Sunday, February 23, 2014

TAARIFA KWA UMMA: SAKATA LA FIDIA YA ENEO LA MLOGANZILA

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika ameendelea kufuatilia kuhusu fidia ya ardhi ya wananchi wa kata ya Kwembe waliohamishwa baada ya kulipwa fidia ya maendelezo pekee kupitisha ujenzi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.

Kwa upande mwingine, Mbunge Mnyika ameendelea pia kuhoji katika mamlaka mbalimbali juu ya kauli za viongozi wa Serikali kutamka kwamba eneo hilo lipo katika Mkoa wa Pwani badala ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam.

Tarehe 19 Januari 2014 Mbunge Mnyika alifika katika kata ya Kwembe na kukutana na wananchi kusikiliza malalamiko yao na mara baada ya mkutano huo alizikutanisha kamati mbili zinazofuatilia suala hilo.

Kufuatia hatua hiyo, Mbunge Mnyika aliwasiliana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwakumbusha kutekeleza ahadi zao za kuupatia ufumbuzi mgogoro huo kufuatia hatua ya mbunge kuhoji suala hilo bungeni kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2011 mpaka 2013. (Baadhi ya rejea kutoka Kumbukumbu Rasmi za Bunge-Hansard zimeambatanishwa).

Saturday, February 22, 2014

Maoni yangu kuhusu matokeo ya kidato cha nne wa mwaka 2013


Maoni yangu kuhusu matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne wa mwaka 2013 yaliyotangazwa na kuelezwa kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 15.17 yamedhihirisha tahadhari niliyotoa kuhusu mabadiliko ya viwango vya ufaulu yaliyotangazwa na Serikali tarehe 30 Oktoba 2013.

Serikali kwa barakoa (veil) ya kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) imeamua kulificha taifa juu ya Matokeo Mabaya ya Sasa (Bad Results of Now). Hivyo, wachambuzi wa masuala ya elimu wanapaswa kutoa takwimu za matokeo yangekuwa namna gani iwapo viwango vya awali vya ufaulu vingetumika ili nchi ijue hali halisi kwa manufaa ya wananchi.

Aidha, natoa mwito kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuweka wazi kwa umma ripoti za uchunguzi zilizoundwa kuwezesha wananchi kuihoji Serikali iwapo kupanda huko kwa ufaulu ni matokeo ya kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunza au ni kiini macho cha mabadiliko ya wigo wa alama na madaraja?

Ukweli ni kuwa hali ya mazingira ya kujifunza na kujifunzia katika shule nyingi za msingi na sekondari hasa za umma sio nzuri kutokana na kutokuwa na vitabu vya kutosha, maabara za kutosha, waalimu wenye sifa wapo wa kutosha na kuboresha maslahi ya waalimu ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa siku nyingi.

Thursday, February 20, 2014

Rasilimali na mchakato wa kuandika Katiba Mpya

Kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini natoa mwito kwa wadau wote wa masuala ya rasilimali kuzingatia kwamba rasimu ya katiba haijazingatia masuala ya msingi kuhusu haki ya wananchi kumiliki na kunufaika na rasilimali za nchi. Hatua hii ni kinyume na mapendekezo niliyoyatoa bungeni tarehe 22 Mei 2013 na maoni yangu niliyoyatoa mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba pamoja na maoni yaliyotolewa na wadau wengine mbalimbali. 

Katika hotuba yangu ya Bungeni nilitaka Serikali isitishe kuendelea kunadi leseni za vitalu vya gesi mpaka kwanza mchakato wa katiba mpya ukamilike na pawepo sera na sheria zitazoongozwa na katiba mpya. Nilieleza kwamba katiba mpya inapaswa kuwa na ibara mahususi ya haki za wananchi kuhusu rasilimali ikiwemo ardhi, madini, gesi, mafuta, maji, misitu na maliasili zingine. Hata hivyo, katika rasimu ya katiba sura ya nne sehemu ya kwanza inayohusu haki za binadamu hakuna haki yeyote iliyotolewa kwa wananchi kuhusu kumiliki na kunufaika na rasilimali. Nitapendekeza kwa Bunge Maalum ibara mahususi kurekebisha udhaifu huo

Kwanini ni muhimu tushirikishe wananchi katika kutunga kanuni za Bunge Maalum

Kwenye kikao cha juzi cha Bunge Maalum nilipendekeza umuhimu wa suala la ushirikishwaji wa wananchi na wadau mbalimbali katika kutengeneza kanuni (Soma hapa: http://goo.gl/b0nQVA) . Wapo wenye mtazamo kwamba kanuni kwa kuwa ni za Bunge Maalum, kuandaa na kupitisha rasimu hiyo ni suala la wajumbe wenyewe pekee; hakuna ulazima wa wadau wala umma kushirikishwa.

Hata hivyo, kwa uzito na unyeti wa kanuni zenyewe na kwa kuzingatia kwamba mjumbe anapaswa kuzingatia maoni ya aliyemtuma ni muhimu umma ujue na kushiriki.

Pia, izingatiwe kwamba Bunge Maalum linapoendelea upo wakati wadau na wananchi wanataka kufuatilia kuhakikisha maoni na maslahi yao yanazingatiwa na wajumbe wao.

Hivyo, ni muhimu kushirikishwa kupata kuwezesha kanuni kuruhusu fursa hiyo. Ni wajulishe tu kwamba rasiu ya Katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. Nitafanya uchambuzi wa vifungu hivyo vibovu na hatimaye nitawasilisha mapendekezo ya maboresho kwa Bunge Maalum.

Wednesday, February 19, 2014

Uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga: CHADEMA yamekea pingamizi CCM!

CHADEMA imemuwekea pingamiza mgombea wa CCM kwamba sio raia wa Tanzania. 

Kazi imeanza!

Mkakato wa Katiba Mpya: Wadau washirikishwe kutunga kanuni Bunge la Katiba

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amesema atawasilisha mapendekezo ya kutaka ratiba ya Bunge Maalumu la Katiba ibadilishwe, ili wadau washirikishwe kwenye mchakato wa kutunga kanuni za Bunge hilo.

Mnyika alisema hayo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.

Alisema ratiba iliyotolewa inaonyesha kwamba baada ya kusomwa kwa tangazo la kuitisha Bunge hilo na uchaguzi wa mwenyekiti wa muda, kazi ya kutunga kanuni itaanza.

Mnyika alisema kanuni ndiyo msingi wa kufikia mwafaka wa kuboresha rasimu ya Katiba badala ya kuchakachua na kwamaba ili zisitungwe kanuni mbovu ipo haja ya wadau wote wanaohusika na mchakato wa Katiba mpya ndani na nje ya Bunge kushiriki. 

“Nakusudia kuwasilisha mapendekezo kwamba ratiba ya Bunge ifanyiwe mabadiliko ili kuwapo na kikao cha kusikiliza umma (Public hearing), juu ya kanuni hizo ili mawazo ya wadau yazingatiwe katika maandaluzi ya kanuni kabla ya Bunge kupitisha azimio la kuridhia kanuni hizo,” alisema Mnyika.

Tafakari ya leo!


Tuwe wepesi wa kusikia si kusema wala kukasirika.

Tuwe watendaji sio wasikiaji tu.

Dini safi ni matendo mema.


-Funzo toka Yak. 1:19-27

Fursa kwa kijana kufanya kazi Ofisi ya Mbunge

Feb 2014 ni mwaka 1 toka nilipowasilisha Bungeni Hoja Binafsi ya kupendekeza Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka kuboresha upatikanaji wa Maji Safi na ushughulikiwaji wa Maji Taka katika jiji la Dar es Salaam. Soma hapa: http://goo.gl/Q770zm Natumia fursa hii kutangaza nafasi ya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini mafanikio na vikwazo kwa kijana wa ndani ya Jimbo la Ubungo (Mwanamke au Mwanaume) aliyetayari kufanya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini hatua za haraka juu ya suala la Maji ndani ya jiji la Dar es Salaam afike Ofisi ya Mbunge, Halmashauri ya Kinondoni.

John J. Mnyika
Mbunge wa Ubungo
19.02.2014

Tuesday, February 18, 2014

Hon. John Mnyika's witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly

IN THE EAST AFRICAN COURT OF JUSTICE
FIRT DIVISION
AT ARUSHA
REFERENCE NO.07 OF 2012
(In the matter of interpretation of Article 50 of the Treaty for the Establishment of the East African Community)
BETWEEN
ANTON CALIST KOMU………………….CLAIMANT
AND
THE HONOURABLE ATTORNEY GENERAL OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA…………………….......RESPONDENT


WITNESS STATEMENT OF JOHN MNYIKA

I, John Mnyika Member of Parliament of the United Republic of Tanzania for Ubungo Constituency, make the following witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly members:

I wrote a letter dated 8th February 2012 with reference no. OMU/BJMT/004/2012 to the Clerk of The Parliament of United Republic of Tanzania requesting amendment  to be  made in the third schedule of the Parliamentary Standing Orders (The East African Legislative Assembly Election Rules).

I made those proposals commensurate with the requirement of sections 3(3)(a) and (b) of the eighth schedule made under standing order 115 of the Parliamentary Standing Orders (2007 Edition).

I requested the Clerk to recall what transpired in the Election of East African Legislative Assembly that was conducted in the Parliament of the United Republic of Tanzania on the 2nd of November 2006. 

In that particular election complains arose and were raised that indicated the need for amendment of the East African Legislative Assembly Election Rules of the Parliament of the United Republic of Tanzania. I also drew to the attention of the Clerk that The East African Assembly had passed the EALA elections Act of 2011.

Monday, February 17, 2014

Mrejesho wa leo Februari 17: Jitihada za kuboresha barabara jimboni Ubungo na mengineyo

1. Barabara ya Goba-Mbezi Louis nawaomba wananchi wenzangu mfuatilie matengenezo yaliyoanza na kutoa mrejesho; lami kidogo nayo itaanza. Tuungane kupendekeza nyongeza bajeti hii

2. Barabara ya Malambamawili-Msigani naombeni tathmini ya matengenezo yaliyofanyika; ujenzi wa lami utaanzia kipande cha Kinyerezi-Kifuru. Kwa hii sasa ni hatua.

3. Barabara ya Bonyokwa-Mavurunza Kimara mwisho; nimewasiliana na Manispaa ya Kinondoni kukumbusha utekelezaji wa ahadi ya matengenezo. Majibu kesho.

4. Barabara ya Matete-Jeshini-Golani haikutengewa fedha KMC, nimewatumia ujumbe TANROADS wakishughilikia Msewe wasogee

5. Barabara ya Mavurunza-Golani-Msewe-Matete hali ya barabara ni tete. Nimewasiliana na diwani Pascal Manota na kumtumia posho ya leo kuweka mafuta grader. Ikiwa unatumia barabara za Mavurunza-Golani-Matete wasiliana na Diwani 0713792966 utuunge mkono sasa; mamlaka zingine nazo tunazifuatilia

Friday, January 31, 2014

Mwito kwa wananchi kutoa maoni kuhusu sheria ndogo

 
Nimerejea jimboni kikazi, pamoja na ufuatiliaji kuhusu kasoro za ujenzi unaendelea katika Barabara ya Morogoro na matengenezo yanayohitajika katika barabara zinaunganika na barabara hiyo katika maeneo ya pembezoni kupunguza foleni, lipo suala linalohitaji mjadala na maoni ya haraka toka kwa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Tangu mwaka 2013 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imekuwa katika mchakato wa kutunga sheria ndogo nne: ya matumizi ya barabara, ushuru wa masoko, ada na ushuru na ushuru wa huduma. Mwanzoni mwa mwaka huu 2014 katika kikao cha Baraza la madiwani ilibainika kwamba sheria hizo zilikaribia kupitishwa bila ya ushirikishwaji wa kutosha wa wadau na wananchi.

Halmashauri iliongeza muda wa kupokea maoni; hata hivyo muda ukiwa unaelekea ukiongoni, ikiwa imesalia takribani wiki moja, tathmini ya ofisi ya mbunge Jimbo la Ubungo inaonyesha kwamba sheria hizo hazijasambazwa vya kutosha kwa wananchi na wadau kwa ajili ya kutoa maoni yao katika kata na mitaa mbalimbali.

Hivyo, ofisi ya mbunge Jimbo la Ubungo leo tarehe 31 Januari 2014 itafanya kazi ya kusambaza Sheria hiyo kwa njia mbalimbali kwa ajili ya wadau na wananchi kupitia na kutoa maoni yao. Mkazi wa Jimbo la Ubungo anayehitaji kutoa nakala anaweza kuwasiliana na Katibu Msaidizi Aziz Himbuka kupitia 0784379542 au 0715379542 au kwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni moja kwa moja.

Wednesday, January 22, 2014

Ufafanuzi kuhusu upanuzi na mgogoro wa kuhusu upana wa barabara ya Morogoro

Kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2004 na 2013 nimezungumzia haja ya upanuzi wa Barabara ya Morogoro kutoka Jimboni Ubungo kupitia Kibaha mpaka Chalinze na mgogoro uliodumu muda mrefu kuhusu upana wa Barabara hiyo.

Ningependa kutoa ufafanuzi kwamba nyakati zote nimeunga mkono upanuzi wa Barabara hiyo ikiwemo ujenzi wa barabara hiyo kuwa njia sita (tatu kwenda na tatu kurudi).

Hata hivyo, mara nyingi nimekosoa masuala manne kuhusu upanuzi na mgogoro kuhusu upana wa barabara ya Morogoro:

Mosi, Serikali kutoa ahadi bila utekelezaji kwa miaka mingi. Mwaka 2012 na 2013 Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli amekuwa akirudia kauli kwamba ujenzi wa Dar Es Salaam-Chalinze express road kuanza. Katika mkutano wangu na wananchi jimboni tarehe 19 Januari 2014 kuhusu ujenzi wa Barabara hiyo, nimesisitiza kwamba fedha za ujenzi wa barabara hiyo hazijatengwa hivyo ujenzi hauwezi kuanza. Badala yake nilifafanua kwamba Serikali inachokifanya kwa sasa ni kutafuta mkandarasi mwenye uwezo wa kutafuta fedha na kujenga. Hivyo, ni muhimu Serikali ikawaeleza wananchi ukweli na kuharakisha kutekeleza ahadi zilizotolewa kwa miaka mingi.

Wednesday, January 15, 2014

TAARIFA KWA UMMA: Kero ya maji Dar na taarifa za kina


Rais Jakaya Kikwete amwondoe Prof. Jumanne Maghembe nafasi ya Waziri wa Maji kwa kushindwa kuchukua hatua za haraka za kuongeza upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika Jiji la Dar Es Salaam na nchini kwa ujumla.

Rais Kikwete azingatie kwamba tarehe 10 Januari 2014 nilimtumia ujumbe Waziri Maghembe kumshauri ajiuzulu kutokana na kujirudia rudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam kinyume na maelezo yake ya uongo aliyoyatoa bungeni tarehe 4 Februari 2013.

Aidha, kufutia maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Hawa Sinare kuhusu sababu za kuchelewa kwa miradi ya maji Jijini na majibu ya Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASCO) Jackson Midala kuhusu kujirudia kwa matatizo ya maji; Rais Kikwete akumbuke ahadi yake ya kuitisha kikao Ikulu kujadili masuala maji mwezi Machi 2013 ambayo mpaka sasa hajaitekeleza.

Ikumbukwe kwamba mara baada ya kujirudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam niliwasiliana na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua na pia nilitaka Wenyeviti wa Bodi na Watendaji wakuu wa Mamlaka zinazohusika na huduma ya maji jijini (DAWASA na DAWASCO) watoe maelezo kwa umma juu ya sababu za kweli za matatizo za matatizo hayo.

Taarifa kwa Umma-Nishati ya Umeme


Kufuatia ukimya wa Wizara ya Nishati na Madini na Mamlaka nyingine tangu nitoe mwito kwao tarehe 9 Januari 2014 juu ya ongezeko la bei ya umeme; namshauri Rais Jakaya Kikwete katika mchakato wa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri kumtaka Waziri Prof. Sospeter Muhongo kujieleza kwake na kwa umma kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa.

Rais Kikwete akumbuke kwamba Waziri Muhongo alisema uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 alipowahakikishia wananchi kwamba bei ya umeme haitapanda hata baada ya TANESCO kuwasilisha mapendekezo ya kupandisha bei ya umeme.

Kinyume na kauli za Waziri Prof. Muhongo; Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kikao chake cha tarehe 10 Desemba 2013 pamoja na mambo mengine, ilitoa maamuzi ya ongezeko la bei za umeme kwa viwango mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya wateja hatua ambayo itaongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi na itaathiri uchumi wa nchi.

Maamuzi hayo yamefikiwa kufuatia tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa EWURA. TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.

Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa kanuni ya kurekebisha bei ya umeme kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta, mfumuko wa bei na mabadiliko ya thamani ya shilingi ya kitanzania hatua ambazo nazo zina athari katika uchumi na maisha ya wananchi.

Thursday, January 9, 2014

Waziri Prof. Maghembe ajiuzulu: DAWASA/DAWASCO warejeshe huduma ndani ya wiki moja katika maeneo yaliyokuwa yakipata mgao wa maji kabla

Nimemtumia ujumbe Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe kumshauri ajiuzulu kutokana na kujirudia rudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam kinyume na maelezo yake ya uongo aliyoyatoa bungeni tarehe 4 Februari 2013.

Aidha, Wenyeviti wa Bodi na Watendaji wakuu wa Mamlaka zinazohusika na huduma ya maji jijini (DAWASA na DAWASCO) watoe maelezo kwa umma juu ya sababu za kweli za matatizo ya maji kujirudia rudia katika Jiji la Dar Es Salaam.

Pia, wajieleze kwa umma ni kwanini wananchi wasipendekeze Rais awachukulie kwa uzembe, kuisababishia hasara Serikali, kuathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa kukosa maji mara kwa mara ambayo ni huduma ya msingi ya binadamu na malighafi muhimu katika uzalishaji.

Itakumbukwa kwamba tarehe 4 Februari 2013 niliwasilisha hoja binafsi bungeni juu ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji katika jiji la Dar Es Salaam, nikipendekeza Bunge kuingilia kati kuweza kuisimamia Serikali kuchukua hatua za haraka.

Iwapo hoja hiyo ingejadiliwa na maazimio yote kutekelezwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam mpaka hatua ya sasa yangekuwa yamepungua katika maeneo mbalimbali kutokana na hatua ambazo nilipendekeza zichukuliwe.

Kauli ya awali kuhusu ongezeko la bei za umeme

Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kikao chake cha tarehe 10 Desemba 2013 pamoja na mambo mengine, ilitoa maamuzi ya ongezeko la bei za umeme kwa viwango mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya wateja hatua ambayo itaongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi na itaathiri uchumi wa nchi.

Maamuzi hayo yamefikiwa kufuatia tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa EWURA. TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.

Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa kanuni ya kurekebisha bei ya umeme kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta, mfumuko wa bei na mabadiliko ya thamani ya shilingi ya kitanzania.

Maamuzi hayo ya Bodi ya EWURA ambacho ni chombo cha Serikali yamethibitisha kwamba Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo alisema uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 alipowahakikishia wananchi kwamba bei ya umeme haitapanda hata baada ya TANESCO kuwasilisha mapendekezo ya kupandisha bei ya umeme.

Monday, January 6, 2014

Kauli kuhusu Uongo wa Waziri Profesa Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ametoa kauli za uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 ndani na nje ya Bunge kuhusu utafiti na uendelezaji wa gesi asilia.

Waziri Muhongo alijibu uongo kwamba hafanyi kazi kwa vyombo vya habari nilipohoji kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge ya kuanzia Novemba 2011 ya kushughulikia ufisadi uliothibitika katika mapato ya mauzo ya gesi na udhaifu mwingine uliobanishwa.

Aidha, Waziri Muhongo aliahidi uongo alipounda alipounda kamati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) na kuahidi kwamba kamati hiyo itafanya mapitio ya mikataba na kuandaa ripoti itakayowezesha mikataba mibovu ya utafiti wa mafuta na gesi asili kufanyiwa marekebisho. Hata hivyo, Wizara ya Nishati na Madini baadaye iliyoa taarifa kwamba matokeo ya ripoti hiyo hayatatumika kwa ajili ya mikataba iliyopita bali mikataba ijayo.

Sunday, January 5, 2014

Mapendekezo ya Mgawanyo Mpya wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam

Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana kujadili mapendekezo ya kuongeza maeneo mapya ya utawala katika Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na ajenda zingine.

Nimeonelea tija kuwasilisha mapendekezo yangu kwa maandishi kwa umma na baadae katika kikao tajwa. Kwa hatua hii, ni fursa kwa kila mwananchi kutoa maoni yake juu ya haya;

Kwa ukuaji wa kasi wa Dar es Salaam ambao ndiyo mji mkubwa nchini Tanzania, jiji kitovu cha biashara na viwanda ambalo kadiri ya takwimu linakadiriwa kuwa na idadi ya watu milioni nne na nusu. Jiji hili limeshika nafasi ya tatu katika miji inayokuwa kwa kasi barani Afrika na miongoni mwa miji kumi inayokuwa kwa kasi duniani.

Ifahamike pia, Jiji la Dar es Salaam ndilo linashikilia asilimia themanini na tatu (83%) ya mapato ya serikali kitaifa na takribani asilimia sabini (70%) ya kodi zote zinazokusanywa nchini Tanzania.

Yafuatayo ndiyo mapendekezo yangu ya wasilisho la nyaraka ya mapendekezo yaliyoletwa katika ofisi yangu toka Manispaa ya Kinondoni;

Mosi, Pendekezo la kutumia “Manispaa” badala ya “Wilaya”:
Kadiri ya wasilisho, imetumika pendekezo la “wilaya”. Ningeshauri na kupendekeza kutokana na uhalisia na ukuaji wa kasi kutumika kwa “Manispaa” badala ya wilaya.

Pili, Pendekezo bora la mgawanyo wa Manispaa:
Katika wasilisho lenye uwepo wa mapendekezo saba. Ninaungana na kuafiki utumiaji wa pendekezo la pili lililowasilishwa la kuwa na Manispaa tano (5) ambazo ni;
i.                    Manispaa ya Ilala
ii.                 Manispaa ya Temeke
iii.               Manispaa ya Kinondoni
iv.                Manispaa ya Kigamboni
v.                  Manispaa ya Ubungo

Sababu muhimu:
1.        Ukubwa kijiografia: Kwa kuongeza wilaya mbili mpya yaani Manispaa ya Kigamboni na Manispaa ya Ubungo hii itasaidia wilaya hizi kuweza kuhimili ukubwa wa eneo wa kijiografia ambalo kwa sasa inaelemea wilaya hizi za sasa yaani Manispaa ya Kinondoni na Manispaa ya Temeke.
2.      Ukuaji wa kasi wa jiji: Katika ukuaji wa kasi unaoendelea jiji la Dar es Salaam maeneo yaliyopo katika wilaya hasa ya Kinondoni na Temeke ndiyo ambayo yanaongoza pia katika ukuaji huo wa kasi wa kimakazi na shughuli za kiuchumi kama viwanda na uwekezaji. Hivyo kwa kuwa na Manispaa mpya mbili(Manispaa ya Ubungo na Manispaa ya Kigamboni) zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kusimamia vyema mipango miji, kuujenga vyema mji na kusimamia kihuduma.
3.       Uwepo wa mipango ya kuimarisha ukuaji wa jiji kupitia miji ya pembezoni “satellite cities”: tayari serikali imeweka dhamira ya kuimarisha ukuaji wa jiji kupitia satellite cities. Hivyo uwepo wa wilaya mbili yaani Kigamboni (Satellite city Kigamboni) na Ubungo (“Luguruni Satellite City” ndani ya Kata ya Kwembe na Kata ya Kibamba) zitamudu kusimamia vyema ujenzi imara wa satellite cities na pia kuwezesha wilaya zitakazoachwa kama wilaya ya Kinondoni kuwa na ahueni ya kuelemewa na kazi hivyo nazo kusimamia vyema mipango ya ujenzi wa satellite cities zilizomo ktk maeneo hayo

Tuesday, December 31, 2013

Kheri na fanaka kwa mwaka mpya 2014. Nimerudi!

Nimerejea toka kwenye mafungo na tafakari, kumradhi kwa wote mlionikosa simuni na mtandaoni. Nawatakia mwaka mpya wenye upendo na uadilifu

Sunday, December 1, 2013

Ujenzi wa Kituo cha Polisi Kata ya Sinza-Mchango wa Mfuko wa Jimbo



Ukaguzi nilioufanya katika Kata ya Sinza; ujenzi wa kituo cha polisi kwa fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo.

Mfuko wa Jimbo umetenga milioni 10; tayari umeshatoa milioni 3.5 zilizofikisha jengo mpaka hatua hiyo. Taratibu za utoaji fedha zilikwamisha mradi toka mwezi Mei mwaka 2013.

Wednesday, November 27, 2013

Taarifa kwa umma kuhusu serikali kupandisha bei ya umeme

Gazeti la Tanzania Daima Toleo na. 3280 la tarehe 26 Novemba 23 limenukuu kauli iliyotolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene wakati akizungumza na kipindi cha Kumepampazuka kilichorushwa na Redio One juu ya Serikali kupandisha bei ya umeme kama Shirika la Umeme (TANESCO) lilivyoomba.

Katika habari hiyo Simbachawene amenukuliwa akisema kwamba endapo kuna mwananchi yeyote atakayeona gharama za umeme ni kubwa ni vema akaamua kuwasha kibatari au akae giza. 

Rais Jakaya Kikwete anapaswa kumwagiza Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospter Muhongo kuwaomba radhi wananchi kwa kauli hiyo iliyotolewa na Naibu Waziri Simbachawene kwa niaba ya wizara anayoiongoza.

Aidha, ni vyema Rais Kikwete kwenye hotuba yake kwa taifa ya mwisho wa mwezi huu akawaeleza wananchi iwapo uamuzi huo wa kupandisha kwa mara nyingine bei ya umeme ndio utekelezaji wa ahadi ya maisha bora aliyoitoa kwa watanzania kuanzia kwenye uchaguzi wa mwaka 2005.

Hii ni kwa sababu kupandisha bei ya umeme kuna athari ya kuchangia katika ongezeko la gharama na ugumu wa maisha kwa kuwa shughuli za uzalishaji na maisha ya kila siku zinategemea kwa kiwango kikubwa nishati.

Thursday, November 21, 2013

Mgao wa umeme na uongo nyuma yake!

Mgawo huu wa umeme ni wa ufisadi wa kimikataba Songosongo/PAT na udhaifu wa Mpango wa Dharura wa Umeme; Bungeni Muhongo alinijibu uongo.

Mgawo wa Umeme ufisadi wa PAT na udhaifu wa ukarabati wa visima ulijulikana toka Julai na Novemba 2011; Prof Muhongo alisema uongo kuficha.

Trilioni 1 ilitumika kuficha uongo wa Prof Muhongo Mgawo wa Umeme kwenye manunuzi ya mafuta mazito; Ufisadi, PAT, visima, gesi umemshinda.

MgawowaUmeme Prof Muhongo alisema uongo mara 2 bungeni; 1. 28 Julai 2012 baada ya kumhoji kwenye hotuba 27 Jul http://mnyika.blogspot.com/2012/07/hotuba-ya-kambi-rasmi-ya-upinzani.html

Uongo wa mara ya 2 wa Prof Muhongo bungeni kuhusu MgawowaUmeme ni wa Mei 23 nilipohoji baada ya hotuba ya 22 Mei: http://mnyika.blogspot.com/2013/05/hotuba-ya-msemaji-wa-kambi-rasmi-ya.html

Halafu kwa maagizo ya IMF/WB wanataka kupandisha bei ya umeme kufidia ufisadi kukodi mitambo ya dharura/ununuzi mafuta na mikataba mibovu.

Thursday, October 24, 2013

Wednesday, October 16, 2013

Ujenzi wa Kisima cha Maji Safi-Msigani!


Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika alipotembelea ujenzi wa kisima cha maji kilichojengwa katika mtaa wa Msigani, Kata ya Msigani, ujenzi wa kisima hicho umechangiwa na fedha za mfuko wa jimbokiasi cha Tsh 3.5 milioni katika kumalizia ujenzi huo.

Thursday, September 12, 2013

Mnyika ahoji ziliko fedha za DECI

na Shehe Semtawa

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemtaka Gavana wa Benki Kuu, Benno Ndulu, kuwaeleza waliokuwa wanachama wa Kampuni ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI) fedha zao zilizotaifishwa na serikali kutoka kwenye taasisi hiyo ziko kwenye akaunti gani.

Mnyika alisema kuwa wakati sakata la DECI linaanza mwaka 2009, serikali ilitaifisha jumla ya sh bilioni 19, sawa na asilimia 40 ya fedha zote ambazo wanachama wa taasisi hiyo iliyokuwa ikiendesha na kusimamia mchezo wa upatu walikuwa wakidai.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara juzi Mtaa wa Mavurunza, Kata ya Kimara baada ya kuulizwa swali na mmoja wa wananchi aliyetaka kujua hatima ya fedha zao, Mnyika alitoa tahadhari kuwa danadana inayotaka kufanywa na serikali inaweza kutia shaka kuwa fedha hizo hazipo.

”Sasa naomba nimjibu yule mwananchi aliyetaka kujua hatima ya fedha za DECI. Mtakumbuka hili suala nimekuwa nikitaka majibu yake bungeni, lakini kila mara wanatumia kisingizio kuwa suala hili liko mahakamani.

Tuesday, September 10, 2013

Mnyika: Serikali imalize tatizo la maji

na Abdallah Khamis

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, ameitaka serikali kuhamisha nguvu na kasi zilizotumika katika ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuelekea jijini Dar es Salaam na kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi hususan katika Jimbo la Ubungo.

Mnyika alitoa kauli hiyo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Mavurunza na kusisitiza hakuna suala muhimu kama maji kwa wananchi na kwamba kunahitajika ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu, ikibidi kwa hali ya dharura.

Alisema kama serikali inaweza kutumia muda mfupi kujenga na kutandaza bomba hilo kwa nini ishindwe kufanya hivyo kwa mabomba ya maji, ambayo ni uhai wa wananchi.

“Tunaendelea kupambana kuhakikisha tatizo la maji tunalipunguza na kuliondoa kabisa, ninachowaomba ni sauti zenu na mshikamano wenu, suala hili ni uhai wa watu, kama maji ni tatizo maana yake uhai wa binadamu uko shakani,” alisema Mnyika.

Wednesday, August 28, 2013

Uzinduzi wa Kampeni ya Kuchangia Maabara na Madawati chini ya Shirika la UDI



Mhe. John Mnyika akishirikiana na Mratibu John Mallya kuonyesha bango lenye ujumbe wa harambee ya kuchangia maabara na maktaba iliyozinduliwa Agosti 21, 2013

Thursday, August 15, 2013

Leo Agosti 15, 2013: Sengerema na Mwanza Mabaraza ya wazi ya Katiba Mpya

Sengerema: Endeleeni kutoa maoni kwa maneno na maandishi kwenye baraza letu la katiba linaloendelea uwanja wa Wenje kata ya Nyamburukano

Mwanza: Baraza la wazi la Jiji likijumuisha pamoja Wilaya za Ilemela na Nyamagana litaanza saa 9 alasiri Uwanja wa Magomeni kata ya Kirumba.

Mwenyekiti Mbowe na mimi tutashiriki katika michakato hiyo.

Maslahi ya Umma Kwanza!!

Monday, August 12, 2013

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; tukutane tushiriki mabaraza ya wazi ya katiba.

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; ni kushiriki kikamilifu baraza la wazi la katiba. Mwenyekiti Mbowe na mimi tutajumuika nanyi kupitia rasimu ya katiba mpya.

Busega: Baraza la wazi la katiba leo litaanza saa 3 asubuhi.

Maswa: Wanachana na wapenzi hudhurieni baraza la wazi la katiba kuanzia saa 5 kamili

Meatu: mtaanza baraza la wazi la katiba saa 7 mchana. Wanachama na waalikwa mkifika anzeni kutoa maoni yenu juu ya rasimu; tuko pamoja!

Bariadi: ni haki na wajibu kushiriki baraza la wazi la katiba leo tarehe 13 Agosti kuanzia saa 9 alasiri.

Shime tushiriki kikamilifu na kuitumia fursa hii kwa maslahi ya taifa letu.

Thursday, August 8, 2013

Salamu za Eid-Al-Fitr na kutembelea kata ya Malamba Mawili!

Saa 5 mpaka 8 mchana nitakuwa pamoja na viongozi wenzangu Malamba Mawili (Eneo la Stendi Mwisho). Tutagawa zawadi kwa watoto pamoja na kutoa salamu za Eid-Al-Fitr. Tutasambaza nakala za rasimu ya katiba mpya vijiweni na kwa wawakilishi wa makundi ya kijamii yenye malengo yanayofanana.

Tunaanza muda huo ili kuheshimu wajib wa salaat ya Eid na sunnah ya khutbah asubuhi. Imekuwa ni kawaida kwa siku ya Eid kuwa pia ni wasaa kwa kusikiliza hotuba juu ya wajibu kwa Allah lakini pia kwa binadamu wengine. Ni wakati wa ummah kukumbushwa masuala muhimu katika jamii. Tunamaliza mapema kutoa fursa ya mikusanyiko mingine.

Nitazungumza na umma kuhusu mchakato wa katiba na kutoa pia mrejesho juu ya masuala ya maendeleo ikiwemo juu ya ujenzi/matengenezo ya Barabara ya Kinyerezi-Malamba Mawili Mbezi, kuhusu maji na juu ya masuala mengine muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Kwa wakazi wa maeneo jirani yanayozunguka Malamba Mawili ya Kifuru, King’azi, Msingwa, Msigani na mengineyo mnaweza kuja kujumuika nasi. 

Kwa maelezo zaidi na maelekezo naomba muwasiliane na Ali Makwilo 0715/0784691449.

Eid Mubarak!

Kwa mkazi wa Kisopwa, Sinza, Manzese, Mbezi Makabe, Malambamawili, Mshikamano au Msigani; naomba usome hapa na kunipa mrejesho juu ya ardhi na mipango miji

Tarehe 12 Julai 2012 katika mchango wangu bungeni ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kuwawakilisha wananchi na kuisimamia Serikali niliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na mambo mengine:

Itatue mgogoro kati ya Manispaa ya Kinondoni na Halmashauri ya Kisarawe kuhusu wananchi wa Kisopwa na Mloganzila kuitwa kwamba wako Kisarawe badala ya Kinondoni.

Ichukue hatua juu ya maeneo ya wazi/umma yaliyovamiwa katika kata ya Sinza ambapo mabango yamewekwa, muda wa notisi umeisha lakini majengo bado yapo.

Imtaje wazi mwendelezaji mwenza wa Mji wa kiungani (satellite town) wa Luguruni, masharti ya mkataba na lini uendelezaji unaanza.

Itoe nakala ya mipango ya uendelezaji upya kata ya Manzese.

Iharakishe mipango ya uhakiki na urasimamishaji katika maeneo ya Mbezi Makabe, Malamba Mawili, Mshikamano na Msigani.

Mwaka mmoja umepita, kuna mambo nimepewa na majibu na kazi imefanyika na kuna masuala bado.

Mkazi wa Mabibo na maeneo jirani nakutaarifu kuwa nitahutubia mkutano wa hadhara kwenye eneo la Sahara leo siku ya 8/8 kuanzia saa 9 alasiri mpaka 11 jioni ulioandaliwa na chama. Njoo na waalike na wengine.

Mkutano huo una malengo matatu: Mosi; kuwasilisha mrejesho wa kazi jimboni za utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyogharamiwa na Mfuko wa Jimbo katika maeneo yenu.

Pili; nitafanya kazi ya kuuchambua mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea ikiwemo kuhusu rasimu ya katiba mpya.

Tatu; kupokea maoni/mapendekezo ya masuala muhimu ya kuyazingatia katika kazi ya kuwawakilisha wananchi kwenye vikao vya kamati za Bunge vinavyoanza wiki ijayo na Mkutano wa Bunge unaoanza mwishoni mwa mwezi huu.

Itakumbukwa kwamba tarehe 21 Julai 2013 nilitaka kutimiza azma hiyo kwenye eneo tajwa lakini Jeshi la Polisi lilizuia mkutano kwa maelezo yasiyokuwa ya kweli kwamba kulikuwa na ziara ya Makamu wa Rais katika Jimbo la Ubungo.

(Msaidizi katika Ofisi yangu ameeleza hapa kwa kirefu: http://www.youtube.com/watch?v=VyHF5O-P-Vk&feature=c4-overview&list=UUs0TcFkgqs2OYd6x5E68nhg ).

Nitashiriki kwenye Iftar nyumbani kwa Marehemu Mbwana Masoud Makurumla leo 8/8 jioni; wasiliana na Aziz (OMU) 0784/0715-379542 kutuunga mkono kwa hali na mali. Ramadan Kareem.

Kwa ndugu zangu na wenzetu waislamu, ni siku ya 30 ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan. Siku ya 30 ni kati ya siku kumi za mwisho za mfungo ambazo wapo wanaomini kwamba usiku ni siku ya “usiku wa nguvu”. Siku na usiku ambao Mtume Muhammad (SAS) alipokea ufunuo wa kwanza wa Q’uran yaani Laylat al-Qadr.

Katika siku hii ya 30 nitaungana pamoja na familia ya Marehemu Mbwana Masoud, majirani zake wakazi wa Kata ya Makurumla na wengine mtakaojumuika nami katika Iftar nyumbani kwa familia ya marehemu . Jioni tutaanza na tende na futari itafuata baada ya swala ya maghrib.

Marehemu Mbwana Masoud alikuwa ni mmoja wa wanachama wa CHADEMA walijitolea kusafiri kwenda Igunga kwa ajili ya kuwa wakala kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 2 Oktoba 2011.

Monday, July 29, 2013

Hali tete na tata ya kituo cha mabasi cha Ubungo (UBT)- Hatua ambazo nimeanza kuzichukua

Katika siku za karibuni nimepokea malalamiko kuhusu hali tete na tata katika Kituo cha Mabasi cha Ubungo (UBT) kinachosimamiwa na kuendeshwa na Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam. 

Kufuatia malalamiko hayo, nimechukua hatua zifuatazo mpaka sasa: Mosi, tarehe 15 Julai 2013 nilifanya ziara ya ghafla kujionea hali halisi, sehemu ya ziara hiyo inaweza kutazamwa kupitia: 
http://www.youtube.com/watch?v=JuPGoz-JI-I , ambapo nilibaini kwamba hatua za haraka zinahitajika. 

Nimeshuhudia hali ya uchafu ikiwemo utiririkaji wa maji machafu ndani ya Kituo cha Mabasi ambayo yanatuama na hadi kubadilika rangi na kuwa ya kijani ambapo ni hatarishi kwa abiria na watu wanaofanya shughuli zao ndani ya kituo. Pia, kuna vyoo vichache ukilinganisha na idadi ya abiria na watumiaji wengine wa Kituo. Hali hiyo inaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko.

Nimejulishwa hali ya usalama ndani ya kituo ni tete; usalama ndani ya kituo ni mdogo sana kwa abiria na nimepewa taarifa za matukio ya uhalifu ambayo yamesababisha pia madhara kwa abiria.

Nimetembelea kituo na kukuta kuna usumbufu mkubwa sana kwa abiria na watumiaji wengine wa Kituo baada ya maeneo ya awali ya kupumzikia kwa abiria na wasindikizaji kubomolewa. 

Thursday, July 25, 2013

Chenge (Mb) amesema kodi ya kadi za simu (SimCardTax) ni sahihi kwa utafiti wao; aulizwe kupitia 0754782577 atoe maelezo zaidi na vielelezo vya ziada

Leo tarehe 25 Julai 2013 chombo kimoja cha habari kimemnukuu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Andrew Chenge (Mb) akisema kwamba uamuzi kuhusu kodi/tozo ya kadi/laini za simu haukuwa wa kubahatisha. Chenge amesema kwamba kamati yake ilifanya utafiti wa kina na kisha kufikia uamuzi wa kuona tozo hiyo ni sahihi.

Ni muhimu akatakiwa kupitia namba yake 0754782577 atoe maelezo zaidi kuhusu usahihi wa tozo hiyo na aeleze ni wapi wananchi na wadau mbalimbali wanaweza kupata vielelezo vya utafiti walioufanya.

Aidha, wenye maswali kuhusu nini hasa kilijiri kwenye kamati ya bajeti mpaka kamati hiyo ikakataa jedwali la marekebisho nililowasilisha tarehe 27 Juni 2013 kabla ya muswada wa sheria ya fedha kupitishwa bungeni tareheb 28 Juni 2013 kwa kuwa yeye ambaye ndiye msemaji wa kamati ameanza kutoa majibu. 

Pia, aeleze iwapo yupo tayari kumshauri Spika aruhusu kamati ya bajeti ikutane kwa dharura wiki ijayo kufanya kazi ya kupitia matumizi ya Serikali kwa lengo la kuanisha maeneo ambayo Serikali inaweza kubana matumizi kwa haraka kufidia pengo la bilioni 178 zinazotafutwa kwenye tozo hiyo ya simu. Hatua hii itawezesha kodi hiyo kuacha kutozwa bila ya kulazimika hata kuongeza vyanzo vingine vya fedha iwapo Serikali inasuasua kupanua wigo wa mapato.

Friday, July 19, 2013

Kufuatia kauli za Serikali magazetini kuhusu mimi na kodi ya umiliki wa kadi za simu; nijibu tu kwa ujumla kwamba SITAACHA. Badala yake naomba kuwapatia namba zao: Makamba 0767783996 na Mgimwa 0754/0684765644, tunachohitaji ni kauli ya Serikali kuwa kodi imesitishwa na itaondolewa na sio siasa chafu.

Kwa mliotaka msimamo wangu juu ya kauli ilinukuliwa jana tarehe 18 Julai 2013 na Gazeti la Majira kwamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba kwamba; “Mnyika anaangalia upepo unakoelekea, akiona watu wanalalamika ndipo anaongea namsihi aache kufanya siasa katika jambo hili”, naomba kutumia mtandao huu kutoa majibu ya ujumla kwa maswali na masuala yote kama ifuatavyo:

Nieleze kwamba sitaacha kufanya siasa kwenye jambo hili mpaka kodi hiyo itakapofutwa kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kubaki na fedha walau kidogo kwa maendeleo.

Sitaacha kufanya siasa kwa sababu ndio kazi yangu ambayo wananchi walinichagua kuifanya ya kuwawakilisha na kuisimamia Serikali ambayo yeye Makamba ni sehemu yake. Sitaacha kufanya siasa kwa sababu Mwalimu Nyerere alisema ili nchi yetu iendelee inahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Ambacho sitafanya ni siasa chafu kama hizo ambazo Makamba amefanya za kusema uongo, kwa kuwa naamini anafahamu kabisa kwamba sijaanza kuongea kuhusu suala hili baada ya malalamiko ya wananchi bali jambo hili nilianza kulishughulikia bungeni mara baada ya Waziri wa Fedha kuwasilisha jedwali la marekebisho la kuanzisha kodi lukuki za simu ikiwemo hii. Katika mchango wangu bungeni, nieleza kwamba muswada huo wa sheria ya fedha kwa kupandisha kodi kwenye mafuta na simu ni ‘muswada wa majanga ya kuwaongezea mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi.

Wednesday, July 17, 2013

Kodi ya kadi ya simu (SimcardTax): Maoni ya awali ya wananchi juu ya hatua za kuchukuliwa

Nawashukuru kwa maoni ambayo mmenitumia kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa kufuatia kuanzishwa kwa ushuru wa bidhaa kwa kadi za simu (sim card) kwa wamiliki wa simu za kiganjani/mkononi.

Bado naendelea kuchambua maelfu ya maoni yaliyotolewa katika mijadala na niliyotumiwa kwa barua pepe. Nitoe mrejesho wa awali kwamba kwa muktasari mapendekezo niliyoyachambua mpaka sasa yanapendekeza hatua zifuatazo kuchukuliwa:

Monday, July 15, 2013

Mnyika aponda sera za michezo za CCM

Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika amesema ukosefu wa maandalizi ya mapema katika micheo kunatokana na sera za Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndiko kunakoibua matokeo mabovu katika sekta hiyo hususan kwa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars.

Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, aliyasema hayo jana wakati akizindua michuano ya Mama Kevin Cup kwenye viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chang’ombe (DUCE), jijini Dar es Salaam.

Mnyika alisema katika ilani ya uchaguzi ya Chadema 2010, waliahidi masualaya michezo hususan Tanzania kucheza fainali za Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia Brazil mwakani endapo wangekabidhiwa cnchi, lakini kutokana na baadhi ya maeneo kutowataka waingie serikali mpya, hayo yameshindikana chini ya sera mbovu za CCM.

Saturday, July 13, 2013

Mkutano wa hadhara leo Julai 13, 2013 Dar es Salaam!

Msimamo wetu kuhusu rasimu ya katiba mpya na mustakabali wa taifa utatolewa leo Jumamosi ya Julai 13, 2013 kwenye mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Ukombozi-Manzese kuanzia saa 8 mchana.

Hotuba zitatolewa na viongozi mbalimbali wakiwemo Dr.W.Slaa, T.Lissu, M.Marando nk nathibitisha nami nitakuwapo kuwakaribisha Jimboni Ubungo.

Wananchi wote mnakaribishwa. Njoo wewe, njoo na yule!

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli!

Muhimu: Shule ipo jirani na Manzese TipTop. Maelekezo wasiliana na: M/Kt wa Kata ya Manzese Ali Makwilo 0784-691449 au 0715-691449 au 0769-658593

Thursday, July 11, 2013

KAULI YA WAZIRI WA FEDHA KUHUSU KODI YA LINE ZA SIMU NI KIELELEZO CHA UDHAIFU WA SERIKALI NA UZEMBE WA BUNGE; NIANDIKIE SASA KUHUSU HATUA ZA KUCHUKUA JUU YA SUALA HILI KUPUNGUZA MZIGO WA GHARAMA ZA MAISHA KWA WANANCHI

Katika kipindi cha Hot Mix cha EATV muda mfupi uliopita Waziri wa Fedha amesema kwamba mawazo ya kutoza elfu moja kwa mwezi kwenye kila laini ya simu ni ya wabunge. 

Kauli inayokaribiana na hiyo imewahi kuandikwa pia na Naibu Waziri wa Wizara yenye dhamana na sekta mawasiliano kwenye mitandao ya kijamii katika siku za karibuni. Baadaye alifuata Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na sasa waziri mwenyewe. Mwaka 2012 nilitahadharisha kuhusu udhaifu wa Rais (na Serikali) na uzembe wa Bunge katika masuala yanayohusu maandalizi ya bajeti, hususan kutozingatiwa kwa mpango wa taifa wa maendeleo na ongezeko la mara kwa mara la gharama za maisha kwa wananchi. Kwa kauli hizi za Serikali udhaifu na uzembe huo unaendelea kujihidhirisha.

Kauli hizi za Serikali ni za kujivua mzigo wa lawama baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu kodi hii na nyinginezo kwa kuhamisha mzigo huo kwa wabunge.

Ni muhimu badala ya kutoa kauli za ujumla za kulaumu wabunge, Serikali ijitokeze itaje kwa majina na wabunge gani hasa walitoa mawazo hayo. Mimi sijawahi kutoa wazo hilo wala kuliridhia. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwenye Hotuba yake juu ya Muswada wa Sheria ya Fedha ilipinga pendekezo hilo lililokuwepo katika jedwali la marekebisho lililowasilishwa na Wizara ya Fedha. Katika kuhakikisha kwamba kifungu hicho hakipitishwi, niliwasilisha jedwali la marekebisho ya sheria kutaka kifungu hicho kiondolewe katika muswada wa sheria ya fedha na marekebisho yake yaliyowasilishwa na Serikali.

Wednesday, May 22, 2013

Maoni na Mapendekezo ya CHADEMA juu ya Rasimu Muongozo uliotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuhusu Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi yenye mlengo yanayofanana


1.0. UTANGULIZI 

Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83 (kifungu cha 18 (3)) imetoa wajibu kwa tume wa kuunda Mabaraza ya Katiba kwa ajili ya kupitia na kutoa maoni juu ya Rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Tume.

Kifungu cha 17 (8) kinaeleza kuwa, isipokuwa kama mazingira yatahitaji vinginevyo, Tume itabuni utaratibu unaofanana ambao utatumika kila upande wa Muungano. 

Kifungu cha 18 (6) kinaeleza aina nyingine ya Mabaraza ya Katiba kwa kueleza kuwa Tume inaweza kuruhusu Asasi, Taasisi au Makundi ya Watu kuwasilisha maoni yao kuhusu Rasimu ya Katiba. 

Ikumbukwe kwamba Kamati Maalum ya CHADEMA ilikutana na Tume ya Mabadiliko ya Katiba tarehe 7 Januari 2013 kuwasilisha maoni ya CHADEMA kuhusu katiba mpya kama ilivyoalikwa lakini pia kutumia fursa hiyo kuwasilisha mapendekezo ya CHADEMA kuhusu marekebisho na maboresho yanayohitajika kuhusu mchakato wa mabadiliko ya katiba ili kupata katiba bora. 

Tarehe 31 Januari 2013 Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilitoa taarifa kwamba imeamua kuwa Mabaraza ya Katiba yatakuwa katika makundi mawili yafuatayo: Mabaraza ambayo Tume itayasimamia na kukusanya Maoni (Mabaraza ya Katiba ya Wilaya – Ngazi ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa) na Mabaraza ambayo Tume haitayasimamia. Mabaraza hayo yatajisimamia yenyewe na kukusanya maoni yatakayowasilishwa kwenye Tume kwa mujibu wa maelekezo. (Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi ya Watu). 

CHADEMA baada ya kupitia muongozo huo na kwa kuzingatia kuwa tayari tume ilishafanya uamuzi kuwa mabaraza ya katiba yatakuwa ya wilaya, tarehe 14 Februari 2013 kiliwasilisha maoni na mapendekezo yake kuhusu uteuzi wa wajumbe ambayo kwa sehemu kubwa hayakuzingatiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na hivyo kusababisha matatizo makubwa katika mchakato mzima wa uteuzi wa mabaraza ya katiba ya wilaya. 

Kufuatia hali hiyo katika Maoni ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu hoja ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tulitangaza kwamba CHADEMA itajitoa ushiriki wake katika mchakato wa Katiba Mpya endapo mambo yafuatayo hayatapatiwa ufumbuzi hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2013: 

HOTUBA YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA NISHATI NA MADINI JOHN JOHN MNYIKA (MB) KUHUSU MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI JUU YA MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2012/2013 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

(Inatolewa chini ya kanuni ya 99(9) toleo la mwaka 2013)


A: UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Waziri wa Nishati na Madini ilianzishwa kwa mujibu wa kipengele cha 21 cha Nyongeza ya Waraka wa Rais uliochapishwa kama Tangazo la Serikali Na. 494 la tarehe 17 Desemba 2010. Majukumu ya Ofisi hii yameainishwa katika Tangazo la Ukasimishaji wa Majukumu ya Kiuwaziri la mwaka 2010 (The Ministers [Assignment of Ministerial Functions] Notice, 2010) lililochapishwa katika Gazeti la Serikali kama Tangazo la Serikali Na. 494A la tarehe 17 Desemba 2010.

Mheshimiwa Spika, Katika kujadili Mapitio ya Utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2012/2013 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2013/2014 naomba tuyatafakari maandiko ya katika muktadha wa uongozi wetu wa leo na hatma ya sekta hizi mbili muhimu za nishati na madini.

Mheshimiwa Spika, Mwalimu Nyerere katika kitabu chake cha TUJISAHIHISHE katika ukurasa wa pili tutafakari kwamba, naomba kumnukuu ‘ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo; haujali adui wala rafiki. Kwake wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa.Ukiniona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa nafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nitalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa.


Mheshimiwa Spika, Tuendelee kutafakari maandiko ya Nyerere kwamba ‘Wakati mwingine, mtu tunayempinga huwa anamakosa kweli, lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake.Nikisema mbili na tatu ni sita, nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nilifikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha.Ni kweli mbili mara tatu ni sita;lakini mbili na tatu ni tano, siyo sita. Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema kuwa meno yangu ni machafu ,au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana, Huu ni mfano wa upuuzi; lakini mara nyingi hoja tunazozitumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda,au kukubali mawazo yetu, huwa hazihusiani kabisa na mambo tunayojadili’.

Sunday, May 19, 2013

Waraka kuhusu muswada wa Baraza la Vijana la Taifa wa Mwaka 2013

Vijana wenzangu na wote wenye dhamira ya kuwezesha maendeleo ya vijana nchini, salaam! 

Mtakumbuka kwamba mwezi Januari 2013 nilitoa taarifa kwa umma ya kueleza kuwa niliwasilisha kwa Katibu wa Bunge Muswada Binafsi wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa na kuomba hatua za ziada toka ofisi ya Bunge kwa kuzingatia Kanuni ya 21 na Kanuni ya 81 ya Kanuni za Kudumu za Bunge. 

Toka wakati huo muswada huo mpaka sasa Mei 2013 haujachapwa katika gazeti la Serikali na nimepokea barua toka kwa ofisi ya Bunge kwamba wamepokea ushauri toka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa muswada huo hauwezi kuchapishwa katika gazeti la Serikali kwa kuwa umekiuka masharti ya ibara ya 99 ya Katiba ya Nchi. 

Sababu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoa ushauri huo ni kuwa muswada unalenga pamoja na mambo mengine kupitia kifungu cha 31 kipengele cha kwanza kuanzisha Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa madhumuni ya kugharamia shughuli za baraza la vijana la taifa, mipango ya baraza na kutekeleza miradi ya vijana kwa ajili ya maendeleo ya vijana. 

Kwa maoni yangu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametoa ushauri huo bila kuzingatia kwamba kifungu cha 31 kipengele cha pili kinataja vyanzo mbalimbali vya fedha za mfuko ikiwemo kutaja kuwa fedha za mfuko zitatokana na fedha zilizotengwa na Serikali na Bunge kwa ajili ya Baraza kwa mujibu wa Ibara ya 135 kifungu cha pili cha katiba ya Nchi.

Monday, March 25, 2013

Mnyika na harakati za kuhakikisha Maji ndani ya Jimbo la Ubungo

21 Machi, 2013 Mnyika aitwa Ikulu, JK awakumbuka Mabwepande
na Asha Bani

HOJA ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) kuhusiana na suala la tatizo la upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Dar es Salaam, inaelekea kupata ufumbuzi kutokana na Rais Jakaya Kikwete kumuita Ikulu mbunge huyo Jumatatu wiki ijayo.

Wengine walioitwa kukutana na rais ni Mkuu wa Mkoa, Mecky Sadick, wakuu wote wa wilaya pamoja na wabunge na wataalamu kutoka Wizara ya Maji.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa daraja la Mtaa wa Golani, Kata ya Saranga, Rais Kikwete alisema kuwa kutokana na wananchi wa kata hiyo kupiga kelele kuhusiana na suala la maji ameamua kukutana na viongozi hao ili kupatiwa ufumbuzi.

Mwaliko wa kushiriki ufuatiliaji wa mradi wa maji na mkutano wa mbunge na wananchi katika kilele cha wiki ya maji kitaifa na siku ya maji kimataifa leo tarehe 22 Machi Mtaa wa Makoka kata ya Makuburi.

Leo tarehe 22 Machi ni kilele cha wiki ya maji kitaifa na siku ya kimataifa ya maji. Katika kazi zake ikiwa ni sehemu ya siku hiyo Mbunge wa Ubungo John Mnyika saa 9 alasiri atakuwepo eneo la Uluguruni Mtaa wa Makoka Kata ya Makuburi kufanya ufuatiliaji wa mradi wa maji.

Mradi umetekelezwa kwa ushirikiano na Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) baada ya kuchochewa kwa kuchangiwa milioni kumi na Mfuko wa Maendeleo (CDCF) Jimbo la Ubungo ambao Mnyika ni mwenyekiti wake pamoja na kuunganisha nguvu za wananchi katika maeneo husika.

Aidha, baada ya kukagua mradi huo kuanzia saa 10 Jioni mbunge atafanya mkutano na wananchi kwa ajili ya kutoa ujumbe kuhusu hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jiji la Dar Es Salaam zinazopaswa kuchukuliwa hata baada ya wiki ya maji.

Pia kufuatia mwaliko wa Rais Jakaya Kikwete wakukutana tarehe 25 Machi 2013 na Mkuu wa Mkoa, DAWASA, DAWASCO, Mnyika na wabunge wengine wa Mkoa wa Dar es Salaam kujadili hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji, mbunge atatumia mkutano wake na wananchi kusikiliza maoni na mapendekezo kuhusu hatua za ziada zinazopaswa kuchukuliwa.

Imetolewa tarehe 22 Machi 2013 na: 

Gaston Shundo 

Afisa katika Ofisi ya Mbunge Ubungo

Picha za Uzinduzi wa Daraja la Suka-Golani!

















Tujikumbushe harakati na jitihada mbalimbali ambazo zilifanywa mpaka kufikia hatua ya sasa kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora ya miundombinu ya barabara ya Suka-Golani hapa:

1 May, 2012  Daraja Golani-Suca na Barabara Mburahati-Mabibo

Mkandarasi aliyepewa zabuni ya ujenzi wa daraja la Golani-Suka anapaswa kuanza mapema ujenzi wa daraja hilo muhimu linalounganisha kata za Kimara na Saranga ili kupunguza kero kwa wananchi hasa wakati wa mvua.

Mwezi huu wa Aprili nimefuatilia kuhusu hatma ya daraja hilo na hatimaye mkataba wa ujenzi wa daraja husika umesainiwa kati ya Manispaa ya Kinondoni na Mkandarasi Kika Co. Ltd kwa gharama za shilingi milioni 447.

Hata hivyo, ujenzi wa daraja husika haujaanza suala ambalo linahitaji Manispaa ya Kinondoni kumsimamia kwa karibu mkandarasi husika ili ujenzi uanze kwa haraka kwa kuwa mchakato wa zabuni ulianza kuanzia mwanzoni mwa mwaka 2012.

Izingatiwe kwamba kutokuwepo kwa daraja katika eneo hilo mwaka miaka mingi kumefanya mawasiliano katikati maeneo hayo kuwa magumu nyakati za mvua na kusababisha madhara ya kibinadamu na mali wananchi wanapovuka mto katika eneo hilo wakati wa mafuriko.

Baada ya kuwawakilisha wananchi kutaka ujenzi wa daraja hilo lilingizwa kwenye bajeti ya Manispaa ya Kinondoni kwa mwaka wa fedha 2011/2012 hata hivyo miezi ikiwa imebaki takribani miwili kabla ya mwisho wa bajeti husika ujenzi wa daraja hilo ulikuwa haujaanza bado.

Hatua kama hiyo inahitajika pia kwa barabara ya Mburahati mpaka Mabibo NIT ambayo inapaswa kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami ikiwa imetengewa kiasi cha shilingi milioni 504 kwa ajili ya kuchangia katika kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Morogoro . 

Tathmini ya utekelezaji wa bajeti inaonyesha kwamba kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ni ndogo pengo ambalo linapaswa kuzibwa kwa kusimamia kwa karibu miradi inayopaswa kuanza katika muhula uliobaki wa mwaka wa fedha 2011/2012.

Rejea: http://mnyika.blogspot.com/2012/05/daraja-golani-suca-na-barabara.html 


January 27, 2012 Kuhusu Msongamano wa Magari DSM na Ziara Kwembe: http://mnyika.blogspot.com/2012/01/kuhusu-msongamano-wa-magari-dsm-na.html

Thursday, March 21, 2013

MNYIKA ATAKA KAULI YA RAIS KIKWETE KUHUSU UJENZI WA MACHINGA COMPLEX NA JUMBA LA VIWANDA VIDOGO JIMBONI UBUNGO

Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika ametoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kueleza sababu za kutokutekelezwa mpaka sasa kwa ahadi zake alizotoa mwaka 2010 za ujenzi wa Machinga Complex na jumba la viwanda vidogo katika jimbo hilo kuchangia katika kupanua wigo wa ajira kwa vijana. 

Mnyika aliyasema hayo akijibu swali la mwakilishi wa vijana katika mkutano wake na wananchi alioufanya katika ofisi za Serikali ya Mtaa wa Muungano katika kata ya Manzese uliofanyika mwishoni mwa wiki (16/03/2013). 

Mwakilishi huyo wa vijana alitaka kufahamu hatua ambazo mbunge amechukua kufuatilia kuhusu maeneo ya kufanyia biashara kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo katika jimbo la Ubungo. 

“Kazi ya mbunge ni kuwawakilisha wananchi na kuisimamia serikali ili kuwezesha utatuzi wa kero, matatizo ya maeneo ya wafanyabiashara ndogo ndogo yamedumu kwa muda mrefu kutokana na udhaifu katika mipango miji na hivyo maeneo ya wafanyabiashara na masoko kuuzwa, kuvamiwa au kuwa machache. Nimefuatilia suala hili, kuna ambao wamepata maeneo na wengine wengi bado”, alijibu Mnyika.

Wednesday, March 20, 2013

RUFAA DHIDI AGIZO LA ACP CHARLES KENYELA KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA KIPOLISI WA KINONDONI KUZUIA MKUTANO WA HADHARA WA MBUNGE NA WANANCHI TAREHE 16 MACHI 2013



Kumb. Na. OMU/US/003/2013                                                                                               18/03/2013 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
S.L.P 9223, 
Dar es Salaam. 

Mheshimiwa: 


RUFAA DHIDI AGIZO LA ACP CHARLES KENYELA KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA KIPOLISI WA KINONDONI KUZUIA MKUTANO WA HADHARA WA MBUNGE NA WANANCHI TAREHE 16 MACHI 2013 


Kwa barua hii nawasilisha rasmi rufaa kwa kutumia kifungu cha 43 (6) cha Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma za Polisi wasaidizi sura ya 322 (The Police Force and Auxilliary Service Act Cap 322 RE 2002) dhidi ya agizo la ACP Charles Kenyela Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni kuzuia mkutano wa hadhara wa mbunge na wananchi tarehe 16 Machi 2013. 

Katika kushughulikia rufaa hii zingatia kuwa tarehe 4 Machi 2013 niliwasilisha taarifa kwake kwa mujibu wa kifungu cha 4 cha Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge na. 3 ya mwaka 1988 (The Parliamentary Immunities, Powers and Privileges Act) kuwa tarehe 16 Machi 2013 nilipanga kufanya mkutano na wananchi Jimboni. 

Katika taarifa hiyo kupitia barua yangu yenye Kumbu. Na. OMU/US/001/2013 ambayo nilitoa pia nakala kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Afisa Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Afisa Mtendaji wa Kata ya Manzese na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Muungano, nilieleza kwamba mkutano huo nilipanga kuufanya katika Kata ya Manzese Eneo la Bakheresa kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 5 Asubuhi. 

Katika taarifa hiyo nilieleza kwamba lengo la mkutano huo ni kuwapa mrejesho wananchi kuhusu masuala niliyoyawasilisha katika Mkutano wa Kumi wa Bunge uliomalizika tarehe 08 Februari 2013 na kupokea mambo ya kuyazingatia kuelekea Mkutano wa Kumi Na Moja wa Bunge unaotarajiwa kuanza tarehe 9 Aprili 2013. 

Hata hivyo, kupitia mkutano wake na vyombo vya habari tarehe 14 Machi 2013 na barua yake iliyoletwa ofisini kwangu tarehe 15 Machi 2013, ACP Charles Kenyela Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni alitoa agizo la kuzuia mkutano wa hadhara wa mbunge na wananchi niliopanga kuufanya tarehe 16 Machi 2013. 

Katika agizo hilo alilolitoa chini ya kifungu cha 43 (2) na 43 (3) Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma za Polisi sababu iliyohusu mkutano kwa mujibu wa barua yake yenye Kumb. Na. DSM/KINONDONI/SO.7/2/CHADEMA/284 ni: 

“Eneo la Manzese Bakhresa ambalo unakusudia kufanyia mkutano siyo eneo halali kwa ajili ya mikutano. Eneo hilo kwa mujibu wa maelekezo ya Manispaa ya Kinondoni kupitia mipango miji ni eneo linalotumika kwa ajili ya kuegesha magari makubwa (malori) na ndio maana liko katika eneo kuu la barabara ya Morogoro ambayo iko katika matengenezo. Kuruhusu mkutano wako kufanyikia hapo ni kukiuka sheria ya mipango miji ya Manispaa ya Kinondoni pamoja na kuingilia shughuli za ujenzi wa barabara unaoendelea hivi sasa na kuwabugudhi watumiaji wengine wa eneo hilo”.

Tuesday, March 19, 2013

LEO NDIO MWISHO; OMBA UWAKILISHI KWENYE MABARAZA YA KATIBA SASA

Leo tarehe 20 Machi 2013 ni siku ya mwisho ya wananchi kuwasilisha maombi ya kuwa wajumbe wa mabaraza ya katiba ya ngazi ya wilaya ambayo yana wajibu muhimu wa kupitia rasimu ya katiba na kutoa maoni iwapo imezingatia maoni ya wananchi yaliyokunywa katika hatua ya wananchi binafsi na makundi mbalimbali katika jamii. 

Nawakumbusha ambao bado hamjawasilisha maombi na mna dhamira ya kutimiza wajibu huu wa kiraia na kikatiba kwa kuwasilisha barua ya maombi kwa watendaji wa mitaa/vijiji. 

Kuna nafasi nane kwa kila mtaa kwa Dar es salaam, nne kwa maeneo mengine ya Tanzania Bara katika makundi yafuatayo; mwanamke, kijana, mtu mzima na mtu mwingine yoyote: kwa Zanzibar tatu kwa kila shehiya. 

Sifa ni raia, miaka 18 au zaidi mwenye kujua kusoma, kuandika, hekima, busara, uadilifu, uwezo wa kujieleza na kupambanua mambo ambao najua wengi mnazo. Sifa nyingine ni kuwa mkazi wa kudumu kwenye mtaa au kijiji ambayo haimaanishi kwamba ni lazima uwe mwenye nyumba, hata wapangaji mnaruhusiwa kuomba. Sio lazima uwe mwanachama wa chama chochote cha siasa na uteuzi wa awali utafanywa na mkutano mkuu wa mtaa wenu au kijiji chenu ambao wajumbe ni wakazi wote wa mtaa/kijiji husika. 

Tuesday, March 5, 2013

TUTAFANYA MAANDAMANO KWENDA WIZARA YA MAJI TAREHE 16 MACHI 2013; NIMESHAWASILISHA NOTISI, TUENDELEE NA MAANDALIZI

Tarehe 16 Machi 2013 nitaongoza maandamano ya amani ya wananchi kwenda kwa Waziri wa Maji kusimamia uwajibikaji kuwezesha hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jimbo la Ubungo na Jiji la Dar es salaam.

Wote mlioshiriki mkutano wa tarehe 10 Februari 2013 (Kwa wale ambao hamkushiriki mnaweza kutazama video hii: http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=O0txSoHqfGY ) , mtakumbuka tulimpa wiki mbili Waziri kujitokeza kwa wananchi kujibu hoja alizokwepa kujibu bungeni.

Tutakusanyika kata ya Manzese eneo la Bakhresa (jirani na daraja) saa 5 asubuhi na tutapita barabara ya Morogoro kuelekea kata ya Ubungo zilipo ofisi za Wizara ya Maji kufuatilia majibu ya ukweli na ukamilifu kuhusu hatua tisa za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka nilizopendekeza kwa niaba ya wananchi bungeni kupitia hoja binafsi na masuala mengine ambayo wananchi watataka yatolewe majibu siku hiyo.

Kila mmoja anaweza kuendelea na maandalizi ya kushiriki kwa kuwa tayari tarehe 4 Machi 2013 nimewasilisha notisi kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni na Maafisa wa Polisi Wasimamizi wa Maeneo kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 43 cha Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma Saidizi Sura ya 322 (The Police Force and Auxiliary Service Act, Chapter 322).

Sunday, March 3, 2013

WAZIRI MKUU PINDA AINGILIE KATI; WIZARA NA TANESCO HAWAJAJIBU UKWELI KUHUSU MGAWO WA DHARURA WA UMEME

Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kwa nyakati mbalimbali kati ya tarehe 28 Februari na 2 Machi 2013 kupitia baadhi ya vyombo vya habari wametoa majibu yasiyokuwa ya kweli juu ya mgawo wa dharura wa umeme uliotokea mwezi wa Februari. 

Katibu Mkuu wa Wizara Eliackim Maswi na Afisa Habari wa TANESCO Badra Masoud wote wameeleza kwamba hakukuwa na mgawo wa umeme bali kilichotokea ni matatizo madogo madogo ya mitambo na kwamba matengenezo yanaendelea. 

Kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini ninazo taarifa kwamba ukweli ni kuwa umetokea mgawo wa umeme wa dharura kutokana na upungufu zaidi wa kina cha maji katika mabwawa ya kufua umeme, upungufu wa fedha za kununua mafuta mazito ya kuendesha mitambo ya kufua umeme wa dharura na upungufu wa gesi asili ya kuendeshea mitambo ya kufua ya umeme. 

Hivyo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anapaswa kuingilia kati kuwaeleza ukweli wananchi ikiwemo hatua zilizochukuliwa kuhakikisha kwamba hali hiyo haiendelei mwezi Machi kinyume na ahadi iliyotolewa bungeni tarehe 28 Julai 2012 kwamba mgawo wa umeme ungekuwa historia. 

John Mnyika (Mb)
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini 

02 Machi 2013

Saturday, March 2, 2013

WANANCHI OMBENI UJUMBE WA MABARAZA YA KATIBA LAKINI PINGENI ‘MIANYA YA UCHAKACHUAJI’ WA UTEUZI KWENYE KATA ILIYOWEKWA NA MUONGOZO ULIOTOLEWA NA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA BILA KUZINGATIA MAONI YA WADAU

Mwongozo kuhusu Muundo, Utaratibu wa kuwapata wajumbe wa mabaraza ya Katiba ya Wilaya (Mamlaka za Serikali za Mitaa) na uendeshaji wake uliotangazwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba haujazingatia maoni ya msingi yaliyotolewa na wadau mbalimbali ikiwemo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). 

CHADEMA inawatahadharisha wananchi kuhusu ‘mianya ya uchakachuaji’ iliyotolewa na muongozo huo kwa kuzingatia kuwa ‘uchakachuaji’ wa uteuzi wa wajumbe wa mabaraza ya katiba, ni ‘uchakachuaji’ wa utoaji maoni kwenye mabaraza ya katiba, ambayo ni hatua ya awali ya ‘uchakachuaji’ wa rasimu ya katiba. 

Kwa mujibu wa Muongozo huo, ‘mianya ya uchakachuaji’ imeachwa kwenye ngazi ya kamati ya maendeleo ya kata ambayo wajumbe wake ni madiwani na wenyeviti wa mitaa/vijiji ambao kwa mujibu wa matokeo ya chaguzi za mwaka 2009 na 2010 kuna hodhi kwenye vikao hivyo ya chama kimoja (CCM).

Friday, March 1, 2013

RUFAA DHIDI YA UENDESHAJI WA BUNGE USIOKUWA WA HAKI NA UKIUKAJI WA KANUNI WA NAIBU SPIKA JOB NDUGAI KATIKA KUONDOA HOJA BINAFSI YA MAJI

Tarehe 28 Februari 2013 nimewasilisha rasmi rufaa kwa mujibu wa Kanuni ya 5 (4) dhidi ya uendeshaji wa Bunge usiokuwa wa haki wa Naibu Spika Job Ndugai kwa kukiuka kanuni ya 58 (5) kwa kulihoji bunge kinyume na kanuni kufanya uamuzi badili wa kuondoa hoja binafsi kuhusu hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jiji la Dar es salaam.

Nimefanya hivyo baada ya kupata kumbukumbu rasmi ya Bunge (Hansard) za kikao cha tano cha tarehe 4 Februari 2013 cha mkutano wa kumi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika Mkutano huo Naibu Spika Job Ndugai alisema na kufanya maamuzi kwamba: “Sasa ninahoji wanaoafiki kwamba hoja hii iondolewe waseme ndiyo…..hoja imeondolewa. Walioafiki Wameshinda”; wakati mtoa hoja sikuwa nimeomba idhini yoyote ya hoja yangu kuondolewa.

Maamuzi hayo ni kinyume na Kanuni ya 58 Fasili 5 ambayo inaelekeza kwamba “Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tu kuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema ‘Ninaomba ruhusa kuondoa hoja’ na papo hapo Spika ataliuliza Bunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokea Wabunge walio wengi watakubali, Spika atasema ‘hoja hiyo inaondolewa kwa idhini ya Bunge’ na hoja hiyo itakuwa imeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata”.

Ushahidi wa Kumbukumbu Rasmi za Bunge (Hansard) za kikao tajwa unathibitisha ukiukwaji huo wa kanuni kama ifuatavyo: