Monday, January 26, 2015

Tumezindua ujenzi wa barabara za; Mbezi mwisho-Goba-Tangi Bovu, Barabara ya External –Kilungule, Barabara ya Msewe-Baruti!

Uwekaji wa jiwe la msingi kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Mbezi mwisho-Goba-Tangi Bovu

Jitihada za kibunge na nje ya bunge katika kupambana na kero ya maji jimboni Ubungo (na Jiji la Dar es Salaam kwa ujumla)

Kwa muda mrefu Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika amekuwa akifanya jitihada za kibunge na hata nje ya bunge kuhakikisha utatuzi wa kero ya maji unapatikana.

Jitihada za kibunge na changamoto zake:


Akiwasilisha kwa wananchi:

Bado msimamo na udhabiti wa kutetea wananchi katika kuhakikisha kero ya maji inatatuliwa ndani ya jimbo la Ubungo inaendelea. 

Maslahi ya Umma Kwanza!

MUHIMU: Je umesoma Katiba Pendekezwa? Soma sasa hapa

Karibuni kusoma nakala ya Katiba Pendekezwa. KATIBA_INAYOPENDEKEZWA_02.10.2014.pdf


Kwa nakala hii inatoa fursa kujua mapendekezo yetu wananchi tuliyoyatoa mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Warioba je yamezingatiwa au lah.

Mshirikishe mwananchi mwenzako mwingine!

Friday, October 31, 2014

WAZIRI MUHONGO, WAZIRI MKUU PINDA NA SPIKA MAKINDA WAJITOKEZE KUTOA MAELEZO JUU YA HATUA WALIZOCHUKUA KUHUSU UFISADI NA UDHAIFU KATIKA WIZARA YA NISHATI NA MADINI; WASIPOFANYA HIVYO NITAUREJESHA MJADALA BUNGENI NOVEMBA 2014

Itakumbukwa kwamba tarehe 29 Aprili 2014 kupitia Hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Nishati na Madini (nimeambatisha nakala)  juu ya mapitio ya utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2013/2014 na makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara tajwa kwa mwaka 2014/2015 nilieleza ufisadi na udhaifu uliopo katika Wizara hiyo na mashirika yaliyo chini yake.

Kutokana na kukithiri kwa ufisadi na udhaifu huo nilipendekeza hatua zifuatazo ziweze kuchukuliwa katika Mkutano wa 15 wa Bunge uliokuwa ukiendelea wakati huo, nanukuu:

Mosi, Spika aruhusu kabla ya mjadala huu kuendelea ziwekwe mezani nakala ya ripoti zote za kamati za uchunguzi kwenye Sekta ya Nishati na Madini zilizoundwa na matokeo yake kutowasilishwa bungeni mpaka sasa.

Thursday, October 23, 2014

Pata hapa nakala ya muswada wa Baraza la Vijana la Taifa; boresha tupate baraza bora

Katika Mkutano wa 14 wa Bunge tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 niliouwasilisha tarehe 31 Oktoba 2013.

Narudia tena kuwashukuru vijana na wadau tulioshirikiana kuandaa muswada huo na naomba kuendelea kupata ushirikiano wenu wa karibu katika hatua zinazoendelea.

Kuanzia tarehe 21 Oktoba 2014 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii imeanza vikao vya kupokea maoni ya wadau kuhusu muswada huo. Nakala tete ya muswada huo inapatikana hapa, tafadhali pakua pitia na wasilisha maoni yako sasa.

Unaweza kuandika maoni yako kwenye mtandao wa http://mnyika.blogspot.com au kutuma kwa barua pepe kwenda mbungeubungo@gmail.com na nakala kwa Kamati husika ya Bunge kupitia tanzparl@parliament.go.tz.

Ikiwa unataka kutumia njia nyingine kuwasilisha maoni yako tafadhali wasiliana na Gaston Garubimbi 0715/0767-825025 kwa maelezo zaidi. Mdau wa masuala ya vijana zingatia kwamba  zaidi ya miaka 18 ahadi za kukamilisha mchakato wa kuanzishwa kwa baraza  la Vijana la Taifa zimekuwa zikitolewa bila utekelezaji kamili na wa haraka.

Wednesday, October 8, 2014

Maharamia wamepitisha Katiba haramu: wameanzisha mgogoro chanya na mwanya wa mabadiliko

Dira ni kuwa na katiba bora itakayojenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli, uhuru wa kweli na maendeleo endelevu kwa watu wake wote. Lakini uharamia katika mchakato wa katiba mpya umelipasua taifa. Mpasuko huu unaweza kuwa mgogoro hasi wenye madhara kwa wananchi au mgogoro chanya utakaoleta mabadiliko nchini. 

Maharamia wanashangilia kilevi katika Bunge Maalum baada ya kukamilisha uharamia dhidi ya rasimu ya katiba ya wananchi kwa kupata theluthi mbili kwa njia kiharamia. Katiba iliyopendekezwa kiharamia ni katiba haramu.

Katiba haramu, katiba ya maharamia, katiba ya mafisadi, katiba ya CCM wahafidhiana na mawakala wake inapaswa kupingwa mtaani na mahakamani kwa mbinu mbalimbali. 

Iwe ni kwa mikutano, migomo, maandamano, mashtaka au katika sanduku la kura. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba mchakato huu wa mabadiliko ya katiba ni mwanya wa mabadiliko katika taifa letu.

Saturday, September 27, 2014

TAARIFA KWA UMMA

Katika Mkutano wa 14 Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.

Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa kwenye kamati zinazohusika;  Nne, ni upi wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Katika Mkutano wa 14 Kikao cha 15 tarehe 21 Disemba 2013 ulisomwa Bungeni Muswada Binafsi wa Mbunge wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa wa mwaka 2013 uliowasilishwa na John Mnyika (Mb).
Baada ya muswada huo kusomwa, Bunge lilielezwa na Mheshimiwa Spika, naomba kununukuu “ Waheshimiwa wabunge, muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Hata hivyo, mpaka sasa maelekezo hayo ya Spika hayajatekelezwa hivyo; Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo inataka Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa kauli ya: Mosi, kuueleza umma sababu ya maelekezo yake ya muswada huo kuwepo kwenye tovuti ya bunge kwa ajili ya kuwa wazi kwa umma mpaka sasa kutokutekelezwa, Pili, ni lini muswada huo utapangiwa tarehe ya kujadiliwa; Tatu, ni kwanini mpaka sasa muswada huo haujapelekwa kwenye kamati zinazohusika;  Nne, ni upi wakati muafaka alioutaja kwenye maelezo yake.
Ofisi ya Jimbo la Ubungo inawakumbusha vijana na wadau wote wa maendeleo yao kwamba kutokuwepo kwa chombo kinachowaunganisha vijana wote bila kujadili itikadi kufuatilia masuala ya maendeleo ya vijana  kunafanya Wizara mbalimbali za kisekta kutokuzingatia masuala yaliyokipaumbele kwa maendeleo ya vijana.
Mathalani, katika Mkutano huu wa Bunge katika Fungu la 65 la Wizara ya Kazi na Ajira Kitabu cha Nne Cha Miradi ya Maendeleo Kifungu cha 2002, pamoja na wabunge na vijana kupewa matumaini kwamba zimepitishwa bilioni tatu kwa ajili ya mikopo na mitaji kwa vijana ukweli ni kwamba fedha hizo zimepangiwa matumizi ambayo kusipokuwa na chombo cha kuyafuatilia kutakuwa na udhaifu, ufisadi na ubadhirifu kama ilivyojitokeza katika fedha za mifuko ya maendeleo ya vijana  kati ya mwaka 1993/1994 mpaka 2013/2014.
Kwa mujibu wa Kasma za Kifungu hicho cha 2002 cha Bajeti iliyopitishwa ya Fungu 65 Wizara ya Kazi na Ajira, fedha hizo zinazopaswa kuwa za mikopo na mitaji kwa vijana zitatumika milioni 700 kwa ajili ya kulipia utaalamu elekezi (consultancy fees) kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa vijana 200 tu; milioni 150 zitatumika kununulia magari Wizarani, milioni 60 zitatumika kwenye matangazo na orodha ndefu nyingine ya  matumizi yasiyo ya lazima ambayo kutokana na ufinyu wa muda sitaendelea kuyataja.
Aidha, katika mjadala wa bajeti hiyo wabunge waliweka bayana kwamba kiwango kinachotengwa katika Mifuko ya Maendeleo ya Vijana iwe ni kwa Serikali Kuu na hata Halmashauri ni kidogo ukilinganisha na uwezo wa nchi, mahitaji ya vijana na mafungu mengine yasiyo na matumizi muhimu yanavyotengewa fedha nyingi katika baadhi ya Wizara.
Hivyo, ili Baraza la Vijana la Taifa na Benki ya Vijana ambavyo ni vyombo muhimu kwa maendeleo ya vijana viweze kuanzishwa kwa wakati, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inamkumbusha Spika wa Bunge kuelekeza muswada binafsi uliokwisha wasilishwa kwa Bunge kwa kamati zinazohusika kwa ajili ya kuanza  kuujadili. Suala hili ni muhimu likapata majibu ya mapema ili muswada huo uweze kuwasilishwa Bungeni katika Mkutano wa 16 wa Bunge unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba mwaka 2014.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inatoa mwito pia kwa vijana na wadau wa maendeleo ya vijana kuingilia kati suala hili na kuisimamia Serikali kwa kuzingatia kwamba katika majumuisho ya Bajeti ya Wizara yenye dhamana ya vijana kwa mwaka 2013/2014 tarehe 21 Mei 2013 mkutano wa 11 kikao cha 30; Serikali ilitumia kisingizio kwamba ‘ni bunge la bajeti’ kukwepa kuwasilishwa kwa muswda Bunge. Hata hivyo, ahadi ya Serikali ya kuwasilisha muswada haikutekelezwa kwenye mikutano mitatu uliyofuatia ya 12, 13, 14 na 15; hivyo mkutano huu wa 16 ni muafaka kuwezesha maamuzi kufanyika kwa ajili ya maendeleo ya vijana nchini.
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Ubungo inaukumbusha umma kwamba Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa  Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007; hata hivyo Serikali imekuwa ikiwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera tajwa yanatekelezwa pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo ya vijana nchini.
Imetolewa tarehe 24 Septemba 2014 na:

Aziz Himbuka
Katibu wa Mbunge

Jimbo la Ubungo

Monday, September 8, 2014

Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) yakabidhiwa Komputa na Kasiki (safe) na Mbunge Mnyika

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika akikabidhi kompyuta na Kasiki (Safe) kwa Kinondoni Vijana Saccoss (KIVISA) ikiwa ni sehemu ya milioni 10 za CDCF tulizotenga kwenye kuchochea vijana na wanawake kujiajiri.

Uzinduzi wa rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake,vijana na wenye ulemavu


John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo Akizindua rasimu ya ripoti ya matokeo ya utafiti kuhusu kuongeza ushiriki na uwakilishi wa wanawake, vijana na wenye ulemavu katika uongozi uliofanywa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)

Monday, September 1, 2014

Mnyika akabidhi vyerahani kutimiza ahadi ya ajira kwa wanawake


Mnyika akibidhi vyerehani na mashine kudarizi kwa VICOBA viwili vya wanawake Kimara na Matete ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya kutoa vifaa vya kuwawezesha kujiajiri vyenye thamani ya jumla ya milioni 10 kwa vikundi mbalimbali jimboni kutoka katika CDCF;

(Kutoka kushoto Diwani Manota, anayekabidhiwa ni Mwenyekiti wa Kikundi na anayeshuhudia ni Mtendaji wa Kata)

Rais Kikwete, Waziri wa Maji Prof Maghembe na Bodi mpya ya DAWASCO

Tarehe 13 Agosti 2014 Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe alizindua Bodi mpya ya Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASCO) na kutoa kauli mbalimbali mbele ya vyombo vya habari ambazo zinaendeleza udhaifu ule ule badala ya kuchukua hatua za haraka kunusuru wananchi katika shida kubwa ya upatikanaji wa maji.

Ni suala lililo wazi kwamba kuzindua bodi mpya ya DAWASCO pekee haitoshi, kwa kuzingatia kuwa majukumu makuu ya kuwezesha hatua za haraka yapo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar Es Salaam (DAWASA) ambayo nayo inahitaji bodi mpya.

Natoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kuvunja bodi iliyopo ya DAWASA na kuunda bodi mpya. Aidha, namkumbusha Rais Kikwete kuitisha kikao ikulu pamoja na DAWASCO, DAWASA na Wizara ya Maji kama alivyoahidi mbele ya wananchi mwezi Machi mwaka 2013.

Thursday, July 31, 2014

Kuhusu uongozi mpya wa wilaya ya CHADEMA Ubungo

Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine (wa kanza kushoto) akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam
UONGOZI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya kichama Ubungo unatarajiwa kujulikana Agosti 3, 2014 baada ya uchaguzi wa ngazi za chini katika wilaya hiyo kukamilika. 

Mbali na viongozi wa wilaya hiyo kujulikana siku hiyo, pia chama hicho kimeeleza kuwa, kimejiandaa vema kuwadhibiti mamluki wasijipenyeze katika uongozi huo. 

Hayo yalibainishwa na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine, wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi wa ngazi za msingi, matawi na kata. 

Nafasi zitakazowaniwa ni ya mwenyekiti, katibu, katibu mwenezi na mhazini na kwamba, kwa ngazi ya mabaraza ni vijana, wazee na wanawake. 

Monday, July 28, 2014

Mnyika ataka matengenezo ya barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni yaharakishwe

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika amemtumia mjumbe Meya wa Manispaa ya Kinondoni kutaka afuatilie kwa karibu matengenezo ya Barabara ya Sinza-Tandale-Magomeni (Barabara ya Mlandizi) kuharakishwa.

Mbunge amechukua hatua hiyo baada ya kupita katika barabara hiyo kuanzia maeneo ya Sinza Kijiweni-Mtogole hadi Makanya na kubaini kwamba bado ukarabati haujaanza na hali ya barabara ni mbaya.

Mnyika amewasiliana pia na Mkurugenzi wa Halmashauri kutaka Ofisi yake itoe taarifa kupitia vyombo vya habari tarehe ngapi matengenezo hayo yataanza na lini yanatarajiwa kumalizika.

Mnyika amekumbusha kwamba pamoja na kero ambazo wananchi wanapata hivi sasa Serikali inapaswa kutambua kwamba barabara hiyo ni muhimu katika kupunguza msongamano kwenye Barabara ya Morogoro na inapaswa kupewa kipaumbele wakati huu ambapo ujenzi wa mradi wa mabasi ya haraka (DART) unaendelea na hivyo kuhitajika kwa barabara mbadala.

Sunday, July 20, 2014

Mkutano wa naibu waziri wa maji waingia dosari katika kata ya Goba.


Mnyika amnusuru Waziri Makala

16 Julai, 2014 Na Abdallah Khamis

Naibu Waziri wa Maji, Amos MakalaMBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemnusuru Naibu Waziri wa Maji, Amos Makala asiendelee kuzomewa na wananchi wakati wa  ziara yake ya ukaguzi wa miundombinu ya maji jimboni humo.
Mapema wanachama wa CCM wakiwa na bendera zao, walionekana kupangwa ili kumzomea Mnyika ambaye hata hivyo hakuwajali, badala yake aliendelea kuhutubia mkutano huku Makala akionekana kufurahishwa na hali hiyo.
Mnyika alieleza jinsi alivyowapigania wakazi wa Kimara Mavurunza na maeneo mbalimbali ya jiji kupata maji pasipo kujali itikadi zao za vyama.
Alisema ziara hiyo ya naibu waziri ni matokeo yake ya kumbana Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, pamoja na watendaji wa Kampuni ya kusambaza maji ya Dawasa kuhakikisha maji yanapatikana kwa wakazi wa Dar es Salaam.

CCM,Chadema wafanya vurugu ziara ya Makalla, Mnyika

Na Mary Geofrey 16th July 2014
Print
Ujumbe ulioongozana na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ukiwa ndani ya tenki la maji lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi jana.
Wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana walifanya vurugu katika ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla na Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika ya kukagua miradi ya maji katika jimbo hilo.

Mbali na kukagua miradi ya maji, Makalla na Mnyika alitumia ziara hiyo pamoja na kuzungumza na wananchi juu ya mipango na mikakati ya serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa maji jimboni humo.

Vurugu hizo zilianza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mavurunza, Kata ya Kimara, baada ya Mnyika kusimama na kutaka kuzungumza na wananchi kuhusu ujio wa Makalla pamoja na juhudi alizozifanya za kuhakikisha maji yanapatikana.

Baada ya Mnyika kusimama wafuasi wa CCM walianza kumshambulia kwa maneno ya kumtaka kuwa muda wake wa kukaa katika jimbo hilo umekwisha na kwamba, hana kazi nyingine anayofanya zaidi ya kutoa hoja bungeni na kuomba mwongozo wa Spika.

Waziri anusurika kichapo


Imeandikwa na Sharifa Marira

*Aondolewa chini ya ulinzi baada Chadema, CCM kuzusha vurugu

*Ni baada ya kudaiwa kuingiza u-CCM katika ziara ya kiserikali


KITENDO cha Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, kumkaribisha Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge, kusalimia wananchi kwenye mkutano wa kiserikali, jana kilizua balaa na kulazimisha nguvu za dola kuingilia kati kumnusuru mteule huyo wa Rais.

Tafrani hiyo ilizuka jana mchana huko Goba, wakati Makalla, ambaye yupo kwenye ziara ya siku nne kukagua miradi ya maji jijini Dar es Salaam, alipokuwa katika mkutano wa mwisho wa hadhara kwa siku hiyo.

Kitendo cha kada wa CCM, Madenge, kuitwa jukwaani, hakikuwapendeza wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwapo kwenye mkutano huo, kwa madai kuwa huo haukuwa mkutano wa kisiasa, ndipo wanachama hao walipokumbana na wenzao wa CCM na kuzusha vurugu kubwa zilizodumu kwa takriban dakika 30.

Habari Picha: Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Jimbo la Ubungo

ZIARA KATA YA KIBAMBA







Tukikagua ujenzi wa tanki la maji katika kata ya Kibamba


John Mnyika, Mbunge wa Ubungo akaiwa amebebwa na wafuasi wa chama chake wakati akiingia eneo la mkutano Kibamba




Diwani wa Kata ya Kibamba akizungumza jambo la Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla


Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia wananchi wa kata ya Kibamba


Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo wakiondoka katika eneo la tanki-Kibamba

ZIARA KATA YA KIMARA


Naibu Waziri wa Maji Amos Makalla, akimsikiliza kiongozi wa ujenzi wa Tanki la maji lililopo Kimara jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika.


Tanki hili litavunjwa na kujengwa jipya





Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza na vyombo vya habari katika ziara hiyo ya kukagua miradi ya maji kata zilizopo Jimboni Ubungo

MKUTANO NA WANANCHI KATIKA UWANJA WA SEKONDARI YA MAVURUNZA


Diwani wa Kimara Pacal Manota, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Sekondari ya Mavurunza


Askari Polisi akiwambeleleza wanaCCM kusikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa meza kuu katika mkutano uliofanyika uwanja wa Sekondari Mavurunza


Wakutanapo Chadema na CCM 


John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza katika mkutano huo na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla uwanja wa Sekondari Mavurunza





Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akizungumza katika mkutano wa hadhara








Katika hati hati ya kutaka kunusuru fujo zilizoanza kutokea katikati ya mkutano wa hadhara







Ujumbe wa wananchi kwa njia ya mabango





Polisi akijaribu kuwasihi wanaCCM kutulia ili mkutano uweze kuendelea


WanaCCM na WanaCHADEMA akutanapo


Ujumbe katika mabango












Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika tukijaribu kuwasihi wananchi toka katika pande zote za vyama kutulia ili mkutano uweze kuendelea









Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akijaribu kuwatuliza Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota














Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu. Huku Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akiendelea kuwasihi Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota


Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu


Shukrani kwa picha: Blogu ya Mzuka Kamili (www.mzukakamili-mzuka.blogspot.com)



Tuesday, July 8, 2014

Mnyika adai kutishiwa maisha

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amewaomba wapiga kura wake kumuombea kila siku kutokana na madai kuwa amekuwa akiwindwa na watu wanaotishia uhai wake.
Mnyika alitoa kauli hiyo juzi jioni katika eneo la Mbezi mjini Dar es Salaam, wakati akihutubia mkutano wa hadhara.
“Nimekuwa nikizungumza mambo mengi ninapokuwa bungeni Dodoma, hasa ninapowatetea wananchi na wapiga kura wangu, lakini kuna watu hawafurahishwi kabisa…sasa wamefikia hatua ya kunitishia maisha yangu.