA ADA KWA WATU HAO, NA FEDHA HIZO ZINGEWEZA KUTUMIKA KUWASOMESHA WATOTO WA MASKINI AMBAO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE WAMEKOSA NAFASI ZA KUSOMA.
2) PILI UMEZUKA MTINDO CHUONI WA KUWALAZIMISHA WANAFUNZI KUSOMA LUGHA KWA MUDA WA MIAKA MIWILI KINYUME NA MKATABA UNAOSEMA WAZI KWAMBA MWANAFUNZI ANAPASWA KUSOMA LUGHA KWA MWAKA MMOJA TU. BILA SABABU ZA MSINGI. NA KATIKA HILI KUNA MKONO WA MOJA KWA MOJA WA KATIBU WA UBALOZI BWANA MBAROUK N. MBAROUK . AFISA HUYO HUFAIDIKA NA UVUNJWAJI WA MKATABA HUO KWANI, MWANAFUNZI ANAPOSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI, HULIPIWA ADA NUSU KWA ULE MWAKA WA KWANZA WA LUGHA. IKUMBUKWE KUWA KILA MWAKA SERIKALI HUTUMA ADA YA MWAKA MZIMA KWA KILA MWANAFUZI, HIVYO NI DHAHIRI KWAMBA NUSU YA ADA INAYOBAKI HUMNUFAISHA AFISA HUYO WA UBALOZI. TUNAOMBA SERIKALI IFANYE UCHUNGUZI WA KINA KWANI DOCUMENTS ZA USHAHIDI WA MALIPO HAYO TUNAZO, NA MOJA YA NYARAKA HIZO TUMEAMBATANISHA NA TAARIFA HII. MAJINA YALIYOWEKEWA TIKI NI YA WANAFUNZI WALIOLAZIMISHWA KUSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI NA KULIPIWA ADA NUSU MWAKA. HUU NI UBADHILIFU WA HALI YA JUU KWA FEDHA ZA WANAFUNZI NA NI UDANGANYIFU KWA TAIFA. MIMI KAMA RAIS WA UMOJA WETU WA WANAFUNZI SITA RUHUSU LITOKEE KWANI NINAIPENDA NCHI YANGU NA NINAWAPENDA WANAFUNZI WENZANGU NA HILI SUALA LA KUSOMA LUGHA MIAKA MIWILI INABIDI LIISHE ,ILI MAFISADI WASIPATE MWANYA ,KWANI SISI TULIOKUJA 2005 KUNA BAADHI YA WANAFUNZI WALICHELEWA KUJA KWANI WALIFIKA URUSI JANUARI BADALA YA SEPTEMBER NA WALISOMA LUGHA KWA MUDA WA MIEZI MITANO BADALA YA MIEZI KUMI BILA KURUDIA MWAKA NA KWA SASA WAPO KOZI YA TATU. KUWALAZIMISHA WANAFUNZI KUSOMA LUGHA KWA MIAKA MIWILI ILI UBALOZI UNUFAIKE NA FEDHA ZA ADA,NI MPANGO MCHAFU UNAORUDISHA NYUMA MAENDELEO YA TAIFA ILI KUWAFAIDISHA WACHACHE.
NDUGU ZANGU WATANZANIA PAMOJA NA YOTE AMBAYO VIONGOZI WA UBALOZI WAMEFANYA ILI KUWEZA KUFICHA MAOVU HAYO MPAKA SASA WAMESHINDWA, NA KWASASA LENGOLAO WANAWATUMIA BAADHI YA WANAFUNZI WENZETU KWA KUWAPA RUSHWA ILI KUWEZA KUTUONDOA KWENYE UONGOZI , PAMOJA NA VITISHO MBALIMBALI KUTOKA CHUONI ILI TUSISIMAMIE HAKI ZETU, LAKINI HATURUDI NYUMA TUNAAMINI KWA DHATI KUWA TANZANIA INAHITAJI MABADILIKO NA MABADILIKO TUTAYALETA WENYEWE VIJANA HIVYO NAOMBA NITUMIE NAFASI HII KUWAOMBA VIJANA WENZANGU ,TUSIMAME IMARA ILI TUWEZE KUIOKOA NCHI YETU HUUNDIO WAKATI WETU.
BAADHI YETU WANASHINDWA KUSIMAMIA UKWELI KWA KUOGOPA KUWA FAMILIA WANAZOTOKA NI MASKINI , NAOMBA NIWAHAKIKISHIE KUWA FAMILIA ZETU MASKINI TUTAWEZA KUZIKOMBOA KWA KUSIMAMA IMARA NA KUTETEA KILE KILICHO CHEMA MBELE ZA MUNGU, NA SIYO VINGINEVYO , SINTORUDINYUMA NA UKWELI LAZIMA UFAHAMIKE ILI HAKI IWEZE KUTENDEKA MIMI KAMA RAIS WA UMOJA WA WANAFUNZI WA KITANZANIA KATIKA CHUOKIKUU CHA PATRICE LUMUMBA MOSCOW, NAOMBA KWAPAMOJA TUUKEMEE UBADHILIFU ILI TAIFA LETU LIWEZE KUSIMAMA IMARA.
TUNAENDELEA NA MGOMO WA AMANI MPAKA MATATIZO YETU YATAKAPO PATA SULUHISHO,KWANI KWA NJIA YA MAZUNGUMZO TUMEJARIBU LAKINI KILA MARA TUMEKUWA TUKIFUNGIWA NJE YA UBALOZI KWENYE BARIDI KALI BILA KURUHUSIWA KUZUNGUMZA NAO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
BONIPHACE ELPHACE KANYATHARE
RAIS WA UMOJA WA WANAFUNZI WA KITANZANIA
(PATRICE-LUMUMBA UNIVERSITY). MOSCOW.RUSSIA



Sunday, November 9, 2008

Taifa lenye utamaduni wa ufisadi

Leo niwapatie mchango wangu nilioutoa hapa kwenye mjadala unaoendelea kuhusu ufisadi: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/20024-ccm-yafanya-maamuzi-mazito-kamati-kuu-22.html#post319258

"Muda mrefu sijachangia JF, ile hii post imenigusa sana.Maudhui yake yamehitimisha kile ambacho nimewahi kukisema na kukiandikia mara kadhaa kwamba nchi yetu imeingia katika 'utamaduni wa ufisadi'. Ambapo ile dhana ya kila 'mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake'(ongezea mahali pake)- soma 'kazini kwake', imekuwa ni jambo la kawaida katika maisha ya watanzania.Hili ndio tatizo na msingi ambalo kama taifa tunapaswa kulishughulikia kurejesha MAADILI na UWAJIBIKAJI.Wazee wetu wanatuambia enzi za miaka ya awali ya Mwalimu ufisadi hakuwa umeshika kazi na kupenya katika mishipa ya wananchi na viongozi kama ilivyo sasa.Swali la kujiuliza- ni kwa vipi tumefika hapa? Na tunarudi vipi katika misingi iliyokuwepo awali?Wengine wanasema ni kwa sababu ya mabadiliko ya kiuchumi kuelekea uchumi wa soko ambao wengine wanajenga hoja kuwa unaambatana na ubinafsi na kutaka kujilimbikizia. Wao wanaamini kwamba ujamaa ungekuwa suluhu ya kuendelea kuwa na maadili.Wengine waamini kuporomoka kwa uchumi kulikoleta hali ngumu ya maisha na hatimaye mishahara kushuka ukilinganisha na gharama za maisha kumepunguzia wananchi uwezo wa kununua na hatimaye sasa wafanyakazi wengine kugeuka wala rushwa mahali pao na watoa rushwa kwa wengine. Hawa wanajaribu kuelezea rushwa ndogo ndogo(petty corruption). Ukiwauliza ni kwa vipi matajiri wakubwa na viongozi wakuu wa serikali wenye mishahara mizuri na maslahi mazuri nao wanapokea na kutoa rushwa kubwa kubwa(grand corruption), wanakosa majibu mazuri.Katika kukubiliana na rushwa, wapo waomini kwamba tukiweka sheria kali na kujenga taasisi zenye nguvu, rushwa itaondoka. Lakini wanasahau kwamba sheria zinapaswa kusimamiwa na watu, taasisi nazo zinasimamiwa na watu. Kama ukiwa na taifa lenye utamaduni wa ufisadi, sheria hata ziwe nzuri haziwezi kusimamiwa(rejea kauli ya rais kwamba watakaorudisha fedha za EPA watasamehewa- nimeijadili kidogo hapa: JJ: Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika ); mnakumbuka pia mfano(rejea hapa:TAKURU inalinda na kutetea Rushwa? ) wa Taasisi ya TAKUKURU(wakati huo TAKURU) ilivyoisafisha RICHMOND na mchakato wake.Wengine wanasema basi tuanzie kwa kuweka viongozi waadilifu, halafu wao kwa maneno na matendo yao watasimamia utawala wa sheria na uwajibikaji wa taasisi hizo. Lakini uchaguzi kwenye taifa lenye utamaduni wa ufisadi mara nyingi huzaa viongozi mafisadi. Wananchi mafisadi huchagua viongozi mafisadi.Kwa hiyo hili suala la ufisadi, ni kama hadithi ya kuku na yai- ni mjadala unaozunguka kusema kwamba kipi kilianza.Kwa maoni yangu, sababu zote kila moja kwa nafasi yake inachangia katika utamaduni wa ufisadi. Ujamaa wa dola(naita ujamaa wa dola kwa kuwa nina mtazamo tofauti sana kuhusu uzuri na udhaifu wa ujamaa mfululizo wa uchambuzi wangu kuhusu hoja hii upo hapa: Tanzania, CHADEMA, CCM na mjadala wa falsafa na itikadi; Lipi ni jibu? ) ,ulizaa urasimu wa bidhaa na huduma ambao ulichangia katika baadhi ya wananchi kuanza kuweka pemebeni misingi ya maadili na uwajibikaji na kujiingiza katika utamaduni wa ufisadi. Viongozi waliochaguliwa baadaye walikuja tu kuchochea utamaduni wa ufisadi ambao tayari ilishaanza. Utadamuni ambao ulijengwa pia kwa raia kuweka mawazo yao yote kwa dola na serikali. Kushuka kwa hali ya maisha na kupungua kwa uwezo wa kununua kulikoambana na mishahara duni kuliongeza tu huu utamadauni wa ufisadi. Halafu ndipo tukaingia katika mduara ya ufisadi(the cycle of corruption); kwamba chama tawala na vingozi wake wanalinda ufisadi, wananchi nao wanazidi kuwa mafisadi katika mahali pao pa kazi na uchaguzi ukija mafisadi wengi zaidi wanachaguliwa; mzunguko unaoendelea. Sasa changamoto ni kuvunja huu mduara.Kwa bahati njema, si raia wote ni mafisadi. Si viongozi wote ni mafisadi. Bado kuna tabaka la watu wachache ambao si mafisadi. Hatua za haraka zinahitajika kuchukuliwa na tabaka hilo kuliokoa taifa. Uzoefu unaonyesha kwamba utamaduni wa ufisadi huwa ukikomaa una kawaida ya ama kuangusha dola au kuazaa taifa lenye matabaka kati ya walionacho na wasionacho na lenye vurugu za kijamii. Tunapaswa tusifike huko kama taifa.Kama ambavyo takaba la watu wachache liliamini kwamba mkoloni anaweza kutoka katikati ya tabaka la waliowengi waliomini kama mkoloni hawezi kushindika na kwamba kutawaliwa ni jambo la kawada na kwamba waafrika wameumbwa kutawaliwa; ndivyo inavyopasa kuwa kwenye suala hili la ufisadi.Suluhisho ni kurudi kwa umma. Hao waadilifu wachache kwenda kwa wananchi kutoa elimu ya uraia, wananchi wakaunga mkono kwamba ufisadi wao ndio kaburi lao; kwamba ufisadi wa watawala ni jeneza tu la kuwabeba na kuwazika. Kwamba ufisadi unawaathiri zaidi wao wenyewe. Wananchi wakaelewa uhusiano kati ya maisha yao kuwa mabaya, huduma za kijamii kuwa mbovu na ufisadi. Wananchi wakajua kwamba ufisadi ni dhambi si ya kuliathiri taifa tu bali kujiathiri mtu mwenyewe. Hapo ndio wananchi watachukua hatua kwa nguvu ya umma. Tararibu tutajenga taifa lenye utamaduni wa maadili ambao mimi huwa napenda kuuita utamaduni wa uwajibikaji. (Niliwahi kugusia kidogo hii dhana hapa: 45th Anniversary: My greetings to you and reflections with Mwalimu Nyerere). Katika taifa la namna hiyo, viongozi wanamachaguo matatu; ama kukubaliana na sauti ya umma na wao kuanza kusimamia uwajibikaji(Rais Kikwete kuunda kamati ya bomani na Bunge kuunda Kamati ya Richmond ni matokeo ya umma kuanza kuchukua hatua baada ya Hoja ya Zitto kuhusu Buzwagi na hoja ya Dr Slaa kuhusu BOT. Kupelekwa kwa kesi za EPA ni matokeo ya yaliyojiri baada ya Kutajwa kwa Orodha ya Mafisadi); ama watawala kunyamaza(na wakati mwingine kugeuka madikteta) na kuruhusu kuzuka kwa utamaduni wa hukumu ya ujmma(mob justice) ambao unaweza kuwa na faida katika usalama wa taifa ama unaweza kutishia utangamano wa umma(unaweza kuwa na mifano ya hivi karibuni) ama wananchi kuvuta subira na kusubiri kuchukua hatua wakati wa chaguzi(kuondoa madarakani utawala na watawala waolinda ufisadi).Lakini hatua hii inapaswa kwenda sambamba na umma kutaka hatua zichukuliwe ili kuboresha pia maeneo mengine mathalani suala la mishahara na usimamizi wa taasisi za uwajibikaji.Hii ni njia ya amani kuelekea maadili na uwajibikaji. Njia nyingine ni kikundi cha watu wachache kujitwalia madaraka ama kwa sanduku la kura lakini mara nyingi kwa mapinduzi na kujivika dhima ya kulitoa taifa kutoka katika utamaduni wa ufisadi na kuelekea katika maadili na uwajibikaji. Hawa huitwa madikteta wakarimu!(mifano imewahi kutokea katiika mataifa mengine). Hawa huweka adhabu kali dhidi ya aina zote za ufisadi na huzisimamia adhabu hizo na hatimaye kujenga hofu katika taifa kwa mafisadi na hiyo watu kuacha ufisadi si kwa kuelewa au kwa kupenda; bali kwa hofu! Tatizo la msingi la njia hiyo ni kuwa linaanzia kwenye njia yenyewe na hivyo baada ya muda fulani watawala hao hao wenyewe hugeuka kuwa mafisadi kwa kujilimbikizia kutokana na mamlaka makubwa wanayokuwa nayo ama huishia kukataa kutoka madarakani na hatimaye kuzua tena utadamuni wa ufisadi.Hivyo, nawapongeza Dr Slaa na Zitto kwa njia mliyoamua kuipitia. Mabadiliko huanzia kwa mtu mwenyewe, naamini kwa kukataa kwako umemuambukiza huyo mzee utamaduni wa uadilifu na uwajibikaji. Majaribu ni mengi lakini hakuna sababu ya kukata tamaa. Uovu hushamiri wema unapokata tamaa.Lakini tukumbuke pia rushwa kubwa kubwa katika mataifa ya Afrika inachangiwa pia na mataifa ya nje hususani kupitia makampuni makubwa(MNC). Nilikuwa napitia sheria za nchi mbalimbali, mataifa mengi yanakataza ndani ya nchi zao mashirika yao kutoa chochote kupata zabuni lakini mataifa hayo hayo yametunga sheria ambazo zinaruhusu mataifa yao kuwahonga viongozi wa kifrika katika kupata zabuni. Hivyo uhusiano wa kimataifa umejengwa katika misingi ya utadamuni wa ufisadi uliojificha katika vivuli vya commission nk.Jambo moja lazima tuamue, kama tunataka maendeleo ya taifa letu-hatuna jinsi zaidi ya kuendeleza utamaduni wa uwajibikaji. Ambapo kila mtu atawajibika kwa nafasi yake na atakayeshindwa kuwajibika atawajibishwa. Umaskini wetu umechangia katika ufisadi, lakini umaskini wetu sio chanzo kikuu cha ufisadi huu. Hivyo, lazima tufikiri zaidi na kuendelea kuchukua hatua.BTW 1: Thread inahusu Kamati Kuu ya CCM, mod aidha badilisheni heading au hii michango kuhusu ufisadi ianzishwe thread yake.BTW 2: Zitto, mpe hongera Chachage Jr.BTW 3: Unaweza kuwa ulishawahi kuwa fisadi, ama ulishawahi kuwa fisadi lakini kama kuna chochote kinaweza kukugusa katika mjadala huu, unaweza kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Kwenye kitabu kitakatifu kimojawapo kuna hadhithi ya Saul ambaye alikuwa anachinja watu wa dini, baadaye akaongoka na kuwa Paulo mweneza dini.BTW 4: Kwa fisadi yoyote anayesoma hapa-aelewe kwamba ufisadi ni uuaji wa taifa na wananchi walio wengi. Ni ubatili, sawa na kufukuza upepo! Ni raha ya muda fulani na karaha ya muda mrefu.Nawakatika mjadala mwema mpaka panapo majaliwa"

Friday, November 7, 2008

TUBADILI MFUMO WA UCHAGUZI KUPATA UONGOZI BORA

TUBADILI MFUMO WA UCHAGUZI KUPATA UONGOZI BORA
Na John Mnyika

Makala yangu ya leo inajikita katika eneo moja tu: “Mfumo wa Uchaguzi Tanzania”. Mfumo ni roho ya uchaguzi na chaguzi ndio msingi wa Siasa. Kama siasa(nikimaanisha siasa safi) ni hitaji muhimu la maendeleo kama alivyowahi kusema hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere; basi uendeshwaji wa uchaguzi(kwa maana ya uchaguzi huru na haki); ndio njia ya kulipata hitaji hili. Uendeshwaji wa uchaguzi huru na haki hutupatia pia hitaji lingine la msingi kwa maendeleo- yaani “Uongozi Bora”.

Wakati suala la mfumo wa uchaguzi limeshawekewa sheria zinazosimamia kwa karibu katika nchi zilizoendelea ambapo demokrasia ya mfumo wa vyama vingi imekuwepo kwa miaka mingi; katika nchi zenye demokrasia changa bado tunaendelea kujiuliza maswali na kuibua masuala kwa lengo kupata mifumo ambayo itakidhi mahitaji yetu.

Shabaha ya makala hii ni kuchochea mjadala ambao utawezesha mapitio ya katiba na sheria zinazotawala siasa Tanzania katika muktadha wa mfumo wa uchaguzi na kuhamasisha marejeo ama mabadiliko yanayostahili. Ni lazima tuhakikishe tunaendelea kuwa na “uchaguzi” badala ya “uchafuzi”.

Mfumo wa uchaguzi unaotumika sasa

Mfumo unatotumika Tanzania ni Mfumo wa Wengi Wape; hata hivyo kuna Viti Maalumu vya Wanawake katika ngazi ya Ubunge na Udiwani ambavyo vinagawanywa kwa misingi ya uwiano. Mfumo wa Wengi Wape (Plurality-Majority) ni mfumo ambao hutumia wilaya/jimbo za/la uchaguzi na mgombea anachaguliwa kuwakilisha wilaya/jimbo husika. Tawi la mfumo huu linaloitwa kwa Kiingereza First-Past-the-Post (FPTP) ndilo lililo maarufu sana na hutumika katika nchi nyingi zilizo katika Jumuiya ya madola. Katika mfumo huu vyama huteua wagombea na kuwadhamini katika majimbo. Mgombea anaeshinda kwa kura nyingi kuliko wenzake hata kama hazifikii nusu ndio huwa amechaguliwa na kunyakua kiti kinachogombewa. Mfumo huu unatumika nchini Uingereza, India, Kenya na Tanzania.Mfumo huu pia hupelekea kuwa na chama kimoja chenye uwezo wa kuunda serikali peke yake bila ya kuhitaji vyama vingine na kuwa na mseto. Mfumo huu husaidia wananchi kuchagua watu na sio vyama vya siasa na hivo mpiga kura anaweza kutathmini utendaji wa mbunge au mwakilishi badala ya utendaji wa chama fulani. Mfumo huu ni rahisi kuutumia na unaeleweka miongoni mwa wananchi, wagombea huwa wachache na hata uhesabuji wa kura unakuwa ni rahisi. Mfumo wa wengi wape hupelekea kuminya nafasi za wanawake kuchaguliwa kuingia bungeni. Kwa tamaduni za nchi za kiafrika kwamba mwanamke hawezi kushindana na mwanaume na pia gharama kubwa za uchaguzi katika majimbo, wanawake wanaochaguliwa kuingia bungeni wanakuwa ni wachache sana. Mfumo huu huua ukuaji wa vyama na hivyo nchi kukosa vyama makini. Hii ni kwa sababu, badala ya vyama kufanya kampeni kwa kutumia sera zao, hutumia majina ya watu ambao ni wagombea wao. Hivyo basi mfumo huu hupelekea vyama kubaki dhaifu na kushindwa kushindana na kutotoa mbadala. Vyama katika mfumo wa wengi wape huwa vigumu sana kuwajibika kwa wananchi kwani badala ya kurekebihsa sera zao vyama hubadili wagombea tu na kuwalaghai wananchi na kushinda tena. Maoni ya wananchi yanakuwa hayaheshimiki na nchi inakosa maendeleo kwa sababu ya demokrasia duni inayosababishwa na mfumo wa wengi wape.
Marekekebisho yanayotaka kufanywa na wanaCCM

Katika mtandao wa www.jamiiforums.com pamezuka mjadala kutokana na marekebisho yanayotarajiwa kusukumwa na wanaCCM kuhusu suala la mfumo wa uchaguzi. Marekebisho hayo yameshadokezwa pia na vyombo kadhaa vya habari. Mmoja wa wachangiaji katika mjadala huo ametoa mchango ambao ni nimeona na vyema nikaukuu kama ulivyo kabla ya kutoa uchambuzi wangu.

Nanukuu: “CCM imebuni kete mpya ya kuizidi CHADEMA na kupunguza nguvu ya upinzani bungeni. Katika mkakati huo mpya ambao umeshapata baraka ya kamati kuu ya chama hicho ukisubiri kupitishwa na NEC hivi karibuni, katiba ya nchi itafanyiwa marekebisho kuweza kutekeleza mkakati huo. Chini ya marekebisho hayo, wabunge wa viti maalum hawatapatikana kwa kuteuliwa na vyama bali watagombea kupitia wilaya ambazo ndizo zitakazo kuwa majimbo ya wanawake pekee. Chini ya mfumo huo mpya, patakuwa na majimbo ya kawaida 232 ambayo yatagombewa na watu wote kwa kama ilivyo utaratibu wa sasa. Kwa upande mwingine viti maalum vya wanawake pekee 75 vitaondolewa na badala yake wanawake watagombea wenyewe kwenye wilaya 130 za Tanzania. Kwa hali hiyo, kutakuwa na ongezeko la wabunge ambalo litalazimisha taifa kupanua tena ukumbi wa bunge na pia bajeti ya matumizi ya wabunge ya mishahara na posho itabidi iongeze kwa zaidi ya bilioni 50. Kwa idadi hiyo ya wabunge, Tanzania itaingia katika kundi la nchi zenye wabunge wengi zaidi.Mkakati huo umebuniwa kupunguza nguvu za kambi ya upinzani hususani CHADEMA ambayo imepata kutokana na kupata wabunge wengi wa viti maalum kutokana na idadi ya kura ambazo chama hicho na vingine vya upinzani vimeokoteza nchi nzima.Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 CHADEMA ilipata wabunge watano tu wa kuchaguliwa lakini ikapata wabunge wa viti maalum sita kutokana na kura ambazo chama hicho kilipata katika uchaguzi. Kama viti maalum vingetolewa kwa idadi ya viti ambavyo chama kimepata chama hicho kingepata kiti maalum kimoja au viwili tu.“Unajua tumeweka sheria inayoisaidia CHADEMA, hawa chini ya Operesheni Sangara hata kama tukitumia nguvu kushinda majimbo bado watapata zaidi ya asilimia 20-40 ya kura katika majimbo mbalimbali hali itayofanya wapate kati ya wabunge 15 mpaka 30 wa viti maalum mwaka 2010. Lazima tutafute njia ya kuwadhibiti mapema kwa kubadili sheria”, alinukuliwa mmoja wa wajumbe wa Kamati kuu ya chama hicho.Timu ya kuandaa mpango huo iliundwa miezi michache iliyopita baada ya kujitokeza fursa ya marekebisho hayo kutokana na Rais Kikwete kutoa ahadi kupitia hotuba yake ya kuongeza uwakilishi wa wanawake bungeni kuwa 50 kwa 50.Timu hiyo ilifanikiwa kushawishi wajumbe wa kamati kuu ya chama hicho kuweka pembeni mapendekezo mengine ya Kamati ya Dr Ghalib Billal ambayo iliundwa baadaye kuchambua kuhusu suala hilo.Kamati hiyo ilikuja na mapendekezo mbalimbali ikiwemo kupanua idadi ya wanawake katika uwakilishi wa uwiano kuwa na orodha yenye uwiano wa majina kijinsia. Aidha pendekezo lingine la kamati hiyo lilitaka uchaguzi uhusishe wagombea wawili mwanamke na mwanaume katika majimbo ya uchaguzi na kupunguza majimbo ya sasa.Mfumo huu mpya unatarajiwa kupata upinzani mkali toka kwa makundi ya kijamii mathalani walemavu na asasi za kiraia.“Unajua mfumo wa sasa wa viti maalum, unatoa fursa ya uwakilishi wa makundi maalum ya wanawake. Kwa mfano, mimi nimechaguliwa kuwakilisha kundi la walemavu. Lakini kwa marekebisho hayo yanayopendekezwa, nitatakiwa nikagombee katika jimbo la uchaguzi. Tunaweza tukapoteza kabisa uwakilishi wa makundi mbalimbali bungeni”, alisema mbunge mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake.Chini ya mfumo mpya hakutakuwa na viti maalum vya makundi kama vijana, walemavu, wawikilishi wa elimu ya juu na mashirika yasiyo ya kiserikali ambavyo vimekuwa vikitengwa na vyama kutokana na uwingi wa viti ambavyo chama kimepata.Makubaliano hayo ya Kamati Kuu yanatarajiwa kuzua mjadala mkali katika kikao cha NEC kutoka kwa wabunge wa majimbo kuhusu hadhi yao katika mfumo mpya.“Inabidi tuelezwe wazi, kati ya wabunge wa wilaya, na wabunge wa majimbo. Ni nani watakuwa na hadhi na mamlaka zaidi chini ya marekebisho hayo”, alisema mbunge machachari wa kanda ya ziwa akitoa maoni yake kuhusu uamuzi wa NEC.Chini ya mapendekezo hayo, mathalani wilaya kama Ilala yenye majimbo mawili ya Ukonga na Ilala itakuwa na wabunge watatu; Mbunge wa Wilaya ya Ilala ambaye atakuwa ni Mwanamke na Wabunge wawili wa majimbo ya Ilala na Ukonga ambao watakuwa ni wa jinsia yoyote.Hata hivyo, ili kupunguza mjadala katika jamii kuhusu mkakati huo, tayari Mkuu wa Mawasiliano amekabidhiwa jukumu la kuundaa umma kukubaliana na marekebisho hayo kupitia propaganda za vyombo vya habari.Kama sehemu ya propaganda hizo imekubaliwa kwamba habari maalum zitolewe na vyombo vya habari kabla zikieleza kwamba marekebisho hayo yanalenga kuundoa migogoro katika vyama vya siasa inayotokana na upendeleo katika uteuzi wa viti maalum kwa kuweka mfumo huu mpya ambao utafanya wanawake washindane wenyewe kwa wenyewe.Habari hizo zitaeleza kwamba CHADEMA ni mfano dhahiri wa migogoro hiyo ya upendeleo wa viti maalum ambayo serikali ya CCM inalenga kuindoa kwa kufanya marekebisho hayo ya katiba ya nchi na sheria za uchaguzi katika upatikanaji wa wabunge wa viti maalum.Changamoto kubwa kwa serikali inatabaki kutumiza ahadi ya kuwa na wabunge kwenye uwiano wa 50 kwa 50 kati ya wanawake na wanaume, ahadi ambayo mfumo huu mpya hauwezi kuitekeleza badala yake mfumo huo umeondoa mfumo wa kuthamini kura ambao umekuwa ukitumika katika nchi mbalimbali” Mwisho wa kunuu.

Mabadiliko yanayostahili kufanywa

Katika mazingira ya majadiliano niliyoyanukuu hapo juu, ni wazi suala hili sasa linahitaji mjadala mkubwa wa umma kwa sababu mabadiliko ya katiba na sheria za nchi si hodi ya chama chochote cha siasa au kikundi cha watu wachache; ni suala la maslahi na matakwa ya umma. Mjadala huo umegusia suala la uteuzi wa viti maalumu katika CHADEMA hoja ambayo nimewahi kuiandikia makala mbili mfululizo kama sehemu ya kuchambua vigezo vilivyotumika; makala hizi zinapatikana kupitia mtandao wa http://mnyika.blogspot.com.

Makala ya leo inalenga zaidi kutoa maoni yangu ya kutokubaliana na marekebisho hayo hapo juu ambayo yameanza kujadiliwa. Kwa maoni yangu mfumo wa Uchaguzi urekebishwe na kuruhusu mfumo mchanyato wa uwiano wa kura na mfumo wa “first-past-the-post” badala ya mifumo hiyo iliyotangulia. Mfumo wetu wa uchaguzi unataka Wabunge na Madiwani kupatikana kutoka katika majimbo na kata tu. Marekebisho yanayopendekezwa yanaturudisha nyuma zaidi. Kwa mfumo wa sasa wabunge wanawake hupatikana kwa uwiano wa kura za Wabunge nchi nzima na Madiwani wa wanawake kutokana na uwiano wa viti vya udiwani ambao kila chama kimepata. Lakini Wabunge Wanawake hawana mamlaka ya kisheria kwa eneo maalumu. Kwa sasa ni rahisi kusema kuwa wanatoka mikoani, lakini hii ni kwa sababu tuna chama kimoja kikubwa na hivyo kupata kura za kuenea mikoa yote. Huko mbele, tena na hawa wagombea binafsi, itatokea mikoa ambayo haitapata wabunge wanawake kwa sababu kura hazitotosha kwa chama kimoja kugawa wabunge kila mkoa. Umefikia wakati sasa kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo wa uchaguzi ili kuingiza uwakilishi wa uwiano. Kama nchi tutafakari mambo yafuatayo yanayohusu mabadiliko ya mfumo wa kisiasa wa nchi yetu: Mosi; Wabunge wa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi watokane na Halmashauri za Wilaya za sasa. Mfano, badala ya Wilaya ya Manispaa ya Kinondoni kuwa na Wabunge watatu, iwe na Mbunge mmoja tu. Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji ndio iwe Jimbo la Uchaguzi. Katika ngazi hii wagombea wasio na vyama waruhusiwe pamoja na wale wenye vyama. Kwa hali ya sasa tutapata Wabunge takribani 130 kutoka kundi hili. Idadi yao itaongezeka kutokana na kuongezeka kwa Halmashauri zitakazoundwa pindi mahitaji yanapotokea. Ikumbukwe kwamba katika ngazi ya chini kitovu cha mamlaka ni halmashauri, ambao ni msingi pia hata katika upangaji wa bajeti taifa.

Haitakuwa tena kazi ya Tume za Uchaguzi kuunda Majimbo ya uchaguzi bali vile vigezo vya kuunda Halmashauri (Baraza la Madiwani) vilivyopo kisheria (Local Government Authorities Acts) ndio vitatumika. Pili; Wabunge kati ya 150 na 200 watokane na kura za uwiano (idadi tofauti inaweza kupendekezwa). Vyama vya siasa vitapata viti kutokana na uwiano wa kura ambao kila chama kimepata katika Mkoa.

Chama cha siasa ni lazima kiwe kimepata kwanza asilimia tano ya kura zote zilizopigwa katika Mkoa husika ili kigawiwe viti. Kwa hiyo kila chama kitatengeneza orodha ya wagombea wake kwa kila Mkoa na kuipeleka Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Orodha hii iwe katika hali ambayo kama jina la kwanza ni Mwanaume la pili awe Mwanamke, hali kadhalika kama jina la kwanza ni Mwanamke katika orodha la pili liwe la mwanaume. Mikoa itapata idadi ya Wabunge kutokana na vigezo maalumu, mfano idadi ya watu n.k. Kwa mapendekezo haya tuna uhakika wa kuwa na Wabunge wanawake zaidi ya theluthi moja katika Bunge. Lakini pia tutakuwa na uhakika kwamba kila Mkoa utakuwa na Mbunge au Wabunge wanawake. Ama kwa lengo la kuongeza idadi kubwa ya wanawake kuelekea uwiano wa hamsini kwa hamsini(50-50), robo tatu ya wabunge wa uwiano inaweza kuwa ni orodha ya wanawake na robo ikabaki kwa ajili ya wanaume. Lengo la kuwa na orodha ni kuwezesha pia vyama kutumia orodha hiyo kuhakikisha uwakilishi wa makundi ya kijamii mathalani walemavu, vijana na viongozi muhimu wa kijamii ambao ni muhimu kuwepo bungeni.

Mabadiliko haya ya mfumo wetu wa Uchaguzi yana faida nyingi sana. Moja ya faida ni kuvigeuza vyama vyetu vya siasa kutoka katika kushindanisha watu tu, bali pia kushindanisha sera. Kwa sababu wananchi watakuwa wanapiga kura mbili. Kura moja ya chama na kura nyingine ya ama diwani au Mbunge na Rais. Kura ya chama ndio itatufanya kupata wabunge wa uwiano. Wala hatutatumia mfumo mmoja kuzalisha mfumo mwingine. Bali kila mfumo utazalisha Wabunge kuunda Bunge letu. Sisi hatutokuwa wa kwanza kufuata mfumo huu wa uwiano-Msumbiji, Afrika ya Kusini, Ujerumani, Uswidi na hata India.

Vyama vikianza kushindanisha sera tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana kama nchi katika kuimarisha mfumo wa demokrasia na kwa kweli hatutokuwa na wasiwasi wa vyama kudhoofika kutokana na wagombea Binafsi kuruhusiwa. Demokrasia ndani ya vyama itaimarika kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi itahakikisha vyama vinapata wawakilishi wake katika Orodha ya Mikoa kidemokrasia. Tubadili mfumo wa uchaguzi tupate viongozi bora!

Wednesday, November 5, 2008

Obama-Tumaini la Mabadiliko ya kweli








Nafurahi ikulu nyeupe imepata Rais mweusi. Ndoto ya Martin Luther King ya kutaka Wamarekani wahukumiane sio kwa rangi bali kwa tabia na uwezo imetimia kwa Obama. Changamoto kwa Rais mteule ni kusimamia mabadiliko aliyoahidi. Pamoja na kuwa Marekani ni Marekani na misingi ya sera zake inajulikana; kupumzishwa kwa Republican na kuingia wa Democrat kunaleta tumaini jipya katika siasa za nchi yao na dunia kwa ujumla. Nawapongeza vijana wa Marekani kwa kuwa mstari wa mbele kufanya kampeni za kisasa zenye hamasa na zilizochangia Barack kushinda. Mwaka 2005 kama ilivyokuwa kwa Obama sasa, CHADEMA tulikuwa na kauli mbiu ya kutaka mabadiliko ya kweli, na wakati huo mimi nikiwa mgombea ubunge jimbo la Ubungo nilisimamia siasa za kizazi kipya kama njia ya kuleta maisha mapya; jambo kubwa ambalo watanzania hususani vijana wanapaswa kujifunza kutoka kampeni za Obama ni kuwa wakala wa mabadiliko wanayotaka kuyaona 2010 na kuendelea. Ni muhimu kwa raia kuunga mkono wagombea na vyama wazi kwa hali na mali kwa siasa safi za sera.



John Mnyika

Kaimu Mkurugenzi wa Mahusiano ya Kimataifa na

Mkurugenzi wa Vijana


Nimesoma hii hotuba ya Obama ya kukubali kuchaguliwa; baadhi ya maudhui niliwahi kuyaandika huko nyuma katika makala hii: http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_15.html


na mengine niliyahubiri sana katika kampeni zangu za uchaguzi mwaka 2005.



"If there is anyone out there who still doubts that America is a place where all things are possible, who still wonders if the dream of our founders is alive in our time, who still questions the power of our democracy, tonight is your answer.It's the answer told by lines that stretched around schools and churches in numbers this nation has never seen, by people who waited three hours and four hours, many for the very first time in their lives, because they believed that this time must be different, that their voice could be that difference. It's the answer spoken by young and old, rich and poor, Democrat and Republican, black, white, Latino, Asian, Native American, gay, straight, disabled and not disabled - Americans who sent a message to the world that we have never been a collection of Red States and Blue States: we are, and always will be, the United States of America.It's the answer that led those who have been told for so long by so many to be cynical, and fearful, and doubtful of what we can achieve to put their hands on the arc of history and bend it once more toward the hope of a better day.It's been a long time coming, but tonight, because of what we did on this day, in this election, at this defining moment, change has come to America.'Unyeilding support'I just received a very gracious call from Senator McCain. He fought long and hard in this campaign, and he’s fought even longer and harder for the country he loves. He has endured sacrifices for America that most of us cannot begin to imagine, and we are better off for the service rendered by this brave and selfless leader. I congratulate him and Governor Palin for all they have achieved, and I look forward to working with them to renew this nation's promise in the months ahead.I want to thank my partner in this journey, a man who campaigned from his heart and spoke for the men and women he grew up with on the streets of Scranton and rode with on that train home to Delaware, the vice president-elect of the United States, Joe Biden. I would not be standing here tonight without the unyielding support of my best friend for the last sixteen years, the rock of our family and the love of my life, our nation’s next First Lady, Michelle Obama. Sasha and Malia, I love you both so much, and you have earned the new puppy that's coming with us to the White House. And while she's no longer with us, I know my grandmother is watching, along with the family that made me who I am. I miss them tonight, and know that my debt to them is beyond measure.To my campaign manager David Plouffe, my chief strategist David Axelrod, and the best campaign team ever assembled in the history of politics - you made this happen, and I am forever grateful for what you’ve sacrificed to get it done.But above all, I will never forget who this victory truly belongs to - it belongs to you.I was never the likeliest candidate for this office. We didn’t start with much money or many endorsements. Our campaign was not hatched in the halls of Washington - it began in the backyards of Des Moines and the living rooms of Concord and the front porches of Charleston. 'Task ahead'It was built by working men and women who dug into what little savings they had to give five dollars and ten dollars and twenty dollars to this cause. It grew strength from the young people who rejected the myth of their generation's apathy, who left their homes and their families for jobs that offered little pay and less sleep, from the not-so-young people who braved the bitter cold and scorching heat to knock on the doors of perfect strangers, from the millions of Americans who volunteered, and organized, and proved that more than two centuries later, a government of the people, by the people and for the people has not perished from this Earth. This is your victory. I know you didn't do this just to win an election and I know you didn't do it for me. You did it because you understand the enormity of the task that lies ahead. For even as we celebrate tonight, we know the challenges that tomorrow will bring are the greatest of our lifetime - two wars, a planet in peril, the worst financial crisis in a century. Even as we stand here tonight, we know there are brave Americans waking up in the deserts of Iraq and the mountains of Afghanistan to risk their lives for us. There are mothers and fathers who will lie awake after their children fall asleep and wonder how they'll make the mortgage, or pay their doctor's bills, or save enough for college. There is new energy to harness and new jobs to be created; new schools to build and threats to meet and alliances to repair.The road ahead will be long. Our climb will be steep. We may not get there in one year or even one term, but America - I have never been more hopeful than I am tonight that we will get there. I promise you - we as a people will get there. There will be setbacks and false starts. There are many who won’t agree with every decision or policy I make as President, and we know that government can’t solve every problem. But I will always be honest with you about the challenges we face. I will listen to you, especially when we disagree.And above all, I will ask you join in the work of remaking this nation the only way it's been done in America for 221 years – block by block, brick by brick, calloused hand by calloused hand. 'Spirit of patriotism'What began twenty-one months ago in the depths of winter must not end on this autumn night. This victory alone is not the change we seek – it is only the chance for us to make that change. And that cannot happen if we go back to the way things were. It cannot happen without you.So let us summon a new spirit of patriotism; of service and responsibility where each of us resolves to pitch in and work harder and look after not only ourselves, but each other. Let us remember that if this financial crisis taught us anything, it’s that we cannot have a thriving Wall Street while Main Street suffers – in this country, we rise or fall as one nation, as one people.Let us resist the temptation to fall back on the same partisanship and pettiness and immaturity that has poisoned our politics for so long. Let us remember that it was a man from this state who first carried the banner of the Republican Party to the White House – a party founded on the values of self-reliance, individual liberty, and national unity.Those are values we all share, and while the Democratic Party has won a great victory tonight, we do so with a measure of humility and determination to heal the divides that have held back our progress. As Lincoln said to a nation far more divided than ours, "We are not enemies, but friends ... though passion may have strained it must not break our bonds of affection." And to those Americans whose support I have yet to earn – I may not have won your vote, but I hear your voices, I need your help, and I will be your President too. And to all those watching tonight from beyond our shores, from parliaments and palaces to those who are huddled around radios in the forgotten corners of our world – our stories are singular, but our destiny is shared, and a new dawn of American leadership is at hand.'Peace and security'To those who would tear this world down – we will defeat you. To those who seek peace and security – we support you. And to all those who have wondered if America’s beacon still burns as bright – tonight we proved once more that the true strength of our nation comes not from our the might of our arms or the scale of our wealth, but from the enduring power of our ideals: democracy, liberty, opportunity, and unyielding hope. For that is the true genius of America – that America can change. Our union can be perfected. And what we have already achieved gives us hope for what we can and must achieve tomorrow. This election had many firsts and many stories that will be told for generations. But one that’s on my mind tonight is about a woman who cast her ballot in Atlanta. She’s a lot like the millions of others who stood in line to make their voice heard in this election except for one thing – Ann Nixon Cooper is 106 years old. She was born just a generation past slavery; a time when there were no cars on the road or planes in the sky; when someone like her couldn’t vote for two reasons – because she was a woman and because of the color of her skin.And tonight, I think about all that she's seen throughout her century in America – the heartache and the hope; the struggle and the progress; the times we were told that we can’t, and the people who pressed on with that American creed: Yes we can. 'Common purpose'At a time when women’s voices were silenced and their hopes dismissed, she lived to see them stand up and speak out and reach for the ballot. Yes we can. When there was despair in the dust bowl and depression across the land, she saw a nation conquer fear itself with a New Deal, new jobs and a new sense of common purpose. Yes we can. When the bombs fell on our harbor and tyranny threatened the world, she was there to witness a generation rise to greatness and a democracy was saved. Yes we can. She was there for the buses in Montgomery, the hoses in Birmingham, a bridge in Selma, and a preacher from Atlanta who told a people that “We Shall Overcome.” Yes we can. 'Fundamental truth'A man touched down on the moon, a wall came down in Berlin, a world was connected by our own science and imagination.And this year, in this election, she touched her finger to a screen, and cast her vote, because after 106 years in America, through the best of times and the darkest of hours, she knows how America can change. Yes we can. America, we have come so far. We have seen so much. But there is so much more to do. So tonight, let us ask ourselves – if our children should live to see the next century; if my daughters should be so lucky to live as long as Ann Nixon Cooper, what change will they see? What progress will we have made? This is our chance to answer that call. This is our moment. This is our time – to put our people back to work and open doors of opportunity for our kids; to restore prosperity and promote the cause of peace, to reclaim the American Dream and reaffirm that fundamental truth – that out of many, we are one, that while we breathe, we hope, and where we are met with cynicism, and doubt, and those who tell us that we can't, we will respond with that timeless creed that sums up the spirit of a people:

Saturday, November 1, 2008

Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika




Rais Kikwete: mene mene na tekel; taifa linagawanyika

Ni saa sita na ushee usiku. Siku mpya imeanza, ni Novemba Mosi; ni siku ya vijana Afrika. Najaribu kutafakari maudhui ya siku hii ya pekee kwa vijana Afrika kama ilivyopitishwa na umoja wa Afrika. Natafakari ujumbe wa mwaka huu “Maadili chanya ya kiafrika, amani na mshikamano”. Tafakari yangu inanirudisha nyuma katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja wa Afrika aliyoitoa usiku wa Oktoba 31 mwaka 2008. Mwangi wa maneno ya Rais wa nchi yangu unarindima katika kichwa changu na kunikosesha usingizi. Si kwa uzito wa maneno bali kwa hofu yangu juu ya madhara ya wepesi wa maneno yenyewe kwa mwelekeo wa taifa.

Nagutuka; nagundua natafakari ubatili, najihisi kama afukuzaye upepo. Haraka nachukua moja ya vitabu vitakatifu, najaribu kutafuta maneno ya kupoza hisia zinazoniandama. Napekua pekua bila kujua nini hasa natafuta kusoma, nakutana na kisa cha Mfalme Nebukadneza. Napata shauku ya kurudia kisa chake nilichokikariri nilipokuwa mtoto, nakutana na maneno ‘mene mene na tekel’. Najikumbusha maana yake; ‘ufalme wake umepimwa na umeonekana haufai’!

