Friday, June 17, 2011

Mabadiliko ya Mbunge kuhusu Mpango wa Miaka Mitano

YAH: KUWASILISHA MABADILIKO KATIKA HOJA YA SERIKALI KUHUSU MPANGO WA MAENDELEO WA MIAKA MITANO (2011/2012 – 2015/2016) ULIOWASILISHWA KWA HATI YA MEZANI TAREHE 13 JUNI, 2011 KATIKA KIKAO CHA NNE CHA MKUTANO WA NNE WA BUNGE.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge kifungu 57 (1) – (a), (b), (c) na 58 (1), napendekeza mabadiliko katika Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano kama ifuatavyo;
Katika Kiambatanishi namba 1

Page 117: Water and Sanitation (A.1.1.4)

In the row of “Rehabilitate and expand water supply scheme of Upper Ruvu for Dar es Salaam”

1. Insert 62,500 in the fiscal year 2012/13 and 43,000 in the fiscal year 2013/2014.

2. Insert 16,000 in the fiscal year 2014/2015 and 3,700 in the fiscal year 2015/2016.

Jumla ya fedha za bajeti ya mpango haijabadilishwa, bali kinachopendekezwa ni kupunguza fedha zilizotengwa kwenye miaka ya mbele ya mpango, yaani 2015/2016 na kuzijazia kwenye miaka ya mwanzoni ya 2012/13 na 2013/2014 ili utekelezaji wa miradi ufanyike mapema kwa kuzingatia pia ahadi alizotoa Rais na Waziri wa Maji za kukamilisha miradi ifikapo mwaka 2013.

In the row of “Rehabilitate and expand water supply scheme of Lower Ruvu for Dar es Salaam”

1. Insert 62,000 in the fiscal year 2012/2013 and 43,800 in the fiscal year 2013/2014.

2. Insert 8,800 in the fiscal year 2014/2015 and 1,300 in the fiscal year 2015/2016.

Jumla ya fedha za bajeti ya mpango haijabadilishwa, bali kinachopendekezwa ni kupunguza fedha zilizotengwa kwenye miaka ya mbele ya mpango, yaani 2015/2016 na kuzijazia kwenye miaka ya mwanzoni ya 2012/13 na 2013/2014 ili utekelezaji wa miradi ufanyike mapema kwa kuzingatia pia ahadi alizotoa Rais na Waziri wa Maji za kukamilisha miradi ifikapo mwaka 2013.

In the row of “Drill 20 high yielding boreholes at Kimbiji and Mpera in Kigamboni and Mkuranga areas”

1. Insert 49,200 in the fiscal year 2012/2013 and 30,000 in the fiscal year 2013/2014.

2. Insert 6,800 in the fiscal year 2014/2015 and 3,600 in the fiscal year 2015/2016.

Jumla ya fedha za bajeti ya mpango haijabadilishwa, bali kinachopendekezwa ni kupunguza fedha zilizotengwa kwenye miaka ya mbele ya mpango, yaani 2015/2016 na kuzijazia kwenye miaka ya mwanzoni ya 2012/13 na 2013/2014 ili utekelezaji wa miradi ufanyike mapema kwa kuzingatia pia ahadi alizotoa Rais na Waziri wa Maji za kukamilisha miradi ifikapo mwaka 2013.


Page 127: Roads Schedule:( A.1.2.1)

In the sub –part of De-congestion of DSM

1. Insert “Kimara –Mavurunza –Bonyokwa - Segerea” in the list of roads
Barabara hii iliahidiwa na Rais tarehe 24 Mei 2010 kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami kama sehemu ya kupunguza foleni katika jiji la Dar salaam.

Page 135: Energy(A.1.3)

In the row of “Increase electricity generation to 2,780 MW by 2015, insert “Stiggler’s Gorge” in the list of activity.

Tayari serikali ilitangaza kwamba mradi huu utapewa kipaumbele maalum cha utekelezaji kuanza katika kipindi cha miaka mitano ya sasa kwa ahadi ya Rais Kikwete Bungeni na pia serikali ilitangaza kuunda kamati ya kuanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi husika.

Page 112: In the row of “Benjamin William Mkapa Special” (1.1.2)

1. Remove “Construction of Sewerage line from BWM-SEZ to Mabibo oxidation ponds”, and then insert “Construction of sewerage line from BWM –SEZ to the nearby “major industrial wastes disposal system”.

Mabwawa ya Mabibo ni madogo na yako katika hali mbaya na hivyo kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira. Mabwawa haya yakiongezewa uchafu wa viwandani toka BWM-SEZ eneo la Mabibo litakuwa na mazingira hatari kwa binadamu. Tayari hivi sasa kuna uchafuzi mkubwa wa maji taka ya toka Hosteli za Chuo Kikuu za Mabibo kumwagwa katika Mto eneo la Ubungo Kisiwani kutokana na kushindwa kusukumwa kuelekea katika mabwawa ya mabibo.

Hivyo, kuna haja ya mfumo wa BWM-SEZ unaokusudiwa kujengwa uunganishwe kwenye mfumo wa maji taka unaohudumia maeneo ya viwanda.

Page 146: In the row of Higher Education(A.1.5)

In the list of Activity

1. Remove “to facilitate construction of 2 higher learning institutions” and then insert “to facilitate construction of 3 higher learning institutions”.

Page 147: In the list of Location

1. Insert “Chuo Kikuu cha Kilimo Butiama”

Pamoja na kuwa kwenye hotuba ya Waziri ya kuwasilisha mpango ametaja Chuo Kikuu cha Kilimo Butiama katika Ukurasa wa 16 hata hivyo Chuo hicho hakijaingizwa katika mpango miaka mitano. Pamoja na kuingiza chuo hicho; serikali iangalie uwezekano wa kuongeza vyuo vikuu zaidi mathalani Chuo Kikuu cha Mafuta Mtwara na kukigeuza Chuo Cha Madini kuwa Chuo Kikuu.
Naomba kuwasilisha;


John John Mnyika
Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA)
13 Juni 2011

No comments: