Uwekaji wa jiwe la msingi kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Mbezi mwisho-Goba-Tangi Bovu
Monday, January 26, 2015
Jitihada za kibunge na nje ya bunge katika kupambana na kero ya maji jimboni Ubungo (na Jiji la Dar es Salaam kwa ujumla)
Kwa muda mrefu Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika amekuwa akifanya jitihada za kibunge na hata nje ya bunge kuhakikisha utatuzi wa kero ya maji unapatikana.
Jitihada za kibunge na changamoto zake:
Akiwasilisha kwa wananchi:
Jitihada za kibunge na changamoto zake:
Akiwasilisha kwa wananchi:
Bado msimamo na udhabiti wa kutetea wananchi katika kuhakikisha kero ya maji inatatuliwa ndani ya jimbo la Ubungo inaendelea.
Maslahi ya Umma Kwanza!
MUHIMU: Je umesoma Katiba Pendekezwa? Soma sasa hapa
Kwa nakala hii inatoa fursa kujua mapendekezo yetu wananchi tuliyoyatoa mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Warioba je yamezingatiwa au lah.
Mshirikishe mwananchi mwenzako mwingine!
Mshirikishe mwananchi mwenzako mwingine!
Friday, October 31, 2014
WAZIRI MUHONGO, WAZIRI MKUU PINDA NA SPIKA MAKINDA WAJITOKEZE KUTOA MAELEZO JUU YA HATUA WALIZOCHUKUA KUHUSU UFISADI NA UDHAIFU KATIKA WIZARA YA NISHATI NA MADINI; WASIPOFANYA HIVYO NITAUREJESHA MJADALA BUNGENI NOVEMBA 2014
Itakumbukwa kwamba tarehe 29 Aprili 2014 kupitia Hotuba ya Msemaji wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Nishati na Madini (nimeambatisha
nakala) juu ya mapitio ya utekelezaji wa
Bajeti ya mwaka wa fedha 2013/2014 na makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara
tajwa kwa mwaka 2014/2015 nilieleza ufisadi na udhaifu uliopo katika Wizara
hiyo na mashirika yaliyo chini yake.
Kutokana na kukithiri kwa ufisadi na udhaifu huo nilipendekeza hatua
zifuatazo ziweze kuchukuliwa katika Mkutano wa 15 wa Bunge uliokuwa ukiendelea
wakati huo, nanukuu:
“Mosi, Spika aruhusu kabla ya mjadala
huu kuendelea ziwekwe mezani nakala ya ripoti zote za kamati za uchunguzi
kwenye Sekta ya Nishati na Madini zilizoundwa na matokeo yake kutowasilishwa
bungeni mpaka sasa.
Thursday, October 23, 2014
Pata hapa nakala ya muswada wa Baraza la Vijana la Taifa; boresha tupate baraza bora
Katika Mkutano wa 14 wa Bunge tarehe
21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza
la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 niliouwasilisha tarehe 31 Oktoba 2013.
Narudia tena kuwashukuru vijana
na wadau tulioshirikiana kuandaa muswada huo na naomba kuendelea kupata
ushirikiano wenu wa karibu katika hatua zinazoendelea.
Kuanzia tarehe 21 Oktoba 2014
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii imeanza vikao vya kupokea maoni
ya wadau kuhusu muswada huo. Nakala tete ya muswada huo inapatikana hapa,
tafadhali pakua pitia na wasilisha maoni yako sasa.
Unaweza kuandika maoni yako
kwenye mtandao wa http://mnyika.blogspot.com
au kutuma kwa barua pepe kwenda mbungeubungo@gmail.com
na nakala kwa Kamati husika ya Bunge kupitia tanzparl@parliament.go.tz.
Ikiwa unataka kutumia njia
nyingine kuwasilisha maoni yako tafadhali wasiliana na Gaston Garubimbi 0715/0767-825025
kwa maelezo zaidi. Mdau wa masuala ya vijana zingatia kwamba zaidi ya miaka 18 ahadi za kukamilisha
mchakato wa kuanzishwa kwa baraza la
Vijana la Taifa zimekuwa zikitolewa bila utekelezaji kamili na wa haraka.