Natabasamu kwa uchungu. Ni kama nimeona kidole kikiandika maandishi hayo katika ukuta wa taifa letu. Naukumbuka mjadala ulioibuliwa na Katibu wa Itikadi wa CCM, John Chiligati, ambaye pia ni Waziri katika serikali ya Rais Kikwete wa kubeza na kutweza wenye kuhoji uwezo wa Rais Kikwete. Nakumbuka kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kwamba nchi imekwama Rais Kikwete ameelemewa. Nakumbuka maneno ya Mbowe akitangaza kwamba Rais Kikwete ameshindwa kuliongoza taifa na hivyo kuna haja ya watanzania kutompa kura yeye na chama chake katika uchaguzi wa mwaka 2010. Nakumbuka maneno ya Waziri Mkuu na Jaji mstaafu Joseph Warioba kwamba nchi si shwari. Mene mene na tekel!

Napata nguvu ya kuamka na kuandika; Rais Kikwete amenidhihirishia mimi niliye mdogo, ambaye sistahili hata kufungua kidamu za viatu vyake kwamba anaipeleka nchi harijojo. Katiba ya nchi yetu inatamka kwamba kila mtu anastahili heshima lakini katika medani ya uongozi; heshima ya mtawala inalindwa kwa maneno na matendo yake. Namheshimu Rais Kikwete lakini maneno na matendo yake, yanastahili kukosolewa. Hakika hotuba ya Rais wetu imenidhihirishia pia kuwa hata wale washauri na wasaidizi wake waliopo pale Ikulu na serikalini wanapaswa kutuambia watanzania kwanini kodi zetu zitumike kuendelea kuwalipa mishahara kama wanashindwa kutimiza wajibu wa kulinda heshima ya taasisi ya Urais. Nakabiliwa na mtanziko bado, kati ya kuandika vile ninavyoamini na kuonekana kwamba sinaheshima kwa Amiri Jeshi mkuu. Ama kusema ukweli, nikiamini kwamba Rais aliye kioo cha taifa letu atachukua hatua za haraka kujirekebisha na kurekebisha hali ya mambo inavyokwenda katika taifa letu. Rais Kikwete aliwahi kusema kwamba alikuwa mwanafunzi mzuri wa Mwalimu Nyerere; hivyo naamini amesoma waraka wake wa ‘tujisahihishe’. Kutenda kosa si kosa, kosa kurudia kosa.

Kadiri hotuba ya Rais ilivyokuwa ikicheleweshwa ndipo matumaini yalipozidi kwamba pengine kulikuwa na mambo mazito ambayo mkuu wa nchi alikuwa akiyaandaa. Shauku ya kukosa hotuba za Rais kwa mwezi wa Septemba tofauti ya utaratibu ambao Rais amejiwekea ikazimwa kwa hotuba ambayo kimaudhui inafafana na hotuba ambayo tayari Rais alishaitoa Bungeni mwezi Agosti na kauli zake zilizofuatia katika ziara zake. Nikajiuliza; yamfaa nini mwanadamu kusema kama hana cha kusema?.

Rais wangu alionekana kuelemewa na mambo moyoni, haiba yake imegubikwa na uchovu pengine kutokana na ziara nyingi ama ni msongo wa mawazo au ni tatizo la macho yangu la kuona yasiyopaswa kuonekana. Rais alikuwa akihutubia kwa kutazama huko na kule kama vile palikuwa na nguvu za giza pembeni zikimzinga asitoe mwanga kwa taifa letu analoliongoza. Wanasaikolojia wanajua, jinsi ujumbe unavyotolewa unaweza kusema mengi kuliko hata ujumbe wenyewe.

Rais akaanza kwa kugusa suala tete la Tanzania kujiunga na OIC. Moja kwa moja akawaasa watanzania wasiuendeleze mjadala huo. Mjadala ambao umeendelezwa na serikali yake yenyewe, mjadala ambao yeye mwenyewe katika hotuba yake ameweka bayana kwamba serikali inauendeleza. Nikashangaa! Lakini nikashangaa zaidi kwa Rais Kikwete kutofautina wazi wazi na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Benard Membe ambaye Rais Kikwete amemuita kuwa ndio ana dhamana ya suala hilo. Wakati Rais anasema kwamba utafiti wa suala hilo bado haujakamilishwa na Waziri Membe, waziri mwenyewe wakati anahutubia bunge Agosti 22 mwaka huu huu alitangaza kwamba wizara yake imeshakamilisha utafiti. Nani mkweli kati yao Mungu ndio ajuaye. Lakini Mwalimu Nyerere, katika kitabu cha Uongozi wetu na hatma ya Tanzania, alizungumza vizuri kuhusu serikali. Mwalimu aliweka wazi, mkusanyiko wa mawaziri wasiokuwa na dira ya pamoja na uwajibikaji wa pamoja, wanabaki kuwa serikali kwa mujibu wa sheria tu. Lakini kimaadili na kimantiki; hakuna serikali! Rais anataka kila mtu akae kimya aiachie Wizara imalize kazi yake, kama vile wizara ni chombo kisikokuwepo Tanzania kisichowajibika kufanya kazi kwa kuzingatia hisia na matakwa ya watanzania. Kwa mtindo huu wa funika kombe, Rais Kikwete anazidi kuligawa taifa chini kwa chini; ni kama kujaribu kufunika moshi na kujifariji kuwa hakuna moto.

Liliamshwa la mpasuko Zanzibar; likajadiliwa, likakwamishwa. Liliibuliwa na mahakama ya kadhi; likakolezwa, likafunikwa. Likaibuliwa la mafisadi; likavumishwa, likatulizwa. Limeibuka la OIC; likachochewa, limefutikwa. Uongozi wa kuahirisha matatizo badala ya kuyatatua! Haya na mengine ni mabomu ya wakati.

Zoezi la kutumia visingizio kuahirisha matatizo likaendelea katika suala la walimu pia. Nilitaraji walau kwa mara hii Rais awaombe radhi walimu kwa ahadi yake aliyoitoa awali ambayo haikutimizwa katika tarehe ambayo aliitaja mwenyewe. Kwa kuwa sakata hili liko mahakamani; niishie hapa, nivute subira. Walimu waendelee tu kusota kwa sababu ya udhaifu wa serikali wa kutoweka kumbukumbu vizuri za waliofariki na zile za kutambua stahiki za kila Mwalimu. Serikali isiyoweza kuwatambua wafanyakazi wake inaweza kweli kuwakumbuka wananchi wa kawaida?

Ndipo Rais alipohamia kwenye changamoto ya hali ya uchumi ya dunia na hasa wa mfumo wa fedha unaozikabili nchi zilizoendelea. Kilichonishangaza ni Rais kutumia muda mrefu kuhutubia yale yale ambayo aliyasema kwa taifa Katika hotuba yake ya Tanga wakati wa sherehe za kuzima Mwenge na maadhimisho ya miaka tisa ya kifo cha, hayati Mwalimu Julius Nyerere. Halafu Rais katika kutafuta suluhisho la suala hilo, hoja kuu aliyoitoa ni kukaribisha wazo la Rais George Bush wa Marekani la kuitisha mkutano maalum wa kimataifa wa kuzungumzia tatizo la kifedha la kimataifa!. Utegemezi wa mawazo toka Washington ndio unaotufanya tusahau kulinda mihimili ya kiuchumi ambayo awamu zilizopita za utawala wa nchi yetu zilijaribu kuiweka. Kubwa zaidi, nilitarajia Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika kuwaeleza watanzania ni jinsi gani anakusudia kuziunganisha nchi zingine za Afrika kuhakisha nafasi ya Afrika inahakikishwa. Badala yake Rais Kikwete ameishia kulalamika tu kwamba “kwa bahati mbaya afrika imesahaulika katika mkutano huo”. Rais Kikwete walau angetumia nafasi hiyo kueleza mikakati ya bara la Afrika hususani ile ya kuunganisha jumuia mbalimbali za kiuchumi iliyojadiliwa nchini Uganda ambapo yeye alishiriki kama sehemu ya ujenzi wa nguvu ya kiuchumi ya bara letu. Uthabiti na ueledi kama huo ungekuwa ni zawadi nzuri kwa vijana wa Tanzania wakati wanaungana na wenzao kuadhimisha siku ya vijana Afrika.

Kama ilivyotarajiwa na wengi Rais Kikwete akagusia suala la mauji ya Maalbino, ikiwa ni siku chache toka alizungumze suala hilo kwa kina Oktoba 19, 2008. Mara hii Rais akiwataka wananchi watoe kwa siri taarifa za watu wanaojihusisha na vitendo hivyo. Binafsi nilitarajia badala ya kutaka orodha mpya, Rais Kikwete kama alitaka kuzungumzia tena suala hili, angeueleza umma wa watanzania orodha za mwanzo za watuhumiwa wa mauaji ya maalbino ambazo ziliwasilishwa kwa vyombo vya dola ikiwemo kwa kufuatilia mtandao ulioanikwa na mwandishi wa habari wa BBC, Vicky Ntetema. Lakini haya mambo ya Rais Kikwete kutaka orodha za siri hayakuanza leo, aliwahi kutaka orodha ya watuhumiwa wa biashara ya madawa ya kulevya, akapatiwa; kimyaaa. Zikafuata orodha nyingine mbalimbali; hakuna hatua zinazoeleweka. Ndipo ikafuata ile orodha ambayo kwa ushujaa wa Dr Wilbroad Slaa(Mb) na viongozi wenzake wa upinzani waliamua kuitoa orodha hiyo hadharani kabisa pale Uwanja wa Temeke Mwembe Yanga. Orodha ya Mafisadi(list of shame) ikawekwa hadharani; hasara ya ufisadi uliotajwa inasababisha vifo vya watanzania wengi zaidi kila siku mpaka leo.

Kama kila siku wakina mama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma bora za kujifungua. Kama kila siku watanzania masikini wanakufa kwa kushindwa kuweza kununua dawa za kutibu malaria. Kama helikopta mbovu zinanunuliwa na kuua. Kama watoto wanakufa kwenye kumbi za disco kwa kukoseshwa hewa. Basi mafisadi ni sawa wauaji! Taifa linazidi kugawanyika, kati ya tabaka lenye kufa taratibu kwa kunyonywa kwa ufisadi na tabaka lililojifungia kwenye pepo ya akaunti za vijisenti mpaka nje ya nchi.

Rais Kikwete akaendelea kuikwepa Orodha ya Mafisadi kwa ukamilifu wake, akaendelea kuzungumzia suala la EPA tu. Akaendelea kukwepa kusema chochote kuhusu Meremeta, Tangold, Deep Green na ufisadi mwingine ambao kwa ujumla wake ni mara kumi ya bilioni 133 za EPA.

Lakini hata kwenye EPA kwenyewe, Rais Kikwete katika hotuba yake ameendelea kukwepa kuchukua uamuzi; amepalilia mche wa mbegu ya ubaguzi katika utawala wa sheria ambayo aliipanda Agosti 21 mwaka 2008 kupitia hotuba yake bungeni.

Rais Kikwete ameendelea kuliganya taifa kwa kuwalinda mafisadi na kugeuza suala lao kuwa la madai badala ya jinai.

Katika hotuba yake Rais Kikwete anatoa pongezi kwa Kamati ya Mwanasheria Mkuu “kwa kazi nzuri iliyofanya ambayo mbali na kubaini namna ya tuhuma za uhalifu zilivyofanywa, pia ilibaini wahusika na kuwabana kiasi cha kufanikiwa kurejeshwa kwa fedha ambazo vinginevyo zingepotea kabisa. “

Kama Rais Kikwete mwenyewe anakiri kwa maneno yake mwenyewe kwamba kamati yake imebaini uhalifu na wahalifu sasa ni vipi Rais huyu huyu anawapa msamaha wahalifu kabla ya kufikishwa mahakamani? Anawapa msamaha huu kwa sheria ya nchi gani? Maana Katiba ya nchi na sheria ambazo Rais ameapa kuvilinda vinampa mamlaka chini ya utaratibu maalum wa kusamehe watu kwa sababu Fulani Fulani baada ya kushtakiwa na kuhukumiwa(clemance/parole). Hakika Rais Kikwete amekiuka katiba kwa kuendesha nchi kwa ubaguzi na kuvunja sheria za nchi kwa kulinda wahalifu. Kwa mantiki hii, na vijana wezi nao wakirudisha mali za wizi nao waachiwe huru tu ili tujenge taifa la misamaha ili wajumuike na hao mafisadi walioghushi nyaraka na kuhujumu uchumi wa taifa. Milango ya magereza na ifunguliwe ili majambazi waachiwe huru, na milango ya mahakama ifungwe ili wezi wasishitakiwe tena; ili tujenge taifa lisilo na utawala wa sheria, linaoendeshwa kwa kanuni za mwituni. Mene mene na tekel!

Namsikiliza Rais wangu kwa mara nyingine akitaja kiwango cha fedha kilichorudishwa bila kuwa na hakika. Kwa mara nyingine akitoa maagizo ya kufungua mashtaka kwa watu ambao hawajarudisha fedha; maagizo ambayo aliyayatoa siku nyingi. Kwa yale makampuni mengine tisa yaliyofisadi bilioni 40 Rais ndio kwanza ‘anakusudia’ kuwataka polisi waendelee na uchunguzi. Na kati ya hayo ipo ile kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota takribani bilioni 30 ambazo nyingine zimeelezwa na vyanzo mbalimbali kuwa zilitumika kwenye kampeni za uchaguzi zilizomweka yeye na chama chake cha CCM madarakani. Rais Kikwete amekosa uthubutu na uthabiti wa kuwataja hadharani maswahiba wake na kuwachukulia hatua. Mene mene na tekel.
Rais Kikwete amemalizia hotuba yake kwa kutusihi watanzania tujiepushe na mambo yanayoweza kutugawa na kupandikiza mbegu za chuki miongoni mwetu na badala yake tuimarishe maelewano, mshikamano na umoja wa kitaifa. Misingi ambayo yeye mwenyewe ameibomoa kwa maneno na matendo yake. Ukiona wananchi wanazomea viongozi, wanarusha mawe, wanalala barabarani ujue migawanyiko imeshapandikiza mbegu ya chuki na kukata tamaa. Vitabu vitakatifu vinaeleza kwamba amani ni tunda la haki. Maelewano tunayopaswa kuyaimarisha ni yale ya kutambua asili na matitizo yanayolikabili taifa letu na kuelewana suluhu tunayohitaji. Mshikamano tunapaswa kuuimarisha ni wa kuunganisha nguvu ya umma katika kuleta mabadiliko tunayoyahitaji. Umoja wa kuimarisha ni unaojengwa kwa misingi ya uadilifu na fikra mbadala zenye kupinga aina zote za ufisadi na kutetea rasilimali za taifa.

Daima tukumbuke; mabadiliko ya kweli katika taifa letu hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale, wa chama kile kile, chenye uoza ule ule, wakiendeleza yale yale kwa ari, nguvu na kasi mpya. Kwa falsafa ya chukua chako mapema(ccm), Tanzania yenye neema haiwezekani. Ni wakati wa kusimama na kujitambulisha; ama upande wa kuliunganisha taifa ama kuligawa, historia itakuhumu kwa kadiri ya maamuzi yako ya leo. Mene mene na tekel. Tuombe ulinzi wa Mungu tuvuke salama!

John Mnyika
Novemba Mosi, 2008-Mwanza, Tanzania