Sunday, July 20, 2014

Habari Picha: Ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Jimbo la Ubungo

ZIARA KATA YA KIBAMBA







Tukikagua ujenzi wa tanki la maji katika kata ya Kibamba


John Mnyika, Mbunge wa Ubungo akaiwa amebebwa na wafuasi wa chama chake wakati akiingia eneo la mkutano Kibamba




Diwani wa Kata ya Kibamba akizungumza jambo la Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla


Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia wananchi wa kata ya Kibamba


Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo wakiondoka katika eneo la tanki-Kibamba

ZIARA KATA YA KIMARA


Naibu Waziri wa Maji Amos Makalla, akimsikiliza kiongozi wa ujenzi wa Tanki la maji lililopo Kimara jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni mbunge wa jimbo la ubungo John Mnyika.


Tanki hili litavunjwa na kujengwa jipya





Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza na vyombo vya habari katika ziara hiyo ya kukagua miradi ya maji kata zilizopo Jimboni Ubungo

MKUTANO NA WANANCHI KATIKA UWANJA WA SEKONDARI YA MAVURUNZA


Diwani wa Kimara Pacal Manota, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Sekondari ya Mavurunza


Askari Polisi akiwambeleleza wanaCCM kusikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa meza kuu katika mkutano uliofanyika uwanja wa Sekondari Mavurunza


Wakutanapo Chadema na CCM 


John Mnyika, Mbunge wa Jimbo la Ubungo akizungumza katika mkutano huo na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla uwanja wa Sekondari Mavurunza





Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akizungumza katika mkutano wa hadhara








Katika hati hati ya kutaka kunusuru fujo zilizoanza kutokea katikati ya mkutano wa hadhara







Ujumbe wa wananchi kwa njia ya mabango





Polisi akijaribu kuwasihi wanaCCM kutulia ili mkutano uweze kuendelea


WanaCCM na WanaCHADEMA akutanapo


Ujumbe katika mabango












Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika tukijaribu kuwasihi wananchi toka katika pande zote za vyama kutulia ili mkutano uweze kuendelea









Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akijaribu kuwatuliza Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota














Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu. Huku Idd Azzan, Mbunge wa Kinondoni akiendelea kuwasihi Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge na Diwani wa Kimara, Pascal Manota


Mama Sanare akishauriana na Naibu Waziri, Amos Makalla na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo baada ya mkutano kuingiwa na vurugu


Shukrani kwa picha: Blogu ya Mzuka Kamili (www.mzukakamili-mzuka.blogspot.com)



Tuesday, July 8, 2014

Mnyika adai kutishiwa maisha

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amewaomba wapiga kura wake kumuombea kila siku kutokana na madai kuwa amekuwa akiwindwa na watu wanaotishia uhai wake.
Mnyika alitoa kauli hiyo juzi jioni katika eneo la Mbezi mjini Dar es Salaam, wakati akihutubia mkutano wa hadhara.
“Nimekuwa nikizungumza mambo mengi ninapokuwa bungeni Dodoma, hasa ninapowatetea wananchi na wapiga kura wangu, lakini kuna watu hawafurahishwi kabisa…sasa wamefikia hatua ya kunitishia maisha yangu.

Tuesday, July 1, 2014

Maghembe awasilisha nyaraka za kuhusu Mnyika

Na Mary Geofrey

Prof. Jumanne Maghembe, Waziri wa Maji
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, amepokea barua kutoka kwa Katibu wa Bunge ikimjulisha kwamba Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, hatimaye amewasilisha nyaraka na ripoti za utekelezaji wa miradi ya maji katika Jiji la Dar es Salaam.

Katika taarifa hiyo iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Katibu Msaidizi wa Mnyika, Aziz Himbuka, inasema kuwa taarifa hiyo imepelekwa katika Ofisi ya Mshauri Mkuu wa Mambo ya Sheria wa Bunge ili iweze kusomwa na hatua zitakazohitajika zichukuliwe.

Alisema Mnyika ataanza kazi ya kuzipitia taarifa hizo katika Ofisi Kuu ya Bunge Dodoma na baada ya kazi hiyo atarejea kuanza ziara ya kikazi jimboni kwake kuanzia mwanzoni mwa mwezi huu (Julai), 2014.

Mnyika anatarajia kufanya ziara katika kata zote 14, ambayo pamoja na mambo mengine atakagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ya maji.

Saturday, April 12, 2014

MAONI YA WAJUMBE WALIO WA WACHACHE KATIKA KAMATI NAMBA NNE KUHUSU SURA YA KWANZA NA SURA YA SITA YA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA [Kanuni ya 32(4) ya Kanuni za Bunge Maalum, 2014]


UTANGULIZI
Mheshimiwa Mwenyekiti,

Sura ya Kwanza na Sura ya Sita ya Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (‘Rasimu’) ndizo msingi ambao Rasimu yote imejengwa juu yao. Wakati Sura ya Kwanza inagusa suala la muundo wa Muungano katika ibara moja tu kati ya ibara tisa, Sura yote ya Sita inahusu ‘Muundo wa Jamhuri ya Muungano.’ Suala la Muungano na hasa Muundo wake limetawala mjadala wa kisiasa na kikatiba wa Tanzania kwa zaidi ya miaka thelathini. Ndio maana katika waraka wake wa siri kwa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (‘CCM’), Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ya chama hicho imetamka kwamba “muundo wa Muungano ndiyo moyo wa Rasimu na ndiyo unaoamua ibara nyingine zikae vipi.”

Suala hili pia limetawala mchakato wa Katiba Mpya tangu ulipoanza miaka mitatu iliyopita. Kama alivyosema Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Joseph Sinde Warioba wakati wa kuwasilisha Ripoti ya Tume yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar tarehe 30 Disemba, 2013: “Moja ya mambo ambayo yamejadiliwa sana na kwa hisia kali tangu Rasimu ya awali ilipotolewa ... ni Muungano wa Tanzania. Jambo kubwa limekuwa juu ya muundo wa Muungano.”[1]

Mafuriko yanayoendelea katika jiji la Dar es Salaam

Nipo bungeni lakini nimepokea taarifa za mafuriko katika maeneo mbalimbali jimboni kama Kibamba, Malambamawili, Makoka nk Nimeshatoa maelekezo kwa Katibu Msaidizi wa Ofisi ya Mbunge Ubungo kufatilia kwa ukaribu na kuzitaarifu mamlaka husika kwa hatua za haraka. Kwa maeneo mengine yenye mafuriko tafadhali mpeni taarifa kupitia: 0715-379542 au 0784-379542

Sunday, April 6, 2014

Sijaridhika na majibu ya Mkuu wa Mkoa kuhusu mgogoro unaoendelea juu ya usafiri wa pikipiki/bodaboda na bajaji katikati ya jiji la Dar es Salaam

Tarehe 4 Aprili 2014 Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Said Meck Sadiq amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kwamba hawezi kusitisha kwa muda agizo lake la kukataza pikipiki/bodaboda na bajaj kuingia katikati ya Jiji. Mkuu wa Mkoa amenukuliwa akisema kwamba hawezi kufanya hivyo kwa kuwa agizo hilo si la kwake bali la sheria ambayo ameamua kuisimamia.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo kufuatia taarifa yangu ya tarehe 2 Aprili 2014 niliyoeleza kuwa nimemwandikia ujumbe kutaka asitishe kwa muda utekelezaji wa tamko alilotoa tarehe 3 Machi 2014 ili kupisha mazungumzo baina ya Serikali, wahusika wa Bodaboda na Bajaji na wadau wengine muhimu ili kupata ufumbuzi.

Kufuatia kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa nimeipitia kwa mara nyingine tena kifungu kwa kifungu Sheria inayohusika ambayo ni The Surface and Marine Transport Regulatory Authority Act; sheria namba 9 ya mwaka 2001. Hakuna kifungu chochote katika sheria hiyo kinachokataza pikipiki/bodaboda au bajaj kuingia katika maeneo ya katikakati ya jiji. Hivyo Mkuu wa Mkoa anapaswa kutoa ufafanuzi kwa umma ni sheria ipi hiyo ambayo anaitumia na kifungu kipi hicho cha sheria ambazo kinamzuia kutengua agizo lake.

Ujumbe kwa Wananchi wa Chalinze:

Leo jumamosi 05 Aprili 2014 ni siku ya mwisho ya kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Chalinze na kesho jumapili 06 Aprili 2014 ni siku ya wananchi kupiga kura. Kwa wananchi wa Jimbo la Chalinze wa kata mbalimbali mnaoweza kupata ujumbe kwa njia ya mtandao nawajulisha kwamba nitazungumza nanyi katika mkutano wa hadhara leo. 

Kampeni za Chalinze zilizinduliwa na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa na zitafungwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Said Issa Mohamed (ZNZ) akiwa na Dr Slaa. Kwa wapenda demokrasia na maendeleo popote mlipo ziungeni mkono timu za viongozi, wanachama na wapenzi kwenye kata na vijiji mbalimbali. Kwa maelezo zaidi wasiliana na Mratibu Mohamed kupitia 0784246764 au 0784246764.

Wasiokuwa na mtandao naamini timu zetu za kampeni ya chini kwa chini na zenye magari ya matangazo kwa pamoja zitakuwa zimeshawaalika kwa kuzingatia ratiba ya kampeni. Tutahutubia kufunga kampeni kupitia mkutano utakaofanyika eneo la Chalinze Mjini (Sokoni) kuanzia saa 8 mchana na mpaka 12 Jioni nikiwa na viongozi wengine wa kitaifa.

Thursday, April 3, 2014

TAARIFA KWA UMMA

Tangu tarehe 3/3/2014 Serikali kupitia kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Ndugu Meck Sadiq ilipotoa tamko la kupiga marufuku biashara ya kusafirisha abiria maeneo ya mijini kwa kutumia usafiri wa bodaboda na bajaji kumekuwa na mgogoro baina ya vijana wanaofanya kazi hiyo kwa upande mmoja na vyombo vya ulinzi na usalama kwa upande mwingine.

Aidha, kufuatia kauli hiyo watumiaji wa kawaida wa pikipiki na bajaji nao wamekuwa wakipata usumbufu wa kukamatwa kamatwa na kusumbuliwa wakidhaniwa kwamba ni sehemu ya biashara ya usafiri kwa kutumia bodaboda na bajaji.

Kadhalika, kuanza tamko hilo limezusha usumbufu kwa abiria ambao walikuwa wakitumia vyombo hivyo vya usafiri kama mbadala wakati huu ambapo ujenzi wa miundombinu ya Mabasi yaendayo kwa Haraka (BRT) imeambatana na ongezeko la foleni katika barabara zinazoelekea mjini.

Kwa upande mwingine pamekuwepo na utata kuhusu mipaka ya Eneo la Katikati ya Mji (Central Business District- CBD) linaloguswa na amri hiyo.

Kwa kuwa mwezi mmoja umepita bila mgogoro huo kupatiwa ufumbuzi na Serikali yenyewe, nimeamua kuingilia kati ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kibunge wa kuwakilisha wananchi na kuisimamia Serikali.

Wednesday, March 26, 2014

Mnyika: Dawasco toeni taarifa mtambo wa Ruvu

26/03/2014 | Posted by Shehe Semtawa

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, ameitaka Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco), kutoa taarifa kwa umma kuhusu kuchelewa kukamilika matengenezo ya mtambo wa Ruvu Juu, kunakosababisha upungufu wa maji katika maeneo ya jiji hilo.

Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima Jumatano jana, Mnyika alisema baada ya kutokea tatizo hilo aliwasiliana na Dawasco ili kujua hatua walizochukua.

Alisema maelezo waliyompatia ni kuanza kwa matengenezo, hivyo hatua ya kuchelewa kukamilika kwa matengenezo hayo ilipaswa Dawasco kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari, matangazo ikiwemo tovuti yake.

Monday, March 24, 2014

Kuhusu Kituo Kipya cha Daladala Ubungo, Uendelezaji wa Kiwanja na. 2005/2/2 Sinza (Former Simu 2000) na fursa kwa Wafanyabiashara Ndogo Ndogo

Leo 25 Machi 2014 Ofisi ya Mbunge wa Jimbo Ubungo itafanya kazi ya kufuatilia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Kinondoni na Kamati ya Wafanyabiashara ndogo ndogo kuhusu utekelezaji wa mapendekezo niliyotoa tulipofanya ziara ya kikazi katika Stendi mpya ya Daladala ya Ubungo tarehe 6 Januari 2014.

Aidha, Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Ubungo itatumia nafasi hiyo kufuatilia kwa mamlaka mbalimbali juu ya masuala ambayo mbunge aliyahoji jimboni na bungeni kuhusu wafanyabiashara ndogo ndogo na wazalishaji wadogo ambayo yako katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Ikumbukwe kwamba tarehe 6 Januari 2014 nilipofanya ziara ya kikazi ya kufuatilia ujenzi wa Kituo kipya cha daladala katika Kiwanja na. 2005/2/2 Kitalu C Sinza eneo ambalo zamani lilikuwa chini ya “Simu 2000” uendelezaji ulikuwa umefanyika katika ekari nne.

Saturday, March 8, 2014

Ujumbe wangu kwenu siku ya Wanawake: Dhima ni mabadiliko kutimiza dira ya usawa kwa maendeleo ya wote

Tarehe 8 Machi ni Siku ya Wanawake Duniani (IWD). Ujumbe wa siku hii kwa mwaka huu wa 2014 kwa mujibu wa internationalwomenday.com ni “inspiring change” (kuhamasisha mabadaliko). Wakati kwa mujibu wa unwomen.org ni “equality for women is progress for all” (usawa kwa wanawake ni maendeleo kwa wote”.

Mchango wa wanawake katika taifa letu unapaswa kuheshimiwa na kila mtu; wanawake ni wazazi, walezi na ni wengi katika jamii yetu. Hata hivyo, ni kundi linalokabiliwa na changamoto nyingi ambazo ni muhimu kuunganisha nguvu za pamoja katika kuzikabili.

Katika kuadhimisha siku hii ofisi ya mbunge jimbo la Ubungo inafanya kazi nne mahususi zenye kuhamasisha mabadiliko na maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla.

Mosi; kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano Ofisi ya Mbunge inapokea mapendekezo toka kwa wanawake na wadau wa masuala ya jinsia ya kuboresha rasimu ya katiba kwenye ibara zenye kasoro. Mkazo haupaswi kuwa kwenye uwiano wa kijinsia na haki za wanawake za ushiriki kwenye chaguzi na uongozi wa kisiasa pekee au kupata ujira sawa kama ilivyo sasa katika rasimu ibara ya 47, bali kuwezesha ushiriki wa wanawake katika uchumi, kumiliki mali na maendeleo kwa upana wake.

Thursday, March 6, 2014

Taarifa kwa Umma: “Kuendelea kwa ‘Kashfa ya IPTL’ mpaka hivi sasa ni matokeo ya udhaifu wa Rais Kikwete, uzembe wa uongozi wa Bunge, ufisadi wa baadhi ya viongozi wa CCM na uongo wa Waziri Muhongo”.

Kwa nyakati mbalimbali kati ya tarehe 27 Februari 2014 na tarehe 5 Machi 2014 vyombo mbalimbali vya habari vimeandika habari na kuchapisha matangazo juu ya TANESCO na IPTL.

Umma uzingatie kwamba ‘kashfa ya IPTL’ ni ya miaka mingi katika taifa letu na inaendelea mpaka hivi sasa kutokana na udhaifu, uzembe, ufisadi na uongo unaotawala. 

Kumbukumbu zangu zinanionyesha kwamba wakati wa kuanzishwa kwake IPTL ilikuwa ni ubia wa kampuni mbili; Mechmar Corporation ya Malysia Bhd na VIPEM ya Tanzania. 

Udhaifu wa Rais unaendeleza ‘kashfa ya IPTL’:

Mwaka 1994 IPTL ilikutana na aliyekuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini wakati huo Jakaya Kikwete na aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO wakati huo Simon Mhaville. 

Thursday, February 27, 2014

Rasimu ya Pili ya Kanuni za Bunge Maalum hizi hapa; na masuala yanayohitaji kuungwa mkono ni haya:

Itakumbukwa kwamba tarehe 19 Februari 2014 Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum Pandu Kificho aliteua Kamati ya Wajumbe ishirini yenye uwakilishi wa makundi yote yanayounda Bunge Maalum kwa ajili ya kumshauri kuhusu Rasimu ya Kanuni za Bunge Maalum.

Rasimu ya kwanza ya Bunge Maalum iliandaliwa na Kamati ya Maandalizi chini ya Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Katibu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (nakala yake niliwapa hapa: http://goo.gl/hEI4aw ).

Kazi ya mjumbe ni kuwakilisha na kuwasilisha; katika kutekeleza wajibu huo, jana 26 Februari 2014 tulikuwa na Semina ya Bunge Maalum kuhusu Rasimu ya Pili ya Kanuni za Bunge Maalum toleo la 2014. 

Katika mjadala wa jana niliunga mkono mapendekezo ya rasimu katika sehemu ya nne kuhusu kupunguzwa kwa mamlaka na madaraka makubwa ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum, tofauti na rasimu ya kwanza; sasa maamuzi ya mwenyekiti hayatakuwa ya mwisho. Mjumbe asiporidhika anaweza kukata rufaa na pia rasimu sasa inapendekeza kwamba mwenyekiti au makamu wanaweza kuondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani.

Niliunga mkono kuruhusiwa kwa utaratibu wa kuwasilisha Taarifa ya Maoni Kinzani (dissenting opionion); hii ni kwa sababu rasimu ya kwanza haikuwa na utaratibu wa uwasilishaji bungeni wa hoja za wabunge, hoja zote ilikuwa ni kamati. Njia pekee ya kuwezesha mawazo mbadala kuweza kufika katika ukumbi wa Bunge kwa ukamilifu ukiondoa michango ya wabunge ni kupitia Taarifa za Maoni Kinzani.

Sunday, February 23, 2014

Pata nakala ya rasimu ya kanuni za Bunge Maalum la Katiba hapa, na shiriki mkutano wa mtandaoni leo tuijadili kutoa maoni na mapendekezo

Ratiba na utaratibu wa Bunge Maalum la Katiba haujatuwezesha kurejea kupata maoni ya mliotutuma au walau kuwekwa utaratibu wa Mwenyekiti wa Muda kuitisha mkutano wa kusikiliza umma/wadau (public/stakeholders hearing) hapa Dodoma.

Nilitoa pendekezo hili kwa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge na kwa wadau; rejea: http://mnyika.blogspot.com/2014/02/kwanini-ni-muhimu-tushirikishe-wananchi.html na http://www.ippmedia.com/frontend/?l=64919

Hata hivyo, mjadala wa bungeni unaanza kesho na hatimaye kanuni kupitishwa kwa kile ambacho vyanzo vyangu vimenidokeza kuwa msimamo wa wenye madaraka ni kwamba “mamlaka ya kujitungia kanuni ni ya bunge maalum lenyewe, kutunga kanuni ni suala la ndani la wajumbe wenyewe”.

Kutokana na ukuu na upekee wa kanuni hizi katika uendeshaji wa Bunge Maalum, ni wazi kasoro katika kanuni zitaacha mianya ya maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. 

Aidha, yapo mambo katika rasimu ya kanuni yanayohusu haki, kinga na maslahi ya wajumbe wa Bunge Maalum ambayo katika mizania ya utawala bora ni vyema katika kuyatunga maoni na mapendekezo ya wadau wengine wa nje ya Bunge la Maalum yakatolewa.

TAARIFA KWA UMMA: SAKATA LA FIDIA YA ENEO LA MLOGANZILA

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika ameendelea kufuatilia kuhusu fidia ya ardhi ya wananchi wa kata ya Kwembe waliohamishwa baada ya kulipwa fidia ya maendelezo pekee kupitisha ujenzi wa Chuo Kikuu cha Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.

Kwa upande mwingine, Mbunge Mnyika ameendelea pia kuhoji katika mamlaka mbalimbali juu ya kauli za viongozi wa Serikali kutamka kwamba eneo hilo lipo katika Mkoa wa Pwani badala ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam.

Tarehe 19 Januari 2014 Mbunge Mnyika alifika katika kata ya Kwembe na kukutana na wananchi kusikiliza malalamiko yao na mara baada ya mkutano huo alizikutanisha kamati mbili zinazofuatilia suala hilo.

Kufuatia hatua hiyo, Mbunge Mnyika aliwasiliana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwakumbusha kutekeleza ahadi zao za kuupatia ufumbuzi mgogoro huo kufuatia hatua ya mbunge kuhoji suala hilo bungeni kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2011 mpaka 2013. (Baadhi ya rejea kutoka Kumbukumbu Rasmi za Bunge-Hansard zimeambatanishwa).

Saturday, February 22, 2014

Maoni yangu kuhusu matokeo ya kidato cha nne wa mwaka 2013


Maoni yangu kuhusu matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne wa mwaka 2013 yaliyotangazwa na kuelezwa kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 15.17 yamedhihirisha tahadhari niliyotoa kuhusu mabadiliko ya viwango vya ufaulu yaliyotangazwa na Serikali tarehe 30 Oktoba 2013.

Serikali kwa barakoa (veil) ya kutekeleza Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) imeamua kulificha taifa juu ya Matokeo Mabaya ya Sasa (Bad Results of Now). Hivyo, wachambuzi wa masuala ya elimu wanapaswa kutoa takwimu za matokeo yangekuwa namna gani iwapo viwango vya awali vya ufaulu vingetumika ili nchi ijue hali halisi kwa manufaa ya wananchi.

Aidha, natoa mwito kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuweka wazi kwa umma ripoti za uchunguzi zilizoundwa kuwezesha wananchi kuihoji Serikali iwapo kupanda huko kwa ufaulu ni matokeo ya kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunza au ni kiini macho cha mabadiliko ya wigo wa alama na madaraja?

Ukweli ni kuwa hali ya mazingira ya kujifunza na kujifunzia katika shule nyingi za msingi na sekondari hasa za umma sio nzuri kutokana na kutokuwa na vitabu vya kutosha, maabara za kutosha, waalimu wenye sifa wapo wa kutosha na kuboresha maslahi ya waalimu ambayo yamekuwa yakilalamikiwa kwa siku nyingi.

Thursday, February 20, 2014

Rasilimali na mchakato wa kuandika Katiba Mpya

Kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini natoa mwito kwa wadau wote wa masuala ya rasilimali kuzingatia kwamba rasimu ya katiba haijazingatia masuala ya msingi kuhusu haki ya wananchi kumiliki na kunufaika na rasilimali za nchi. Hatua hii ni kinyume na mapendekezo niliyoyatoa bungeni tarehe 22 Mei 2013 na maoni yangu niliyoyatoa mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba pamoja na maoni yaliyotolewa na wadau wengine mbalimbali. 

Katika hotuba yangu ya Bungeni nilitaka Serikali isitishe kuendelea kunadi leseni za vitalu vya gesi mpaka kwanza mchakato wa katiba mpya ukamilike na pawepo sera na sheria zitazoongozwa na katiba mpya. Nilieleza kwamba katiba mpya inapaswa kuwa na ibara mahususi ya haki za wananchi kuhusu rasilimali ikiwemo ardhi, madini, gesi, mafuta, maji, misitu na maliasili zingine. Hata hivyo, katika rasimu ya katiba sura ya nne sehemu ya kwanza inayohusu haki za binadamu hakuna haki yeyote iliyotolewa kwa wananchi kuhusu kumiliki na kunufaika na rasilimali. Nitapendekeza kwa Bunge Maalum ibara mahususi kurekebisha udhaifu huo

Kwanini ni muhimu tushirikishe wananchi katika kutunga kanuni za Bunge Maalum

Kwenye kikao cha juzi cha Bunge Maalum nilipendekeza umuhimu wa suala la ushirikishwaji wa wananchi na wadau mbalimbali katika kutengeneza kanuni (Soma hapa: http://goo.gl/b0nQVA) . Wapo wenye mtazamo kwamba kanuni kwa kuwa ni za Bunge Maalum, kuandaa na kupitisha rasimu hiyo ni suala la wajumbe wenyewe pekee; hakuna ulazima wa wadau wala umma kushirikishwa.

Hata hivyo, kwa uzito na unyeti wa kanuni zenyewe na kwa kuzingatia kwamba mjumbe anapaswa kuzingatia maoni ya aliyemtuma ni muhimu umma ujue na kushiriki.

Pia, izingatiwe kwamba Bunge Maalum linapoendelea upo wakati wadau na wananchi wanataka kufuatilia kuhakikisha maoni na maslahi yao yanazingatiwa na wajumbe wao.

Hivyo, ni muhimu kushirikishwa kupata kuwezesha kanuni kuruhusu fursa hiyo. Ni wajulishe tu kwamba rasiu ya Katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. Nitafanya uchambuzi wa vifungu hivyo vibovu na hatimaye nitawasilisha mapendekezo ya maboresho kwa Bunge Maalum.

Wednesday, February 19, 2014

Uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga: CHADEMA yamekea pingamizi CCM!

CHADEMA imemuwekea pingamiza mgombea wa CCM kwamba sio raia wa Tanzania. 

Kazi imeanza!

Mkakato wa Katiba Mpya: Wadau washirikishwe kutunga kanuni Bunge la Katiba

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), amesema atawasilisha mapendekezo ya kutaka ratiba ya Bunge Maalumu la Katiba ibadilishwe, ili wadau washirikishwe kwenye mchakato wa kutunga kanuni za Bunge hilo.

Mnyika alisema hayo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.

Alisema ratiba iliyotolewa inaonyesha kwamba baada ya kusomwa kwa tangazo la kuitisha Bunge hilo na uchaguzi wa mwenyekiti wa muda, kazi ya kutunga kanuni itaanza.

Mnyika alisema kanuni ndiyo msingi wa kufikia mwafaka wa kuboresha rasimu ya Katiba badala ya kuchakachua na kwamaba ili zisitungwe kanuni mbovu ipo haja ya wadau wote wanaohusika na mchakato wa Katiba mpya ndani na nje ya Bunge kushiriki. 

“Nakusudia kuwasilisha mapendekezo kwamba ratiba ya Bunge ifanyiwe mabadiliko ili kuwapo na kikao cha kusikiliza umma (Public hearing), juu ya kanuni hizo ili mawazo ya wadau yazingatiwe katika maandaluzi ya kanuni kabla ya Bunge kupitisha azimio la kuridhia kanuni hizo,” alisema Mnyika.

Tafakari ya leo!


Tuwe wepesi wa kusikia si kusema wala kukasirika.

Tuwe watendaji sio wasikiaji tu.

Dini safi ni matendo mema.


-Funzo toka Yak. 1:19-27

Fursa kwa kijana kufanya kazi Ofisi ya Mbunge

Feb 2014 ni mwaka 1 toka nilipowasilisha Bungeni Hoja Binafsi ya kupendekeza Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka kuboresha upatikanaji wa Maji Safi na ushughulikiwaji wa Maji Taka katika jiji la Dar es Salaam. Soma hapa: http://goo.gl/Q770zm Natumia fursa hii kutangaza nafasi ya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini mafanikio na vikwazo kwa kijana wa ndani ya Jimbo la Ubungo (Mwanamke au Mwanaume) aliyetayari kufanya kazi ya mwezi 1 ya kutathmini hatua za haraka juu ya suala la Maji ndani ya jiji la Dar es Salaam afike Ofisi ya Mbunge, Halmashauri ya Kinondoni.

John J. Mnyika
Mbunge wa Ubungo
19.02.2014

Tuesday, February 18, 2014

Hon. John Mnyika's witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly

IN THE EAST AFRICAN COURT OF JUSTICE
FIRT DIVISION
AT ARUSHA
REFERENCE NO.07 OF 2012
(In the matter of interpretation of Article 50 of the Treaty for the Establishment of the East African Community)
BETWEEN
ANTON CALIST KOMU………………….CLAIMANT
AND
THE HONOURABLE ATTORNEY GENERAL OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA…………………….......RESPONDENT


WITNESS STATEMENT OF JOHN MNYIKA

I, John Mnyika Member of Parliament of the United Republic of Tanzania for Ubungo Constituency, make the following witness statement regarding The Election of Tanzania’s East African Legislative Assembly members:

I wrote a letter dated 8th February 2012 with reference no. OMU/BJMT/004/2012 to the Clerk of The Parliament of United Republic of Tanzania requesting amendment  to be  made in the third schedule of the Parliamentary Standing Orders (The East African Legislative Assembly Election Rules).

I made those proposals commensurate with the requirement of sections 3(3)(a) and (b) of the eighth schedule made under standing order 115 of the Parliamentary Standing Orders (2007 Edition).

I requested the Clerk to recall what transpired in the Election of East African Legislative Assembly that was conducted in the Parliament of the United Republic of Tanzania on the 2nd of November 2006. 

In that particular election complains arose and were raised that indicated the need for amendment of the East African Legislative Assembly Election Rules of the Parliament of the United Republic of Tanzania. I also drew to the attention of the Clerk that The East African Assembly had passed the EALA elections Act of 2011.

Monday, February 17, 2014

Mrejesho wa leo Februari 17: Jitihada za kuboresha barabara jimboni Ubungo na mengineyo

1. Barabara ya Goba-Mbezi Louis nawaomba wananchi wenzangu mfuatilie matengenezo yaliyoanza na kutoa mrejesho; lami kidogo nayo itaanza. Tuungane kupendekeza nyongeza bajeti hii

2. Barabara ya Malambamawili-Msigani naombeni tathmini ya matengenezo yaliyofanyika; ujenzi wa lami utaanzia kipande cha Kinyerezi-Kifuru. Kwa hii sasa ni hatua.

3. Barabara ya Bonyokwa-Mavurunza Kimara mwisho; nimewasiliana na Manispaa ya Kinondoni kukumbusha utekelezaji wa ahadi ya matengenezo. Majibu kesho.

4. Barabara ya Matete-Jeshini-Golani haikutengewa fedha KMC, nimewatumia ujumbe TANROADS wakishughilikia Msewe wasogee

5. Barabara ya Mavurunza-Golani-Msewe-Matete hali ya barabara ni tete. Nimewasiliana na diwani Pascal Manota na kumtumia posho ya leo kuweka mafuta grader. Ikiwa unatumia barabara za Mavurunza-Golani-Matete wasiliana na Diwani 0713792966 utuunge mkono sasa; mamlaka zingine nazo tunazifuatilia

Friday, January 31, 2014

Mwito kwa wananchi kutoa maoni kuhusu sheria ndogo

 
Nimerejea jimboni kikazi, pamoja na ufuatiliaji kuhusu kasoro za ujenzi unaendelea katika Barabara ya Morogoro na matengenezo yanayohitajika katika barabara zinaunganika na barabara hiyo katika maeneo ya pembezoni kupunguza foleni, lipo suala linalohitaji mjadala na maoni ya haraka toka kwa wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Tangu mwaka 2013 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imekuwa katika mchakato wa kutunga sheria ndogo nne: ya matumizi ya barabara, ushuru wa masoko, ada na ushuru na ushuru wa huduma. Mwanzoni mwa mwaka huu 2014 katika kikao cha Baraza la madiwani ilibainika kwamba sheria hizo zilikaribia kupitishwa bila ya ushirikishwaji wa kutosha wa wadau na wananchi.

Halmashauri iliongeza muda wa kupokea maoni; hata hivyo muda ukiwa unaelekea ukiongoni, ikiwa imesalia takribani wiki moja, tathmini ya ofisi ya mbunge Jimbo la Ubungo inaonyesha kwamba sheria hizo hazijasambazwa vya kutosha kwa wananchi na wadau kwa ajili ya kutoa maoni yao katika kata na mitaa mbalimbali.

Hivyo, ofisi ya mbunge Jimbo la Ubungo leo tarehe 31 Januari 2014 itafanya kazi ya kusambaza Sheria hiyo kwa njia mbalimbali kwa ajili ya wadau na wananchi kupitia na kutoa maoni yao. Mkazi wa Jimbo la Ubungo anayehitaji kutoa nakala anaweza kuwasiliana na Katibu Msaidizi Aziz Himbuka kupitia 0784379542 au 0715379542 au kwa kuwasiliana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni moja kwa moja.

Wednesday, January 22, 2014

Ufafanuzi kuhusu upanuzi na mgogoro wa kuhusu upana wa barabara ya Morogoro

Kwa nyakati mbalimbali kati ya mwaka 2004 na 2013 nimezungumzia haja ya upanuzi wa Barabara ya Morogoro kutoka Jimboni Ubungo kupitia Kibaha mpaka Chalinze na mgogoro uliodumu muda mrefu kuhusu upana wa Barabara hiyo.

Ningependa kutoa ufafanuzi kwamba nyakati zote nimeunga mkono upanuzi wa Barabara hiyo ikiwemo ujenzi wa barabara hiyo kuwa njia sita (tatu kwenda na tatu kurudi).

Hata hivyo, mara nyingi nimekosoa masuala manne kuhusu upanuzi na mgogoro kuhusu upana wa barabara ya Morogoro:

Mosi, Serikali kutoa ahadi bila utekelezaji kwa miaka mingi. Mwaka 2012 na 2013 Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli amekuwa akirudia kauli kwamba ujenzi wa Dar Es Salaam-Chalinze express road kuanza. Katika mkutano wangu na wananchi jimboni tarehe 19 Januari 2014 kuhusu ujenzi wa Barabara hiyo, nimesisitiza kwamba fedha za ujenzi wa barabara hiyo hazijatengwa hivyo ujenzi hauwezi kuanza. Badala yake nilifafanua kwamba Serikali inachokifanya kwa sasa ni kutafuta mkandarasi mwenye uwezo wa kutafuta fedha na kujenga. Hivyo, ni muhimu Serikali ikawaeleza wananchi ukweli na kuharakisha kutekeleza ahadi zilizotolewa kwa miaka mingi.

Wednesday, January 15, 2014

TAARIFA KWA UMMA: Kero ya maji Dar na taarifa za kina


Rais Jakaya Kikwete amwondoe Prof. Jumanne Maghembe nafasi ya Waziri wa Maji kwa kushindwa kuchukua hatua za haraka za kuongeza upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika Jiji la Dar Es Salaam na nchini kwa ujumla.

Rais Kikwete azingatie kwamba tarehe 10 Januari 2014 nilimtumia ujumbe Waziri Maghembe kumshauri ajiuzulu kutokana na kujirudia rudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam kinyume na maelezo yake ya uongo aliyoyatoa bungeni tarehe 4 Februari 2013.

Aidha, kufutia maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Hawa Sinare kuhusu sababu za kuchelewa kwa miradi ya maji Jijini na majibu ya Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASCO) Jackson Midala kuhusu kujirudia kwa matatizo ya maji; Rais Kikwete akumbuke ahadi yake ya kuitisha kikao Ikulu kujadili masuala maji mwezi Machi 2013 ambayo mpaka sasa hajaitekeleza.

Ikumbukwe kwamba mara baada ya kujirudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam niliwasiliana na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua na pia nilitaka Wenyeviti wa Bodi na Watendaji wakuu wa Mamlaka zinazohusika na huduma ya maji jijini (DAWASA na DAWASCO) watoe maelezo kwa umma juu ya sababu za kweli za matatizo za matatizo hayo.

Taarifa kwa Umma-Nishati ya Umeme


Kufuatia ukimya wa Wizara ya Nishati na Madini na Mamlaka nyingine tangu nitoe mwito kwao tarehe 9 Januari 2014 juu ya ongezeko la bei ya umeme; namshauri Rais Jakaya Kikwete katika mchakato wa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri kumtaka Waziri Prof. Sospeter Muhongo kujieleza kwake na kwa umma kuwezesha hatua stahiki kuchukuliwa.

Rais Kikwete akumbuke kwamba Waziri Muhongo alisema uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 alipowahakikishia wananchi kwamba bei ya umeme haitapanda hata baada ya TANESCO kuwasilisha mapendekezo ya kupandisha bei ya umeme.

Kinyume na kauli za Waziri Prof. Muhongo; Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kikao chake cha tarehe 10 Desemba 2013 pamoja na mambo mengine, ilitoa maamuzi ya ongezeko la bei za umeme kwa viwango mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya wateja hatua ambayo itaongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi na itaathiri uchumi wa nchi.

Maamuzi hayo yamefikiwa kufuatia tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa EWURA. TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.

Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa kanuni ya kurekebisha bei ya umeme kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta, mfumuko wa bei na mabadiliko ya thamani ya shilingi ya kitanzania hatua ambazo nazo zina athari katika uchumi na maisha ya wananchi.

Thursday, January 9, 2014

Waziri Prof. Maghembe ajiuzulu: DAWASA/DAWASCO warejeshe huduma ndani ya wiki moja katika maeneo yaliyokuwa yakipata mgao wa maji kabla

Nimemtumia ujumbe Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe kumshauri ajiuzulu kutokana na kujirudia rudia kwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam kinyume na maelezo yake ya uongo aliyoyatoa bungeni tarehe 4 Februari 2013.

Aidha, Wenyeviti wa Bodi na Watendaji wakuu wa Mamlaka zinazohusika na huduma ya maji jijini (DAWASA na DAWASCO) watoe maelezo kwa umma juu ya sababu za kweli za matatizo ya maji kujirudia rudia katika Jiji la Dar Es Salaam.

Pia, wajieleze kwa umma ni kwanini wananchi wasipendekeze Rais awachukulie kwa uzembe, kuisababishia hasara Serikali, kuathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa kukosa maji mara kwa mara ambayo ni huduma ya msingi ya binadamu na malighafi muhimu katika uzalishaji.

Itakumbukwa kwamba tarehe 4 Februari 2013 niliwasilisha hoja binafsi bungeni juu ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji katika jiji la Dar Es Salaam, nikipendekeza Bunge kuingilia kati kuweza kuisimamia Serikali kuchukua hatua za haraka.

Iwapo hoja hiyo ingejadiliwa na maazimio yote kutekelezwa matatizo ya maji katika Jiji la Dar Es Salaam mpaka hatua ya sasa yangekuwa yamepungua katika maeneo mbalimbali kutokana na hatua ambazo nilipendekeza zichukuliwe.

Kauli ya awali kuhusu ongezeko la bei za umeme

Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), katika kikao chake cha tarehe 10 Desemba 2013 pamoja na mambo mengine, ilitoa maamuzi ya ongezeko la bei za umeme kwa viwango mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya wateja hatua ambayo itaongeza mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi na itaathiri uchumi wa nchi.

Maamuzi hayo yamefikiwa kufuatia tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa EWURA. TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.

Vilevile TANESCO waliomba kuidhinishwa kwa kanuni ya kurekebisha bei ya umeme kulingana na mabadiliko ya bei za mafuta, mfumuko wa bei na mabadiliko ya thamani ya shilingi ya kitanzania.

Maamuzi hayo ya Bodi ya EWURA ambacho ni chombo cha Serikali yamethibitisha kwamba Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo alisema uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 alipowahakikishia wananchi kwamba bei ya umeme haitapanda hata baada ya TANESCO kuwasilisha mapendekezo ya kupandisha bei ya umeme.

Monday, January 6, 2014

Kauli kuhusu Uongo wa Waziri Profesa Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ametoa kauli za uongo kwa nyakati mbalimbali mwaka 2012 na 2013 ndani na nje ya Bunge kuhusu utafiti na uendelezaji wa gesi asilia.

Waziri Muhongo alijibu uongo kwamba hafanyi kazi kwa vyombo vya habari nilipohoji kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge ya kuanzia Novemba 2011 ya kushughulikia ufisadi uliothibitika katika mapato ya mauzo ya gesi na udhaifu mwingine uliobanishwa.

Aidha, Waziri Muhongo aliahidi uongo alipounda alipounda kamati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) na kuahidi kwamba kamati hiyo itafanya mapitio ya mikataba na kuandaa ripoti itakayowezesha mikataba mibovu ya utafiti wa mafuta na gesi asili kufanyiwa marekebisho. Hata hivyo, Wizara ya Nishati na Madini baadaye iliyoa taarifa kwamba matokeo ya ripoti hiyo hayatatumika kwa ajili ya mikataba iliyopita bali mikataba ijayo.

Sunday, January 5, 2014

Mapendekezo ya Mgawanyo Mpya wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam

Nimepokea mwaliko wa kikao maalumu cha kikao cha fedha na uongozi wa tarehe 3/01/2014 kikao kufanyika tarehe 06/01/2013 saa nane mchana kujadili mapendekezo ya kuongeza maeneo mapya ya utawala katika Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na ajenda zingine.

Nimeonelea tija kuwasilisha mapendekezo yangu kwa maandishi kwa umma na baadae katika kikao tajwa. Kwa hatua hii, ni fursa kwa kila mwananchi kutoa maoni yake juu ya haya;

Kwa ukuaji wa kasi wa Dar es Salaam ambao ndiyo mji mkubwa nchini Tanzania, jiji kitovu cha biashara na viwanda ambalo kadiri ya takwimu linakadiriwa kuwa na idadi ya watu milioni nne na nusu. Jiji hili limeshika nafasi ya tatu katika miji inayokuwa kwa kasi barani Afrika na miongoni mwa miji kumi inayokuwa kwa kasi duniani.

Ifahamike pia, Jiji la Dar es Salaam ndilo linashikilia asilimia themanini na tatu (83%) ya mapato ya serikali kitaifa na takribani asilimia sabini (70%) ya kodi zote zinazokusanywa nchini Tanzania.

Yafuatayo ndiyo mapendekezo yangu ya wasilisho la nyaraka ya mapendekezo yaliyoletwa katika ofisi yangu toka Manispaa ya Kinondoni;

Mosi, Pendekezo la kutumia “Manispaa” badala ya “Wilaya”:
Kadiri ya wasilisho, imetumika pendekezo la “wilaya”. Ningeshauri na kupendekeza kutokana na uhalisia na ukuaji wa kasi kutumika kwa “Manispaa” badala ya wilaya.

Pili, Pendekezo bora la mgawanyo wa Manispaa:
Katika wasilisho lenye uwepo wa mapendekezo saba. Ninaungana na kuafiki utumiaji wa pendekezo la pili lililowasilishwa la kuwa na Manispaa tano (5) ambazo ni;
i.                    Manispaa ya Ilala
ii.                 Manispaa ya Temeke
iii.               Manispaa ya Kinondoni
iv.                Manispaa ya Kigamboni
v.                  Manispaa ya Ubungo

Sababu muhimu:
1.        Ukubwa kijiografia: Kwa kuongeza wilaya mbili mpya yaani Manispaa ya Kigamboni na Manispaa ya Ubungo hii itasaidia wilaya hizi kuweza kuhimili ukubwa wa eneo wa kijiografia ambalo kwa sasa inaelemea wilaya hizi za sasa yaani Manispaa ya Kinondoni na Manispaa ya Temeke.
2.      Ukuaji wa kasi wa jiji: Katika ukuaji wa kasi unaoendelea jiji la Dar es Salaam maeneo yaliyopo katika wilaya hasa ya Kinondoni na Temeke ndiyo ambayo yanaongoza pia katika ukuaji huo wa kasi wa kimakazi na shughuli za kiuchumi kama viwanda na uwekezaji. Hivyo kwa kuwa na Manispaa mpya mbili(Manispaa ya Ubungo na Manispaa ya Kigamboni) zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kusimamia vyema mipango miji, kuujenga vyema mji na kusimamia kihuduma.
3.       Uwepo wa mipango ya kuimarisha ukuaji wa jiji kupitia miji ya pembezoni “satellite cities”: tayari serikali imeweka dhamira ya kuimarisha ukuaji wa jiji kupitia satellite cities. Hivyo uwepo wa wilaya mbili yaani Kigamboni (Satellite city Kigamboni) na Ubungo (“Luguruni Satellite City” ndani ya Kata ya Kwembe na Kata ya Kibamba) zitamudu kusimamia vyema ujenzi imara wa satellite cities na pia kuwezesha wilaya zitakazoachwa kama wilaya ya Kinondoni kuwa na ahueni ya kuelemewa na kazi hivyo nazo kusimamia vyema mipango ya ujenzi wa satellite cities zilizomo ktk maeneo hayo

Tuesday, December 31, 2013

Kheri na fanaka kwa mwaka mpya 2014. Nimerudi!

Nimerejea toka kwenye mafungo na tafakari, kumradhi kwa wote mlionikosa simuni na mtandaoni. Nawatakia mwaka mpya wenye upendo na uadilifu

Sunday, December 1, 2013

Ujenzi wa Kituo cha Polisi Kata ya Sinza-Mchango wa Mfuko wa Jimbo



Ukaguzi nilioufanya katika Kata ya Sinza; ujenzi wa kituo cha polisi kwa fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo.

Mfuko wa Jimbo umetenga milioni 10; tayari umeshatoa milioni 3.5 zilizofikisha jengo mpaka hatua hiyo. Taratibu za utoaji fedha zilikwamisha mradi toka mwezi Mei mwaka 2013.

Wednesday, November 27, 2013

Taarifa kwa umma kuhusu serikali kupandisha bei ya umeme

Gazeti la Tanzania Daima Toleo na. 3280 la tarehe 26 Novemba 23 limenukuu kauli iliyotolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini George Simbachawene wakati akizungumza na kipindi cha Kumepampazuka kilichorushwa na Redio One juu ya Serikali kupandisha bei ya umeme kama Shirika la Umeme (TANESCO) lilivyoomba.

Katika habari hiyo Simbachawene amenukuliwa akisema kwamba endapo kuna mwananchi yeyote atakayeona gharama za umeme ni kubwa ni vema akaamua kuwasha kibatari au akae giza. 

Rais Jakaya Kikwete anapaswa kumwagiza Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospter Muhongo kuwaomba radhi wananchi kwa kauli hiyo iliyotolewa na Naibu Waziri Simbachawene kwa niaba ya wizara anayoiongoza.

Aidha, ni vyema Rais Kikwete kwenye hotuba yake kwa taifa ya mwisho wa mwezi huu akawaeleza wananchi iwapo uamuzi huo wa kupandisha kwa mara nyingine bei ya umeme ndio utekelezaji wa ahadi ya maisha bora aliyoitoa kwa watanzania kuanzia kwenye uchaguzi wa mwaka 2005.

Hii ni kwa sababu kupandisha bei ya umeme kuna athari ya kuchangia katika ongezeko la gharama na ugumu wa maisha kwa kuwa shughuli za uzalishaji na maisha ya kila siku zinategemea kwa kiwango kikubwa nishati.

Thursday, November 21, 2013

Mgao wa umeme na uongo nyuma yake!

Mgawo huu wa umeme ni wa ufisadi wa kimikataba Songosongo/PAT na udhaifu wa Mpango wa Dharura wa Umeme; Bungeni Muhongo alinijibu uongo.

Mgawo wa Umeme ufisadi wa PAT na udhaifu wa ukarabati wa visima ulijulikana toka Julai na Novemba 2011; Prof Muhongo alisema uongo kuficha.

Trilioni 1 ilitumika kuficha uongo wa Prof Muhongo Mgawo wa Umeme kwenye manunuzi ya mafuta mazito; Ufisadi, PAT, visima, gesi umemshinda.

MgawowaUmeme Prof Muhongo alisema uongo mara 2 bungeni; 1. 28 Julai 2012 baada ya kumhoji kwenye hotuba 27 Jul http://mnyika.blogspot.com/2012/07/hotuba-ya-kambi-rasmi-ya-upinzani.html

Uongo wa mara ya 2 wa Prof Muhongo bungeni kuhusu MgawowaUmeme ni wa Mei 23 nilipohoji baada ya hotuba ya 22 Mei: http://mnyika.blogspot.com/2013/05/hotuba-ya-msemaji-wa-kambi-rasmi-ya.html

Halafu kwa maagizo ya IMF/WB wanataka kupandisha bei ya umeme kufidia ufisadi kukodi mitambo ya dharura/ununuzi mafuta na mikataba mibovu.

Thursday, October 24, 2013

Wednesday, October 16, 2013

Ujenzi wa Kisima cha Maji Safi-Msigani!


Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika alipotembelea ujenzi wa kisima cha maji kilichojengwa katika mtaa wa Msigani, Kata ya Msigani, ujenzi wa kisima hicho umechangiwa na fedha za mfuko wa jimbokiasi cha Tsh 3.5 milioni katika kumalizia ujenzi huo.

Thursday, September 12, 2013

Mnyika ahoji ziliko fedha za DECI

na Shehe Semtawa

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amemtaka Gavana wa Benki Kuu, Benno Ndulu, kuwaeleza waliokuwa wanachama wa Kampuni ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI) fedha zao zilizotaifishwa na serikali kutoka kwenye taasisi hiyo ziko kwenye akaunti gani.

Mnyika alisema kuwa wakati sakata la DECI linaanza mwaka 2009, serikali ilitaifisha jumla ya sh bilioni 19, sawa na asilimia 40 ya fedha zote ambazo wanachama wa taasisi hiyo iliyokuwa ikiendesha na kusimamia mchezo wa upatu walikuwa wakidai.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara juzi Mtaa wa Mavurunza, Kata ya Kimara baada ya kuulizwa swali na mmoja wa wananchi aliyetaka kujua hatima ya fedha zao, Mnyika alitoa tahadhari kuwa danadana inayotaka kufanywa na serikali inaweza kutia shaka kuwa fedha hizo hazipo.

”Sasa naomba nimjibu yule mwananchi aliyetaka kujua hatima ya fedha za DECI. Mtakumbuka hili suala nimekuwa nikitaka majibu yake bungeni, lakini kila mara wanatumia kisingizio kuwa suala hili liko mahakamani.

Tuesday, September 10, 2013

Mnyika: Serikali imalize tatizo la maji

na Abdallah Khamis

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, ameitaka serikali kuhamisha nguvu na kasi zilizotumika katika ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuelekea jijini Dar es Salaam na kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi hususan katika Jimbo la Ubungo.

Mnyika alitoa kauli hiyo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Mavurunza na kusisitiza hakuna suala muhimu kama maji kwa wananchi na kwamba kunahitajika ufumbuzi wa muda mfupi na mrefu, ikibidi kwa hali ya dharura.

Alisema kama serikali inaweza kutumia muda mfupi kujenga na kutandaza bomba hilo kwa nini ishindwe kufanya hivyo kwa mabomba ya maji, ambayo ni uhai wa wananchi.

“Tunaendelea kupambana kuhakikisha tatizo la maji tunalipunguza na kuliondoa kabisa, ninachowaomba ni sauti zenu na mshikamano wenu, suala hili ni uhai wa watu, kama maji ni tatizo maana yake uhai wa binadamu uko shakani,” alisema Mnyika.

Wednesday, August 28, 2013

Uzinduzi wa Kampeni ya Kuchangia Maabara na Madawati chini ya Shirika la UDI



Mhe. John Mnyika akishirikiana na Mratibu John Mallya kuonyesha bango lenye ujumbe wa harambee ya kuchangia maabara na maktaba iliyozinduliwa Agosti 21, 2013

Thursday, August 15, 2013

Leo Agosti 15, 2013: Sengerema na Mwanza Mabaraza ya wazi ya Katiba Mpya

Sengerema: Endeleeni kutoa maoni kwa maneno na maandishi kwenye baraza letu la katiba linaloendelea uwanja wa Wenje kata ya Nyamburukano

Mwanza: Baraza la wazi la Jiji likijumuisha pamoja Wilaya za Ilemela na Nyamagana litaanza saa 9 alasiri Uwanja wa Magomeni kata ya Kirumba.

Mwenyekiti Mbowe na mimi tutashiriki katika michakato hiyo.

Maslahi ya Umma Kwanza!!

Monday, August 12, 2013

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; tukutane tushiriki mabaraza ya wazi ya katiba.

Leo Agosti 13, 2013 Busega, Maswa, Meatu, na Bariadi; ni kushiriki kikamilifu baraza la wazi la katiba. Mwenyekiti Mbowe na mimi tutajumuika nanyi kupitia rasimu ya katiba mpya.

Busega: Baraza la wazi la katiba leo litaanza saa 3 asubuhi.

Maswa: Wanachana na wapenzi hudhurieni baraza la wazi la katiba kuanzia saa 5 kamili

Meatu: mtaanza baraza la wazi la katiba saa 7 mchana. Wanachama na waalikwa mkifika anzeni kutoa maoni yenu juu ya rasimu; tuko pamoja!

Bariadi: ni haki na wajibu kushiriki baraza la wazi la katiba leo tarehe 13 Agosti kuanzia saa 9 alasiri.

Shime tushiriki kikamilifu na kuitumia fursa hii kwa maslahi ya taifa letu.

Thursday, August 8, 2013

Salamu za Eid-Al-Fitr na kutembelea kata ya Malamba Mawili!

Saa 5 mpaka 8 mchana nitakuwa pamoja na viongozi wenzangu Malamba Mawili (Eneo la Stendi Mwisho). Tutagawa zawadi kwa watoto pamoja na kutoa salamu za Eid-Al-Fitr. Tutasambaza nakala za rasimu ya katiba mpya vijiweni na kwa wawakilishi wa makundi ya kijamii yenye malengo yanayofanana.

Tunaanza muda huo ili kuheshimu wajib wa salaat ya Eid na sunnah ya khutbah asubuhi. Imekuwa ni kawaida kwa siku ya Eid kuwa pia ni wasaa kwa kusikiliza hotuba juu ya wajibu kwa Allah lakini pia kwa binadamu wengine. Ni wakati wa ummah kukumbushwa masuala muhimu katika jamii. Tunamaliza mapema kutoa fursa ya mikusanyiko mingine.

Nitazungumza na umma kuhusu mchakato wa katiba na kutoa pia mrejesho juu ya masuala ya maendeleo ikiwemo juu ya ujenzi/matengenezo ya Barabara ya Kinyerezi-Malamba Mawili Mbezi, kuhusu maji na juu ya masuala mengine muhimu ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Kwa wakazi wa maeneo jirani yanayozunguka Malamba Mawili ya Kifuru, King’azi, Msingwa, Msigani na mengineyo mnaweza kuja kujumuika nasi. 

Kwa maelezo zaidi na maelekezo naomba muwasiliane na Ali Makwilo 0715/0784691449.

Eid Mubarak!

Kwa mkazi wa Kisopwa, Sinza, Manzese, Mbezi Makabe, Malambamawili, Mshikamano au Msigani; naomba usome hapa na kunipa mrejesho juu ya ardhi na mipango miji

Tarehe 12 Julai 2012 katika mchango wangu bungeni ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kuwawakilisha wananchi na kuisimamia Serikali niliitaka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na mambo mengine:

Itatue mgogoro kati ya Manispaa ya Kinondoni na Halmashauri ya Kisarawe kuhusu wananchi wa Kisopwa na Mloganzila kuitwa kwamba wako Kisarawe badala ya Kinondoni.

Ichukue hatua juu ya maeneo ya wazi/umma yaliyovamiwa katika kata ya Sinza ambapo mabango yamewekwa, muda wa notisi umeisha lakini majengo bado yapo.

Imtaje wazi mwendelezaji mwenza wa Mji wa kiungani (satellite town) wa Luguruni, masharti ya mkataba na lini uendelezaji unaanza.

Itoe nakala ya mipango ya uendelezaji upya kata ya Manzese.

Iharakishe mipango ya uhakiki na urasimamishaji katika maeneo ya Mbezi Makabe, Malamba Mawili, Mshikamano na Msigani.

Mwaka mmoja umepita, kuna mambo nimepewa na majibu na kazi imefanyika na kuna masuala bado.

Mkazi wa Mabibo na maeneo jirani nakutaarifu kuwa nitahutubia mkutano wa hadhara kwenye eneo la Sahara leo siku ya 8/8 kuanzia saa 9 alasiri mpaka 11 jioni ulioandaliwa na chama. Njoo na waalike na wengine.

Mkutano huo una malengo matatu: Mosi; kuwasilisha mrejesho wa kazi jimboni za utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyogharamiwa na Mfuko wa Jimbo katika maeneo yenu.

Pili; nitafanya kazi ya kuuchambua mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea ikiwemo kuhusu rasimu ya katiba mpya.

Tatu; kupokea maoni/mapendekezo ya masuala muhimu ya kuyazingatia katika kazi ya kuwawakilisha wananchi kwenye vikao vya kamati za Bunge vinavyoanza wiki ijayo na Mkutano wa Bunge unaoanza mwishoni mwa mwezi huu.

Itakumbukwa kwamba tarehe 21 Julai 2013 nilitaka kutimiza azma hiyo kwenye eneo tajwa lakini Jeshi la Polisi lilizuia mkutano kwa maelezo yasiyokuwa ya kweli kwamba kulikuwa na ziara ya Makamu wa Rais katika Jimbo la Ubungo.

(Msaidizi katika Ofisi yangu ameeleza hapa kwa kirefu: http://www.youtube.com/watch?v=VyHF5O-P-Vk&feature=c4-overview&list=UUs0TcFkgqs2OYd6x5E68nhg ).

Nitashiriki kwenye Iftar nyumbani kwa Marehemu Mbwana Masoud Makurumla leo 8/8 jioni; wasiliana na Aziz (OMU) 0784/0715-379542 kutuunga mkono kwa hali na mali. Ramadan Kareem.

Kwa ndugu zangu na wenzetu waislamu, ni siku ya 30 ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan. Siku ya 30 ni kati ya siku kumi za mwisho za mfungo ambazo wapo wanaomini kwamba usiku ni siku ya “usiku wa nguvu”. Siku na usiku ambao Mtume Muhammad (SAS) alipokea ufunuo wa kwanza wa Q’uran yaani Laylat al-Qadr.

Katika siku hii ya 30 nitaungana pamoja na familia ya Marehemu Mbwana Masoud, majirani zake wakazi wa Kata ya Makurumla na wengine mtakaojumuika nami katika Iftar nyumbani kwa familia ya marehemu . Jioni tutaanza na tende na futari itafuata baada ya swala ya maghrib.

Marehemu Mbwana Masoud alikuwa ni mmoja wa wanachama wa CHADEMA walijitolea kusafiri kwenda Igunga kwa ajili ya kuwa wakala kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 2 Oktoba 2011.

Monday, July 29, 2013

Hali tete na tata ya kituo cha mabasi cha Ubungo (UBT)- Hatua ambazo nimeanza kuzichukua

Katika siku za karibuni nimepokea malalamiko kuhusu hali tete na tata katika Kituo cha Mabasi cha Ubungo (UBT) kinachosimamiwa na kuendeshwa na Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam. 

Kufuatia malalamiko hayo, nimechukua hatua zifuatazo mpaka sasa: Mosi, tarehe 15 Julai 2013 nilifanya ziara ya ghafla kujionea hali halisi, sehemu ya ziara hiyo inaweza kutazamwa kupitia: 
http://www.youtube.com/watch?v=JuPGoz-JI-I , ambapo nilibaini kwamba hatua za haraka zinahitajika. 

Nimeshuhudia hali ya uchafu ikiwemo utiririkaji wa maji machafu ndani ya Kituo cha Mabasi ambayo yanatuama na hadi kubadilika rangi na kuwa ya kijani ambapo ni hatarishi kwa abiria na watu wanaofanya shughuli zao ndani ya kituo. Pia, kuna vyoo vichache ukilinganisha na idadi ya abiria na watumiaji wengine wa Kituo. Hali hiyo inaweza kusababisha magonjwa ya mlipuko.

Nimejulishwa hali ya usalama ndani ya kituo ni tete; usalama ndani ya kituo ni mdogo sana kwa abiria na nimepewa taarifa za matukio ya uhalifu ambayo yamesababisha pia madhara kwa abiria.

Nimetembelea kituo na kukuta kuna usumbufu mkubwa sana kwa abiria na watumiaji wengine wa Kituo baada ya maeneo ya awali ya kupumzikia kwa abiria na wasindikizaji kubomolewa. 

Thursday, July 25, 2013

Chenge (Mb) amesema kodi ya kadi za simu (SimCardTax) ni sahihi kwa utafiti wao; aulizwe kupitia 0754782577 atoe maelezo zaidi na vielelezo vya ziada

Leo tarehe 25 Julai 2013 chombo kimoja cha habari kimemnukuu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Andrew Chenge (Mb) akisema kwamba uamuzi kuhusu kodi/tozo ya kadi/laini za simu haukuwa wa kubahatisha. Chenge amesema kwamba kamati yake ilifanya utafiti wa kina na kisha kufikia uamuzi wa kuona tozo hiyo ni sahihi.

Ni muhimu akatakiwa kupitia namba yake 0754782577 atoe maelezo zaidi kuhusu usahihi wa tozo hiyo na aeleze ni wapi wananchi na wadau mbalimbali wanaweza kupata vielelezo vya utafiti walioufanya.

Aidha, wenye maswali kuhusu nini hasa kilijiri kwenye kamati ya bajeti mpaka kamati hiyo ikakataa jedwali la marekebisho nililowasilisha tarehe 27 Juni 2013 kabla ya muswada wa sheria ya fedha kupitishwa bungeni tareheb 28 Juni 2013 kwa kuwa yeye ambaye ndiye msemaji wa kamati ameanza kutoa majibu. 

Pia, aeleze iwapo yupo tayari kumshauri Spika aruhusu kamati ya bajeti ikutane kwa dharura wiki ijayo kufanya kazi ya kupitia matumizi ya Serikali kwa lengo la kuanisha maeneo ambayo Serikali inaweza kubana matumizi kwa haraka kufidia pengo la bilioni 178 zinazotafutwa kwenye tozo hiyo ya simu. Hatua hii itawezesha kodi hiyo kuacha kutozwa bila ya kulazimika hata kuongeza vyanzo vingine vya fedha iwapo Serikali inasuasua kupanua wigo wa mapato.

Friday, July 19, 2013

Kufuatia kauli za Serikali magazetini kuhusu mimi na kodi ya umiliki wa kadi za simu; nijibu tu kwa ujumla kwamba SITAACHA. Badala yake naomba kuwapatia namba zao: Makamba 0767783996 na Mgimwa 0754/0684765644, tunachohitaji ni kauli ya Serikali kuwa kodi imesitishwa na itaondolewa na sio siasa chafu.

Kwa mliotaka msimamo wangu juu ya kauli ilinukuliwa jana tarehe 18 Julai 2013 na Gazeti la Majira kwamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Januari Makamba kwamba; “Mnyika anaangalia upepo unakoelekea, akiona watu wanalalamika ndipo anaongea namsihi aache kufanya siasa katika jambo hili”, naomba kutumia mtandao huu kutoa majibu ya ujumla kwa maswali na masuala yote kama ifuatavyo:

Nieleze kwamba sitaacha kufanya siasa kwenye jambo hili mpaka kodi hiyo itakapofutwa kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini kubaki na fedha walau kidogo kwa maendeleo.

Sitaacha kufanya siasa kwa sababu ndio kazi yangu ambayo wananchi walinichagua kuifanya ya kuwawakilisha na kuisimamia Serikali ambayo yeye Makamba ni sehemu yake. Sitaacha kufanya siasa kwa sababu Mwalimu Nyerere alisema ili nchi yetu iendelee inahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.

Ambacho sitafanya ni siasa chafu kama hizo ambazo Makamba amefanya za kusema uongo, kwa kuwa naamini anafahamu kabisa kwamba sijaanza kuongea kuhusu suala hili baada ya malalamiko ya wananchi bali jambo hili nilianza kulishughulikia bungeni mara baada ya Waziri wa Fedha kuwasilisha jedwali la marekebisho la kuanzisha kodi lukuki za simu ikiwemo hii. Katika mchango wangu bungeni, nieleza kwamba muswada huo wa sheria ya fedha kwa kupandisha kodi kwenye mafuta na simu ni ‘muswada wa majanga ya kuwaongezea mzigo wa gharama za maisha kwa wananchi.

Wednesday, July 17, 2013

Kodi ya kadi ya simu (SimcardTax): Maoni ya awali ya wananchi juu ya hatua za kuchukuliwa

Nawashukuru kwa maoni ambayo mmenitumia kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa kufuatia kuanzishwa kwa ushuru wa bidhaa kwa kadi za simu (sim card) kwa wamiliki wa simu za kiganjani/mkononi.

Bado naendelea kuchambua maelfu ya maoni yaliyotolewa katika mijadala na niliyotumiwa kwa barua pepe. Nitoe mrejesho wa awali kwamba kwa muktasari mapendekezo niliyoyachambua mpaka sasa yanapendekeza hatua zifuatazo kuchukuliwa:

Monday, July 15, 2013

Mnyika aponda sera za michezo za CCM

Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Ubungo, John Mnyika amesema ukosefu wa maandalizi ya mapema katika micheo kunatokana na sera za Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndiko kunakoibua matokeo mabovu katika sekta hiyo hususan kwa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars.

Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, aliyasema hayo jana wakati akizindua michuano ya Mama Kevin Cup kwenye viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chang’ombe (DUCE), jijini Dar es Salaam.

Mnyika alisema katika ilani ya uchaguzi ya Chadema 2010, waliahidi masualaya michezo hususan Tanzania kucheza fainali za Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia Brazil mwakani endapo wangekabidhiwa cnchi, lakini kutokana na baadhi ya maeneo kutowataka waingie serikali mpya, hayo yameshindikana chini ya sera mbovu za CCM.

Saturday, July 13, 2013

Mkutano wa hadhara leo Julai 13, 2013 Dar es Salaam!

Msimamo wetu kuhusu rasimu ya katiba mpya na mustakabali wa taifa utatolewa leo Jumamosi ya Julai 13, 2013 kwenye mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Ukombozi-Manzese kuanzia saa 8 mchana.

Hotuba zitatolewa na viongozi mbalimbali wakiwemo Dr.W.Slaa, T.Lissu, M.Marando nk nathibitisha nami nitakuwapo kuwakaribisha Jimboni Ubungo.

Wananchi wote mnakaribishwa. Njoo wewe, njoo na yule!

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli!

Muhimu: Shule ipo jirani na Manzese TipTop. Maelekezo wasiliana na: M/Kt wa Kata ya Manzese Ali Makwilo 0784-691449 au 0715-691449 au 0769-658593

Thursday, July 11, 2013

KAULI YA WAZIRI WA FEDHA KUHUSU KODI YA LINE ZA SIMU NI KIELELEZO CHA UDHAIFU WA SERIKALI NA UZEMBE WA BUNGE; NIANDIKIE SASA KUHUSU HATUA ZA KUCHUKUA JUU YA SUALA HILI KUPUNGUZA MZIGO WA GHARAMA ZA MAISHA KWA WANANCHI

Katika kipindi cha Hot Mix cha EATV muda mfupi uliopita Waziri wa Fedha amesema kwamba mawazo ya kutoza elfu moja kwa mwezi kwenye kila laini ya simu ni ya wabunge. 

Kauli inayokaribiana na hiyo imewahi kuandikwa pia na Naibu Waziri wa Wizara yenye dhamana na sekta mawasiliano kwenye mitandao ya kijamii katika siku za karibuni. Baadaye alifuata Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na sasa waziri mwenyewe. Mwaka 2012 nilitahadharisha kuhusu udhaifu wa Rais (na Serikali) na uzembe wa Bunge katika masuala yanayohusu maandalizi ya bajeti, hususan kutozingatiwa kwa mpango wa taifa wa maendeleo na ongezeko la mara kwa mara la gharama za maisha kwa wananchi. Kwa kauli hizi za Serikali udhaifu na uzembe huo unaendelea kujihidhirisha.

Kauli hizi za Serikali ni za kujivua mzigo wa lawama baada ya malalamiko ya wananchi kuhusu kodi hii na nyinginezo kwa kuhamisha mzigo huo kwa wabunge.

Ni muhimu badala ya kutoa kauli za ujumla za kulaumu wabunge, Serikali ijitokeze itaje kwa majina na wabunge gani hasa walitoa mawazo hayo. Mimi sijawahi kutoa wazo hilo wala kuliridhia. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwenye Hotuba yake juu ya Muswada wa Sheria ya Fedha ilipinga pendekezo hilo lililokuwepo katika jedwali la marekebisho lililowasilishwa na Wizara ya Fedha. Katika kuhakikisha kwamba kifungu hicho hakipitishwi, niliwasilisha jedwali la marekebisho ya sheria kutaka kifungu hicho kiondolewe katika muswada wa sheria ya fedha na marekebisho yake yaliyowasilishwa na Serikali.