Wednesday, October 8, 2014
Maharamia wamepitisha Katiba haramu: wameanzisha mgogoro chanya na mwanya wa mabadiliko
Dira ni kuwa na katiba bora itakayojenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo endelevu kwa watu wake wote. Lakini uharamia katika mchakato wa katiba mpya umelipasua taifa. Mpasuko huu unaweza kuwa mgogoro hasi wenye madhara kwa wananchi au mgogoro chanya utakaoleta mabadiliko nchini.
Maharamia wanashangilia kilevi katika Bunge Maalum baada ya kukamilisha uharamia dhidi ya rasimu ya katiba ya wananchi kwa kupata theluthi mbili kwa njia kiharamia. Katiba iliyopendekezwa kiharamia ni katiba haramu.
Katiba haramu, katiba ya maharamia, katiba ya mafisadi, katiba ya CCM wahafidhiana na mawakala wake inapaswa kupingwa mtaani na mahakamani kwa mbinu mbalimbali.
Iwe ni kwa mikutano, migomo, maandamano, mashtaka au katika sanduku la kura. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba mchakato huu wa mabadiliko ya katiba ni mwanya wa mabadiliko katika taifa letu.
Saturday, September 27, 2014
TAARIFA KWA UMMA
Katika Mkutano wa 14
Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge
wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John
Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo
kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa
wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na
utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye
kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo
hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka
Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya
maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa
wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa
tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa
kwenye kamati zinazohusika; Nne, ni upi
wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Katika Mkutano wa 14
Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge
wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John
Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo
kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa
wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na
utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye
kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo
hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka
Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya
maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa
wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa
tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa
kwenye kamati zinazohusika; Nne, ni upi
wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Ofisi ya Jimbo la Ubungo
inawakumbusha vijana na wadau wote wa maendeleo yao kwamba kutokuwepo kwa
chombo kinachowaunganisha vijana wote bila kujadili itikadi kufuatilia masuala
ya maendeleo ya vijana kunafanya Wizara
mbalimbali za kisekta kutokuzingatia masuala yaliyokipaumbele kwa maendeleo ya
vijana.
Mathalani, katika
Mkutano huu wa Bunge katika Fungu la 65 la Wizara ya Kazi na Ajira Kitabu cha
Nne Cha Miradi ya Maendeleo Kifungu cha 2002, pamoja na wabunge na vijana
kupewa matumaini kwamba zimepitishwa bilioni tatu kwa ajili ya mikopo na mitaji
kwa vijana ukweli ni kwamba fedha hizo zimepangiwa matumizi ambayo kusipokuwa
na chombo cha kuyafuatilia kutakuwa na udhaifu, ufisadi na ubadhirifu kama
ilivyojitokeza katika fedha za mifuko ya maendeleo ya vijana kati ya mwaka 1993/1994 mpaka 2013/2014.
Kwa mujibu wa Kasma za
Kifungu hicho cha 2002 cha Bajeti iliyopitishwa ya Fungu 65 Wizara ya Kazi na
Ajira, fedha hizo zinazopaswa kuwa za mikopo na mitaji kwa vijana zitatumika
milioni 700 kwa ajili ya kulipia utaalamu elekezi (consultancy fees) kwa ajili
ya kutoa mafunzo kwa vijana 200 tu; milioni 150 zitatumika kununulia magari
Wizarani, milioni 60 zitatumika kwenye matangazo na orodha ndefu nyingine
ya matumizi yasiyo ya lazima ambayo
kutokana na ufinyu wa muda sitaendelea kuyataja.
Aidha, katika mjadala
wa bajeti hiyo wabunge waliweka bayana kwamba kiwango kinachotengwa katika
Mifuko ya Maendeleo ya Vijana iwe ni kwa Serikali Kuu na hata Halmashauri ni
kidogo ukilinganisha na uwezo wa nchi, mahitaji ya vijana na mafungu mengine yasiyo
na matumizi muhimu yanavyotengewa fedha nyingi katika baadhi ya Wizara.
Hivyo, ili Baraza la
Vijana la Taifa na Benki ya Vijana ambavyo ni vyombo muhimu kwa maendeleo ya
vijana viweze kuanzishwa kwa wakati, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inamkumbusha
Spika wa Bunge kuelekeza muswada binafsi uliokwisha wasilishwa kwa Bunge kwa
kamati zinazohusika kwa ajili ya kuanza
kuujadili. Suala hili ni muhimu likapata majibu ya mapema ili muswada
huo uweze kuwasilishwa Bungeni katika Mkutano wa 16 wa Bunge unaotarajiwa
kufanyika mwezi Novemba mwaka 2014.
Ofisi ya Mbunge Jimbo
la Ubungo inatoa mwito pia kwa vijana na wadau wa maendeleo ya vijana kuingilia
kati suala hili na kuisimamia Serikali kwa kuzingatia kwamba katika majumuisho
ya Bajeti ya Wizara yenye dhamana ya vijana kwa mwaka 2013/2014 tarehe 21 Mei
2013 mkutano wa 11 kikao cha 30; Serikali ilitumia kisingizio kwamba ‘ni bunge
la bajeti’ kukwepa kuwasilishwa kwa muswda Bunge. Hata hivyo, ahadi ya Serikali
ya kuwasilisha muswada haikutekelezwa kwenye mikutano mitatu uliyofuatia ya 12,
13, 14 na 15; hivyo mkutano huu wa 16 ni muafaka kuwezesha maamuzi kufanyika
kwa ajili ya maendeleo ya vijana nchini.
Ofisi ya Mbunge Jimbo
la Ubungo inaukumbusha umma kwamba Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya
mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa
Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007;
hata hivyo Serikali imekuwa ikiwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera
tajwa yanatekelezwa pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo
ya vijana nchini.
Imetolewa tarehe 24
Septemba 2014 na:
Aziz Himbuka
Katibu wa Mbunge
Jimbo la Ubungo
Monday, September 8, 2014
Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) yakabidhiwa Komputa na Kasiki (safe) na Mbunge Mnyika
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika akikabidhi kompyuta
na Kasiki (Safe) kwa Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) ikiwa ni sehemu ya
milioni 10 za CDCF tulizotenga kwenye kuchochea vijana na wanawake kujiajiri.
Uzinduzi wa rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake,vijana na wenye ulemavu
John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo Akizindua rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake, vijana na wenye ulemavu katika uongozi uliofanywa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)
Monday, September 1, 2014
Mnyika akabidhi vyerahani kutimiza ahadi ya ajira kwa wanawake
Mnyika
akibidhi vyerehani na mashine kudarizi kwa VICOBA viwili vya wanawake Kimara na
Matete ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya kutoa vifaa vya kuwawezesha
kujiajiri vyenye thamani ya jumla ya milioni 10 kwa vikundi mbalimbali jimboni
kutoka katika CDCF;
Rais Kikwete, Waziri wa Maji Prof Maghembe na Bodi mpya ya DAWASCO
Tarehe 13 Agosti 2014 Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe alizindua Bodi mpya ya Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASCO) na kutoa kauli mbalimbali mbele ya vyombo vya habari ambazo zinaendeleza udhaifu ule ule badala ya kuchukua hatua za haraka kunusuru wananchi katika shida kubwa ya upatikanaji wa maji.
Ni suala lililo wazi kwamba kuzindua bodi mpya ya DAWASCO pekee haitoshi, kwa kuzingatia kuwa majukumu makuu ya kuwezesha hatua za haraka yapo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASA) ambayo nayo inahitaji bodi mpya.
Natoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kuvunja bodi iliyopo ya DAWASA na kuunda bodi mpya. Aidha, namkumbusha Rais Kikwete kuitisha kikao ikulu pamoja na DAWASCO, DAWASA na Wizara ya Maji kama alivyoahidi mbele ya wananchi mwezi Machi mwaka 2013.
Thursday, July 31, 2014
Kuhusu uongozi mpya wa wilaya ya CHADEMA Ubungo
Katibu wa CHADEMA Wilaya ya
Ubungo, Goodluck Justine (wa kanza kushoto) akiongea na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam
|
UONGOZI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya kichama Ubungo unatarajiwa kujulikana Agosti 3, 2014 baada ya uchaguzi wa ngazi za chini katika wilaya hiyo kukamilika.
Mbali na viongozi wa wilaya hiyo kujulikana siku hiyo, pia chama hicho kimeeleza kuwa, kimejiandaa vema kuwadhibiti mamluki wasijipenyeze katika uongozi huo.
Hayo yalibainishwa na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine, wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi wa ngazi za msingi, matawi na kata.
Nafasi zitakazowaniwa ni ya mwenyekiti, katibu, katibu mwenezi na mhazini na kwamba, kwa ngazi ya mabaraza ni vijana, wazee na wanawake.
Monday, July 28, 2014
Mnyika ataka matengenezo ya barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni yaharakishwe
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika amemtumia mjumbe Meya wa Manispaa ya Kinondoni kutaka afuatilie kwa karibu matengenezo ya Barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni (Barabara ya Mlandizi) kuharakishwa.
Mbunge amechukua hatua hiyo baada ya kupita katika barabara hiyo kuanzia maeneo ya Sinza Kijiweni-Mtogole hadi Makanya na kubaini kwamba bado ukarabati haujaanza na hali ya barabara ni mbaya.
Mnyika amewasiliana pia na Mkurugenzi wa Halmashauri kutaka Ofisi yake itoe taarifa kupitia vyombo vya habari tarehe ngapi matengenezo hayo yataanza na lini yanatarajiwa kumalizika.
Mnyika amekumbusha kwamba pamoja na kero ambazo wananchi wanapata hivi sasa Serikali inapaswa kutambua kwamba barabara hiyo ni muhimu katika kupunguza msongamano kwenye Barabara ya Morogoro na inapaswa kupewa kipaumbele wakati huu ambapo ujenzi wa mradi wa mabasi ya haraka (DART) unaendelea na hivyo kuhitajika kwa barabara mbadala.
Sunday, July 20, 2014
Mnyika amnusuru Waziri Makala
16 Julai, 2014 Na Abdallah Khamis
MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemnusuru Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala asiendelee kuzomewa na wananchi wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa miundombinu ya maji jimboni humo.
Mapema wanachama wa CCM wakiwa na bendera zao, walionekana kupangwa ili kumzomea Mnyika ambaye hata hivyo hakuwajali, badala yake aliendelea kuhutubia mkutano huku Makala akionekana kufurahishwa na hali hiyo.
Mnyika alieleza jinsi alivyowapigania wakazi wa Kimara Mavurunza na maeneo mbalimbali ya jiji kupata maji pasipo kujali itikadi zao za vyama.
Alisema ziara hiyo ya naibu waziri ni matokeo yake ya kumbana Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, pamoja na watendaji wa Kampuni ya kusambaza maji ya Dawasa kuhakikisha maji yanapatikana kwa wakazi wa Dar es Salaam.
CCM,Chadema wafanya vurugu ziara ya Makalla, Mnyika
Na Mary Geofrey 16th July 2014
Email
Print
Ujumbe ulioongozana na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ukiwa ndani ya tenki la maji lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi jana.
Mbali na kukagua miradi ya maji, Makalla na Mnyika alitumia ziara hiyo pamoja na kuzungumza na wananchi juu ya mipango na mikakati ya serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa maji jimboni humo.
Vurugu hizo zilianza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mavurunza, Kata ya Kimara, baada ya Mnyika kusimama na kutaka kuzungumza na wananchi kuhusu ujio wa Makalla pamoja na juhudi alizozifanya za kuhakikisha maji yanapatikana.
Baada ya Mnyika kusimama wafuasi wa CCM walianza kumshambulia kwa maneno ya kumtaka kuwa muda wake wa kukaa katika jimbo hilo umekwisha na kwamba, hana kazi nyingine anayofanya zaidi ya kutoa hoja bungeni na kuomba mwongozo wa Spika.
Waziri anusurika kichapo
Imeandikwa na Sharifa Marira
*Aondolewa chini ya ulinzi baada Chadema, CCM kuzusha vurugu
*Ni baada ya kudaiwa kuingiza u-CCM katika ziara ya kiserikali
KITENDO cha Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, kumkaribisha Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge, kusalimia wananchi kwenye mkutano wa kiserikali, jana kilizua balaa na kulazimisha nguvu za dola kuingilia kati kumnusuru mteule huyo wa Rais.
Tafrani hiyo ilizuka jana mchana huko Goba, wakati Makalla, ambaye yupo kwenye ziara ya siku nne kukagua miradi ya maji jijini Dar es Salaam, alipokuwa katika mkutano wa mwisho wa hadhara kwa siku hiyo.
Kitendo cha kada wa CCM, Madenge, kuitwa jukwaani, hakikuwapendeza wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwapo kwenye mkutano huo, kwa madai kuwa huo haukuwa mkutano wa kisiasa, ndipo wanachama hao walipokumbana na wenzao wa CCM na kuzusha vurugu kubwa zilizodumu kwa takriban dakika 30.
Habari Picha: Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Jimbo la Ubungo
ZIARA KATA YA KIBAMBA
Tukikagua ujenzi wa tanki la maji katika kata ya Kibamba
John Mnyika, Mbunge wa Ubungo akaiwa amebebwa na wafuasi wa chama chake wakati akiingia eneo la mkutano Kibamba
Diwani wa Kata ya Kibamba akizungumza jambo la Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia wananchi wa kata ya Kibamba
Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo wakiondoka katika eneo la tanki-Kibamba
ZIARA KATA YA KIMARA
Naibu Waziri wa Maji Amos Makalla, akimsikiliza kiongozi wa ujenzi wa Tanki la maji lililopo Kimara jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika.
Tanki hili litavunjwa na kujengwa jipya
Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza na vyombo vya habari katika ziara hiyo ya kukagua miradi ya maji kata zilizopo Jimboni Ubungo
MKUTANO NA WANANCHI KATIKA UWANJA WA SEKONDARI YA MAVURUNZA
Diwani wa Kimara Pacal Manota, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Sekondari ya Mavurunza
Askari Polisi akiwambeleleza wanaCCM kusikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa meza kuu katika mkutano uliofanyika uwanja wa Sekondari Mavurunza
Wakutanapo Chadema na CCM
John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza katika mkutano huo na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla uwanja wa Sekondari Mavurunza
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akizungumza katika mkutano wa hadhara
Katika hati hati ya kutaka kunusuru fujo zilizoanza kutokea katikati ya mkutano wa hadhara
Ujumbe wa wananchi kwa njia ya mabango
Polisi akijaribu kuwasihi wanaCCM kutulia ili mkutano uweze kuendelea
WanaCCM na WanaCHADEMA akutanapo
Ujumbe katika mabango
Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika tukijaribu kuwasihi wananchi toka katika pande zote za vyama kutulia ili mkutano uweze kuendelea
Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akijaribu kuwatuliza Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota
Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu. Huku Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akiendelea kuwasihi Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota
Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu
Shukrani kwa picha: Blogu ya Mzuka Kamili (www.mzukakamili-mzuka.blogspot.com)
Tuesday, July 8, 2014
Mnyika adai kutishiwa maisha
Na
Veronica Romwald, Dar es Salaam
MBUNGE
wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amewaomba wapiga kura wake kumuombea kila
siku kutokana na madai kuwa amekuwa akiwindwa na watu wanaotishia uhai wake.
Mnyika
alitoa kauli hiyo juzi jioni katika eneo la Mbezi mjini Dar es Salaam, wakati
akihutubia mkutano wa hadhara.
“Nimekuwa
nikizungumza mambo mengi ninapokuwa bungeni Dodoma, hasa ninapowatetea wananchi
na wapiga kura wangu, lakini kuna watu hawafurahishwi kabisa…sasa wamefikia
hatua ya kunitishia maisha yangu.

